QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

SEHEMU YA 90



Ninahisi hivyo kwani tukio hilo
limetokea baada tu ya kitabu hicho
kutoweka” akajibu Marcelo
“ Unamfahamu mtu mwenye hizo
namba alizokupa baba yako ? akauliza
tena Austin
“ Hapana simfahamu”
Austin na Ernest wakatazamana
kisha Austin akasema
“ Suala hili linaonekana si suala
dogo.Ninasita kujiingiza huko kwa sababu
tayari kuna masuala mazito
yanayotukabili.Kwa kuwa tayari suala hili
liko katika mikono ya polisi basi hatuna
budi kuwaacha waendelee na uchunguzi”
akasema Austin
“ Uko sahihi Austin.Nitaweka mkazo
pia kwa jeshi la polisi wahakikishe
wanawasaka na kuwapata watu hao
waliotaka kukuua.Kwa sasa hadi hapo
tutakapopata maelekezo mengine toka
kwa David Zumo utaendelea kukaa hapa
pamoja na Austin.Hii ni sehemu salama
sana kwako kwa sasa.Utafuata yale yote
utakayoelekezwa na Austin”
“ Ahsante mheshimiwa rais.Mungu
awabariki sana” akasema Marcelo.Ernest
na Austin wakatoka mle chumbani
“ Suala la Dr Marcelo linaonekana ni
suala tata sana.David zumo ameingiaje
katika suala hili? Hicho kitabu alichopewa
na baba yake kina nini ndani yake?
Maswali haya yanalifanya jambo hili kuwa
gumu” akasema Ernest
“ Ni kweli mheshimiwa rais.Suala hili
linaoneana si suala jepesi.Ni suala pana
.Lazima kuna kitu kimejificha hapa na
ndiyo maana Marcelo anataka
kuuawa.Nahisi labda yawezekana ukawa
ni mtandao wa mambo haramu kama vile
madawa ya kulevya n.k Lakini hata mimi
uhusika wa David Zumo katika jambo hili
unanila akili sana.Anamfahamu Marcelo
lakini
Marcelo
hamfahamu
David.Inakanganya kidogo.Mheshimiwa
rais naomba tusiumize vichwa vyetu kwa
suala hili.Tuwaachie jeshi la polisi
watafanya uchunguzi wao na kupata
ukweli” akasema Austin wakaagana Ernest
akaondoka.
********************
Wakati rais wa jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Ernest Mkasa
akiondoka katika nyumba anayoishi
Austin,ukumbi mmoja mdogo wenye
kuweza kuchukua watu zaidi ya hamsini
uliopo ndani ya jumba moja kubwa la
kifahari lililoko kandoni mwa bahari
,kikao kizito kilikuwa kinafanyika
kilichowakutanisha watu zaidi ya
arobaini.Katika ukumbi huo kulikuwa na
luninga nne kubwa ambazo kulikuwa na
watu wakionekana waliokuwa nje ya nchi
wakiunganana wenzao wa hapa Tanzania
katika kikao kile.Kikao kile kilihudhuriwa
na makamu wa rais wa Tanzania,waziri
mkuu aliyevuliwa madaraka pamoja na
baadhi ya viongozi na wafanya biashara
wakubwa ambao ni wajumbe wa kamati
kuu ya Alberto’s Tanzania.
“ Kabla ya kiongozi wa kikao
kuwasili kulikuwa na minong’ono ya hapa
na pale na wajumbe wakijadiliana hili na
lile.Kiongozi wa kikao kile aliyevaa suti
nyeusi mfanya biashara tajiri mtanzania
mwenye asili ya Ghana,Obi Ochukwu
akatokea akiwa ameongozana na wajumbe

 
SEHEMU YA 98



DAR ES SALAAM – TANZANIA
Habari kubwa iliyoliamsha taifa
asubuhi hii ni hotuba ya rais aliyoitoa
usiku .Maamuzi aliyoyafanya yaliendelea
kuwa gumzo kila kona ya nchi.Wengi
walipiga simu katika vituo vya redio na
televisheni wakimpongeza rais Ernest
Mkasa kwa maamuzi yake ya busara
kuhusiana na muswada ule wa haki za
binadamu pamoja na kulivunja baraza la
mawaziri.Wakati mjadala wa maamuzi
yale ya rais ukiendelea ,kurugenzi ya
mawasiliano ikulu ikatoa taarifa kwa
vyombo vya habari ambayo ilizidi
kuwashangaza wengi.Taarifa hiyo ilieleza
kwamba rais wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania amemvua wadhifa mkuu wa
majeshi na Jenerali Bonifasi Kandima na
papo hapo amempandisha cheo Luteni
jenerali Lameck Msuba kuwa jenerali na
kumteua kuwa mkuu wa majeshi kushika
nafasi iliyoachwa wazi na jenerali
Bonifasi.Uteuzi huo unaanza mara
moja.Taarifa hii ilizidi kuukoleza moto wa
mjadala uliokuwa ukiendelea.
Austin akiwa sebuleni akifuatilia
habari zilizoliamsha taifa pamoja na
uchambuzi wa magazeti ,mara mtangazaji
aliyekuwa akichambua kurasa za magazeti
akasitisha na kutangaza habari
iliyowafikia pale muda huo kuhusiana na
rais kutengua uteuzi wa mkuu wa majeshi
na kumteua jenerali Lameck Msuba kuwa
mkuu mpya wa majeshi.Austin akaruka
kwa furaha
“ Good !! Very good.Sasa vita imeanza
rasmi” akaongea mwenyewe pale sebuleni
“ Vita gani Austin? Akauliza Dr
Marcelo baada ya kuingia pale sebuleni na
kumkuta Austin akizungumza mwenyewe
kuhusiana na vita.Austin akastuka na
kugeuka akajikuta akitazamana na
Marcelo
“ Marcelo,vipi maendeleo yako?
Akauliza

Ninaendelea
vizuri
Austin.Nimekusikia unaongea mwenyewe
kuhusu vita,ni vita ipi hiyo unaiongelea?
“ Forget about that.Nilikuwa
natazama taarifa ya habari rais ameteua
mkuu mpya wa majeshi”
“ Austin nini kinaendelea? Jana rais
kaufuta muswada wa haki za binadamu
pamoja na kulivunja baraza la
mawaziri,leo kamvua wadhifa mkuu wa
majeshi ,nini kinaendelea? Akauliza Dr
Marcelo.Kabla Austin hajajibu Marcelo
akauliza tena
“ Who are you Austin? Kuna kitu gani
kinaendelea kati yako na rais?
“ Dr Marcelo itakuwa vyema endapo
hutajihusisha na masuala yoyote
yanayohusiana na mimi wala rais.Kikubwa
unachopaswa kukitilia mkazo kwa sasa ni
kupona na kuhakikisha wale wote
wanaokuwinda wakuue wanapatikana.”
Akasema Austin.Dr Marcelo akamtazama
Austin kwa makini na kusema
“ Austin kuna jambo ambalo
limeninyima usingizi kabisa.Kama
nilivyowaeleza jana kwamba nimestuka
sana kusikia eti rais wa Congo ndiye
aliyemuomba rais wetu anisaidie kunitoa
pale hospitali.Sijapata usingizi usiku wa
leo nikitafakari namna David Zumo

Nimeamua kuanza safari upyaaaaaaa
 
SEHEMU YA 110



hiyo nitahakikisha Monica na Marcelo
hawaonani tena.Nitaongea na rais wa
Tanzania na kumsisitizia Marcelo
aendelee kuhifadhiwa mahala salama na
ikiwezekana nitafanya mpango wa
kumuhamisha na kumleta Congo
atahifadhiwa mahala ambako hatatoka
hadi kifo chake au kama nitalazimika
kumtoa uhai nitafanya hivyo.Kwa ajili ya
Monica nitajifunza kuwa mkatili.Monica ni
wangu peke yangu”akawaza David na
kumpigia simu Ernest Mkasa rais wa
jamuhuri ya muungano wa Tanzania
wakaongea akamuomba Ernest eandelee
kumuhifadhi Marcelo mahlala alikofichwa
na asiruhusiwe kutoka hadi hapo
atakapotoa
maelekezo
mengine.Alipomaliza kuzungumza na
Ernest Mkasa akampigia Monica
“Monica nimezungumza na rais wa
Tanzania amesema kwamba atanipa
maelekezo baadae ya mahala alipo
Marcelo ili umtembelee”
“ Ahsante sana David kwa msaada
wako huu mkubwa” akasema Monica
wakaagana tena
“ Ngoja nipumzike kidogo nahisi
uchovu
mwingi.Sintakwenda
kuwatembela wazazi leo nataka
nipumzike hadi kesho asubuhi ndipo
nitawatembelea” akawaza Monica.
*******************
Saa tisa na nusu za alasiri ndege ya
shirika la ndege la Emirates iliwasili
katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa
Julius nyerere jijni Dar es salaam ikitokea
Dubai na miongoni kwa abiria walioshuka
katika ndege hiyo ni Maria mpenzi wa
Austin
Alikamilisha taratibu za uhamiaji
hapo uwanjani kisha akatoka nje ya
uwanja na kwa kuwa hakukuwa na mtu
yeyote aliyekuja kumpokea uwanjani
ikamlazimu akodishe teksi kuelekea
hotelini
“ Austin yuko ndani ya jiji hili na
ndiye aliyepaswa kuja kunipokea hapa
uwanjani leo lakini toka jana hakunitafuta
kama
tulivyokuwa
tumekubaliana.Ameniumiza sana lakini
kwa kuwa ninampenda sina budi
kumtafuta.Inaonyesha wazi hataki nije
Dar es salaam kwani toka nilipomueleza
nia yangu ya kuja Dar amekuwa akitoa
kisingizio cha usalama.Kuna kitu gani
Austin hataki nikijue? Ninahisi lazima
lazima atakuwa na mwanamke huku
Dar.Nitajua tu kinachoendelea na
ambacho hataki nikifahamu” akawaza
Maria akiwa garini akipelekwa hotelini
“ Dar es salaam imebadilika
sana.Limekuwa jiji la kisasa na la
kupendeza.Serikali ya Tanzania inastahili
pongezi kwa kulifanya jiji kuu la
kibiashara Tanzania kuwa zuri namna hii”
akaendelea kuwaza Monica huku
akitazama nje kushuhudia uzuri wa jiji la
Dar es salaam.

1
 
SEHEMU YA 10


hatari .Ni wafanya biashara wa dawa za
kulevya na wanafanya kazi kwa huyu
mtu niliyekupa namba zake.Kaa mbali
nao ni wauaji hatari.Mwisho kabisa
nataka nikuweke wazi kwamba hata
mimi tayari nimewekeza mtaji katika
biashara hiyo kwa hiyo mtu niliyekupa
namba zake ndiye anayefahamu kila
kitu na atakupa maelekezo na hiyo
ndiyo njia rahisi ya kujenga mazoea
naye
kwani
ataamini
kwamba
unaendeleza mradi wa baba yako
kumbe una ajenda nyingine.
Marcelo narudia tena kukusisitiza
kwamba wewe ndiye pekee ambaye
ninaamini
unaweza
kuokoa
nchi
yetu.Wewe ni kijana mwenye akili na
jasiri na ninaamini utafanya kila
unaloweza kulifanya ili kufanikisha
jambo hili.Ukishindwa au kupuuzia
utakuwa umefanya kosa kubwa sana na
taifa letu zuri litabomolewa.
Mwishi kabisa naomba haya mengi
niliyokueleza kuhusu maisha yangu
yabaki kuwa siri yako na asifahamu mtu
mwingine yeyote na hasa uhusika
wagnu katika biashara ya dawa za
kulevya.
Natumai
umenielewa
na
utayatekeleza yale yote niliyokuagiza
.Jambo la mwisho kabisa naomba kila
siku kabla ya kulala usiache kuniombea
kwa
Mungu
ili
anifutie
makosa
yangu.Nimekosa sana na katika saa
zangu za mwisho ninauona ubaya wa
yale yote niliyoyatenda.Niombee bila
kuchoka.Wewe ni kijana mwenye hofu
ya
Mungu
usije
kutenda
yale
niliyoyatenda
mimi
katika
maisha
yangu
Mungu akulinde na akubariki
Dr Richard
Boaz akashusha pumzi .Uso wake
ulionekana kuloa jasho jembamba. Kwa
sekunde kadhaa alionekana kama
amechanganyikiwa
“ Is everything ok Mr Boaz? Akauliza
Julieth
“Your father was a devil !! akasema
Boaz kwa hasira
“Laiti kama ningemfahamu kabla Dr
Richard ni mtu wa aina gani naapa
ningemuua kwa mkono wangu
mwenyewe” akasema Boaz huku akihema
kwa kasi.
“What’s wrong Boaz? Nini
kimetokea? Akauliza Julieth
“Unamfahamu Vera? Boaz akauliza
“Vera?!!..Julieth
akaonekana
kushangaa
“Ndiyo.Unafahamumahala anakoishi?
Huku akionekana kuzidi kushangaa
Julieth
akacheka
kidogo..Boazi
akamtazama kwa macho makali na
kusema
“Julieth this is a very very serious
matter.Tell me where Vera is please!!!
Akasema Boaz
“ Boaz I’m not jocking.I real don’t
know where Vera is.Whos is Vera ?
Boaz akaendelea kumkazia macho
Julieth halafu akampa barua ile aisome.
“Oh my gosh !! akasema Julieth baada
ya kumaliza kuisoma barua ile
“Sasa umefahamu namna baba yako
alivyo shetani.Naapa kama ningemfahamu
yuko hivi kabla hajafariki ningemuua kwa
mikono yangu.How could he do this to me?
Nimestuka sana.Sikutegemea kabisa kama
Dr Richard anaweza akanifanyia hivi”
akasema Boaz
“Hata mimi nimestuka sana .Hili ni
jambo la kushangaza mno” akasema
Julieth.Boaz akakishika kitabu kile na
kumtupia Julieth
“Kitabu hiki sicho kile nilichokuwa
nakitafuta .Hiki kimejaa upuuzi mtupu na
hakina msaada wowote kwangu .Kitabu
ninachokihitaji ni hicho ambacho
amemuelekeza Marcelo kwamba
amekihifadhi kwa Vera na ndiyo maana
nahitaji sana kumfahamu huyo Vera ni
nani? Ninaamini huyo Vera anafahamu
alipo Marcelo na kama tukifanikiwa
kumpata
atatuelekeza
mahala
alipojificha.Kwa sasa tumerudi katika
sifuri.” Akasema Boaz na kuinamisha
kichwa
“I’m so sorry Boaz.Hata mimi
sikujua” akasema Julieth
“Si kosa lako Julie.Hata hivyo
tunatakiwa kuanza upya tena na
tunatakiwa kufanya kila ,liwezekanalo
kuhakikisha kwamba kwa gharama zozote
zile tunampata Marcelo na hicho
kitabu.Bila kumpata Marcelo au hicho
kitabu tumekwisha kwani kitabu hicho
kina maelezo yote kuhusiana na sisi kama
ulivyosoma katika barua .Naamini tayari
Marcelo atakuwa amekwisha anza
kutekeleza maagizo ya baba yake na tayari
anao watu anaoshirikiana nao ambao ni
watu wenye uwezo mkubwa .Namna
alivyoweza kutolewa hospitali ni
kithibitisho tosha kwamba watu anao
shirikiana nao si watu wa mchezo.”
Akasema Boaz huku sura yake ikionyesha
wasi wasi mkubwa.
“Rais Ernest amewasaliti wenzake na
kwa sasa anaendelea kuwaondoa Alberto’s
katika nyadhifa zao ndani ya serikali na hii

10
 
SEHEMU YA 28


biashara hao ili tuweze kupambana nao na
ameahidi kunipatia orodha hiyo .Baada ya
kuisikia historia yako ninahisi kuna
uwezekano mkubwa hata huyo dogo Bill
aliyepelekea ukaishi katika maisha haya
naye yumo katika hiyo orodha .It’s tme to
fight back.Ni wakati wetu wa kuwa
huru.Hatuwezi kuwa huru endapo
hatutawaondoa wale wote waliotufanya
tuishi maisha ya namna hii ,wale ambao
wameibinafsisha nchi hii na kuifanya
yao,hatutakuwa
huru
endapo
hatutafanikiwa kuwaondoa Alberto’s hapa
nchini.Mpaka lini nitaikimbia nchi yangu?
Makaburi ya wazazi wangu yako hapa
Tanzania kwa hiyo hata kama nitabadili
uraia lakini sintaweza kuibadili damu ya
Tanzania.Lazima mambo haya yafike
mwisho na yatafika mwisho endapo
tutaweza kuwaondoa Alberto’s na mizizi
yake hapa nchini.Nani wa kuwaondoa
Alberto’s hapa nchini? Ni mimi ,wewe na
wazalendo wengine wachache walio tayari
kuifia nchi yao.Tunaweza tusifanikiwe au
tusifike mbali katika vita hii lakini
tukianzisha tutaungwa mkono na watu
wenye nia njema na nchi hii.Naomba
usiogope Job,hii ni nafasi ya pekee
imejitokeza ambayo itakusaidia kulipiza
kisasi kwa wale wote waliofanya maisha
yako kuwa hivi pia kupata ukweli kuhusu
mke na mtoto wako walipo.This is our
chance brother” akasema Austin .Michirizi
ya machozi ikaonekana machoni mwa Job
“Austin umenichoma mno moyo
wangu na kuyaamsha tena machungu
niliyonayo dhidhi ya Dogo Bill na kundi
lake.Wamenifanyia unyama mkubwa
kuniachanisha na mke wangu.I loved Mona
so much lakini kwa tamaa ya pesa
akachagua kunikimbia.You are right.Its
pay back time.Austin nitaungana nawe
katika haya mapambano lakini si kwa
kuingia katika timu ya kumlinda
rais.Nataka niwe pembeni yako
tupambane kwa pamoja.Nitakusaidia
kutafuta watu watakaounda hicho kikosi
cha ulinzi wa rais.Nataka niwepo katika
uwanja wa mapambano na nihakikishe
ninamkamata dogo Bill kwa mikono yangu
mwenyewe.Nikubalie kwa hilo Austin”
akasema Job .Austin akamtazama kwa
muda halafu akatabasamu na kumpa Job
mkono
“Karibu
katika
operesheni
fagio.Tunakwenda kufagia nchi hii na
kuuondoa uchafu wote na kuifanya safi
tena kama ilivyokuwa awali enzi za
waasisi wetu” akasema Austin
“Mungu atusaidie “ akasema Job
“Austin baada ya kuwa tumekuwa
kitu kimoja naomba sasa unipe mikakati
yako namna ulivyopanga kuiendesha
operesheni hii.Lakini kabla hujanieleza
chochote nina ombi moja kwako”
“Omba chochote Job” akasema Austin
“Ahsante sana.Naomba ukubali
kumuingiza Amarachi katika operesheni
hii.She’s a great asset to us”
Austin akakuna kichwa akafikiri
kidogo halafu akamtazama Job
“ Job I have to be honest with you.Hii
ni opereseni tofauti sana na nyingi ambazo
tumewahi kuzifanya kwa hiyo napata
ugumu kidogo kulikubali ombi
lako.Tunakwenda kupambana na adui
mwenye nguvu na mbinu nyingi kwa hiyo
tunahitaji kuwa na watu wenye uwezo
mkubwa kama wewe.Zaidi ya yote I cant
work with people I don’t trust” akasema
Austin
“Nafahamu msimamo wako Austin
lakini
naomba
uniamini
ninachokwambia.This
woman
is
wonderfull.Ana uwezo mkubwa kiasi cha
kunishangaza hata mimi .Nakuhakikishia
anaweza kuwa na msaada mkubwa
kwetu.She’s well trained .Please let her in”
Austin akafikri tena kidogo na
kusema
“Sawa Job ,nimekuelewa lakini kabla
sijaamua chochote kama nimjumuishe ama
vipi I’ll have to talk to her in person. I want
her to understand how important this
mission is for me,you and for our nation”
akasema Austin
“Thank you”akajibu Job
“Ningetaka sasa nifahamu mikakati
yako kuhusiana na suala hili” akasema Job
“Kitu cha kwanza tunachotakiwa
kukifanya ni kutafuta namna ya kumlinda
rais.Nguvu aliyonayo ni msaada mkubwa
sana kwetu kwa hiyo lazima tumlinde kwa
nguvu zetu zote.Tunatakiwa haraka sana
tupate kikosi kipya cha kumlinda.Kwa sasa
tunaendelea kujipanga ,nitakapomaliza
kazi aliyonipa rais tutakaa pamoja na
kujadili nini cha kufanya na wapi kwa
kuanzia.” Akasema Austin
“Austin we have to make things
faster.Tukizidi kuchukua muda mrefu
tutawapa nafasi ya kujipanga na
wakatuzidi maarifa.Naamni hivi sasa
watakuwa katika mstuko mkubwa kwa hili
lililotokea so we have to take them by
surprise.Tusiwape nafasi” akasema Job
“Uko sahihi Job,lakini watu hawa
wamejiimarisha sana na mizizi yao tayari
imesambaa katika sehemu kubwa kwa
hiyo basi inabidi tukae chini tujipange
namna ya kuwakabili.Kwa pamoja
tutaamua namna bora ya kuwandoa”
Austin akanyamaza kidogo na kusema

