Huyo mpenzi wako ulimtoa bikra au ulishakutwa kadinywa????.....ishi na mwanamke kwa akili na usipoangalia waweza kugombana na kila mtu mpaka wazaz wako!!!!
JF kuna magumegume balaa, we ni mwanamke kweli?
Hakuna wasiwasi hapo.....achunguze kwa umakini juu ya swala hlo ili achukue maamuz,huyo binti ni mtu mzima.Je aliowakubali alikuja kusema???ukiona hivyo hajampenda.......awe makini ktk mambo ya mapenzi!!
Sasa mpaka mtu amewekwa kwenye loudspeaker unataka uchunguzi gani? I doubt, nyie wengine ndo mnaona sawa tu kutembea na shemeji zenu.
Fuatilia ukipata chembe za ukwel bas mwambie ukweli huyo rafiki.
Hata ukitaka kumnasa ni rahis kupitia mwanamke ili isije onekana kasingjziwa!!!
Hivi umesoma vizuri alichokiandika? Au ni ule utaratibu wa kila thread lazima kuchangia hata kama hujui nini kinazungumziwa!
Nmeyasema mimi.........watu tunaona mbaliiiii!!!!
Mmmh
Ukute anataka biashara afanye yeye na bwana ake......sasa hyo ni sababu yakumgombanisha!!!!!
Kuna wimbo unaitwa "siku hizi hawalali"
Kwa mentality hizi hamwezi kumiliki ndoa
Ajifunze kujitegemea......sio kila jambo kuripoti unaweza vunja mahusiano ya watu.
Wanaume watu wa tamaa hata baba yake mzaz anaweza akamtongoza,je atakwenda kusema????.....hajampenda huyo!!!
Hivi mtu umemkatalia mpaka basi, ukimwambia ntasema hasikii na mnaonana mara kwa mara kwa sababu ni shemeji yako unahitaji hatua ipi zaidi ya kumwambia? Watu wa hivi hawachelewi kuja na tactics za tukose wote, akikutongoza ukachomoa atahamia kusema yeye ndo anatongozwa, so mwanaume akiambiwa na rafiki yake kwamba demu wake ni muhuni, fasta anamtema.
lakini rafiki yangu hakuelewa na mpenzi wangu akanambia na kuna siku alipiga simu mpenzi wangu akamuweka loudspeaker nikawa namsikia akimuambia mpenzi wangu mambo mengi ya uongo kuhusu mimi ikiwepo kuwa nina mahusiano na wapenzi wengine wengi na ni kitu sio cha kweli
Jaribu kuufanyia kazi huu ushauri!
Tengana naye kibiashara haraka iwezekanavyo kabla hamjafika mbali, watu wa namna hii wana hulka ya kuona vya wenzio ndo vizuri, au wenzio hawastahili hivyo walivyonavyo. Itafikia sehemu ukinunua kitu chochote kizuri hata kama ni kwa fedha ya nje ya biashara ataona wivu na kusema umeiba kwenye biashara.
Usimwambie habari za yeye kumtongoza mpenzi wako, we achana naye haraka sana na urafiki upungue kabisa. Kama mtu anadiriki kukusemea mbaya kwa mpenzi wako tena uongo, ujue atakuchomea kwa polisi ili ufungwe yeye abaki na biashara.
Ukisha achana naye mkataze mpenzi wako kufanya mawasiliano yoyote na huyo mtu, siku ukiona hilo limekiukwa ujue na huyo ni wa kupiga chini.
Marafiki wanafiki ni wabaya sana kufanya nao biashara.