Jaman, hebu nisaidieni ktk hili, mimi nimeolewa na nnampenda sn mume wangu, sijawahi kumsaliti tokea nimekutana naye.
Hivi keribuni amenitambulisha kwa rafiki yk ambaye alionekana mstaarabu kumbe mnafiki. Rafiki yake huyo ameoa ila cha kushangaza ananitaka mimi wakati mi ni mke wa mtu. Amekuwa akinishawishi kwa kw mme wangu ni mtu wa safari na yeye mke wake anafanya kazi mkoani. Mi nimemgomea kabisaa.
Asa nisaidieni, je nimweleze mume wangu, ila naogopa kuharibu mahhusiano yao, na vlvl naogopa siku mume wangu akijua km jamaa ananitokea! Naombeni ushauri!
Usimwambie mumeo kama huyo jamaa aliyekutongoza hakubughudhi sana maana kuna wanaume akikutongoza inakuwa kero.
Kama ikizidi na ukalazimika umwambie mumeo basi jitahidi kutumia indirect method, mfano tu unaweza tu kumwambia mumeo. Hivi mume wangu fulani ulijuana nae vipi? Ni lazima atakuuliza kwa nini? Unamjibu, mimi ninavyomuona kama hajatulia vile yaani macho yake yapo juu juu.
Akikuambia amekutongoza nini? Hapana ila naona kwa jinsi anavyoniangalia ni kama anataka kusema kitu ila anashindwa.
Akija jamaa unamwambia ukiendelea kunisumbua nitamwambia mume wangu maana nimeshakwambia sitaki.
Jambo lingine kama ushauri kwako,
Usimpe nafasi akushike hata kiungo chako kimoja hata kwa kukusifia kisha akajitia anataka kukugusa. Akifanya hivyo kuwa mkali na uonyeshe haupendi ujinga wake huo kabisa.
Pili kama akipiga simu usimchekee kama unongea na mpenzi wako, just be straight, hallow hallow, vipi safi. Eeeh nikusaidie nini au una shida gani? Ajue huna matani na wala haitakaa uitokee umsaliti mumeo kwa ajili yake.
Ni hayo tu.
Jaman, hebu nisaidieni ktk hili, mimi nimeolewa na nnampenda sn mume wangu, sijawahi kumsaliti tokea nimekutana naye.
Hivi keribuni amenitambulisha kwa rafiki yk ambaye alionekana mstaarabu kumbe mnafiki. Rafiki yake huyo ameoa ila cha kushangaza ananitaka mimi wakati mi ni mke wa mtu. Amekuwa akinishawishi kwa kw mme wangu ni mtu wa safari na yeye mke wake anafanya kazi mkoani. Mi nimemgomea kabisaa.
Asa nisaidieni, je nimweleze mume wangu, ila naogopa kuharibu mahhusiano yao, na vlvl naogopa siku mume wangu akijua km jamaa ananitokea! Naombeni ushauri!
keshakulegeza magoti???
Ukiona unashindwa mkataa mtu hadi usaidiwe, jua kuna tatizo mahali.
Hii mambo inakera! Jitahidi usolve mwenyewe hiyo issue. Usimchekee kabisa huyo shem wako. Hivi wanaume mkoje nyie!!
I guess na wanawake wa hivi pia wapo..!!!, anyway it takes two to tango.
Ni kweli sababu ni wanaume wengi ndio huwa rahisi kuwaanza wanawake na wana tamaa zaidi ila kwa kuwasaidia wanaume wa hivi na nyie kina dada inabidi kuwa wakali na kutokuwapa upenyo yaani ukiona tabia za hivi tu unapiga na marufuku hakuna kusogea karibu yangu kama rafiki yako hayupo (unamwambia rafiki yako ni yule kwangu unafata nini) yaani hakuna kumpa nafasi ya kutia neno la pili zaidi ya kwaheri na tusionane baadaeaaaaggggrhh! Nyie mmezidi bhana..
Ni kweli sababu ni wanaume wengi ndio huwa rahisi kuwaanza wanawake na wana tamaa zaidi ila kwa kuwasaidia wanaume wa hivi na nyie kina dada inabidi kuwa wakali na kutokuwapa upenyo yaani ukiona tabia za hivi tu unapiga na marufuku hakuna kusogea karibu yangu kama rafiki yako hayupo (unamwambia rafiki yako ni yule kwangu unafata nini) yaani hakuna kumpa nafasi ya kutia neno la pila zaidi ya kwaheri na tusionane baadae
Inaonekana na wewe unajiachia sana manake mwanaume simjinga hadi aanze kukutongoza ni kwamba tayari kaona kamwanya cha kufanikiwa maombi yake.Cha kufanya kwanza embu kaa kidini kwanza la sivyo yatakushinda