28
 
SEHEMU YA 12


“ Anaitwa Maria”
“ Yuko wapi sasa hivi?
“ Yuko hapa nyumbani
kwangu.Nimemuhifadhi sehemu salama
kwa ajili ya mahojiano.”
“ Good.Kuna jambo lingine kuhusu
huyo binti.Baba yake anaitwa Boaz
.Huyo Boaz ndiye aliyemkomboa Austin
katika mikono ya Alshabaab akamsaidia
kuanza maisha mapya Afrika ya
kusini.Boaz ndiye aliyemsaidia Austin
kufika hapa alipofika.Hata mimi
nimelazimika kupitia kwa Boaz ndipo
nikafanikiwa kumpata Austin.Boaz
amenipgia simu muda mfupi uliopita
akanijulisha kwamba Maria ameondoka
hotelini usiku wa jana akaelekea kwa
Austin .Nilimueleza kwamba Austin
amepigwa risasi akastuka sana na
ameanza kuhoji alipo
mwanae.Nimemuhakikishia kwamba
vyombo vya uchunguzi vitampata
mwanae hivyo asijali.Hivi tuongeavyo
ameanza safari ya kuelekea hospitali
kumtazama Austin.Nimeona nikujulishe
ili Austin apewe taarifa haraka kwamba
asimueleze Boaz chochote kuwa
mwanae ndiye aliyempiga risasi jana
usiku.Umenielewa Job? Akauliza rais
“ Nimekuelewa mzee lakini kuna
jambo nataka niombe msaada wako”
“ nakusikiliza Job” akasema rais
“ jana nilikueleza kwamba mimi na
Austin tayari tumeanza uchunguzi
kuhusu Mukasha na mmoja wa watu
ambao tunawahitaji kutupatia taarifa za
Mukasha ni huyo Boaz.Tunamuhitaji
sana na ninadhani huu ni wakati
muafaka wa kumpata”
“ That’s a good idea.Hata mimi
ninakubaliana nanyi.Ni kweli Mukasha
ndiye aliyeniunganisha na Boaz kwa
kudai kwamba ni marafiki kwa hiyo
ninakubaliana kabisa na mpango wenu
wa kumtumia Boaz kumfahamu zaidi
Mukasha.Nitawaelekeza vijana wangu
pale hospitali ili Boaz atakapojitokeza tu
basi achukuliwe mara moja na
wamkabidhi kwenu ili mumfanyie
mahojiano”
“Ahsante mheshimiwa rais
nitakupa taarifa za kila tutakachokuwa
tunakifanya.” Akasema Job na rais
akakata simu.Job akampigia Amarachi
“Hallow Job” akasema Amarachi
baada ya kupokea simu .
“Amarachi kuna habari yoyote
mpya hapo hospitali?
“Hakuna habari mpya.Austin
anaendelea vizuri .Nimetoka kuongea
naye muda si mrefu amesema anahitaji
supu.Nimeagiza hotelini waniletee supu
haraka.He’s so strong”
“ That’s a good news.Nashukuru
kwa maendeleo hayo ya haraka.Huku
nyumbani kuko salama.Mtu wetu naye
anaendelea vizuri.”
“ Good.” Akajibu Amarachi
“ Amarachi rais amenipigia simu
muda mfupi uliopita tumezungumza na
kuna jambo amenieleza.Baba yake
Maria ameanza kumtafuta
mwanae.Huyu ni mtu muhimu sana
kwetu ambaye alikuwa tayari katika
orodha ya watu tunaowatafuta.Hivi
tuongeavyo yuko njiani anaelekea
hospitali kuja kumuona
Austin.Tunatakiwa kuitumia fursa hiyo
kumpata.Rais amekwisha toa Baraka
zake na kuturuhusu tumchukue Boaz”
akasema Job na kumpa Amarachi
maelekezo
“Usijali Job nitafanya kama
ulivyoelekeza” akasema Amarachi

12
 
Sehemu ya 38

Amarachi na Job waliwasili katika jengo iliko saluni kubwa ya Julieth.Job akampigia simu Julieth akamfahamisha kuwa tayari amekwisha fika pale na kumuelekeza aina ya gari alimo
.Alipomaliza kuongea na Julieth
akampigia simu Amarachi
“ Tayari nimempigia simu na muda wowote atashuka.Kuwa makini”
akasema Job
“Niko makini Job.Mpaka sasa sijaona hatari yoyote” akasema
Amarachi aliyekuwa makini katika gari lake akitazama kama kuna hatari yoyote.Job hakukata simu akachomeka
spika za masikioni na kuiweka simu
mfukoni ili mawasiliano kati yake na
Amarachi yaendelee
Mlango wa gari la Job ukafunguliwa na mwanamke mmoja mwembamba mrefu mwenye umbo la uanamitindo akaingia
“ Are you Julieth? Akauliza Job
“ yes” akajibu Yule mwanamke
“Njoo ukae huku mbele.Sitaki mtu akae nyuma yangu” akasema Job na Julieth akahamia kiti cha mbele
“ Switch off you phone” akaamuru Job
“ Why ?? akauliza Julieth
“ Unataka kuonana na Marcelo ? “Ndiyo nataka”
“kama unataka kumuona tena
Marcelo basi utafuata maelekezo yangu.Zima simu yako” akaamuru Job na huku sura yake ameikunja Julioeth
akaizima simu yake
“Good.Now we can go” akasema
Job na kugeuza gari wakaondoka
“Job mpaka hapa sijaona hatari yoyote.Niko nyuma yenu” Amarachi akamwambia Job aliyekuwa anamsikia kupitia spika za masikioni alizokuwa amevaa
Safari ilikuwa ya kimya kimya hadi walipofika nyumbani kwa Job
“Marcelo amekuja kujificha mbali
namna hii !!akasema Julieth
“ Yah” akajibu Job na kufungua mlango akashuka ,Julieth naye akashuka wakaelekea sebuleni
Mara tu walipoingia sebuleni Julieth akakutanisha macho na Marcelo.Wote wawili wakabaki wanatazamana.Julieth akamkimbilia Marcelo na kumkumbatia
“ Oh Marcelo !!! akasema kwa
furaha
“ mambo vipi Julieth? Akauliza
Marcelo
“ mambo poa Marcelo unaendeleaje? Oh gosh hatulali tunakuwaza wewe kama uko mzima.Nashukuru sana uko salama Marcelo” akasema Julieth
“ Julieth tafadhali nenda uketi pale”Job akamuelekeza Julieth sehemu ya kuketi na muda huo huo Amarachi akaingia
“ It’s clear.Hakuna anayetufuatilia” akasema Amarachi ,Julieth akaonekana kushangaa
“Bila kupoteza muda naomba nikutambulishe Julieth kwa watu waliomo humu ndani” akasema Job
“ Yule aliyelala pale sofani anaitwa
Austin ndiye mkubwa wetu hapa. Mimi naitwa Job na huyu mwanamama
anaitwa Amarachi.Sisi ndio tunaomlinda kaka yako Marcelo dhidi ya wale wanaomtafuta wamuue na
wewe ukiwa mmoja wao” akasema Job na kumstua Julieth
“Julieth kuanzia sasa utakuwa mikononi mwetu na pengine hutaondoka salama katika jengo hili kama hutatueleza kile tunachotaka kukisikia” akasema Job
“ Samahani kaka Job.Sijakuelewa
unamanisha nini? Mimi ni ndugu yake Marcelo na siwezi katu kumfanyia kitu kama hicho.Unafahamu ni uchungu kiasi gani tulio nao kwa hayo yaliyompata ndugu yetu? Marcelo tafadhali waeleweshe wenzako” akaongea Julieth kwa ukali
“ Taratibu Julieth” akasema Marcelo
“ Julieth tunataka kufahamu
mahusiano yako na Boaz” akauliza Austin
“ Boaz??!! Julieth akauliza kwa mshangao
“ ndiyo”
“ Simfahamu mtu yeyote anaitwa
Boaz” akajibu Julieth
“ Are you sure? Akauliza tena Austin
“ yes I’m sure” akasema Julieth
“ Marcelo nini kinaendelea hapa? Mbona siwaelewi wewe na wenzako? Akauliza Julieth
“ Job” akaita Austin
“ Make her talk” akasema Austin aliyekuwa amelala sofani
“ Julieth welcome to the hell.You are going to answer all my questions.If you cant give me the right answers
you’ll never see the sun again!! Akasema Job huku akimtazama Julieth kwa macho makali
“ Tueleze wewe na Boaz mna mahusiano gani? Akauliza Job
“Jamani nimekwisha waeleza kwamba simfahamu mtu yeyote anayeitwa Boaz.Kama mna lengo la kuniua basi niueni lakini simfahamu Boaz” akasema Julieth .Job akachukua simu ya Boaz
“ Hii ni simu ya Boaz.Mawasiliano yako naye tunayo na hata ujumbe wa mwisho uliomtumia uko hapa” akasema Job na kumuonyesha Julieth ule ujumbe aliomtumia Boaz.Midomo ya Julieth ikamtetemeka akashindwa kuongea.
“ Nataka unijibu sasa.Unamfahamu
Boaz” akauliza Job
“ Hapana simfaham……..” Kabla hajamaliza Amarachi akaichomoa bastora
“ Huyu mwanamke anatuchezea
akili zetu!! Akasema na kumlenga
Julieth miguuni
“ Basi… basi!! Nitawaeleza kila kitu
!! akapiga ukelele Julieth .Bado Amarachi aliendelea kumtazama kwa hasira
“ It’s ok Amarachi .Let her talk”
akasema Job
Julieth akavuta pumzi ndefu akafuta machozi na huku akitetemeka akasema
“Ni kweli mimi na Boaz tuna mahusiano ya kimapenzi kwa muda mrefu toka angali baba hajafariki.” Akasema Julieth
“ tell us more !!! akafoka Job
“ Boaz ni mfanyabiashara wa dawa za kulevya na alikuwa rafiki wa baba ambaye naye alikuwa anajihusisha na biashara hiyo ya dawa za kulevya.”
“ What ?!! Marcelo akashangaa
“ Marcelo kuna mambo ambayo huyafahamu kuhusu baba .Kuna mambo mengi aliyokuwa anayafanya kwa siri
.Nilipoanza mahusiano na Boaz ndipo nilipofahamu kwa baba alikuwa anajihusisha na biashara hiyo na utajiri wake mkubwa ulitokana na hiyo biashara.” Akanyamaza akafuta machozi na kuendelea
“ Baada ya baba kufariki ,Boaz alinifuata akanieleza kuwa anakihitaji kitabu muhimu ambacho baba alikuachia.Alinipa namba za siri za kasiki lako nikaingia chumbani kwako na kukichuka kitabu hicho pamoja na
nyaraka zako mbali mbali likiwemo faili lenye historia ya ugonjwa wako ambalo lilipelekwa kwa mwanamke anaitwa Monica lengo likiwa ni kukuchanganya
ili usikumbuke kuhusu kitabu kwani ilisemekana kuwa wewe na Monica ni
wapenzi.Baada ya kukipata kitabu hicho nikasikia umepigwa risasi na yote hii ilikuwa ni mipango ya
Boaz.Ulipotoweka hospitali nilimtaarifu
Boaz akaja mara moja.Nilimpa kitabu kile nilichokichukua toka katika kasiki lako akakifungua na kudai kuwa si kile anachokihitaji.Ndani ya kitabu hicho kuna barua ambayo baba alikuandikia.Baada ya kugundua kitabu alichokihitaji si chenyewe Boaz amewekeza nguvu kubwa katika kukutafuta ili aweze kukipata kitabu hicho kwa gharama zozote.Uliponipigia nilimtaarifu Boaz kuwa umenipigia ili tukutafute na tukipate kitabu hicho.” Akasema Julieth na kunyamaza akatazama chini
“ Why are you doing this to me
Julieth? Akauliza Marcelo
“ I’m sorry Marcelo” akasema
Julieth na kuanza kulia.Amarachi akaufungua mkoba wa Julieth akatoa kitabu cheusi akampatia Marcelo
“ Kabla ya kifo chake baba alinipa kitabu hiki na sikuwahi kukifungua kujua nini kiliandikwamo ndani yake.” Akasema Marcelo
“ Hukuwahi kukifungua? Hujui kilichomo ndani? Akauliza Julieth
“ Ndiyo sijawahi kukifungua kitabu hiki na wala sifahamu kina nini ndani yake” akasema Marcelo na kuanza kukifungua kitabu kile kwa umakini mkubwa .Ndani ya kitabu kile akaikuta barua akaisoma kwa umakini na alipomaliza akampatia Austin
“ Dah ! akasema Austin alipomaliza kuisoma halafu akawapa Job na
Amarachi nao pia waipitie barua ile.Wote wakabaki kimya wakitazamana
baada ya kuisoma barua ile
“Job mfungie Julieth chumbani tutaendelea naye baadae” akaamuru Austin.Job akamshika mkono
“ Marcelo tafadhali naomba unisaidie!! Akasema Julieth lakini Marcelo hakujibu kitu.Job akampeleka katika mojawapo ya vyumba akamfungia na kurejea sebuleni
“ nadhani nyote mmeisoma barua na kuilewa vyema”akasema Austin
“ Mimi bado kuna mambo nahitaji kufafanuliwa.Dr Richard aliyeandika barua hii anaeleza kwamba alikuwa mfuasi wa Alberto’s na kwamba alikuwa anasimamia kukusanya mapato toka
kwa wafanya biashara wa dawa za kulevya walio chini ya Alberto’s.Hawa Alberto’s ni akina nani? Akauliza Amarachi
“Hata mimi ninataka kulifahamu
hilo kundi linalojiita Alberto’s” akasema Marcelo
Austin akawafahamisha Amarachi na Marcelo kila kitu kuhusiana na Alberto’s na kuwaacha na mshangao mkubwa
“ kwa hiyo “ akaendelea Austin
“ Dr Richard alikuwa akiwasimamia akina Boaz ambao ndio wafanya biashara ya dawa za kulevya walio chini ya mtandao wa Alberto’s.Nimeishi na Boaz kwa miaka kadhaa na amenitunza kama mwanae
na hata siku moja sikuwahi kuhisi kuwa ni mfuasi wa Alberto’s au anafanya biashara ya dawa za kulevya.Ni mtu
anayejua sana kuficha nyendo zake.Hata hivyo arobaini yake imewadia.hawezi kuchomoa kabhali yangu” akasema
Austin
“ This is a big war” akasema
Amarachi
“ Ni vita kubwa kwani watu tunaopambana nao ni watu wakubwa na wenye nguvu si hapa Tanzania tu bali duniani kwa ujumla.Pamoja na
ukubwa wao tusikate tamaa tupambane tuhakikishe tunaisafisha nchi” akasema Austin
“ kwa hiyo nini kinafuata ?
akauliza Amarachi
“ Tunatakiwa tukipate kitabu hicho anachokitafuta Boaz ambacho
kina orodha nzima ya wafanya biashara wa dawa za kulevya walio chini ya Alberto’s.Katika barua hii Dr Richard ameandika kwamba kitabu hicho amekihifadhi nyumbani kwa Vera.Huyu Vera ni nani? Austin akauliza
“ Vera ni mdogo wetu.Baba
alimzaa nje ya ndoa na hajawahi kumuonyesha mtu mwingine zaidi
yangu.Ninafahamu nyumbani kwake naweza kuwapeleka” akasema Marcelo
“ Good.Utaongozana na Job
kwenda huko sasa hivi .Hakikisheni mnakipata kitabu hicho” akasema Austin.Job akapanda ghorofani akarejea akiwa na begi dogo akamchukua
Marcelo wakaondoka
“ Amarachi niliambiwa na Job kwamba unamiliki hoteli? Akauliza Austin
“ Ndiyo ninamiliki hoteli kubwa hapa dar es salaam” akajibu Amarachi “Good.Nataka kiandaliwe chakula
katika hoteli yako kwa ajili ya usiku wa
leo.Kumbuka ni chakula maalum kwa ajili ya rais” akasema Austin
“ Sawa Austin ngoja nitoe maelekezo sasa hivi maandalizi yaanze mara moja” akasema Amarachi.

********************
Ni saa kumi na mbili za jioni Job na
Marcelo waliporejea nyumbani
wakitokea katika jukumu walilopewa na Austin kwenda kuchukua kitabu nyumbani kwa Vera.
“ Karibuni” akasema Amarachi
“ Austin yuko wapi? Akauliza Job
“ Nimemuacha chumbani anapumzika.Huko mtokako kuna mafanikio? Akauliza Amarachi
“ Ndiyo tumefanikiwa kukipata kitabu.Kuna lolote jipya hapa?
“ Hakuna jipya.Tunajiandaa kwa
ajili ya zoezi la usiku wa leo” akasema Amarachi.Job hakutaka maongezi zaidi akamfuata Austin ghorofani
“ Vipi Marcelo unajisikiaje?
Amarachi akamuuliza marcelo
“ Naendelea vizuri.Tumefanikiwa
kukipata kitabu japokuwa haikuwa rahisi lakini Job ametumia mbinu zake tukafanikiwa kuingia na kukichukua kitabu hicho”
“ Good.Mimi na Austin tutaondoka muda si mrefu kwenda kuonana na Monica usiku huu.Utabaki hapa na Job,jambo moja ninalotaka kukufahamisha kuhusu Job ni kwamba
ni mtu mwenye hasira za haraka ila fuata maelekezo yake na usibishane naye” akasema Amarachi
“ Ahsnate Amarachi kwa tahadhari hiyo.” Akajibu Marcelo
Austin akiwa katika chumba cha
kulala ,mlango ukagongwa na akumruhusu mgongaji aingie ndani,alikuwa ni Job.
“ Karibu Job” akasema Austin
aliyekuwa amekaa kitandani
“ Ahsante sana Austin” akajibu Job
na kuufungua mkoba akatoa kitabu cha kuhifadhia kumbu kumbu akamkabidhi Austin
“ Tumefanikiwa kukipata .Haikuwa rahisi hata hivyo Vera hatujamkuta ikanilazimu kutumia mbinu zetu na kuingia ndani tukakichukua kitabu”
“ Kazi nzuri.Mimi na Amarachi tunajiandaa kwenda kuonana na Monica usiku wa leo kwa hiyo nitakuachia kazi,nataka ukisome kitabu hiki chote ukielewe vyema kurasa kwa kurasa na nitakaporejea usiku wa leo utanipa
ripoti ya nini umekipata katika kitabu hicho.Baada ya hapo tutaanza mahojiano na watu wetu.Mgeni wa
kwanza atakuwa Boaz.” Akasema Austin
“ Sawa Austin.Kila kitu kitafanyika kama ulivyoelekeza.Utakaporejea
utakuta maandalizi ya mahojiano na watu wetu yamekamilika” akasema Job
akamsaidia Austin kushuka chini hadi katika gari la Amarachi wakaondoka Toka nyumbani kwa Job
walielekea moja kwa moja nyumbani kwa Amarachi.Aliingia ndani mwake akatoka na begi dogo akaingia garini wakaondoka
“ Mbona hujabadili mavazi? Austin akauliza
“ Nimeogopa
kuchelewa.Nimepakia kila kitu kwenye begi nitakwenda kuvalia hotelini tunakopita kuchukua chakula na wahudumu wa kutuhudmia” akasema Amarachi
“ Samahani sana kwa kuupoteza muda wako mwingi.Toka jana hujapata hata wasaa wa kupumzika.Hata hivyo umekuwa ni mtu wa muhimu sana kwetu zaidi ya nilivyotegemea”
akasema Austin
“ Oh Austin,usiwaze kuhusu mapumziko.Kuna kazi kubwa iko mbele yetu na tutapumzika baada ya kuikamilisha .Kwa sasa tuelekeze akili zetu kwanza katika afya na usalama
wako na pili majukumu mazito
tuliyoyabeba” akasema Amarachi
Waliendela na safari yao huku wakizungumza mambo mbali mbali hadi walipofika katika hoteli ya Amarachi.Austin hakushuka garini
.Amarachi akaichukua begi lake na kuingia hotelini akajiandaa wakati wakati wahukudmu wakipakia chakula na vitu vingine katika gari maalum.Austin akaitumia nafasi hiyo kumtumia ujumbe Monica kumuuliza kama tayari amekwishajiandaa na kumtaka amuelekeze alipo ili amtume
Amarachi akamchukue.Monica
akamuelekeza nyumbani kwake
Baada ya dakika kumi na tano,Amarachi akatokea akiwa amependeza vilivyo.
“Wow !Sijawahi kufanya operesheni iliyonikutanisha na wanawake wazuri kama hii.” Akawaza Austin akimshuhudia Amarachi akishuka ngazi
Kila kitu kinachohitajika kikapakiwa katika gari maalum wakaondoka..
“ Amarachi” akaita Austin
“ Nitakuwa sijatenda haki kama sintakupa hongera kwa namna ulivyopendeza usiku wa leo.” Akasema Austin na uso wa Amarachi ukajenga tabasamu kubwa
“ Ahsante sana Austin .Ni heshima
kubwa umenipa kuwa karibu yako na kufanya nawe kazi.Kupitia kwako
nimeweza kukutana na watu wakubwa kama rais wa nchi.Kwa kukutana nawe nimejiamini zaidi na ninaweza kufanya jambo lolote kwa muda wowote” akasema Amarachi na safari ikaendelea
“Austin kuna kitu nataka kukuuliza naomba uwe muwazi kwangu tafadhali”
“Uliza Amarachi”
“Leo asubuhi pale hospitali niliwashuhudia kwa mara ya kwanza wewe na Monica nikagundua kuna kitu kipo kati yenu ambacho aidha mnakijua au bado hamjakijua “
“ Kitu gani?
“Mnavutia sana mkiwa pamoja.Niliona namna Monica alivyokuwa akikulisha matunda.Kuna kitu kinawazunguka.”
Austin akatabasamu na kusema
“ Amarachi usiende huko tafadhali
.Mimi na Monica ni marafiki tu tena tumefahamiana muda si mrefu.Nilijenga urafiki naye baada ya kupewa kazi na
rais ya kutafuta sampuli kwa ajili ya kipimo cha vinasaba.Moyo wangu niliufungua kwa mwanamke mmoja tu ambaye ni Maria na mpaka sasa bado siamini kama Maria ambaye niliufungua moyo wangu kwake peke yake ndiye aliyetaka kunitoa uhai” akasema Austin
“ Pole sana Austin” akasema
Amarachi wakaendela na safari yao.
Walifika katika makazi ya Austin aliyopewa na rais.Jumba lilikuwa kimya sana japo taa za nje zilikuwa zikiwaka.Austin akafungua geti
wakaingia ndani akamkaribisha Amarachi na wale wahudumu na maandalizi yakaanza.Wakati wahudumu wakiendelea kuandaa
Austin akamtaka Amarachi akamchukue
Monica

