Rafiki yangu anaitwa mtoto wa mama...

Rafiki yangu anaitwa mtoto wa mama...

IGADESA

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2021
Posts
389
Reaction score
1,051
Habari za majukumu members, ngoja nielekee moja kwa moja kwenye kisa husika. Nimepanga chumba hapa moro, vyumba viwili vinavyofuata baada ya chumba changu ni vya mshikaji wangu ambaye ni mtoto wa mwenye nyumba anaishi hapo kwao na mkewe pamoja na mtoto wake mmoja.

Siku moja akaniambia twenzetu tukapige vyombo kidogo kuna kuna kitu nataka unisaidie. Basi tukaenda baa ya karibu na maskani, tukaagiza vinywaji na jamaa akafunguka kwamba anaomba ushauri kuhusu masahiba yanayomkuta akiwa chumbani na mke wake, anasema mkewe anamlalamikia sana kwa nini bado wanaishi kwenye nyumba ya wazazi wa mwanaume ( ingawa vyumba vya mbele vinawapangaji nikiwemo na mimi), mkewe anataka wahamie eneo lingine maana anavyoendelea kubaki hapo kwao eti yeye mumewe anaendelea kubakia kuwa mtoto wa mama. Akaendelea kuniambia kwamba eti mkewe anadai anachukia kila siku kwenda kula nyumba kubwa na familia ya mumewe.

Jamaa yangu huyo ni dereva wa mafuso anasema aliamuaga kuishi hapo kwao kwavile kwanza hapo halipi kodi zaid ya kuchangia umeme na maji, pili kupunguza masimango ya kwenda kuishi kwenye nyumba za kupanga, mimi binafsi nikamwambia anipe muda wa kutafakari ili nimpe ushauri wenye tija, nikaona itakuwa vyema kama nitapata mawazo yenu wadau ili wikiendi hii jamaa akirudi toka mkoani nikae nae nimpe ushauri sahihi kama kuishi nyumbani kwa wazazi wake akiwa pamoja na mkewe ni kweli anabaki kuwa mtoto wa mama au lah..
 
Hukuwa na hata haja kuja kuuliza mkuu. NI MTOTO WA MAMA 101%

Anaogopa masimamango eti, khaa! Alafu mwanaume mzima na familia unaogopaje kodi? Kama hataki kulipa kodi si ajenge nyumba yake?

Dada anamzidi akili mumewe full stop
 
Kwa kuwa ni dereva wa masafa na muda mwingi hayupo abaki hapo hapo kwao hiyo itakuwa ni mbinu ya mkewe kutaka kukaa mbali na waangalizi/wazazi ili kipindi jamaa akiwa safari wahuni wachakate papuchi kwa kujinafaaas.

Zaidi anachokipata awekeze aanze ujenzi wa makazi yake.

Tuliambiwa tuishi nao kwa akili.
 
Hukuwa na hata haja kuja kuuliza mkuu. NI MTOTO WA MAMA 101%

Anaogopa masimamango eti, khaa! Alafu mwanaume mzima na familia unaogopaje kodi? Kama hataki kulipa kodi si ajenge nyumba yake?

Dada anamzidi akili mumewe full stop
Labda mshkaji hana uhakika na ajira bado, kazi za udereva hazina mikataba leo upo kazini kesho upo juu ya mawe.
 
Sasa huyo mwanaume ni driver wa magari makubwa, anashindwa vipi kwenda kuishi kwa kulipa kodi huko sehemu nyingne? Mkewe yupo sahihi sana, watoke hapo tena haraka iwezekanavyo.
 
Kabla sijashauri, hebu jibu kwanza - Ni rafiki yako ama hii stori inakuhusu wewe mwenyewe?
Mimi siyo mtoto wa mwenye nyumba. Nimekuja kuiwasilisha kwa wadau ili nimpe ushauri unaoleweka. kwa hiyo we shauri tu.
 
Kwa kuwa ni dereva wa masafa na muda mwingi hayupo abaki hapo hapo kwao hiyo itakuwa ni mbinu ya mkewe kutaka kukaa mbali na waangalizi/wazazi ili kipindi jamaa akiwa safari wahuni wachakate papuchi kwa kujinafaaas.

Zaidi anachokipata awekeze aanze ujenzi wa makazi yake.

Tuliambiwa tuishi nao kwa akili.
Unadhani akibaki hapo hawezi kusaliti hata kama moyo wake utamtuma kufanya hivyo?
 
Kuishi kwenye Nyumba ya wazazi ni kosa ktk maisha, hupumbaza akili, ajipange kwa kutafuta pesa, ili akapange aanze maisha yake, angetakiwa kwa sasa anajiandaa kuhamia kwenye Nyumba Yake au anabiashara imesimama anajipanga kujenga au kuhamia kwenye nyumba ambayo haitampa kero za kupanga.
 
Back
Top Bottom