*****************
Saa mbili na dakika kumi na nane Ernest Mkasa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania akawasili
katika nyumba aliyompa Austin aishi.Ujio wake ulimstua Austin kwani haukuwa ule ujio wake wa kawaida aliouzoea.Hakuwa ameongozana na walinzi wake wa kawaida.Alikuwa ameongozana na makomando zaidi ya
kumi
Rais akawataka makomando wale wabaki nje akaingia ndani peke yake akiongozana na Austin.
“ Austin sikuwa nimekutaarifu mapema kuna maamuzi niliyafanya”
akasema rais na kunyamaza kidogo
halafu akasema
“ Nimebadilisha walinzi wa rais na kwa sasa ninalindwa na makomando wa jeshi.Kwa hiyo usisumbuke tena kuunda kile kikosi tulichokuwa tumekubaliana ukiunde.Ulinzi huu nilionao sasa ni wa uhakika mkubwa .Kwa sasa kilichopo mbele yetu ni kuendeleza mapambano” akasema rais
“ Oh !hilo ni jambo zuri umefanya mheshimiwa rais.Hata hivyo bado sikuwa nimekiandaa kikosi kile tulichokuwa tumeafikiana nikiunde.Limekuwa ni jambo zuri umenipunguzia kazi.” Akasema Austin
“ Vipi maendeleo yako ? akauliza rais
“ Ninaendelea vizuri .Ni maumivu
tu makali ndiyo yanayonisumbua lakini hilo ni jambo la kawaida tumekwishalizoea.Ninatumia dawa za kunisiadia
kuondoa maumivu ndiyo maana unaona ninaweza hata kutembea namna hii bila shida” akasema Austin.Ernest akamtazama na kusema
“ Austin you are amazing.Nikikutazama nashindwa niseme nini.Ni jana tu usiku risasi nne zimetolewa mwilini mwako lakini leo hii unaweza hata kutembea.You are so strong.Taifa linawahitaji wapambanaji kama wewe” akasema rais.
Austin akatabasamu na bila kusema chohote akamkaribisha rais sofani
“Maandalizi yanakwendaje?
Monica amekwisha fika” akauliza rais
“ Hapana bado hajafika.Amarachi amekwenda kumchukua”
“ Good.Vipi kuhusu Yule binti
aliyekujeruhi tayari mmemuhoji na kumfahamu ni nani? Boazi je kuna
lolote mmelipata toka kwake?
“ Hapana mheshimiwa rais,bado hatujawahoji ila usiku wa leo tutakapotoka hapa tutalifanya hilo zoezi.Tulichofanikiwa kukipata ni kitabu ambacho Boaz amekuwa anakitafuta kwa gharama kubwa na ndiye sababu ya kutaka kumuua Marcelo kwani pekee ndiye aliyekuwa anafahamu mahala kilipo kitabu
hicho.Dr Marcelo aliachiwa kitabu hicho
na baba yake ambaye naye alikuwa katika mtandao wa dawa za kulevya.Kitabu hicho kina orodha ya wafanya biashara wote wa dawa za kulevya walio chini ya Alberto.Tutakipitia kitabu hicho kwa
makini na tutakupatia orodha hiyo kwa ajili ya kuifanyia kazi.”
“ Hiyo ni hatua kubwa sana
mmeipiga Austin.kama tayari mmekipata kitabu chenye orodha hiyo kazi yetu itakuwa rahisi sana.Hakuna kati yao atakayesalimika.Wote watakutana na mkono wa sheria.Hii ni vita Austin kwa hiyo sintakuwa na mchezo na hawa jamaa hata kidogo.Nakuhakikishia nitawafyeka
wote na nchi hii itakuwa safi.” Akasema rais Ernest
“ Huo ndio hasa ujasiri unaotakiwa
kwa rais.Watu hawa wameiharibu mno nchi hii na vijana wetu.Vipi kuhusu Mukasha?.Tutahitaji pia kuufahamu mtandao wake .Mmoja wa watu walio katika mtandao wa Mukasha anaitwa dogo Bill ndiye sababu ya Job kuishikama kichaa kwa muda wa zaidi
ya miaka mitatu.Huyu dogo Bill
alimchukua mke wa Job na mwanae na mpaka leo hii hawajulikani walipo.Muda
ukiwadia tutaomba utusaidia kumpata Mukasha ili aweze kutusaidia kufahamu alipo mtoto wa Job” akasema Austin
“ Kuhusu Mukasha kama nilivyokueleza nitashughulika naye na muda utakapofika mkihitaji kumuhoji nitawasaidia kumpata” akasema rais na kunyamaza baada ya kengele ya getini kulia .Rais akamtaka Austin apumzike akafungua mlango na kumtaka mmoja
wa walinzi wake akafungue
geti.Alikuwa ni Amarachi.Akahojiwa na kujieleza akaingiza gari ndani .Austin akatoka kwenda kuwalaki.Amarachi ndiye aliyekuwa wa kwanza kushuka akafuatiwa na Monica
“ Hallo handsome Zombie!! Akatania Monica huku akicheka .Austin naye akacheka na Monica akamfuata
“ Karibu sana Monica.Hapa ndipo
ninapoishi”akasema Austin
“ Ahsante sana Austin.Vipi maendeleo yako”
“ Naendelea vizuri kama unavyoniona”
“ Austin take me inside .I’m scared of how these soldiers are looking at me” Monica akamnong’oneza Austin ambaye
alitabasamu wakaelekea sebuleni
“ Hawa wanajeshi wote unaowaona hapa ni walinzi wa rais.Tayari amekwisha fika” Austin
akamwambia Monica na kuwakaribisha sebuleni yeye na Amarachi
“ Hello ladies.Welcome” akasema
rais akiwa katika tabasamu
.Monica na Amarachi wakamsalimu kwa adabu.Amarachi akawaacha na
kwenda kusimamia maandalizi ya
chakula
“ karibu sana Monica .Nimefurahi kuonana nawe tena” akasema rais
“ Hata mimi nimefurahi sana mheshimiwa rais kupata fursa hii ya kuonana nawe” akajibu Monica kwa sauti yenye woga ndani yake
Waliendelea na maongezi mbali mbali hadi pale Amarachi alipowataarifu kuwa chakula kiko tayari.Wote wakaenda kujumuika mezani .Baada ya kula wahudumu
wakafanya usafi na kuondoka .Ndani ya nyumba wakabaki rais,Austin ,Amarachi na Monica
“Monica uluomba nafasi ya kuonana na rais .Uwanja ni wako sasa unaweza ukamueleza rais shida yako” akasema Austin huku akiinuka
“ Ahsnate sana Austin.Mungu
akubariki ” akajibu Monica na Austin akatoka pale sebuleni akaelekea katika chumba kingine na kuwaacha Monica na rais peke yao
“ karibu Monica .Austin alinieleza kuhusu ombi lako la kutaka kuonana nami na kwa kuwa alinisisitiza sana ikanilazimu kusitisha baadhi ya
shughuli zangu nyingine na kuja kukusikiliza.Kuwa huru kunieleza chochote unachotaka kunieleza” akasema rais
“ Ahsante sana mheshimwia rais
kwa kunipa heshima hii kubwa na sipati neno zuri la kukushukuru toka ndani ya moyo wangu nasema ahsante sana” akasema Monica
Ernest akatabasamu .Monica akaendelea
“ Mheshimiwa rais nina shinda
ambayo nataka unisadie kwani iko ndani ya uwezo wako.Ninaye rafiki yangu anaitwa Marcelo ambaye alipigwa risasi na watu wasiojulikana lakini kwa maajabu ya Mungu alipona na anaendelea vizuri.Akiwa hospitali aligundua kwamba kuna watu bado wanaendelea kumfuatilia wamuue na
akaniomba msaada wa kumtorosha pale hospitali bila ya mtu yeyote kufahamu.Sikujua ningemsaidia vipi
.Wakati nikitafuta namna ya kumsaidia nilipata safari ya ghafla ya kwenda Congo na nikiwa huko nikalazimka kumuomba msaada rais wa Congo
David Zumo ambaye alikupigia simu akakuomba umsaidie Marcelo.Nashukuru ulimsikia na kumsaidia Marcelo.Baada ya kurejea toka Congo nilihitaji sana kuonana na
Marcelo lakini kila nikimuomba David
awasiliane nawe akuulize mahala alipo Marcelo nimekuwa Napata majibu ya kusubiri.Leo asubuhi nilipofahamu
kuwa una ukaribu na Austin na vile vile wazazi wangu nilifurahi na ndiyo maana nikamuomba Austin anikutanishe nawe
ili niweze kukuomba mimi mwenyewe
unionyeshe mahali alipo Marcelo nikamtazame.Ni mtu wangu wa
muhimu sana” akasema Monica.Ernest akatabasamu na kusema
“ Nilijiuliza maswali mengi David aliponipigia simu kuniomba nimsaidie kumtoa Marcelo hospitali.Sikujua kama lilikuwa ni ombi lako”akasema Ernest huku akitabasamu
“ Ni mimi ndiye niliyemuomba anisaidie” akasema Monica.
“ Samahani kwa Swali hili Monica
wewe na David Zumo mmefahamiana vipi?
“ Mimi na David Zumo ni wachumba na tuko katika maandalizi
ya kufunga ndoa.”akajibu Monica huku akitabasamu.Jibu lile la Monica lilimstua sana Ernest lakini akajitahidi
kutabasamu
“ Hongera sana .Kumbe maandalizi yamekwisha anza.Mbona mimi sijapewa taarifa wakati ni mtu wa karibu na
familia yenu? Nitazungumza na wazazi wako wanieleze kwa nini wananitenga katika jambo kubwa kama hili ”
akasema Ernest huku akitabasamu
“ Bado tuko katika taratibu za awali za uchumba na utakapofika
wakati wa kujulishwa nyote mtafahamu
“ akasema Monica
“ Naweza kusema una bahati sana
Monica kwa kumpata Dav………….” Kabla hajamaliza sentensi yake
Amarachi akaingia akiwa na sinia lenye
glasi mbili za mvinyo .Akampatia moja
Amarachi na nyingine akampa rais.
“ Karibuni vinywaji”akasema huku akitabasamu na kutoka
“ Monica naomba tugonganishe glasi na tunywe kwa ajili ya kukutakia maisha mema na mafanikio katika mambo yako yote.” Akasema Ernest wakagonganisha glasi na kila mmoja akanywa funda kubwa
“ Monica nimelipokea ombi lako na nitakusaidia .Dr Marcelo amehifadhiwa sehemu salama.Utapelekwa kwenda kuonana naye na endapo kuna chochote ambacho ungependa nikusaidie usisite kunitaarifu.” Akasema Ernest
“ Ahs…..aahsante… ….ahsante sana
mheshimiwa rais” akajibu Monica ambaye tayari alianza kulemewa na usingizi mzito baada tu ya kunywa mvinyo ule
Baada ya dakika mbili akalala usingizi pale sofani.Amarachi na Austin wakaingia pale sebuleni wakiwa wamejianda tayari kabisa kwa zoezi la kuchukua sampuli
“ Mheshimiwa rais kila kitu kiko tayari sasa tunaweza kufanya zoezi letu
la kuchukua sampuli mbele yako”
akasema Austin
“ Austin una hakika hamjazidisha dawa za usingizi mlizomuwekea Monica
? Nimeshangaa muda umekuwa mfupi sana toka alipokunywa kinywaji na kupata usingizi wa ghafla”
“ Usihofu mheshimiwa rais kila
kitu kinakwenda sawa na hakuna tatizo.Baada ya kumaliza zoezi letu
tutamzindua” akasema Austin.Amarachi akaanza zoezi la kuchukua sampuli walizozihitaji
Walifanikiwa kuchukua sampuli kadhaa toka kwa Monica halafu wakachukua pia sampuli kama hizo toka kwa rais Ernest na zoezi likakamilika.Monica akachomwa sindano ya kumzindua
“ Mheshimiwa rais ahsante sana kwa ushirikiano wako katika zoezi hili
.Kinachofuata sasa ni kupeleka sampuli hizi maabara kwa ajili ya vipimo .Kama nilivyokufahamisha awali kwamba vipimo vitafanyika hapa hapa dar es salaam.kesho au kesho kutwa tutapata majibu” akasema Austin wakati wakimsubiri Monica azinduke
“ nashukuru sana Austin kwa
nnamna ulivyojitoa kuhakikisha jambo hili linafanikiwa.Licha ya misuko suko
yote lakini bado umesimama imara kuhakikisha hakuna kinachoharibika na kila kitu kinakwenda kama tulivyopanga.By the way kuna jambo ambalo sikuwa nimekujulisha bado” akasema rais akanyamaza na
kumtazama Austin kisha akaendelea
“Mdogo wako Linda kesho anaondoka kuelekea Canada.Tayari
kuna nyumba imepatikana kule kubwa na nzuri ,ataishi humo na atafunguliwa duka kubwa la kuuza bidhaa za kiutamaduni kutoka Afrika.Tayari
maelekezo yote nimekwisha mpa balozi wetu Canada ambaye ndiye atakayempokea na kuhakikisha kila kitu kinakwenda vizuri.Sikutaka kukueleza kuhusu suala hili sasa hivi lakini kwa namna unavyojituma katika kufanikisha kazi zangu nimeona nikueleze ili ufahamu kuwa hata mimi ninakujali pia
na ninayaheshimu makubaliano yetu.Kwa hiyo Austin kaa ukifanya kazi zako kwa amani ukifahamu kuwa
mdogo wako yuko katika mikono salama” akasema rais na tabasamu
kubwa likajengeka katika sura ya Austin
“ Ahsante mheshimiwa rais kwa hili ulilolifanya” akasema na wote wakageuka baada ya kusikia mguno toka kwa Monica aliyezinduka.Rais akamfuata
“ Monica ..Monica..” akaita rais Monica akajaribu kufumbua macho lakini yalikuwa mazito sana
“ Bado anahitaji muda kidogo wa
kupumzika” akasema Austin
“ Austin mimi nitamuacha Monica mikononi mwako hakikisha anafika nyumbani kwake salama.kama kuna lolote litatokea unijulishe mara moja”
akasema rais Ernest na kuagana na
Austin akaondoka
“ Good Job Amarachi.Wewe ni mtu mwenye vipaji vingi sana.Umenishanganza kwa namna ulivyoweza kuchukua zile sampuli toka kwa Monica kama wafanyavyo madaktari” akasema Austin na
Amarachi akatabasamu .Austin akaelekea sebuleni ambako tayari Monica alikwisha zinduka usingizini
“ Monica” akaita Austin
“ Austin sijui nini kimenitokea lakini nimejikuta nikipata usingizi wa ghafla sana baada ya kunywa kile kinywaji alichotuletea Amarachi.” Akasema Monica kwa uchovu
“ Pole sana Monica.Mvinyo ule aliowaletea Amarachi ni moja kati ya mvinyo mkali mno na anapenda
kutumia rais.Amarachi alikosea kukupa mvinyo bila kukuuliza
kwanza.Unajisikaje?
“ Nahisi mwili mzito na kila kiungo kinauma.Kuna chumba cha wageni hapa kwako nipumzike? Akauliza Monica
“ sawa Monica ngoja Amarachi akuandalie chumba ukapumzike” akasema Austin na kutoka akamuelekeza Amarachi akaandae chumba kwa ajili ya Monica.Chumba kilipokuwa tayari Monica akaenda kupumzika.
“ Sampuli zote zimekamiliika kwa hiyo kinachofuata ni kuziwasilisha maabara.Mimi nitabaki hapa na Monica kwani kwa hali hii hataweza kurejea nyumbani kwake.Wewe peleka sampuli hizi maabara na ukitoka huko uende nyumbani ukapumzike tutaonana asubuhi.” Akasema Austin
“ Hapana Austin siwezi kwenda
kupumzika nyumbani kwangu nikakuacha peke yako.Nikitoka
maabara nitarejea hapa.Unahitaji kuwa
na mtu karibu kwa hiyo nitarejea hapa na kama ni kupumzika nitapumzika hapa” akasema Amarachi wakaagana akaondoka kuelekea katika hospitali aliyokuwa ameipendekeza .
“ Imekuwa ni siku nzuri yenye mafanikio makubwa.Kila kitu tulichokipanga leo kimekwenda vyema.Ni wakati wa kupumzika sasa” akawaza Austin na kuelekea chumbani kujipumzisha.

********************

.
 
SEHEMU YA 2: SEASON 5
Evans aliwasili ikulu na moja
kwa moja akaenda kuonana na rais
“Evans hebu nieleze kilichotokea
hadi ukashindwa kuikamilisha kazi
niliyokutuma” akauliza rais
akionekana kujawa hasira
“Mheshimiwa rais utanisamehe
kwa kushindwa kuikamilisha ile kazi
uliyonituma.Mpango nilikuwa
nimeuandaa vizuri sana .Kuna watu
niliokuwa nimewaweka wakimfuatilia
Mukasha na uliponipa ruhusa ya
kumuondoa nilimfuata sehemu
alikokuwa amekwenda
usiku.Nilifanikiwa kuingia na
kujificha katika gari lake hadi
alipotoka hotelini na kuingia katika
gari na kuondoka.Lengo langu
lilikuwa ni kumpoteza kabisa yeye na
gari lake na tayari nilikwisha andaa
kivuko ili nikamzamishe majini yeye
na gari na hakuna ambaye angemuona
tena.Tatizo lilitokea pale nilipojitokeza
na kumuamuru atii kila
nitakachomuelekeza na akaanzisha
vurugu na kupambana nami ,hali
iliyosababisha gari liserereke na
kutaka kutumbukia
mtaroni.Nilifanikiwa kumdhibiti
lakini ghafla akatokea mtu na kuvunja
kioo cha gari nikapigwa ngumi nzito
nikatetereka kidogo na nilipogeuka
nikajikuta nikitazamana bastora na
yule mtu akaniamuru nishuke
niondoke zangu.Nikashuka na
kukimbia yeye akaondoka na
Mukasha.Kwa hiyo mheshimiwa rais
hivyo ndivyo ilivyotokea na
kusababisha nishidwe kummaliza
Mukasha” akasema Evans
“Oh my God !! akasema rais na
kumtazama Evans kwa hasira
“Ulibahatika kumuona huyo
jamaa aliyekuvamia na kuondoka na
Mukasha? Rais akauliza
“Ndiyo nilibahatika
kumuona..Ana nywele nyingi na
pembeni ya jicho lake la kulia kuna
kovu.”
“Jesu christ !! akasema rais kwa
mstuko
“Mukasha alikugundua?
Akauliza rais Evans akakaa kimya
“Nakuuliza Evans Mukasha
alikugundua?
“Ndiyo mzee alinifahamu.Yule
jamaa aliponidhibiti akamuamuru
Mukasha anivue kofia niliyoitumia
kufunika uso na nikatazamana na
Mukasha”
Sura ya rais ikabadilika na
kumtazama Evans kwa hasira
kali.Akachukua simu na kuzitafuta
namba fulani akapiga.Hakutaka
kuongea mbele ya Evans akaelekea
chumbani kwake
**********************
Kengele iliyoashiria kuna mtu
getini ilimuamsha Austin .Akatazama
saa ilionyesha ni saa kumi na mbili
kasoro dakika ishirini na tatu
“Tayari kumekucha.Usiku
umekuwa mfupi sana” akawaza
Austin akainuka na kuhisi maumivu
hasa ya kifua.Akajikaza na huku
akisaidiwa na fimbo akaenda getini na
kumkuta Amarachi ,wakasalimiana
akaingia ndani
“Samahani Austin sikuweza
kurejea jana usiku kama
nilivyokuahidi.Ilinilazimu kumfuata
daktari nyumbani kwake ili aanze
mara mohja kushughulikia zile
sampuli.Baada ya kutoka hospitali
nikapita nyumbani kuchukua baadhi
ya vitu vyangu vidogo vidogo vya
lazima .Vipi maendeleo yako?akauliza
Amarachi
“Pole sana Amarachi kwa
kukubebesha mzigo huu mzito”
akasema Austin
“Usijali Austin.Ninajisikia fahari
kuwepo katika timu hii yenye watu
walioyatoa maisha yao kwa ajili ya
nchi yao.Ninaipenda Tanzania kwani
imenihifadhi na kunifanya niyafurahie
maisha kwa hiyo yeyote yule mwenye
nia ovu na nchi hii ni adui yangu
mkubwa.” Akasema Amarachi na
wote wakatabasamu.
“Vipi maendeleo yako?
Amarachi akauliza
“Ninaendelea vizuri sana.Mwili
unapata nguvu kwa kasi ya
kushangaza.”
“Hizo ni habari nzuri sana .Vipi
Monica anaendeleaje?
“ Bado amelala.Anatakiwa
aamshwe aende nyumbani kwake
atupe nafasi ya kuendelea na mambo
mengine” akasema Austin na
Amarachi akaenda katika chumba
alimolala Monica akamuamsha
“Mhh !!kumepambazuka !!
akasema Monica kwa uchovu huku
akiinuka na kukaa kitandani akashika
kichwa.
“Mwili umechoka na macho
mazito mno.Natamani niendelee
kulala” akasema Monica
“Monica tayari ni asubuhi kwa
hiyo natakiwa kukurejesha nyumbani
kwako kuendelea na majukumu
mengine” akasema Amarachi
“You are right.How’s Austin?
“Austin anaendelea
vyema.Anazidi kuimarika” akasema
Amarachi
“Good” akasema Monica na
kuinuka akaenda kujitazama katika
kioo
“I look like a pig” akasema huku
akiziweka vizuri nywele zake
“Jana nilitokewa na kitu cha
ajabu sana na cha aibu.Kusinzia mbele
ya rais ni aibu kubwa” akasema
Monica
“ Mimi ndiye wa kulaumiwa
Monica kwa kukuletea mvinyo ule
bila ya kukuuliza kama ni mtumiaji
wa vilevi vikali.Mvinyo ule
anaoutumia rais ni mkali
mno.Samahani sana”
“Usijali Amarachi” akajibu
Monica
“Kabla sijaondoka nahitaji
kumuona Austin.Unaweza nipeleka
nikaonana naye? Akasema Monica
“Hakuna neno hata naye
atafurahi pia” akasema Amarachi
wakatoka na kuelekea katika chumba
alimolala Austin.Amarachi akagonga
mlango na sauti ya Austin ikaruhusu
waingie ndani.Sura ya Austin
ikaonyesha tabasamu baada ya
kuwaona Monica na Amarachi.
“Hallow Austin.Vipi maendeleo
yako? Monica akauliza
“Ninaendelea vizuri .Afya yangu
inaimarika kwa kasi ya ajabu.Vipi
wewe unaendeleaje?
“Uhhm ! Ninaendelea vyema
japokuwa mwili bado mzito sana na
ninahisi uchovu mwingi.Natamani
kutwa nzima ya leo nishinde
nimelala.Utanisamehe Austin kwa
kitendo cha aibu nilichokifanya jana
cha kujifanya mnywaji wa mvinyo
halafu nikajikuta nikiuchapa usingizi
mbele ya rais.It was so embarrasing.I
don’t know how it happened na sijui
rais atanichukuliaje lakini naomba
uniombee msamaha sana na mueleze
wazi kwamba mimi si mtumiaji wa
vileo vikali “ akasema Monica
“Usijali Monica.Rais ameelewa
kilichotokea jana.Hata yeye
mwenyewe alishangaa sana kusikia
kwamba tumekupatia mvinyo ule
anaokunywa yeye ambao ni mvinyo
mkali sana.Utatusamehe sana sisi kwa
kukupa mvinyo ule bila kukuuliza”
akasema Austin
“Usijali Austin yamekwisha pita”
“Thank you.Vipi maongezi yenu
yalikwenda vizuri? Austin akauliza
“ Ndiyo tuliongea na
tukaelewana lakini bado hatukuwa
tumemaliza maongezi ndipo
nilipopatwa na hali ile .Naomba
endapo utaonana na rais mkumbushe
kuhusu maongezi yetu na ataelewa
atakupa jibu kisha utanijulisha”
akasema Monica
“Nitafanya hivyo.Monica na
kushukuru sana kwa kututembelea na
ninaomba isiwe ni mara ya mwisho
kufika hapa.Nakukaribisha tena siku
nyingine kwa chakula na hata
maongezi na ninakuomba usiseme
hapana pale nitakapokualika”
akasema Austin na wote
wakatabasamu
“Usihofu Austin nitakaribia.Uwe
na siku njema na upone
haraka.Nitakupigia simu baadae kujua
maendeleo yako.Hakikisha
unaendelea kufuata maelekezo yote
uliyopewa na daktari” akasema
Monica wakaagana akaongozana na
Amarachi wakaondoka
“Nahisi mwili kama si wa
kwangu” akasema Monica wakiwa
garini akirejeshwa nyumbani
“Pole sana Monica”
“Usijali Amarachi.Mvinyo ule
lazima utakuwa ni mkali sana.Mimi
hutumia mvinyo lakini mwepesi sana
kuliko kile kigongo nilichokutana
nacho jana.Hapa nilipo mwili wote
unaniuma na ninahisi kama vile
nimechomwa sindano katika baadhi
ya sehemu.” Akasema Monica na kwa
mbali akasikia mlio wa simu yake
.Zilikuwa namba ngeni
kabisa.Akaipokea simu ile
“Hallow “ akasema
“Hallow Monica.Ni mimi David”
ikasema sauti ya upande wa pili
“Ouh David habari yako
mpenzi”
“Habari yako
Monica.Nimekupigia sana jana usiku
lakini hukupokea.Kuna tatizo lolote?
Akauliza David
“Hakuna tatizo lolote David.Jana
nilichoka sana nikaisahau simu
sebuleni katika chaji nikaenda
kulala.Nisamehe mpenzi wangu.Vipi
maendeleo ya huko?
“ Nilikupigia simu ili kukupa
taarifa za huku.Si taarifa nzuri.Pauline
ametutoka saa saba na dakika nane za
usiku akiwa katika chumba cha
upasuaji.Madaktari walijitahidi sana
kwa kadiri ya uwezo wao lakini
hayakuwa mapenzi ya Mungu apone”
Kikapita kimya na mara Monica
akasikika akilia kwa kwikwi
“Monica “ akaita David
“David taarifa hii imenistua
mno.Pole sana kwa tatizo hili
kubwa.Mungu akupe nguvu za
kuhimili kipindi hiki kigumu”
“Pole nawe Monica.Najua
umeumizwa pia na kifo hiki cha
Pauline”
“Nimeumizwa mno
.Nimemfahamu Pauline katika siku za
mwisho wa uhai wake.Alikuwa
mwanamke mwenye upendo wa ajabu
na sijui namna ya kumuelezea.Vipi
kuhusu shughuli za msiba?
“Bado hatujapanga chochote .Ila
nitakuwa na kikao na viongozi na
wana ukoo ili kupanga taratibu za
mazishi.Nitakutaarifu kila kitu
tutakachokiamua” akasema David
“David nimekosa neno la kusema
kwa namna nilivyoumizwa na taarifa
hizi.” Akasema Monica
“Monica pole sana.Kitu cha
muhimu kwa sasa ni kuendelea na ule
mchakato wetu .Ujumbe tayari
umekwisha fika Dar es salaam kama
nilivyokueleza jana na ninatumai
tayari mmekwisha fanya maandalizi
ya kuwapokea na kukutana nao
.Usiku wa leo baada ya kumaliza
kikao wataondoka kurejea
Kinshasa.Taratibu zitakapokamilika
za mazishi nitatuma ndege kuja
kuwachukua wewe na wazazi wako ili
mshiriki katika kumsindikiza Pauline
katika safari yake ya mwisho.”
Akasema David
“David Mungu akupe nguvu ya
kuhimili kipindi hiki kigumu.”
Akasema Monica wakaagana na
kukata simu.Monica akainama na
kulia kwa kwikwi
“Monica kuna tatizo? Nini
kimetokea? Nimesikia unazungumza
kuhusu msiba nani kafariki? Akauliza
Amarachi.Pauline akafuta machozi na
kusema
“Mke wa rais wa Kongo anaitwa
Pauline kafariki.Imeniumiza
sana.kweli vizuri havidumu”
“Pole Monica”
“Ahsante ” akajibu Monica
“Mambo yanazizi
kuniandama.Kila siku linaibuka jambo
jipya.Kwa kweli kifo hiki cha Pauline
kimenichoma sana .Hata hivyo hatuna
budi kumshukuru Mungu kwa kila
jambo yeye ndiye mwenye kutoa na
kutwaa.Nakumbuka nilivyokuwa
naonge na Pauline huku akionekana
ni mtu mwenye afya njema na hakuna
ambaye angehisi kuwa alikuwa katika
siku zake za mwisho.Mungu ampe
pumziko la milele” akawaza Monica

SEHEMU YA 3 : SEASON 5
Amarachi alirejea baada ya
kumfikisha Monica nyumbani kwake
“Monica amefika salama lakini
bado analalamika mwili mchovu sana
ila mpaka sasa bado hajagundua
chochote” Amarachi akamwambia
Austin
“ Good” akajibu Austin
“Kuna jambo lingine” akasema
Amarachi
“Jambo gani?
“ Tukiwa garini Monica alipewa
taarifa za msiba .Anasema mke wa
rais wa Kongo amefariki dunia”
“Mke wa rais wa Kongo? Monica
anahusiana nini na msiba huo?
“Hata mimi nilijiuliza lakini
inaonekana wana uhusiano kwani
nilisikia akilitaja jina la David na
inaonekana alikuwa anazungumza na
David Zumo.Halafu …” akasema
Amarachi na kusita
“Ah ! tuachane na mambo
hayo.Nini kinaendelea sasa? Akauliza
Amarachi
“Kwa sasa tunarejea kwa Job .Leo
tuna kazi nyingi za kufanya.Tunahitaji
kufahamu mambo mengi toka kwa
Maria na baba yake Boaz” akasema
Austin na kabla hawajatoka ikaingia
simu toka kwa rais Austin akaipokea
“Shikamoo mzee” akasema
“Marahaba Austin.Vipi
maendeleo yako? Akauliza Rais
“Ninaendelea vizuri sana mzee”
“Nafurahi kusikia hivyo.Vipi
Monica naye anaendeleaje?
Alifanikiwa kurejea kwake salama?
“Amerejea kwake asubuhi
hii.Alishindwa kurejea kwake jana
usiku alikuwa anahisi uchovu mwingi
hivyo akalala hapa na ameondoka
asubuhi hii.Hata hivyo anaendelea
vizuri.Kuhusu zile sampuli tayari
zimewasilishwa maabara na tayari
zimeanza kufanyiwa kazi na majibu
yatakapotoka tutakukabidhi.”
“Ahsante sana
Austin.Nawatakieni maendeleo
mazuri katika shughuli zenu
zote.Simu yangu iko wazi na endapo
kuna lolote unahitaji usisite
kunitaarifu mara moja”
“Nitafanya hivyo mzee” akajibu
Austin wakaagana rais akakata
simu.Austin na Amarachi
wakaondoka kurejea nyumbani kwa
Job
Iliwachukua zaidi ya saa moja
kufika nyumbani kwa Job kutokana na
uwingi wa magari barabarani asubuhi
hii.Hawakutaka kuwasumbua akina
Job hivyo Amarachi akashuka ili
kufungua geti lakini akastuka baada
ya kukuta geti halijafungwa
akalisukuma na kuingiza gari
ndani.Gari la Job halikuwepo mle
ndani.Mara akatokea Marcelo
“karibuni sana .Habari za toka
jana? Vipi maendeleo yako Austin?
Akauliza Marcelo huku akimsaidia
Austin kupanda ngazi kuelekea
sebuleni
“Naendelea vyema.Afya yangu
inaimarika kwa kasi kubwa.Habari za
hapa? Anaendeleaje Job na wageni
wetu?
“Habari za hapa nzuri ila Job
sijaonana naye toka nimeamka.Jana
usiku aliniambia anatoka kuna
sehemu anakwenda .Usiku nilisikia
milango ya gari ikibamizwa nikahisi
ni Job au ninyi mmemrejea
nikaendelea kulala.Nimeshangaa
asubuhi kukuta Job wala ninyi
hampo.” Akasema Marcelo.Austin na
Amarachi wakatazamana.Austin
akamtaka Amarachi aende
akawatazame akina Maria na Marcelo
akaanza kushughulikia majeraha ya
Austin
Wakati Marcelo akiendelea
kumuhudumia Austin,Amarachi
akashuka ngazi kwa kasi ya ajabu
akiwa ameshika kitu mkononi.
“Amarachi kuna tatizo lolote?
Akauliza Austin
“Kuna kitu kimetokea hapa
ndani jana usiku” akasema na
kukikunjua kitambaa alichokishika na
kuwaonyesha akina Austin sikio la
mtu.Wote wakabaki na mshangao
mkubwa
“Nini kimetokea hapa? Hili sikio
la nani? Maria na Boaz wote wazima?
Akauliza Austin
“Maria na Boaz wote wako
salama ila katika chumba cha Maria
kumetapakaa damu nyingi na humo
ndimo nimelitoa sikio hili.” Akajibu
amarachi
“Marcelo nini kimetokea hapa
ndani jana? Austin akamuuliza
Marcelo
“Austin sifahamu nini kimetokea
hapa jana kama nilivyokueleza
kwamba baada ya Job kuondoka na
mimi nikaenda kupumzika na sikujua
kilichoendelea” akajibu Marcelo
“Amarachi mpigie simu Job
tufahamu yuko wapi” akasema Austin
na bila kuchelewa Amarachi
akampigia simu Job.Simu ya Job ikaita
bila kupokelewa,akapiga tena na
safari hii ikakatika na haikupatikana
tena
“Somethinhg is wrong here”
akasema Austin na kumtazama
Amarachi
“Twendeni chumbani kwa
Maraia” akaamuru Austin na wote
wakaelekea katika chumba cha
Maria.Mara tu mlango ulipofunguliwa
Austin akakutana na harufu ya damu
“Nini kimetokea humu?
Akajiuliza na mara akakutanisha
macho na Maria wakatazamana.Maria
aliyekuwa amefungwa kitini
alionekana kudhoofu .Austin
akapandwa na hasira za ghafla
alipomuona Maria akajitahjidi
kujizuia.
“Marcelo nenda kaandae mlo wa
asubuhi niache mimi na Amarachi”
akasema Austin na Marcelo akatoka
mle chumbani.
“Amarachi mfungue Maria
ajisafishe kisha usafishe humu
chumbani hatuwezi kuhojiana kukiwa
katika hali hii” akasema Austin na
Amarachi akampa Austin bastora
yake kisha akamfungua Maria
akampeleka bafuni akamswafi na
kumrejesha chumbani .Akaenda
kuchukua baadhi ya nguo zake
akambadilisha Maria halafu akafanya
usafi ndani ya kile chumba kukawa
safi.
“Now we can talk” akasema
Austin lakini kabla hawajaanza
kuzungumza chochote Marcelo
akatokea akiwa na sinia lenye
chakula,Maria akafunguliwa mikono
akala mlo ule uliokuwa ni supu na
chapati tatu,alionekana kuwa na njaa
kwani alimaliza chakula chote ndani
ya muda mfupi.Amarachi akataka
kumfunga tena mikono Austin
akamzuia
“Let her relax” akasema Austin
na kuketi akamtazama Maria kisha
akasema
“Hello Maria”
Maria hakujibu kitu akainamisha
kichwa.Hakutaka kumtazama Austin
usoni
“Nafahamu unahitaji sana kujua
maendeleo yangu .Ninaendelea
vyema na hali yangu inazidi kuboreka
kila uchao.Mungu amenipigania na
kusudio lako la kutaka kunitoa uhai
limeshindikana.Nitaongea nawe
baadae kuhusu suala hilo lakini kwa
sasa nataka kufahamu kilichotokea
humu ndani jana usiku.”
Maria hakujibu kitu bado
aliendelea kuinamisha kichwa.
“Maria tafadhali naomba
unieleze ni kitu gani kimetokea humu
chumbani jana usiku? Austin akauliza
tena lakini bado Maria hakutaka
kujibu chochote
“Hutaki kujibu? Akauliza Austin
“Austin this girl is trying us”
akasema Amarachi
“Anataka kuongea kwa lazima”
Austin akamtazama Maria kisha
akamgeukia Amarachi
“Do it Amarachi.Make her talk”
akasema Austin na bila kupoteza hata
sekunde moja Amarachi akafungua
sanduku lenye vifaa mbalimbali
akachukua koleo ndogo mbili
akamfunga Maria mikono katika kile
kiti kisha akakibana kidole kimoja
kwa koleo na kuanza kubandua
kucha.Maria akapiga ukelele mkubwa
sana kwa maumivu makali
aliyoyapata.
“Can you talk now? Akauliza
Amarachi
“Yes !! Yes!!! Akasema Maria
.Amarachi akachukua kichupa fulani
chenye dawa akaimimina katika
kidole kile na kukifanya kiwe na ganzi
hivyo kupunguza maumivu
“Now tel us what happened in
here last night? Akauliza
Amarachi.Maria akavuta pumzi ndefu
na kusema
“Job alikuja humu usiku akiwa
na mzee mmoja akanitambulisha
kuwa ni msaidizi wa rais lakini
anajihusisha na mtandao wa dawa za
kulevya.Alimtaka mzee yule amtajie
majina ya watu anaoshirikiana nao
lakini yule mzee hakuwa tayari na
ndipo alipomkata sikio.Baada ya
kukatwa sikio Yule mzee alimueleza
mambo fulani ambayo sikuyasikia
kisha wakatoka humu na hawajareja
tena.”
“Mukasha!!! Akasema Austin
“Job alimchukua
Mukasha.Amempeleka wapi? Kwani
nini akafanya hivyo bila ya
kutushirikisha? Akauliza
Amarachi.Austin akafkiri kidogo na
kusema
“Maria nitarejea baadae bado
mimi na wewe tuna mengi ya
kuzungumza” akasema na kisha
wakatoka mle chumbani
“Kwa mara ya kwanza toka
nimefahamiana na Job
amenikasirisha.Kwa nini kafanya hivi
bila ya kutushirikisha?We’re working
together so why he did this to
us?akauliza Amarachi akionekana
kuwa na hasira
“Calm down Amarachi.Job
amekosea lakini tunatakiwa tuelekeze
nguvu kumtafuta mahala aliko”
akasema Austin
“I don’t like this.Tunakwenda
mbele na kurudi nyuma .Kwa sasa
itatulazmu kusimamisha baadhi ya
mipango mingine ili kumtafuta.This is
not good.Amef…………” Amarachi
akanyamz baadaya simu yake
kuita.Akastuka baada ya kuliona jina
la mpigaji alikuwa Job
“It’s him” akasema huku
akimuonyesha Austin kisha
akabonyeza kitufe cha kupokelea.
“Halow Job,where are you ??
akauliza Amarachi
“Hallow” ikasema sauti ya
upande wa pili na sura ya Amarachi
ikabadilika baada ya kugundua kuwa
sauti ile haikuwa ya Job.Akamtazama
Austin kisha akasema kwa sauti
ndogo.
“It’s not him”
“Hallow habari yako? Nani
mwenzangu? Akauliza Amarachi
“Naitwa Kinyogoli,nashughulika
na uvuvi.Mwenye namba hizi
unamfahamu?
“Ndiyo namfahamu.Uko naye
karibu nizungumze naye?
“Nisikilize vizuri shangazi.Huyu
jamaa tumemuokota alfajiri ya leo
hapa ufukweni baada ya kutoka
katika shughuli zetu za uvuvi
.Alikuwa na majeraha makubwa
.Tumejitahid kumpa huduma zetu za
kienyeji na tukamuhifadhi ili baadae
tumpeleke hospitali lakini tunaona
hali yake inazidi kubadilika.Bado
hajaamka mpaka sasa.Naomba uje
umchukue umkimbize hospitali.Hali
yake ni mbaya.” Akasema yule jamaa.
“Ahsante sana ndugu kwa taarifa
hiyo.Naomba unielekeze tafadhali
mahala ulipo ili nije hapo mara moja
kumchukua na kumkimbiza
hospitali.” Akasema Amarachi na yule
jamaa akamuelekeza mahala walipo
“Nenda huko mara
moja.Utaongozana na Marcelo.”
Akasema Austin.Amarachi akamfuata
Marcelo na kumtaka waondoke
haraka wamfuate Job.Kabla
hawajaondoka Austin akamtaka
Amarachi amlete Julieth pale sebuleni
anahitaji kuzungumza naye.
“Hallo Julieth.Vipi hali yako?
Akauliza Austin .Julieth akamtazama
na kusema
“Ninyi ni watu katili
sana.Mmeniweka katika chumba
kisicho na kitu chochote hata
godoro.Nimelala sakafuni tena bila
hata kupewa chakula.Kwa nini mna
roho mbaya kiasi hicho? Akauliza
Julieth kwa ukali
“Naitwa Austin” akasema Austin
“Sihitaji
kukufahamu.Ninachohitaji mimi ni
kutoka hapa”
“Not so fast Julieth.Uwezekano
wa kutoka hapa ni mdogo sana labda
kama utaonyesha ushirikiano kwetu
tunaweza kukuachia ukaenda zako
lakini kwa sasa sahau kabisa habari ya
kurejea nyumbani”
“Mnataka nini toka kwangu?
Jana mmeniuliza kuhusu Boaz
nikawaeleza kila kitu.Mnataka nini
kingine? Akauliza Julieth kwa
ukali.Austin akamtazama kwa
sekunde kadhaa na kusema
“Naitwa Austin January.Mimi ni
mtanzania ambaye kwa sasa ninaishi
nchini Afrika ya kusini .Kazi yangu ni
upelelezi.Nimekuja Tanzania hivi
karibuni kwa ajili ya kazi moja tu ya
kumuokoa mtu aliyekuwa katika
hatari ya kuuawa.Nilifanikiwa
kumuokoa mtu huyo ambaye ni kaka
yako Marcelo.Mimi ndiye nliyemtoa
hospitali na kumpeleka sehemu
salama.Marcelo is a good
person.Nilijiuliza sana sababu za yeye
kutakiwa kuuawa na nilipomuhoji
hata yeye hakuwa anafahamu kwa
nini anatafutwa auawe.Tukiwa katika
kutafuta sababu za yeye kutaka
kuuawa nikakutana na Boaz ambaye
ninaishi naye Afrika kusini na mimi
ndiye msimamizi wa miradi yake yote
na nina uhusiano wa kimapenzi na
mwanae anaitwa Maria kwahiyo Boaz
ninamuheshimu kama baba
yangu.Boaz alinitaka nimtafute
Marcelo hadi nimpate.Akanipa
maelezo kwamba kuna kitabu
ambacho Marcelo aliachiwa na baba
yake ambacho kina maelezo yote
kuhusiana na biashara za ubia kati
yake na baba yake Marcelo.Boaz alidai
kwamba Marcelo amekificha kitabu
hicho kwa lengo la kumiliki miradi
yote peke yake.Yote haya yalikuwa ni
uongo mtupu kumbe kitabu
alichokuwa anakitafuta ni kitabu
chenye orodha ya wafanya biashara
wa dawa za kulevya .Tayari tunacho
kitabu hicho na muda si m refu
wataanza kukamatwa mmoja baada
ya mwingine.Hakuna atakayebaki
salama katika hili na tayari tumeanza
na Boaz mwenyewe na hautamuona
tena katika maisha yako yaliyobaki”
akasema Austin na kumstua sana
Julieth
“Mmemuua” akauliza
“Hapana sisi si wauaji
hatujamuua bali hataonekana
tena.You and him its over” akasema
Austin na kumtazama Julieth kwa
muda na kusema
“Julieth wewe ni msichana
mrembo na nafsi yangu inaniambia
nisikuharibie maisha yako kama
tutakavyowafanya hawa wengine
akina Boaz.Nataka unieleze ni kitu
gani hasa kilichokufanya uungane na
Boaz na kumsaliti ndugu yako wa
damu? Boaz anakulipa kiasi gani hadi
utake kumuua ndugu yako? Ungepata
faida gani endapo Marcelo angeuawa?
Nijibu tafadhali na pengine unaweza
kunishawishi nikafikiria kukuachia”
akasema Austin .Macho ya Julieth
yakajaa machozi
“Kuwa huru Julieth.Nieleze
tafadhali.Nini hasa unakipata katika
mahusiano na yule mzee? Anakupa
pesa kiasi gani hadi ukafikia maamuzi
ya kutaka kumtoa roho ndugu yako?
Akauliza Austin Julieth akaendelea
kulia
“Julieth kulia hakutakusaidia
kitu.Tafadhali nijibu maswali yangu”
akasema Austin.Julieth akafuta
machozi akamtazama Austin na
kusema
“Machozi yamenitoka kutokana
na haya maswali uliyoniuliza.Nafsi
yangu imeumia sana hasa
nikikumbuka mambo maovu
niliyoyafanya” akanyamaza akafuta
machozi na kuendelea
“Boaz hakunitafuta bali mimi
ndiye niliyemtafuta” akafuta tena
,machozi na kuendelea
“Mimi na Marcelo baba yetu ni
mmoja lakini mama tofauti.Baada ya
mama yake Marcelo kufariki dunia
baba yake akamuoa mama
yangu.Baba alimpenda mno Marcelo
na alimpatia kila kitu,elimu bora nje
ya nchi lakini mimi sikubahatika hata
kupanda ndege lichaya utajiri
mkubwa wa baba.Upendo huu
mkubwa kwa Marcelo ulianza kujenga
chuki kati yetu na tulianza kumchukia
Marcelo.Siku moja mama alibahatika
kuusoma kwa siri wosia aliouandika
baba na katika wosia huo karibu mali
zote zilikuwa za Marcelo.Nilimuuliza
mama kwa nini baba afanye vile ndipo
akanieleza siri ambayo sikuwa
nikiifahamu hapo kabla.Aliniambia
kwamba yule hakuwa baba yangu bali
mimi ninaye baba yangu.Baada ya
kumzaa Marcelo Dr Richard hakuwa
tena na uwezo wa kuzaa hivyo
ikalamzimu mama kutoka nje ya ndoa
kutafuta mtoto na kitendo hicho
kilimchukiza mno baba na ndiyo
sababu ya kumpendelea zaidi Marcelo
kuliko mimi.Baada ya kuufahamu
ukweli huo ndipo na mimi nilipoamua
kuingia rasmi katika utafutaji wa pesa
ili niwe na maisha mazuri .Boaz
alikuwa ni rafiki yake baba na alikuwa
akija nyumbani mara kwa mara hivyo
nikaanza kujiweka karibu naye na
hapo ndipo uhusiano wetu
ulipoanza.Nilianza kujifundisha
biashara ya dawa za kulevya .Nilianza
kwa kubeba na kufikisha mzigo
mahala nilikoagizwa na kisha kulipwa
fedha nyingi.Nilivutiwa na biashara
hiyo kwani kwa muda mfupi nilianza
kuwa na mafanikio na nikaamua hiyo
iwe ndiyo kazi yangu ya
kudumu.Hivyo ndivyo nilivyokutana
na Boaz na tukawa na mahusiano hadi
hii leo.Nilikubaliana na mpango wa
Boaz wa kumuua Marcelo kwa lengo
la kurithi mali kwani Marcelo hadi leo
hii bado hajausoma wosia alioachiwa
na baba yake na bado hafahamu kama
mimi na yeye si ndugu wa
damu.Maswali yako yamenichoma
moyo sana na kuamia kukueleza
ukweli wote.Sijawahi kumweleza mtu
yeyote mambo haya niliyokueleza”
akasema Julieth na kufuta machozi
“Kwa nini ukafanya maamuzi
haya Julieth.Huoni kwamba
umeyaharibu maisha yako mwenyewe
kwa kujiingiza katika biashara ya
dawa za kulevya?Boaz
alikundanganya sana .He was just
using you.Amekutumia kujinufasha
yeye mwenyewe.Unadhani Marcelo
angefariki ungezipata mali
zake?Umejidanganya sana Julieth”
“I’m sorry Austin.Please help
me.Ni wivu tu na tamaa ya mali
vimeniponza” akasema
Julieth.Marcelo akamtazama kwa
zaidi ya dakika tatu na kusema
“Nilijawa na hasira nawe sana
baada ya kufahamu kuwa wewe ni
chanzo cha mahangaiko ya Marcelo
.Amenusurika kuuawa kwa risasi na
chanzo ni wewe.Ukweli huu
ulionieleza pamoja na kukiri kosa lako
ninatamani nikusaidie.Bado ni
msichana mdogo na mrembo pia na
unaweza ukabadilikana ukaachana na
biashara hizi haramu ukafanya
biashara za halali.Nikikutazama
naiona picha ya mdogo wangu
anaitwa Linda ambaye ni makamu
yako na yeye alikuwa amefungwa
nchini China kwa sababu ya biashara
hiyo ya dawa za kulevya.Nimefanya
juhudi na kufanikiwa kumtoa na sasa
ninamtengenezea maisha
mapya.Sitaki ajihusishe tena na
biashara hii haramu.Natamani sana na
wewe nikusaidie kama mdogo
wangu”
“Mdogo wako anaitwa Linda
nani? Akauliza Julieth
“Linda January”
“Linda January ni mdogo wako?
“Ndiyo.Unamfahamu?
“Linda aliwahi kuwa na
mahusiano na Boaz.Huyu mzee ndiye
sababu ya Linda kufungwa.Ana
kawaida ya kutafuta wasichana
wadogo akajenga mahusiano nao
akawadanganya kwa pesa na vitu
vizuri na mwishowe huwaingiza
katika bisahara ya dawa za
kulevya.Linda ni mmoja wa
waathirika wa mchezo huo.Wasichana
wengi wamepotea kwa sababu ya
huyu mzee” akasema Julieth na sura
ya Austin ikabadilika
“Haya unayonieleza ni ya kweli
Julieth?
“Kweli kabisa.Kukamatwa kwa
Linda ulikuwa ni mpango wa Boaz na
aliwahi kunieleza kwamba anataka
msichana yule aozee gerezani na
hivyo akasuka mpango ili Linda
akamatwe” maneno yake ya Julieth
yakazidi kumpandisha hasira Austin
“ Austin” akaita Julieth
“Toka jana nilipoletwa hapa
nimejiuliza maswali mengi ni vipi
iwapo ningekamatwa na polisi ?
Nimetafakari sana kuhusu biashara hii
niifanyayo na maisha yangu kwa
ujumla.Nimeamua kubadilika na
kuachana na maisha haya ninayoishi
.Niko tayari kuwaeleza kila kitu
kuhusu Boaz na hata kama mkitaka
naweza kuwapeleka sehemu ambako
Boaz na wenzake huwa wanajificha na
huko ndiko huwa wanaficha mizigo
yao ya dawa za
kulevya.Nitawaonyesha kila kitu
lakini kwa sharti moja tu mniachie
huru na mnihakikishie
ulinzi.Nakuomba sana Austin nisaidie
kama mdogo wako.Usiniache
nikapotea tafadhali.” Akaomba
Julieth.Bado sura ya Austin ilikuwa na
hasira
“Nitaangalia namna ya
kukusaidia lakini ni lazima umueleze
ukweli wote Marcelo na yeye ndiye
atakayeamua kukusamehe au
vipi.Hata hivyo naahidi kukusaidia
kwani umenisaidia sana kufahamu
kuhusu mdogo wangu Linda.Sikujua
kama mtu niliyemuheshimu kama
baba yangu ndiye aliyemtenda hivi
mdogo wangu.Boaz ameniumiza
sana” akasema Austin na kumpeleka
Julieth jikoni akachukua chakula na
kumrejesha katika chumba
alimofungwa.
“Alichokisema Julieth kimenistua
sana.Kumbe ni Boaz ndiye
aliyeyaharibu maisha ya Linda.Kwa
nini lakini? How could he do that to
me? Mambo haya yote niliyomfanyia
hii ndiyo shukrani yake? Ameniumiza
mno.Bahati yake ninaumwa lakini
ningekuwa mzima angenena lugha
kumi na mbili leo.Ningemtesa mno
leo.Hata hivyo nitamkabidhi
Amarachi kazi hiyo amfundishe
adabu.Huu ni mwisho wa enzi zake
za kuishi kama malaika na sasa
anaanza kuishi kama
shetani.Nitahakikisha anaujutia ubaya
wake wote alioutenda.Ameharibu
maisha ya wasichana wengi.Yeye na
mwanae lazima wajute kunifahamu”
akawaza Austine akiwa na hasira
zisizomithilika.
SEHEMU YA 4 :SEASON 5
Amarachi ambaye siku zote ni
mwanamke jasiri alishindwa kuzuia
machozi kumtoka kwa hali
aliyomkuta nayo Job.Alikuwa
amelazwa katika mtumbwi kuu kuu
na hakuwa na fahamu huku akiwa na
majeraha kichwani na mwilini.Hali
yake ilikuwa mbaya.
“Who did this to you Job?
Akasema Amarachi huku akilia.
“Nyamaza kulia Amarachi.We
have to help him !!! akasema Marcelo
na kumpima Job
“He’s still breathing !! akasema
Marcelo na kumchoma Job sindano
“Tunatakiwa kumpeleka
hospitali haraka” akasema Marcelo
.Wavuvi wakambeba Job hadi katika
gari la Amarachi kisha Amarachi
akawapa shilingi laki mbili
akawashukuru kwa msaada mkubwa
walioufanya
“Tunampeleka hospitali ipi?
Akauliza Amarachi
“Tumpeleke katika hospitali
yangu.Tukimpeleka katika hospitali
nyingine watahitaji taarifa ya polisi”
akasema Marcelo na kumuelekeza
Amarachi iliko hospitali yake
“Kwa nini Job aliamua kufanya
kazi peke yake bila kutushirikisha
hadi yakamkuta haya? Angeweza hata
kuuawa.Please Lord save this
man.He’s very important to me”
akasema Amarachi kwa sauti ndogo
Waliwasili katika hospitali ya
familia ya Marcelo ambayo ni maalum
kwa ajili ya kutibu wagonjwa wa
maradhi ya saratani.Kwa takribani
dakika tatu Dr Marcelo alizungukwa
na madaktari na wauguzi wa hospitali
ile wakimkumbatia na kumpa pole
huku wengine wakilia.Hawakuamini
kumuona tena Marcelo pale
hospitali.Marcelo akawafahamisha
kwamba amekuja na mgonjwa katika
gari ambaye ana hali mbaya.Haraka
haraka Job akashushwa garini na
kukimbizwa katika chumba cha
wagonjwa mahututi akaanza
kushughulikiwa
“Amarachi tafadhali usihofu.Job
atapata huduma nzuri kwani hapa
kuna madaktari wazuri sana.”Marcelo
akamwambia Amarachi aliyekuwa
amekaa nje ya chumba alimoingizwa
Job
“Marcelo siwezi kuacha kuwa na
hofu.Job ni mtu wangu wa muhimu
mno.Toka tumefahamiana hii ni mara
ya kwanza amenifanya niumie.Kwa
nini afanye hivi? Kwa nini afanye kazi
kimya kimya bila kutushirikisha
wenzake” akauliza kwa hasira
Amarachi
“Punguza hasira
“Relax Amarachi.Job will be
fine.Endelea kupumzika hapa mimi
nakwenda kuungana na madaktari
kumuhudumia Job” akasema Marcelo
na kuingia ndani ya chumba cha
wagonjwa mahututi
“Nafahamu Job ana hasira nyingi
dhidi ya wale waliomtenda ubaya na
kumsababisha aishi maisha magumu
kwa miaka kadhaa lakini hakutakiwa
kufanya jambo hili kwa haraka namna
hii.Watu hawa wanapaswa
kuwaendea kwa akili nyingi.They are
very smart and animals.Alinitaka
nijenge urafiki na dogo Bill ili niweze
kumchunguza lakini mpaka sasa
sijafanikiwa kugundua lolote kwani ni
watu waangalifu mno na wana mbinu
nyingi za kujificha.Amefanya kosa na
endapo akiamka nitamnasa vibao kwa
hili alilofanya” akawaza Amarachi na
kuchukua simu akampigia Austin
“Hallo Amarachi.Nipe taarifa za
huko? Mmefanikiwa kumuona
Job?akauliza Austin
“Tumefanikiwa kumpata .He’s in
bad shape.Ana majeraha makubwa
kichwani na mwilini.Mpaka sasa bado
hajapata fahamu na imetulazimu
kumleta katika hospitali ya Dr
Marcelo.Hivi sasa ameingizwa katika
chumba cha wagonjwa mahututi
madaktari wanajitahidi kuokoa
maisha yake.” Akasema Amarachi
“Thank God.Tumuombee kwa
Mungu aweze kupona kwani
tunamuhitaji sana.Kwa kuwa tayari
yuko katika uangalizi wa madaktari
muache Marcelo aendelee
kumshughulikia wewe rudi huku
kuna kazi za kufanya.” Akasema
Austin
“Vipi kuhusu Marcelo,are you
sure he’ll be safe here alone? Akauliza
Amarachi
“Marcelo is safe.Mtu aliyekuwa
anamtafuta ni Boaz ambaye tayari
tunamshughulikia kwa hiyo yuko
salama ingawa bado ataendelea kukaa
nasi hapa hadi hapo
tutakapohakikisha kwamba hakuna
tisho lolote la usalama kwake.”
Akasema Austin
“Sawa Austin ninakuja hapo
nyumbani muda si mrefu” akajibu
Amarachi na kukata simu.Sekunde
kadhaa baada ya kuongea na
Amarachi ikaingia simu toka kwa rais
“Shikamoo mzee” akasema
Austin
“Marhaba Austin .Unaendeleaje?
“Naendelea vizuri sana mzee.”
“Good to hear that.Wengine wote
wako salama? Akauliza rais
“Wako salama isipokuwa
Job.Amepatwa na tatizo na hali yake si
nzuri”
“Amepatwa na nini Job?
“Jana usiku tukiwa kule
nyumbani tulimuacha hapa na
akaondoka bila kututaarifu
amekwenda wapi na hajarejea hadi
asubuhi ya leo tulipopokea simu toka
kwa wavuvi waliotujulisha kwamba
Job ameokotwa ufukweni akiwa
hajitambui.Hivi sasa anatibiwa katika
hospitali ya Dr Marcelo.Tunasubri
apate nafuu ili atueleze kilichotokea”
“Pole sana .Pamoja na hayo yote
yanayoendelea kutokea nawasihi
msikate tamaa endeleeni kupambana
.Endapo kuna msaada wowote
mnaouhitaji toka kwangu msisite
kunijulisha mara moja.Vipi kuhusu
vipimo kuna taarifa zozote?
“Hapana mzee bado hakuna
taarifa zozote .Watakapokuwa tayari
tutajulishwa na tutakukabidhi wewe
majibu hayo.”
“Thank you Austin.Make sure
I’m the first one to see the results”
akasema rais wakaagana akakata
simu.
“Rais hajagusia chochote kuhusu
Mukasha ina maana hana taarifa
zozote za Mukasha kukatwa sikio? Au
mtu aliyemchukua Job hakuwa
Mukasha? Ngoja tusubiri Job
azinduke atueleze ukweli.” Akawaza
Austin
Alipomaliza kuzungumza na
Austin rais akazitafuta namba fulani
katika simu yake akapiga
“Hallo Mr Persident” ikasema
sauti ya upande wa pili
“You did a huge mistake last
night.You didn’t kill him.He’s alive”
“What ?! That’s not true Mr
president.Mimi mwenyewe
nilihakikisha amekata pumzi
nikawatuma vijana wakamtupe
.Nashangaa kusikia eti yuko hai
.That’s a miracle then”akasema mtu
yule aliyekuwa akiongea na rais
simuni
“He’s alive but in critical
condition.Nimetoka kuzungumza na
mwenzake muda si mrefu na
amenieleza kuwa Job yuko hai bado”
“ Kwa hiyo tufanye nini mzee?
“Kwa sasa msifanye chochote
,tusubiri kwanza maendeleo ya hali
yake halafu tutajua nini cha kufanya
lakini safari nyingine ukipewa kazi
jitahidi kuifanya kwa ukamilifu
wake.Watu kama hawa si wa kufanyia
mchezo hata kidogo.They have more
lives than a cat” akasema rais
“Sawa mzee ninasubiri taarifa
toka kwako” akasema yule jamaa
“One more thing” akasema rais
“Tunatakiwa kumundoa
Mukasha haraka sana.Huyu ni mtu
hatari mno kwetu kwa sasa”
Kimya kikapita na yule mtu
aliyekuwa anaongea na rais akasema
“Mr President,Mukasha he’s one
of ours.”
“I know that, lakini kwa sasa ni
mtu hatari mno kwetu .Bado
hafahamu kama mimi na wewe ni
washirika ingawa mimi nafahamu
mambo yake yote.Hawa vijana tayari
wameanza kumchunguza na
ninakuhakikishia vijana hawa ni
hatari mno na wakidhamiria jambo
lazima walifanikishe.Lengo lao ni
kumchimba Mukasha na kuufahamu
mtandao wake wote kwa hiyo lazima
tujihami mapema kwa kumuondoa
Mukasha.Tukimuondoa Mukasha na
tutamuondoa pia yule kijana kule
hospitali ndipo tutakapopumua kwani
yule ndiye aliyeelezwa mambo mengi
na Mukasha.We don’t have to wait for
the situation to get ugly,we have to
clear everythig now!! Akasema rais
“Nimekuelewa mzee.Toka jana
usiku Mukasha alipelekwa hospitali
kutibiwa jeraha na kwa taarifa
nilizonazo alikuwa amelazwa.Niachie
suala hili nilishughulikie haraka
iwezekanavyo”
“Thank you.Nitawasiliana nawe
baadae kukupa taarifa nitakazokuwa
nimezipata” akasema rais na kukata
simu
SEHEMU YA 5; SEASON 5
Amarachi ashuka garini akaingia
sebuleni akakutana na Austin.Sura
yake ikaonyesha wazi alikuwa
mawazo mengi.
“Habari za hapa? Akauliza
Amarachi
“Habari za hapa nzuri .Vipi huko
utokako? Kuna taarifa zozote za
maendeleo ya Job?
“Mpaka naondoka hakukuwa na
taarifa zozote bado madaktari
wanaendelea kumtibu.Why Job did
that? Akauliza Amarachi na machozi
yakamtoka,Austin akainuka na
kumfuata sofani akamshika bega
“Nitazame usoni Amarachi”
akasema Austin.Amarachi akafuta
machozi na kumtazama Austin
“Nafahamu umeumizwa kuhusu
Job hata mimi nimeumizwa pia lakini
hatufahamu bado kwa nini aliamua
kufanya vile alivyofanya bila
kutushirikisha? .Nafahamu lengo lake
kubwa ni kumpata mwanae Millen na
nimekwishamuadi kuwa lazima
tutampata mwanae sasa sijui nini
kilitokea akafanya vile
alivyofanya.Hata hivyo tunapaswa
kumuombea ili apone na kutueleza
nini hasa kilichotokea.Kuna mengi
anayotakiwa kutujibu.Usiwaze sana
he’s in good hands and he’ll wake
up.Kitu kikubwa unachopaswa
kukitambua ni kwamba tuko katika
mapambano na na kuumia kwa
mmoja wetu hakuwezi kuturudisha
nyuma.Lazima tuliobaki tuendeleze
mapambano kwa niaba
yake.Tulikuwa watatu na sasa
tumebaki wawili kwa hiyo lazima
tuifanye kazi ya watu
watatu.Amarachi I need you more that
ever.I need you to focus.Maumivu
yote tunayoyapata kwa kilichomtokea
Job tuyaelekeze katika kuikamilisha
kazi iliyoko mbele yetu.Umenielewa
Amarachi ? akauliza Austin .Amarachi
akafuta machozi na kusema
“Nimekuelewa Austin.Lets do
this for Job”
“Good” akasema Austin na
ukimya mfupi ukapita
“Sina hakika kama nimekwisha
kueleza historia yangu” akasema
Austin
“Job alinieleza kwa ufupi sana”
akajibu Amarachi.Austin akamueleza
Amarachi historia yake hadi
alipokombolewa na Boaz toka katika
mikono ya Alshabaab
“Kwa hiyo Boaz ni mtu ambaye
binafsi namuheshimu sana kama baba
yangu.Kama ilivyo katika filamu
ambapo kuna mambo tusiyoyajua
yanafanyika nyuma ya pazia,hata
mimi na Boaz kuna mambo
yaliyokuwa yanaendelea nyuma ya
pazia ambayo sikuyafahamu”
akanyamaza kwa muda halafu
akaendelea
“baada ya Boaz kunikomboa toka
kwa Alshabaab alinipeleka kuishi
Afrika kusini na nikawa msimamizi
mkuu wa miradi yake yote.Nikiwa
Afrika kusini Boaz alianzisha
mahusiano na mdogo wangu Linda
na baadae akamuingiza katika
biashara ya dawa za
kulevya.Kukamatwa kwa Linda
nchini China ulikuwa ni mpango wa
Boaz.Amekuwa na tabia ya
kuwatumia wasichana wadogo katika
biashara zake za dawa za kulevya na
mdogo wangu Linda ni mmoja wa
waathirika .Jambo hili limeniumiza
sana.Huyu Boaz ni mnyama mno”
akasema Austin
“Umemuhoji akakiri ? akauliza
Amarachi
“Hapana sijamuhoji.Julieth ndiye
aliyenieleza kila kitu”
“Julieth? Akauliza Amarachi
“Ndiyo .Amenieleza kila kitu
kuhusu chanzo cha mahusiano yake
na Boaz na kwa nini anataka kumuua
Marcelo”
“Do you believe her?
“Yes I do .”akajibu Austin
“Kumbe yule baba ni shetani
mkubwa.Muonekano wake na
matendo yake haviendani kabisa”
“Ni mtu anayejitahidi sana
kuficha maovu yake lakini arobaini
yake imewadia na safari hii hataweza
kuchomoka katika kabali yangu.”
Akasema Austin
“Kile kitabu tulichokipata jana
umekipitia? Amarachi akauliza
“Hapana bado
sijakipitia.Tutakipitia baadae lakini
kwa sasa ni wakati wa kuzungumza
na Boaz.” Akasema Austin na
kuongozana na Amarachi kuelekea
katika chumba alimofungwa
Boaz.Chumba kilikuwa giza ,taa
ikawashwa na Boaz aliyekuwa
amelala akaamka.Alistuka mno
alipojikuta akitazamana na Austin
“ Austin ??.. Boaz akasema kwa
mstuko.Hakuamini alichokiona mbele
yake
“I cant believe this.Is that you my
son? Akauliza
“Hallow Boaz.Hii si ndoto bali ni
kitu cha kweli kabisa
unakishuhudia.Its me Austin”
akasema Austin akavuta kiti na kuketi
akamuamuru Amarachi amfungue
Boaz mikono akainuka na kukaa
akamtazama Austin na kutikisa
kichwa
“Bado siamini macho yangu
kama ni wewe kweli Austin ndiye
uliyenifanya hivi.Nimekukosa nini
Austin hadi umenifanyia hivi?Shetani
gani amekuingia na kukudanganya
unifanyie hivi kijana wangu?
Nilikutoa katika mikono ya Alshabaab
lakini haya ndiyo malipo yake?
akauliza Boaz
“Maswali yako hayatakusaidia
kitu Boaz,tayari umeingia katika
himaya yangu na huu ni mwisho wa
enzi zako za kuishi kama malaika na
sasa utaanza kuishi kama
shetani.Unapoingia katika himaya
yangu haijalishi ni ndugu yangu au
nini umenifanyia,unapata nafasi ya
kunifahamu vyema mimi ni nani
hasa.Katika himaya yangu I’m a
monster.” Akasema Austin .Uso wa
Boaz ulionekana kuloa jasho
“Are you trying to scare me? Are
you starting a war with me son?
Please don’t do that.You don’t know
me at all.baada ya kugundua kwamba
wewe ndiye uliye nyuma ya ujinga
huu nakuomba unifungue niende
zangu.Nakuambia hivi angali
mapema na endapo utanifungua
nitakusemehe lakini endapo
utaendeleza ujinga wako huu Iswear
you’ll pay for this!!! Akafoka
Boaz.Austin akatabasamu kidogo na
kusema
“Mr Boaz,nilikwambia toka awali
kwamba tayari umeingia katika
himaya yangu na huna uwezo wa
kuniamuru chochote.I’m the boss
here.Wakati wako umefika and I’ll
destroy you completely” akasema
Austin
“ Unataka kunifanya
nini,kuniua? Kwa wema wote huu
niliokutendea unataka kuniua? What
kind of a man are you? I gave you
good life,I gave you my daughter and
this is how you repay me?? Akafoka
Boaz.Austin akavua fulana aliyokuwa
amevaa
“Just the day before I was shot
four times.Risasi moja ilipita karibu
sana na moyo wangu na lengo la
aliyenipiga risasi hizo ni kuniua na
kwa bahati mbaya kwake na nzuri
kwangu mkono wake ulicheza kidogo
hivyo lengo lake
halikutimia.Hayakuwa mapenzi ya
Mungu niondoke duniani hadi pale
nitakapokuwa nimekamilisha zoezi la
kuifanyia usafi nchi hii yenye watu
wachafu kama wewe !! akasema
Austin huku akimtazama Boaz kwa
hasira
“Unafahamu nani aliyetaka
kunitoa uhai? Its yor daughter
Maria.You are the family of monsters
!!
Boaz akaonyesha mshangao
mkubwa
“Maria ndiye aliyekupiga risasi”
akauliza
“Ndiyo .Binti yako mpendwa
ndiye aliyetaka kuniua”
“I cant believe you.Maria katu
hawezi kufanya kitu kama hicho.Si
Maria huyu ninayemfahamu mimi”
akasema Boaz
“Tuachane na hayo ya Maria
nataka unieleze kwa nini uliyaharibu
maisha ya Linda?
“Linda? I don’t know any Linda”
akasema Boaz
“Linda mdogo wangu.Wakati
ukifahamu kabisa kwamba sina
mpango wa kurejea Tanzania
ukamrubuhi ,ukamchezea utakavyo
na haikutosha hadi ukamuingiza
katika biashara ya dawa za kulevya na
mwisho ukasuka mpango
akakamatwa nchini China na dawa za
kulevya akafungwa gerezani.Kwa nini
ukamfanyia hivi yule binti ambaye ni
sawa na mwanao? Kwa nini umekuwa
na roho ya kikatili kiasi hicho?
Akauliza Austin
“Austin I don’t know any
Linda.Simfahamu msichana yeyote
anayeitwa Linda.Nakumbuka uliwahi
kuniambia kwamba unaye mdogo
wako simkumbuki jina na ukaniambia
nijapo Tanzania niwe napita
kumtazama na kumsaidia kama ana
tatizo.Sikuwahi kuonana naye
nashangaa leo hii unanituhumu kwa
kumuharibia maisha yake.Huu ni
ukosefu mkubwa wa adabu
Austin.Najuta kwa nini nilipoteza
fedha zangu nyingi kukukomboa mtu
kama wewe usiye na shukrani hata
chembe.Sikujua kama ninafuga nyoka
ambaye sasa umegeuka na kuniuma
mwenyewe” akasema Boaz
“Tayari nafahamu kila kitu Boaz
ila ninachotaka ni wewe ukiri kwa
mdomo wako kitu ulichokifanya
lakini kwa kuwa unaonekana mjeuri
unanilazimisha nikufumbue mdomo
kwa lazima” akasema Austin na
kumtaka Amarachi amfunge Boaz
mikono
“He’s all yours.Make him talk”
akasema Austin na kutoka mle
chumbani.Hakutaka kuona namna
Amarachi anavyoshughulikia Boaz
“Austin what’s the meaning of
this?? Akapiga ukelele Boaz lakini
Austin hakugeuka akaelekea
sebuleni.Muda mfupi tu baada ya
Austin kutoka mle chumbani
ukasikika ukelele mkubwa sana.Boaz
alikuwa analia kama mtoto mdogo.
SEHEMU YA 6; SEASON 5
Silvanus Herman Kiwembe
mkuu wa idara ya usalama wa taifa
aliwasili ikulu kwa mwito wa
rais.Sura yake ilionyesha wasi wasi
mwingi kwani hakujua ni kitu gani
alichoitiwa na rais.Alishuka garini na
kuelekea moja kwa moja ofisini kwa
rais
“Mr kiwembe ,karibu sana” Rais
akamkaribisha
“Nashukuru sana mheshimiwa
rais.habari za siku mbili tatu?
“Nashukuru naendelea
vizuri.Mikiki mikiki ya hapa na pale
lakini naendelea vyema.”
“Nashukuru kusikia hivyo
.Nimeitika wito wako mheshimiwa
rais” akasema Silvanus au Silva kama
alivyozoeleka.
“Ahsante kwa kufika kwa wakati
Silva.Kuna jambo mimi na wewe
nataka tulizungumze lakini si
hapa.Tutatoka kidogo kuna mahala
tutakwenda.Mwambie dereva wako
aondoke kwani tutakuwa na siku
ndefu kidogo” akasema rais na sura
ya Silva ikabadilika na kuonyesha
wasi wasi mwingi,akachukua simu
akampigia dereva wake na kumtaka
aondoke.
Silva akaongozana na rais
wakaelekea katika helkopta wakaingia
na helkopta ikaondoka bila ya Silva
kujua walikokuwa wanaelekea.Safari
ilikuwa ya kimya kimya .Waliruka juu
ya anga la Dar es salaam kuelekea nje
kabisa ya jiji na taratibu helkopta
ikatua katika eneo lenye majengo
mfano wa kiwanda
kilichotelekezwa.Helkopta ikagusa
ardhi na mlango
ukafunguliwa.Kulikuwa na watu
wanne waliovalia suti nyeusi
waliokuwa wamesimama karibu
kabisa na mahala helkopta
ilikotua,wakaisogelea helkopta , rais
akashuka akiwa ameongozana na
Silva pamoja na makomando wanne
wanaomlinda .
“This way Mr president”
akasema mmoja wa wale jamaa
“Is everything set? Akauliza rais
“Yes Mr president” akajibu yule
jamaa
Rais na wote aliokuwa
ameongozana nao wakaingia ndani ya
mojawapo ya jengo ambalo lilikuwa
tupu.Rais akawaambia wale walinzi
wake wamsubiri pale ila Silva
akamtaka aongozane naye pamoja na
wale jamaa wenye suti.Walitembea
kimya kimya wakashuka ngazi na
kufika katika mlango wa chumba
fulani mmoja wa wale jamaa
akaufungua na rais akaingia Silva
naye akafuata.Ndani kile chumba
kulikuwa na sofa nzuri na meza
ilionekana ni kama ofisi.Silva
akaelekezwa sehemu ya kukaa na
kisha akaamriwa avue
shati.Akamtazama rais kwa mshangao
“Mr President what’s the
meaning of this? Akauliza
“Just do it Silva” akajibu rais
Silva akavua shati na wale jamaa
wakamkagua endapo kuna kifaa
chochote amekivaa kinachoweza
kuwa kinarekodi maongezi,kisha
akaruhusiwa avae shati
“Thank you gentlemen I’ll take it
from here” Rais akawaeleza wale
jamaa wenye suti nyeusi wakatoka.
“What is this place Mr President?
Why am I here? Akauliza Silva.Rais
akamtazama kwa muda na kusema
“Silva nimekuleta hapa kwa ajili
ya maongezi nyeti na ya muhimu
sana.kabla sijakueleza nilichokuitia
hapa nataka nikufahamishe kwamba
wewe ni mmoja wa Alberto’s walio
katika nafasi za juu ambaye mpaka
sasa sijakuondoa katika nafasi
yako.Nimefanya hivi kwa sababu
maalum kwani naamini mimi na
wewe bado kuna mambo tunayoweza
kufanya kwa pamoja licha ya tofauti
zangu na Alberto’s”
“Nashukuru kusikia hivyo
mheshimiwa rais lakini ningependa
kufahamu kuna tatizo gani limetokea
hadi ukaamua kutofautiana na
Alberto’s” akauliza Silva
“Hayo ni mambo yangu binafsi
na siwezi kukueleza
chochote.Kikubwa nilichokuitia hapa
nataka kufahamu kuhusu mwanamke
mmoja anaitwa Yasmin Esfahani.”
Silva akastuka baada ya kusikia
jina lile likitajwa.
“Yasmin Esfahani? Akauliza
“Ndiyo.Nataka taarifa zake,ni
nani,yuko wapi na kwanini mpaka leo
hii sijapewa taarifa zake? Akauliza
rais.Silva akabaki kimya akimtazama
rais
“Nahitaji jibu Silva” akasema rais
“Mheshimiwa rais hilo ni jina
geni kabisa kwangu na nimelisikia
toka kwako leo hii .Sifahamu chochote
kuhusiana na huyo mwanamke.”
Uso wa rais Ernest ukaanza
kubadilika kwa jibu lile la Silva
“Sijabahatisha kuhusu jambo hili
Silva.Nafahamu mwanamama huyu
yuko hapa Tanzania amefungwa
mahala nataka kufahamu ni wapi na
kwa nini amefungwa na mwisho kwa
nini sijataarifiwa?
“Mheshimwa rais ,kama
nilivyokueleza kuwa ni mara yangu
ya kwanza kusikia jina hilo.Idara
yangu haina taarifa zozote za
kumuhusu huyo Yasmini.kama
tungekuwa na taarifa zake
tungekwisha zifikisha kwako .”
“Silva mimi na wewe ni marafiki
na ndiyo maana mpaka sasa
sijakugusa katika nafasi yako kwa
sababu naamini kuna mambo mengi
mimi na wewe tunaweza
kusaidiana.Naomba tafadhali unieleze
kuhusiana na huyu mama”
“Mheshimwa rais sina sababu ya
kukuficha jambo lolote.Sina taarifa
zozote kuhusiana na huyo
mtu.Yawezekana waliokupa taarifa
hizo hawakukupa taarifa sahihi”
“Are you sure you don’t know
anything about Yasmin Esfahani?
Akauliza rais
“Yes I am Mr president” akajibu
Silva.Rais akainuka akabonyeza kitufe
kidogo chini ya meza yake na mlango
ukafunguliwa wakaingia wale jamaa
wanne waliovaa suti nyeusi.
“Silva sisi ni watu wazima na
haipendezi kucheza michezo ya
kitoto.Nimekuuliza swali rahisi lakini
badala ya kunijibu unaleta dana
dana.Muda huo wa kuzungushana
sinao kwa hiyo nakukabidhi kwa
hawa jamaa ambao wataendelea
kukuuliza badala yangu.Hawataki
mchezo give them answers” akasema
rais na kuwageukia wale jamaa
“Gentlemen do your job”
akasema rais na wale jamaa
wakamkamata Silva wakamvua nguo
zote na kumfunga katika kiti.Rais
akakaa pembeni kabisa akishuhudia
kilichokuwa kinaendelea.Mashine
kadhaa zikaingizwa mle ndani kwa
ajili ya kumtesa Silva
“Mr President don’t do this to me
please” akapiga ukelele Silva
“Silva nakupa nafasi ya mwisho
kabla vijana hawajaanza kuifanya kazi
yao.Nieleze kuhusu Yasmin”akasema
rais
“Sifahamu chochote mheshimiwa
rais”akasema Silva na rais akawapa
ishara wale jamaa waendelee na kazi
yao
Silva akamwagiwa maji ya baridi
yaliyochanganyika na barafu halafu
akafungwa kitu fulani katika mkono
wake ambacho kiliunganishwa katika
mashine na mmoja wa wale jamaa
akaiwasha na kuweka kiwango cha
umeme kinachotakiwa na kuruhusu
umeme upite.Silva akauma meno kwa
nguvu huku akitetemeshwa kwa chaji
za umeme.Yule jamaa aliyekuwa
anaongoza mashine akapewa ishara
akazima
“ Uko tayari kuongea? Akauliza
jamaa aliyekuwa amesimama mbele
ya Silva.Bado alikuwa anatetemeka
“Uko tayari kuzungumza ?
akauliza yule jamaa kwa ukali.Bado
Silva hakujibu kitu alibaki
kimya,mashine ikawashwa tena.Baada
ya sekunde kadhaa ikazimwa na Silva
akaulizwa tena kama yuko tayari
kuongea lakini alionekana kutokuwa
tayari kuzungumza chochote.
Baada ya kurudia mara tatu na
kuonekana bado hataki kuzungumza
rais akaomba zoezi lile lisimamishwe.
“Silva kwa nini unakubali
uteseke kiasi hiki? Tell me about that
woman.Hautatoka humu hadi
unieleze kuhusiana na
Yasmin.Endapo hautakuwa tayari
nitakwenda moja kwa moja kwa
familia yako.Hivi tuongeavyo kuna
watu tayari wamewekwa katika kila
sehemu alipo mmoja wa wanafamilia
yako na wanachosubiri ni simu yangu
tu ili wote wachukuliwe na
kupelekwa katika sehemu ambayo
hautawaona tena katika maisha
yako.Kwa nini unataka kuiharibu
familia yako? Nipe ninachohitaji na
uiokoe familia yako” akasema rais na
huku akitetemeka mwili Silva
akapandwa na hasira
“Don…don’t..touch my family or
I’ll kill you!! Akasema Silva
“Kwa sasa hauna uwezo wa
kuniamuru chochote na kama
utaendelea na kiburi chako
nitaiangamiza familia yako.I’m a
father too na inaniuma sana kutaka
kuigusa familia yako lakini sina
namna nyingine ya kufanya
,ningekuwa wewe nisingekubali hata
kidogo familia yangu kuingizwa
katika hatari.” Akasema rais
“You touch my family I’ll kill you
I swear !!! akasema Silva .Rais
akawapa ishara wale jama waendelee
na zoezi lao.Safari hii akafungwa kitu
Fulani katika uume wake na mashine
ilipowashwa akapiga yowe
kubwa.Mashine ikazimwa rais
akamfuata
“Silva answer me !! akasema rais
kwa ukali.Silva hakujibu kitu alikuwa
analia kwa kwikwi.
“Gentlemen this is not
working.I’m taking down his family”
akasema rais kwa hasira na kuchukua
simu yake kabla hajapiga silva
akapiga ukelele
“Stop !!
Rais akamtazama
“Are you ready to talk now?
“Nitakueleza unachokitaka
.Swear to me you wont touch my
family”
“I swear I wont touch your
family” akasema rais na kuwataka
wale jamaa watoke mle chumbani
akabaki yeye na Silva
“Now tell me” akasema rais.Silva
akainamisha kichwa na kusema
“Ni kweli Yasmin Esfahani
anashikiliwa hapa Tanzania kwa zaidi
ya miaka kumi sasa.” Akanyamza
akavuta pumzi ndefu bado mwili
wake ulikuwa unamtetemeka.Rais
akainuka na kumfunika koti.Silva
akaendelea
“ Yasmin ni mwanamke mwenye
asili ya Afrika lakini ana uraia wa Iran
na kwa muda mrefu amekuwa akiishi
nchini Syria.Huyu ni mfuasi wa
kikundi cha kigaidi cha dola ya
kiislamu na inasemekana kwamba ni
mtu hatari.Kikundi hiki cha dola ya
kiislamu kilianza kujitanua katika
bara la Afrika hususan katika afrika
mashariki.Tulipata taarifa za
kiintelijensia toka shirika la ujasusi la
Iran kwamba Yasmin anaishi hapa
nchini na lengo lake ni kuanzisha
kikundi cha dola ya kiislamu
Tanzanian na Afrika mashariki kwa
ujumla.Tulizifanyia kazi taarifa hizo
na kumkamata Yasmin ambaye ni
kweli alikuwa anaishi hapa nchini na
alikuwa amezaa na raia mtanzania
mtoto mmoja na tulimkamata akiwa
katika harakati za kutoroka baada ya
kugundua kwamba
anatafutwa.Hatukufanikiwa kumpata
mtoto wake wala mwanaume
aliyekuwa akiishi naye.Baada ya
kumkamata Yasmin aliwekwa mahala
pa siri ambako hana mawasiliano na
mtu yeyote na hapo ndipo
tunapowahifadhi wale wote
wanaokuwa hatari kwa
taifa.Mheshimiwa rais kuna gereza la
siri hapa nchini ambalo tunalitumia
kuwaficha wale wote ambao
wanahatarisha usalama wa nchi.Ni
mahala pa siri mno na si rahisi kwa
mtu wa kawaida kupafahamu na hata
rais wa nchi huwa hataarifiwi kuhusu
gereza hili la siri.Wote wanaohudumu
katika gereza hili hula kiapo cha
kutunza siri hata ikiwalazimu kufa.”
Akasema Silva na kuinamisha kichwa
“Kwa nini hukunieleza mapema
kuhusu jambo hili hadi
ukanisababisha nikufanyie hivi? Mimi
ndiye mkuu wako na ulipaswa
kunifahamisha kuhusu jambo hili
mapema”akasema rais
“Mheshimiwa rais nisingeweza
kukueleza chochote juu ya jambo hili
kwani niko chini ya kiapo na leo hii
nimevunja kiapo changu kwa sababu
ya kuiokoa familia yangu.Naomba
tafadhali ukumbuke ahadi yako ya
kutoigusa familia yangu”akasema
Silva
“Nimekwisha kuahidi kwamba
sintaigusa famila yako.Nataka
kufahau mnapata wapi fedha za
kuwahudumia hawa mnaowahifadhi
katika hilo gereza? Jambo hili
halifahamiki serikalini na hakuna
fungu lolote katika bajeti kwa ajili ya
kuhudumia gereza hili.Mnamudu
vipi?
“Ni kweli mheshimiwa rais
hakuna fungu toka serikalini kwa ajili
ya kuendesha gereza hili la siri lakini
pesa zote za uendeshaji zinatoka kwa
mataifa makubwa ya nje ya
nchi.Wanaofungwa katika gereza hili
ni watu kutoka mataifa ya Marekani
na Uingereza na hao ndio wachangiaji
wakuu .Kuna watu ambao
wanawaletwa ili kuja kufichwa huku
kwa maisha yao yote au kuja kuuawa”
“Mpaka sasa mnawashikilia
watu wangapi katika hilo gereza?
“Hilo siwezi kukujibu
mheshimiwa rais .Ulitaka kufahamu
kuhusu Yasmin na tayari nimekujibu”
Rais akamtazama Silva kwa
sekunde kadhaa na kusema
“Kuna mambo mawili ambayo
nataka uyafanye.Moja kuna watu
ambao nataka waingie katika hilo
gereza na kupotelea humo kwa
maisha yao yote yaliyobaki.Jambo la
pili namuhitaji Yasmin Esfahani.”
“Mheshimiwa rais ,gereza hili
tunaliongoza sisi pamoja na watu
walioko Marekani kiasi kwamba
hatuwezi kumtoa au kuingiza mtu
yeyote bila ya wenzetu kufahamu na
lazima idhini ya kuingiza mtu itoke
kwao.Kwa umuhimu wa gereza hilo
wameelekeza satelaiti maalum ili
waweze kufuatilia kile kinachofanyika
hapo.Kwa hiyo mheshmiwa rais si
rahisi kumpata Yasmin”
“Namuhitaji Yasmin .Namuhitaji
mno.Ili mimi na wewe tuende sawa
utakwenda kumchukua Yasmin na
watu hao ninaokuambia utawaingiza
katika hilo gereza .Kwa sasa
utaendelea kukaa hapa na jioni ya leo
nitakuja kukuchukua ukanipatie
Yasmin” akasema rais na kutoka
akawaagiza wale jamaa wenye suti
nyeusi waendelee kumlinda Silva
kisha akaondoka.
SEHEMU YA 7: SEASON 5
Austin akiwa sebuleni katika
tafakari nzito,akainua kichwa baada
ya kusikia hatua za mtu akishuka
ngazi.Amarachi alikuwa anashuka
ngazi taratibu huku akiwa
amechafuka damu.Akasimama mbele
ya Austin wakatazamana kwa muda
“He’s ready to talk” akasema
Amarachi
“Thank you Amarachi.Good Job”
akasema Austin huku akinyanyuka
“Go wash yourself.We still have
job to do” akasema Austin huku
akipanda ngazi kuelekea chumbani
alimo Boaz.Akaingia ndani kumkuta
Boaz akigugumia maumivu.Hakuwa
anatazamika usoni alikuwa ameloa
damu
“Uko tayari kuzungumza sasa?
Akauliza Austin
“Siamini Austin kama leo
umenifanyia hivi.You are such a
monster”
“Boaz sina muda wa kupoteza
.Are you ready to talk or not” akauliza
Austin.Boaz hakujibu kitu
“You are not ready.Ngoja
nimuite Amarachi aendelee na zoezi
lake hadi pale utakapokuwa tayari
“No ! No ! No !!.” akasema Boaz
“Tafadhali usimlete tena yule
mwanamke shetani humu chumbani.
Sitaki kumuona tena” akasema Boaz
“Ukitaka nisimlete tena anza
kunieleza kwa nini uliamua
kuyaharibu maisha ya mdogo wangu?
“Nisamehe sana Austin.Ni
shetani alinipitia .Nilikuwa na nia
nzuri ya kumsaidia lakini niliingiwa
na tamaa nikaanza kumtumia
kimwili.Ni yeye mwenyewe
aliyependa kuingia katika biashara ya
dawa za kulevya ili kujiongezea
kipato na sikuona sababu ya
kumkatalia.Austin sina maneno mengi
ya kuongea.Najua nimekukosea sana
na ninachokihitaji toka kwako ni kitu
kimoja tu.Nahitaji msamaha
wako.Naomba unisamehe sana kwa
yote niliyokukosea .Sina neno zuri la
kukuomba msamaha lakini nakuahidi
nitafanya kila niwezalo kuhakikisha
ninayajenga upya maisha ya
Linda.Nakuahidi Austin nitatoa pesa
nyingi kwa ajili ya Linda.Naomba
uniamini” akasema Boaz
“It’s too late Boaz.Tayari
umechelewa mno.Ulipaswa kufanya
hayo kabla sijafahamu kuwa wewe
ndiye uliyeyaharibu maisha ya mdogo
wangu.Kwa nini Boaz ukanifanyia
hivi? Nilikuchukulia kama baba
yangu lakini kumbe ni shetani
mkubwa.Wewe na genge lako
mnaoshirikiana kuwaharibu mabinti
wadogo kwa kuwatumia katika
biashara zenu za dawa za kulevya
mwisho wenu umefika.Nitaonana
nawe tena baadae.Maongezi nawe
hayajamalizika” akasema Austin
akiinuka
“Austin!! Austin !!!! ..akaita Boaz
lakini Austin hakugeuka
“Amarachi amefanya kazi nzuri
sana.Kweli huyu ni jembe la kazi.Sasa
ni zamu ya Maria” akawaza Austin na
kushusha pumzi.Akashuka sebuleni
na kumkuta Amarachi tayari
amekwisha badili mavazi
“Umefanya kazi nzuri sana
Amarachi.Thank you” akasema
Austin
“Siku ya leo imenikumbusha
maisha yangu ya msituni chini ya
Boko haram.Walinifundisha mambo
mengi hata namna ya kumfanya
mateka hata awe mgumu kiasi gani
aongee.Kwa hiyo Austin kama kuna
mtu yeyote ambaye unahitaji aongee
nikabidhi mimi na ninakuahidi lazima
ataongea tu labda awe ni bubu”
akasema Amarachi .Ile sura yake
iliyojaa tabasamu ilikuwa imetoweka
na sasa alikuwa na sura ya kazi.
“Good.Ni zamu ya Maria sasa”
akasema Austin na kutazamana na
Amarachi
“Kwa nini usiniache
nikamalizane naye? Yule alikuwa
mpenzi wako na unaweza kuingiwa
na moyo wa huruma .Niache niende
peke yangu” akasema Amarachi
“ Ahsante Amarachi ila
tunakwenda pamoja.” Akasema
Austin
“Are you sure? Amarachi
akauliza
“ Yes” akajibu Austin
Amarachi akaufungua mlango
wa chumba alimofungwa Maria
wakaingia,Austin akavuta kiti akaketi
na bila kupoteza muda akasema
“ Sweetheart I’m back”
akanyamaza na kumtazama Maria
“Nilipokuja awali nilikuonya
kwamba nataka ushirikiano na
endapo utashindwa kunipa
ushirikiano wako utanisababisha
nichukue maamuzi ya kutumia nguvu
kitu ambacho sikitaki” akanyazama
tena akamtazama Maria na kusema
“ Nataka unipe namba za siri za
kufungulia hii kompyuta yako”
Maria akamtazama Austin na
kubetua midomo kwa dharau
“Umenisikia Maria? Nataka
namba za siri unazotumia kufungulia
hii kompyuta yako” akasema
Austin.Maria hakujibu kitu
akainamisha kichwa.Austin akainuka
na kumfuata akamshika kichwa
“Look at me Maria.I’m not the
same Austin you loved.Nitakufanyia
kitu kibaya sana endapo utaendelea
kuwa na kiburi” akasema Austin
“Unanitishia kuniua? You are so
fool .I’m not scared of death
Austin.Ninakuhakikishia hata unitese
vipi hutaweza kupata chochote toka
kwangu.Ni bora uniue kuliko
kuendelea kupoteza muda wako”
akasema Maria
“Austin huyu hatakueleza
chochote.Naomba unipe dakika kumi
tu na atasema” akasame Amarachi
.Austin akainuka na kutoka
akamuacha Amarachi na Maria
“Nimekuwa katika mahusiano na
Maria kwa muda wa miaka kadhaa
kwa nini nilishindwa kugundua kama
yuko hivi? Who is she? Akajiuliza
Ausytin huku akishuka ngazi
kuelekea sebuleni.Hakutaka kabisa
kuwepo eneo lile wakati Amarachi
anaifanya kazi yake.
“Nimeishi na nyoka ambaye
alikuwa anatafuta siku ili
animeze.Bahati mbaya kwake Mungu
amenionyesha mapema ni mwanamke
wa aina gani niliyekuwa naye.Hata
hivyo mwisho wao umefika yeye na
baba yake”
Baada ya dakika kumi kama
alivyoahidi Amarachi akarejea
sebuleni akiwa na kompyuta
iliyofunguliwa akaiweka mezani
“ Tayari ameifungua” akasema
Amarachi.Austin akamtazama na
kusema
“Thank you”
“She need a doctor.She’s
bleeding “ akasema Amarachi
“Dah! Ama kweli leo nimekutana
na kifaa.Sijui hawa watu anawafanya
nini hadi wanafunguka na
kuongea.Nashukuru Job
kunikutanisha na huyu mtu muhimu
sana ambaye naweza kumuta ni binti
wa chuma” akawaza Austin na
kumuomba Amarachi akamfungulie
mlango wa chumba alimo Maria
Chumba chote kilitapakaa
damu.Maria hakuwa anatazamika,uso
wake uliloa damu
“Kulikuwa na shughuli pevu
humu ndani.Huyu Amarachi ni
mwanamke wa hatari sana.Ukimpa
nafasi ya kumuhoji mtu unapaswa
uwe karibu vinginevyo anaweza
akaua.Huyu anafaa sana kuwa
mshirika wangu katika kazi” akawaza
Austin na kumwambia Amarachi
amfungue Maria .Akamtaka Maria
asimame lakini hakuweza.Miguu
ilikuwa imetobolewa na kifaa cha
kutobolea vitu vigumu.Amarachi
akamshika mabegani akamvuta hadi
bafuni akamuogesha kisha
akamrudisha chumbani akaenda
kuchukua nguo nyingine akamvisha
kisha kwa pamoja wakasadia kumtibu
majeraha yake na walipomaliza
Austin akasema
“Pumzika kwa sasa.Tutarudi
baada ya muda mfupi kuendelea na
maongezi.Endapo utakuwa kiburi
utapata mateso mara mbili ya haya
uliyoyapata” akasema Austin na
kutoka
“Austin utanisamehe kwa
nilichomfanyia mpenzi wako lakini
naomba ufahamu kwamba
nilichokiona kwa Maria ni kitu cha
kushangaza sana.Ni mwanamke
mwenye uwezo mkubwa wa
kuvumilia mateso
makali.Nilifundishwa namna ya
kutesa nikiwa msituni na Boko Haram
na ndiyo maana nimeweza
kumfungua mdomo lakini watu wa
aina hii ya Maria ni watu waliokula
kiapo cha kutokutoa siri hata
ikiwalazimu kufa.Utanisamehe kwa
hili nitakalolisema bali watu wa aina
hii ya Maria mara nyingi huwa
wanabeba siri kubwa na aidha ni watu
waliobeba siri za nchi au ni
magaidi.Nimeishi na Boko Haram
kwa miaka kadhaa na tukiwa masituni
tulifundishwa namna ya kuficha siri
hata kama itakulazimu kutoa uhai
wako na hiki ndicho nilichokiona kwa
Maria.Anacho kitu kikubwa endapo
tukimbana anaweza akatueleza.”
Akasema Amarachi
“Nakubaliana nawe
Amarachi.Maria ni mtu ambaye
hatujamfahamu bado kwa undani na
tunapaswa kumbinya hadi atueleze
yeye ni nani na tuifahamu siri
aliyonayo.Tuanze kwanza kuipekua
kompyuta yake.” Akasema Austin
Walianza kuipekua kompyuta ile
ya Maria lakini hawakuweza kupata
kitu chochote cha kuwasaidia kwani
mafaili mengi yalikuwa yanahusu
mambo ya kazi.Wakaiunganisha
kompyuta ile na mtandao wa intanet
ili waweze kutazama katika
mawasiliano yake ya barua pepe na
hapo walifanikiwa kugundua kitu
fulani
Katika kumbukumbu ya barua
pepe alizotuma Maria kulikuwa na
barua pepe aliyotuma kwa mtu mmoja
anaitwa Bin Omar iliyosomeka
“Sintaweza kuja huko kama
ulivyotaka , nakwenda Tanzania
.Nimeamua kwenda mwenyewe kumtafuta
mama kwani nimekuwa nikipewa ahadi
mara kwa mara kuhusiana na kumtoa
mama lakini mpaka leo hii hakuna
chochote kilichofanyika.Ninakwenda Dar
es salaam kuna mtu yuko kule atanisaidia
kumtafuta mama”
Baada ya ujumbe huo kukawa na
ujumbe mwingine wa majibu toka
kwa Bin Omar uliosomeka
“Shamim hicho unachotaka
kukifanya ni kitu cha hatari sana.Kuna
watu wetu wenye ujuzi wa kutosha
wanalifanyia kazi suala hilo”
Baada ya ujumbe huo Maria
akajibu
“Nina uhakika na mtu ninayetaka
kumtumia kwa ajili ya kazi ya kumtafuta
mama.Ni mtu mwenye uwezo mkubwa na
amewahi kufanya kazi katika idara ya
usalama wa taifa Tanzania
.Nimemuandaa mtu huyu kwa muda
mrefu na kwa gharama kubwa kwa ajili ya
kunisaidia katika kazi hii.Endapo
nitashindwa kufanikiwa nitakujulisha”
Hakukuwa tena na majibu toka
kwa Bin Omar .Austin na Amarachi
wakatazamana
“Hatimaye mwanga umeonekana
na tunaanza kumfahamu huyu Maria
ni nani” akasema Austin
“ Her name is not Maria.Ana jina
lingine anaitwa Shamim.Amefanya
mawasiliano na huyu mtu anaitwa Bin
Omar siku moja kabla hajaja Dar es
salaam.Huyu Bin Omar ni nani?
Akauliza Austin
“ Katika maelezo yake Maria au
Shamim anaeleza kwamba kuna mtu
wake ambaye atamtumia katika
mpango wa kumpata mama
yake.Hapa nina uhakika alikuwa
anamaanisha wewe.kwa muda huu
wote uliokuwa naye amekuweka
karibu kwa dhumuni la kukutumia
katika mpango wake.Mwanamke
mshenzi sana huyu!!! Akasema
Amarachi
“How could I be so stupid? Kwa
nini kwa muda huu wote niliokuwa
naye sijabahatika kugundua kama
Maria ni mtu hatari? Hakukuwa na
hata chembe ya mapenzi kati
yetu,kumbe ulikuwa ni uongo
mkubwa na alikuwa anataka
kunitumia kwa manufaa
yake.Imeniumiza sana kwa kuwa
mjinga kiasi hiki na kushindwa
kugundua hili” akasema Austin na
kuinamisha kichwa
“Huyu mama yake ni nani hasa?
Yuko wapi na kwa nini? Maria
hajawahi kukutamkia chochote
kuhusu mama yake? Amarachi
akamuuliza Austin aliyekuwa
ameinamisha kichwa akainua kichwa
na kumtazama Amarachi na kusema
“Wote wawili Boaz na mwanae
walinihakikishia kwamba mama yake
Maria alifariki angali Maria akiwa
bado mdogo .Kwa mujibu wa maelezo
yao ni kwamba Maria hakuwahi
kumuona mama yake.Kumbe huu
wote ulikuwa uongo mkubwa .Hii
familia imekuwa ikiishi kwa uongo
mkubwa lakini mwisho wao
umewadia.Twende kwa Maria
akatueleze ukweli” akasema Austin
wakaelekea chumbani kwa Maria”
akasema Austin wakaelekea chumbani
kwa Maria.Austin akavuta kiti na
kuketi karibu na Maria akamtazama
na kusema
“kwa mara ya kwanza katika
maisha yangu niliyafurahia maisha ya
mapenzi baada ya kukutana
nawe.Nilijua nini maana ya kupenda
na kupendwa.Nilikupenda kwa moyo
wangu wote na nilikuwa tayari
kuacha kila kitu kwa ajili ya kuwa na
wewe.Niliamini wewe ndiye
mwanamke yule ambaye umeumbwa
kwa ajili yangu na tayari nilikwisha
amua kuanza maisha mapya ya
familia nikiwa nawe.Nilikupenda
kweli toka moyoni lakini kumbe
nilikuwa namwaga maji ndani ya
pakacha.Wakati nikijitoa kukuonyesha
namna gani ninakupenda kumbe
mwenzangu ulikuwa unanifanyia
maziongaombwe.Ulikuwa na malengo
yako.Hili limeniumiza mno.How
could you do that to me Maria? How
could you be so cruel? Akauliza
Austin huku akimtazama Maria kwa
macho makali
“Sihitaji maelezo yoyote toka
kwako kwani ukweli wote tayari
ninaufahamu .Ninachohitaji toka
kwako kwa sasa ni majibu sahihi ya
maswali yangu.” Austin akamtazama
Maria kwa hasira kisha akauliza
“Tumekuta mawasiliano ya
barua pepe kati yako na mtu anaitwa
Bin Omar.Katika mawasiliano hayo
umemwambia Omar kwamba unakuja
Dar es salaam kumtafuta mama yako
ambaye wewe na baba yako
mliniambia kwamba alifariki angali
ukiwa mdogo. Omar anakukataza
kwamba usifanye hivyo kwani kuna
watu wenye ujuzi wanalishughulikia
jambo hilo lakini unamuhakikishia
kwamba kuna mtu yuko dar es salaam
ambaye unamuamini na
umemtayarisha kwa miaka kadhaa
kwa ajili ya kazi hii na una imani
atakusaidia kumpata mama yako na
mtu huyo nina uhakika ulikuwa
unamaanisha mimi na hii
inadhihirisha wazi kwamba hukuwa
na mapenzi yoyote nami bali lengo
lako ni kunitumia kwa ajili ya mambo
yako binafsi.Nataka kufahamu huyo
Bin Omar ni nani na yuko wapi?
Mama yako ni nani na yuko wapi?
Naomba tafadhali unipe majibu ya
maswali yangu ama ukishindwa
kufanya hivyo nitakuharibu Maria na
mipango yako yote ya kuonana tena
na mama yako itakuwa imefikia
ukingoni.” Akasema Austin
Baada ya sekunde kadhaa Maria
akainua kichwa akamtazama Austin
na kuuma meno kwa maumivu kasha
akasema
“It’s ok..Its over.Let’s put and
end to this” akanyamaza akafumba
macho akionekana kuwa katika
maumivu
“Austin you can’t get anything
from me unless we have a deal”
“A deal ? Austin akasema kwa
ukali
“ Yes .A deal “ akajibuMaria
“ Siwezi kufanya makubaliano
yoyote nawe na utanieleza kila kile
ninachokihitaji” akasema Austin
“ Kama umekataa kufanya
makubaliano nami basi hutaisikia tena
sauti yangu .I’d rather die than tell
you anything .The choice is yours”
akasema Maria
“ Naomba unielewe vizuri
Maria,sintofanya makubaliano yoyote
nawe.Kwa sasa kile tulichokuwa
nacho kimekwisha kwa hiyo sioni
tatizo kukuharibu.I’ll destroy you
Maria!! Akasema Austin.Maria
akainamisha kichwa.Amarachi
akamtaka Austin watoke nje ya kile
chumba wazungumze
“ Austin I’m sorry to say this but
she’s not going to tell us
anything.Kama nilivyokueleza awali
kuna siri kubwa anayo huyu Maria na
ili kuifahamu inatulazimu
kukubaliana na anachokitaka.Make a
deal with her.She’d rather die than tell
us what we want” akasema Amarachi
Austin akamtazama Amarachi na
kusema
“ She lied to me,She nearly killed
me.Are you sure you want me to make
a deal with her? Akauliza Austin kwa
ukali.Amarachi akamshika bega na
kusema
“ Nimeishi kwa miaka kadhaa na
watu hatari na magaidi wakubwa na
wamenifundisha mambo mengi na
hata kumtambua mtu ambaye yuko
tayari kufa kuliko kutoa siri na
nikimtazama Maria ni kweli yuko
tayari kufa kuliko kusema chochote”
akasema Amarachi.Austin
akainamisha kichwa akafikiri kwa
muda na kusema
“ Sawa Amarachi .Nakubaliana
na ushauri wako.Ngoja tusikie
anachokitaka Maria” akasema Austin
wakarejea tena ndani ya kile chumba
“ Ok tell me what do you want”
Austin akamuuliza Maria ambaye
aliinua kichwa akamtazama na
kusema
“ Are you sure you want this?
“ Yes tell me what do you want”
akasema Austin.Maria akavuta pumzi
ndefu na kusema
“ Nitakueleza kile unachotaka
kwa sharti moja tu.”
“ Acha kuzunguka sema
unachokihitaji”
“ It’s my mother.Her name is
Yasmin Esfahani.Anashikiliwa na
serikali ya Tanzania .Kuna sehamu ya
siri amefungwa kwa zaidi ya miaka
kumi sasa na mahala alikofungwa
hatatoka kwa maisha yake yote.I want
you to get her out of
there.Ukilifanikisha hilo I promise you
I’m going to tell you a very big secret
that I have” akasema Maria .Austin
akamtazama na kusema
“ Mama yako amefungwa wapi
hapa tanzani?
“Sifahamu ni sehemu gani but
you have many connectins so find out
where she is.Ukimpata utapata jambo
kubwa ila ukishindwa kufanikisha
hilo I’ll die with my secret.Big things
are about to happen so hurry up,give
me my mother and I’ll tell you
everything” akasema Maria .Austin na
Amarachi wakatazamana
“ Let me see what I can do”
akasema Austin halafu wakatoka mle
chumbani
“ Yasmin Esfahani..” akasema
Austin
“ Ni mara ya kwanza kulisikia
jina hili.Ni nani huyu mwanamke?
Kwa nini anashikiliwa mahala pa siri?
Is she dangerous? Akajiuliza Austin
“ Ni wazi lazima atakuwa ni mtu
hatari na ndiyo maana anashikiliwa
mahala pa siri kwa miaka hiyo yote.”
Akasema Amarachi
“ Kama mama yake ni mtu hatari
hata Maria naye ni mtu hatari na watu
wanaoshirikiana nao pia ni watu
hatari pia” akasema Austin
wakaelekea sebuleni
“ Kuna njia moja tu ya kuweza
kumpata huyo mwanamke” akasema
Austin na kuchukua simu yake
akazitafuta namba za simu za rais
akampigia
“ Hallow Austin.Vipi maendeleo
yako? Akauliza rais baada ya kupokea
simu
“ Naendelea vizuri mzee.”
“ Good.Kuna taarifa gani mpya?
Vipi Job anaendeleaje?
“ Bado tunasubiri taarifa toka
hospitali anakotibiwa na nitakujulisha
maendeleo yake.” Akasema Austin na
kunyamaza kidogo kisha akasema
“ Mzee samahani kwa usumbufu
mchana huu”
“ Hakuna usumbufu wowote
Austin.Simu yako muda wowote ni ya
muhimu mno kwangu na hata kama
niko kati kati ya jambo lolote kubwa
nitasimamisha na kuipokea.”
“ Nashukuru mheshimiwa
rais.Nimekupigia kuomba msaada
wako .Kuna mwanamke mmoja
anashikiliwa na serikali ya Tanzania
mahala pa siri anaitwa Yasmin
Esfahani.Ninamuhitaji huyu
mwanamke kwa haraka” akasema
Austin na kumstua sana rais
“ Umesema Yasmin Esfahani?
Akauliza rais
“ Ndiyo mzee. Namuhitaji sana
huyo mwanamke siku ya leo”
akasema Austin na zikapita sekunde
kadhaa kisha rais akajibu
“ Ni nani huyo mwanamke?
Mbona mimi sina taarifa zake?
“ Hauna taarifa zake? Austin
akashangaa
“ Ndiyo Austin sina taarifa zake
zozote.Una hakika mwanamke huyo
yuko Tanzania? Anashikiliwa na
chombo gani cha ulinzi hapa nchini?
Inanishangaza kidogo kwani mimi
ndiye amiri jeshi mkuu na vyombo
vyote vya ulinzi na usalama viko chini
yangu lakini sina taarifa za
kushikiliwa mtu kama huyo hapa
Tanzania.Una uhakika Austin
kwamba mwanamke huyo yuko hapa
nchini?
“ Mheshimiwa rais nina uhakika
mwanamke huyo yupo na
anashikiliwa hapa nchini.Tafadhali
nisaidie kufahamu mahala
alipo,namuhitaji ni muhimu sana
kwangu”
“Unamuhitaji kwa ajili ya
shughuli gani?
“Kuna jambo nalifuatilia na
nitakapolikamilisha nitakufahamisha
lakini ili likamilike lazima nimpate
Yasmin”
“ Jambo hilo unalolichunguza
liko katika ile mipango yetu dhidi ya
Alberto’s? akauliza rais
“ Hapana mheshimiwa rais.Hili
ni suala ambalo halina uhusiano wa
moja kwa moja na Alberto’s
“ Austin nitajaribu kuwauliza
wakuu wa idara za usalama wa nchi
kama kuna idara yoyote
inayomshikilia huyo mwanamama
lakini ningependa kukushauri
kwamba kwa sasa ungeelekeza nguvu
kubwa katika suala kubwa lililo mbele
yetu la kupambana na Alberto’s na
baada ya kulikamlisha hilo
utaendelea na huo uchunguzi wako
mwingine.Tukiweka mambo mengi
kwa mara moja tutapoteza uelekeo
.Umenisikia Austin? Akauliza rais
“Nimekuelewa mzee” akajibu
Austin
“Good.Nitakupigia simu endapo
nitafanikiwa kufahamu chochote
kuhusiana na huyo mwanamke
unayemtafuta” akasema rais na
kukata simu
“This is strange.Inashangaza eti
rais hana taarifa za huyo mwanamke
Yasmin Esfahani.Kama kweli Yasmin
anashikiliwa kwa siri hapa Tanzania
lazima rais afahamu.Au amefichwa
jambo hili?.Kama ni hivyo kwa nini
basi afichwe jambo hili kwa miaka hii
yote?akauliza Austin
“Maria hawezi kutudanganya,ni
kweli mama yake yuko hapa Dar es
salaam kwani amekuja kwa dhumuni
la kumtafuta kwa hiyo tufanye kila
namna ili tumpate.” Akasema
Amarachi
“ Tusubiri taarifa toka kwa rais
kama atafanikiwa kumpata au
vipi.Endapo hatafanikiwa kumpata
itatulazimu sisi wenyewe kuingia
kazini kumtafuta hadi tumpate.Kwa
sasa tuendelee kukipitia kile kitabu
chenye orodha ya wauza unga wote
wakubwa wa hapa nchini “ akasema
Austin
SEHEMU YA 8: SEASON 5
Ernest Mkasa rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania alistuka sana
kwa Austin kulitaja jina la
Yasmin.Aliegemea kiti chake kwa
sekunde kadhaa akitafakari baada ya
kumaliza kuongea na Austin simuni
“ Hili sasa ni jambo jipya
limeibuka.Austin amefahamu vipi
kuhusu Yasmin?Anamtaka kwa ajili
ya jambo gani? Kuna nini
anakichunguza? Inawezekana akawa
amefahamu kuhusiana na mpango
wangu wa kumuachia huru Yasmin
na sasa anataka kuuvuruga? Lakini
mpango huu ni wa siri sana na nina
hakika bado hafahamu chochote na
nitahakikisha hafahamu chochote.Yule
kijana anaanza kuonekana kuwa
hatari kwangu.Nisipokuwa makini
anaweza akaikwamisha mipango
yangu mingi .Nadhani kuna jambo
natakiwa kulifanya.Mara tu
atakaponikabidhi majibu ya kipimo
kile cha vinasaba nitalazimika
kumuondoa haraka sana ili asije
kunivurugia huko mbeleni.Natakiwa
kumuwahi kabla
hajaniwahi.Wenz……” Rais
akaondolewa mawazoni na mlio wa
simu akatazama mpigaji na kuipokea
haraka haraka
“ Mheshimiwa rais samahani
kama nimekusumbua ila kuna jambo
nataka kukutaarifu” akasema mtu
aliyempiga simu ile
“ Go ahead” akasema rais
“ Kuna jambo
limetokea.Mukasha ametoweka”
“ What ???Rais akashangaa.
“Nimewatuma vijana wangu
wamfuate Mukasha katika ile hospitali
aliyokuwa amelazwa jana usiku na
kumkosa.Inasemekana aliondoka
usiku bila hata ya kuruhusiwa.Vijana
wakaenda hadi nyumbani kwake na
kumkosa pia yeye na familia yake na
inaonekana wameondoka haraka
haraka kwani nyumba imevurugwa
sana.I’m sorry mr President I failed
you again”
Ukimya mfupi ukapita rais
akasema
“ Sawa nitawatuma vijana wangu
wamsake kokote aliko na
atapatikana.Kwa sasa elekeza nguvu
kwa yule kijana aliyeko hospitali.Kuna
mambo mengi atakuwa ameyafahamu
toka kwa Mukasha kwa hiyo
tunatakiwa tuhakikishe kwa namna
yoyote ile hatoki pale hospitali
salama.Anatibiwa katika hospitali ya
saratani ya Dr Richard
Memorial.Peleka vijana pale.This time
no mistake!! Akasema rais
“Sawa mheshimiwa
rais.Nitafanya hivyo.” Akasema yule
jamaa na kukata siku .Rais akagonga
meza kwa hasira
“ Mambo yanaanza kwenda
ndivyo sivyo.Endapo nitamruhusu
Mukasha atoweke nitakuwa
nimefanya kosa kubwa sana kwani
yule ni mtu anayefahamu mambo
yangu mengi kwa hiyo ni mtu hatari
na anaweza kuwa adui yangu
mkubwa.Nitatumia uwezo wangu
wote kumtafuta Mukasha hadi
nihakikishe nimempata.Sitaki
operesheni yangu ya kusafisha nchi
iiingiliwe na tatizo lolote.”
SEHEMU YA 9; SEASON 5
Job alitolewa katika chumba cha
wagonjwa mahututi baada ya jitihada
za madaktari kufanikiwa ,akapelekwa
katika chumba cha uangalizi
maalum.Hii ilimpa fursa Marcelo
kusalimiana na wafanyakazi na
kupata taarifa fupi kuhusiana na
mambo yanavyokwenda pale hospitali
katika kipindi ambacho hakuwepo
halafu akaelekea ofisini kwake akaketi
kitini na kutabasamu
“ Ni kama muujiza kukalia tena
kiti hiki .Sikutegemea kabisa kuwa
huru tena .Shukrani za pekee
zimuendee Austin na wenzake ambao
wamefanya kazi kubwa usiku na
mchana kuhakikisha ninakuwa
salama.Lakini bado swali moja
linaendelea kuzunguka
kichwani,David Zumo alipataje taarifa
zangu na kuamua kunisaidia?
Akajiuliza na kumkumbuka Monica
“ Nadhani ni wakati sasa wa
kumtafuta Monica na kufahamu
kilichompata na kwa nini sikuwahi
kumuona tena kuja kunitazama?
Kama hakuwa na uwezo wa
kunisaidia kwa nini asingekuja na
kunieleza ukweli kuliko kutokomea
kabisa? Monica ni mtu niliyemuamini
mno hadi nikamshirikisha katika
jambo hili kubwa na nyeti ”
akaendelea kuwaza ,akalifungua
kabati na kutoa kitabu ambacho
hukitumia kuhifadhi namba za simu
za watu mbali mbali akaitafuta namba
ya simu ya Monica kisha akatumia
simu ya ofisi akampigia.
“Hallo” ikasema sauti laini ya
Monica.Marcelo akababaika na ulimi
ukawa mzito kutamka chochote
“ Hallow” Monica akaita tena
“ Hallow Monica “ akasema
Marcelo
“ Who is this? Monica akauliza
“ It’s…it’s me …Marcelo”
“Marcelo? Is that real you?
“ Yes it’s me.How’re you
Monica? Akauliza Marcelo .Monica
akasikika simuni akipiga makelele ya
furaha
“ Huu ni muujiza.Vipi
maendeleo yako? Uko wapi sasa hivi?
” akasema Monica
“Kwa sasa niko hapa hospitali
kwangu na kuhusu maendeleo yangu
ninaendelea vyema.Vipi wewe
unaendeleaje?
“Mimi ninaendelea vyema.Tayari
umetoka mafichoni? Are you sure you
are safe? Monica akauliza
“ Monica uko wapi sasa
hivi?Tunaweza kuonana? Kuna
mambo mengi ambayo nahitaji
kuzungumza nawe”
“ Hata mimi nina mengi ya
kuzungumza nawe lakini kwa muda
huu au kwa siku ya leo kuna jambo
kubwa limenibana na sintaweza
kabisa kupata nafasi ya kuonana nawe
ila kesho asubuhi kabla sijaenda kazini
nitakutafuta ili tuongee.” Akasema
Monica
“ Sawa Monica,tutaonana hiyo
kesho japokuwa nilihitaji sana
kuonana nawe leo”
“ Laiti kama ningekuwa na
uwezo hapa nilipo ningepaa na kuja
kuonana nawe lakini haitawezekana
Marcelo.kesho asubuhi na mapema
nitakutafuta kama
nilivyokuahidi.Kwa heri Marcelo”
akasema Monica na kukata simu
“Nimefurahi kuongea na Monica
na ningefurahi mno endapo
ningeonana naye ana kwa ana kwa
sababu kesho sina hakika kama
ninaweza kupata wasaa wa kuonana
naye tena kwani ninarejea kule kwa
akina Austin.Kwa sasa ngoja niende
nyumbani kwangu nikachukue baadhi
ya vitu vyangu vya muhimu”
akawaza Marcelo akatoka akachukua
mojawapo ya magari ya hospitali
akaelekea kwake.
Alifika nyumbani kwake na
kusalimiana kwa furaha na
mfanyakazi wake wa ndani ambaye
alimwaga machozi mengi baada ya
kumuona tena mwajiri wake .Marcelo
hakutaka kupoteza muda mwingi
hapo akachukua baadhi ya vitu vyake
vya muhimu na kutoka akaondoka
kurejea hospitali.Alipowasili hospitali
akapewa taarifa kwamba wakati
hayupo kuna watu wawili
wasiofahamika walionekana
wakizunguka zunguka katika chumba
alimolazwa Job na walipoulizwa
shida yao waliondoka haraka haraka.
“Job is in great danger.I must
take him ot of here now.Naamini
kabisa watu hao walitumwa kuja
kummaliza” akawaza Marcelo na
haraka haraka akaamuru Job apakiwe
katika gari la wagonjwa na baadhi ya
vifaa alivyovielekeza kisha akaagana
na wafanyakazi wa hospitali ile bila
kuwaeleza anaelekea wapi akaondoka
“ Nimeingia katika ulimwenu
mpya ambao sijauzoea wenye maisha
yaliyojaa hatari nyingi.Kila uchao
uhakika wa kuimaliza siku ni mdogo
kwani kila siku maadui
wanaongezeka.Hawa watu hawana
maisha ya kawaida,hawafurahii
maisha kama sisi.Muda wote wako
kazini kuhakikisha nchi inakuwa
salama.Watu hawa wanastahili
heshima ya pekee kabisa kwani
wanayatoa maisha yao kwa ajili ya
wengine.I’m proud to be just a part of
them” akawaza Dr Marcelo akikatisha
mitaa mbali mbali ya jiji la Dar akiwa
na gari lile la wagonjwa akieleka
nyumbani kwa Job waliko akina
Austin
SEHEMU YA 10: SEASON 5
Ulikuwa ni mshangao mkubwa
kwa Amarachi aliyetoka kutazama
mtu aliyekuwa getini pale alipokutana
na gari la kubebewa wagonjwa
.Haraka haraka akaupeleka mkono
wake ilipo bastora lakini kabla
hajafanya chochote akamuona
Marcelo ndani ya gari akatabasamu na
kufungua geti.Wakasaidiana
kumshusha Job na kumuingiza ndani
“ What happened Marcelo?
Akauliza Austin .Marcelo akamaliza
kumtundikia Job chupa ya maji kisha
akawaeleza kilichotokea hadi
akaamua kumuhamisha Job na
kumleta pale nyumbani.
“Thank you Marcelo for saving
his life.You did a great thing to bring
him here” akasema Austin
“ Vipi maendeleo yako Austin?
“ Naendelea vyema.Mwili
unaimarika kwa kasi kubwa.”
“ I’m glad to hear that .Hata
hivyo ni muda sasa wa kupata dawa
na nimekuja na vifaa mbali
mbali,ninaweza kufungua hospitali ya
muda humu ndani hadi pale
mapambano yatakapokwisha”
akasema Marcelo ,Austin na Amarachi
wakatabasamu.
“ Marcelo kuna mambo mawili
ambayo nataka yafanyike” Akasema
Austin
“ Kwanza utawahudumia wageni
wetu majeraha yao ambayo
wameyapata wakati wakifanyiwa
mahojiano.Mara nyingi huwa ni
vigumu kupata taarifa toka kwa watu
tunaowahoji kwa hiyo hulazimika
kutumia nguvu ndogo hadi kubwa
pale inapobidi ili kupata kile
tunachokihitaji kwa hiyo
usishangazwe na majeraha
utakayoyaona.Ni jambo la kawaida
kwetu.Baada ya hapo kuna jambo la
pili” akanyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Nilipata nafasi ya kukaa na
kuzungumza na Julieth.Kuna mambo
amenieleza ambayo nadhani
unapaswa kuyafahamu.Tafadhali
naomba umsikilize kwa makini na
baada ya hapo utafanya
maamuzi.Hatima ya Julieth naiweka
mikononi mwako wewe ndiye
utakayeamua nini kifuate.Yule ni
ndugu yako kwa hiyo endapo
ukiamua kumsamehe sisi hatuna
tatizo lolote .Ukiamua kumpoteza vile
vile hatuna tatizo na hilo kwa hiyo
msikilize kwa umakini na utafanya
maamuzi wewe mwenyewe.”
Akasema Austin.Marcelo akainamisha
kichwa kwa muda akawaza na
kusema
“ Austin wewe ni kiongozi
wangu hapa na chochote
utakachonielekeza
nitakitii.Nitazungumza naye na
nitatoa msimamo wangu baada ya
kusikia hicho anachotaka kunieleza.”
Akasema Marcelo kisha akaongozana
na Amarachi wakaelekea ghorofani
kwa ajili ya kuwahudumia akina Boaz
majeraha yao.
“ Ni nani hawa wanaotaka
kumuua Job? Wamefahamuje kama
job yuko pale hospitali? Mtu pekee
tuliyemtaarifu kama Job yuko
hospitalki ni rais sasa hawa jamaa
wamefahamu vipi kama Job yuko
pale? Hii inashangaza sana.Kama
waliweza kumfuata hadi hospitali
kuna uwezekano mkubwa
wakamfuata hadi hapa
nyumbani.Kuna ulazima wa
kuimarisha ulinzi eneo hili” akawaza
Austin akiwa amesimama pembeni ya
kitanda alicholazwa Job,akamtazama
kwa makini na kusema
“ Please Job wake up and tell us
what real happened out th….” Austin
akakatisha mawazo yake baada ya Job
kuchezesha kichwa halafu akafumbua
macho
“ Job !! Job !! akaita Austin kwa
furaha.Job akajitahidi kutaka
kunyanyuka Austin akamzuia.
“ Pumzika Job.Usinyanyuke
tafadhali”
Job akazungusha macho
kutazama huku na huku
“Where am I? akauliza
“ Uko hapa nyumbani kwako”
akasema Austin .Baada ya muda Job
akasema
“ Mukasha …Mukasha.”
“ Job endelea kwanza kupumzika
hadi hapo utakapopata nguvu kisha
utatueleza nini kilitokea” akasema
Austin
“ Austin find him!! Find
Mukasha..” akasema Job kwa sauti
dhaifu.Austin akamtazama na kusema
“ Kitu gani kilitokea Job.Can you
tell me? Akauliza Austin
Job akamtaka asogee karibu
akamnong’oneza kitu sikioni
“ Thank you Job.Kwa sasa
endelea kupumzika.Niachie suala hili
nilishughulikie” akasema Austin na
kuwafuata akina Marcelo ghorofani
akawakuta katika chumba cha Maria
“ Mambo yanakwendaje hapa?
Akauliza
“ Ninamalizia kumtibu
Maria.Baba yake tayari “ akasema
Marcelo na Maria akastuka sana
“ My father is here? Akauliza
kwa mshangao
“Yes,he’s here too.You family is
complete” akasema Amarachi huku
akitabasamu
“ You are so cruel you devils!!
Austin please don’t do anything to my
father!! Akapiga ukelele Maria.
“I’m done” akasema Marcelo
baada ya kumaliza kumfunga Maria
majeraha
“ Good.Job is awake” Austin
akawaambia
“ Real ?! akauliza Amarachi kwa
furaha.
“ Marcelo nenda kamtazame
Job,Amarachi I need to talk to you”
akasema Austin
“ What is it Austin? Akauliza
Amarachi walipotoka nje ya kile
chumba
“ Kuna jambo amenieleza Job”
“ Can he talk? Akauliza
Amarachi
“ Yes he can” akajibu Austin
“ Amenieleza kwamba jana
alifanikiwa kumpata Mukasha na
akamtaka amueleze alipo mkewe na
mwanae.Alimkata sikio moja na ndipo
alipomueleza kwamba mtu ambaye
alikuwa anaamini kuwa ndiye
aliyemtorosha mkewe na mtoto yaani
dogo Bill si yeye bali kuna mtu
mwingine mkubwa ambaye hata yeye
hamfahamu anayefahamika kwa jina
moja tu la Don.Ni dogo Bill pekee
anayemfahamu mtu huyo na huyo
ndiye anayefahamu mke wa Job na
mwanae waliko.Job anadai kwamba
walikwenda katika klabu moja kwa
ajili ya kuonana na Dogo Bill na huko
ndiko alikovamiwa na walinzi
anaoamini ni wa Bill wakampiga hadi
alipopoteza fahamu na kuzinduka
mchana huu” akasema Austin
“ Hata hivyo suala hili tutaliweka
kwanza pembeni na tutalishughulikia
pale tutakapokuwa tumekamilisha
masuala yetu makubwa ya
msingi.Kuna mambo kadhaa
yanatukabili kama kupambana na
Alberto’s,kumtafuta Yasmin na kwa
uchache wetu huu hatuwezi kujigawa
katika mambo hayo yote kwa hiyo
tutaliweka pembeni suala hili la Job
.Hata hivyo nitazungumza na rais na
kumfahamisha kuhusu maendeleo ya
Job na kumuomba atusaidie
kumdhibiti Mukasha hadi pale
tutakapomuhitaji” akasema Austin
akachukua simu na kumpigia rais
“ Hallo Austin.Unaendeleaje?
akasema rais baada ya kupokea simu
“ Naendelea vizuri mzee”
“ Good.Kuna taarifa yoyote
mpya? Akauliza rais
“ Ndiyo mzee.Nimekupigia
kukufahamisha kwamba Job
amezinduka mchana huu na
anaendelea vizuri.Tumemuondoa
hospitali baada ya kugundua kwamba
kuna watu walikuwa wanamfuatilia
ambao hatufahamu lengo lao lilikuwa
nini.Tuko naye hapa nyumbani .”
“ That’s good news” akasema
rais
“ Kuna mambo amenieleza
ambayo alielezwa na Mukasha.Katika
mtandao wa akina Mukasha kuna mtu
ambaye anajulikana kwa jina moja tu
la Don ambaye anayemfahamu ni mtu
mmoja tu dogo Bill.Inasemekana mtu
huyo ndiye anayefahamu waliko mke
na mtoto wa Job.Hata hivyo
tutalishughulikia suala hilo baada ya
kukamilisha operesheni zetu
tulizonazo.Lakini mara
tutakapokamilisha operesheni zetu za
kuisafisha nchi tutaanza kuuchimba
mtandao wa akina Mukasha na hadi
tutampata huyo Don .Tunachokiomba
mheshmiwa rais tusaidie kumdhibiti
dogo Bill weka vijana wamfuatilie ili
asije akatoroka na kwenda nje ya
nchi.Huyo ndiye njia ya kutufikisha
aliko Don” akasema Austin na ukimya
ukatanda
“Mheshimiwa rais” akaita Austin
“ Uhmm !! Austin nimekusikia
na kukuelewa.Nitayafanyia kazi hayo
uliyonieleza”
“ Ahsante mzee.Vipi kuhusu
Yasmin tayari umepata taarifa zake
zozote?
“ Mpaka sasa bado sijapata
chochote kuhusiana na huyo Yasmin
.Vyombo vyangu vinaendelea na
uchunguzi na pindi nikipata chochote
nitakujulisha mara moja.” Akasema
rais wakaagana akakata simu na
kuvuta pumzi ndefu
“ Sitakiwi kabisa kulipuuzia
suala hili.Mukasha amekwisha wapa
mwanga akina Austin na sasa tayari
wanafahamu kuhusu Don na
hawatalala usingizi hadi wahakikishe
wamemtia mikononi.I wont let them
find out who that Don is.Wakifahamu
kama huyo Don ni mimi utakuwa ni
mwisho wangu.Yule kijana Job
ambaye ameishi kama mwenda
wazimu kwa miaka kadhaa
atanitafuna nyama.Natakiwa
kuwadhibiti kuanzia sasa ili wasifike
huko wanakotaka kufika na njia pekee
ya kuwadhibiti ni kuwanyamazisha
wote na hata Bill naye natakiwa
kumuondoa kwani ni yeye pekee
anayenifahamu.Endapo wakimpata
Bill watamtesa sana kama
walivyomtesa Mukasha na atatoa
siri.Huyu Bill naweza kumjumuisha
katika hoteli ile wakatayokuwemo
Alberto’s kesho ili naye awe ni mmoja
wa watakaokufa.Nitampigia simu na
kumtaka tukutane pale .Hawa vijana
akina Austin nasubiri kwanza
wanikabidhi majibu ya kipimo kile
cha vinasaba baada ya hapo
nitawafutilia mbali.” Akawaza na
mara sura ya mwanamke mmoja
ikamjia kichwani akatabasamu
“ Nampenda sana Monalisa na
siwezi kumuacha.Bill alifanya kosa
kubwa kumuacha Job hai akidhani
kweli ni kichaa kumbe alikuwa
anaigiza na sasa ameibuka na kuwa
tishio kwetu na kama hatadhibitiwa
haraka anaweza kusababisha madhara
makubwa.” Akawaza na kuchukua
simu akazitafuta namba fulani
akapiga
“ Hallow my love” ikasema sauti
nzuri laini ya mwanamke upande wa
pili
“ Monalisa my angel,vipi hali
yako? Sijakujulia hali kwa siku kama
mbili hivi kutokana na mambo mazito
yanayonikabili kwa sasa.Natumai
umesikia kinachoendelea hivi sasa”
akasema rais Ernest
“Pole sana mpenzi.Nafahamu
mambo yanayoendelea hivi sasa na
ndiyo maana hata mimi nimekaa
kimya nisikusumbue hadi
utakapomaliza kuweka sawa mambo
hayo.Vipi maendeleo yako?
“ C’mon Mona hutakiwi kukaa
kimya malaika wangu.Nakuhitaji sana
hasa katika kipindi kama hiki.Wewe
ndiye mfariji wangu na kila kitu
changu” akasema rais
“ Nafurahi kusikia hivyo.Mambo
yanakwendaje lakini?
“ Mambo yanakwenda vizuri na
ninashukuru ninakabiliana vilivyo na
kila changamoyo ninayokutana
nayo.Mona nimekupigia kukutaarifu
jambo moja.Kwa kuwa Millen
anakaribia kufunga shule nataka
muende mapumzikoni ulaya.Mtakaa
huko kwa muda wa mwezi mzima na
mtakaporejea hapa mtakuta tayari
mambo yametulia na tutaendelea na
maisha yetu kama kawaida na safari
hii nitawahamishia Dar es salaam
kwani hakutakuwa na kikwazo tena”
akasema rais
“ Really my love? Akauliza
Monalisa kwa furaha
“ Kweli kabisa
Mona.Ningetamani sana kama
ningeungana nanyi katika mapumziko
hayo lakini kutokana na mambo
yanayoendelea hapa nchini kwa sasa
sintaweza kuungana nanyi.Nataka
mkazunguke katika nchi mbalimbali
duniani kwa mwezi mzima.”
“ Sijui nikushukuruje mpenzi
wangu kwa namna unavyotujali mimi
na mwanangu.Nimefurahi mno kwa
hili ulilonieleza .”
“ Mona ni wajibu wangu
kuhakikisha katika siku zote za
maisha yenu hapa duniani mnakuwa
na furaha.Ninawapenda sana zaidi ya
ninavyoweza kuwaeleza”
“ Ahsante sana mpenzi
wangu.Mungu akubariki sana”
“ Amina mpenzi wangu.Anza
kufanya maandalizi na siku chache
zijazo mtaondoka kwenda
ulaya.Nikipata nafasi usiku wa leo
nitakupigia tena simu” akasema rais
na kukata simu
“ Sauti ya Monaliza hupenya
ndani kabisa ya ubongo wangu na
hunifanya nijihisi kama vile niko
mbingu ya saba.Nitafanya kila lililo
ndani ya uwezo wangu kuhakikisha
kwamba hakuna atakaye vuruga
uhusiano wangu na Mona.Ni
mwanamke niliyempenda mara tu
nilipomtia machoni kwa mara ya
kwanza na nimetumia gharma kubwa
hadi kumpata kwa hiyo siko tayari
mtu yeyote amuondoe katika himaya
yangu” akawaza Ernest
SEHEMU YA 11: SEASON 5
Zaidi ya saa mbili ,Marcelo
alitumia kwa maongezi na dada yake
.Wakiwa sebuleni Austin na Amarachi
wakawashuhudia Marcelo na Julieth
wakishuka ngani wakiwa
wameshikana mikono
“ Amarachi na Austin ,napenda
kuwataarifu kwamba nimezungumza
na Julieth kwa takribani saa mbili na
amenieleza mambo mengi.Mambo
aliyonieleza yanasikitisha sana lakini
amekiri kosa alilofanyana na kulijutia
.Kuna mambo ya kifamilia
amenieleza ambayo sikuwa
nikiyafahamu .Baada ya kusikia hayo
yote,toka ndani kabisa mwa moyo
wangu nimeamua kumsamehe dada
yangu na tunakwenda kufungua
ukurasa mpya.Ameniahidi kuachana
na biashara zote haramu na badala
yake tutashirikiana kuendeleza mali
na miradi aliyoiacha baba.Kwa hiyo
ndugu zangu kama mimi
nilivyomsamehe dada yangu
nawaomba nanyi pia mumsamehe
kwa yale yote aliyokosa” akasema
Marcelo .Austin na Amarachi
wakatazamana
“ Marcelo” akasema Austin
“ Kama nilivyokueleza awali
kwamba hatima ya ndugu yako iko
juu yako na kwa vile umeamua wewe
mwenyewe kwa hiari yako
kumsamehe Julieth sisi hatuna neno
.Binafsi ninaamini sana katika nguvu
ya msamaha kwa hiyo naamini Julieth
atakuwa mtu mpya baada ya kutoka
hapa.Kwa sasa ataendelea kukaa hapa
ndani hadi pale tutakaporidhika kuwa
kweli ameamua kubadilika ndipo
tutakapomuachia.Tumeelewana
Julieth?
“ Nimekuelewa Austin na
ahsante saba kwa kunisaidia
nimeweza kuonana na ndugu yangu
na kwa pamoja tumeanza ukurasa
mpya.Sikuwa nimelitegemea kabisa
jambo hili.Nakuahidi kuwa sintarejea
tena katika njia zangu ovu” akasema
Julieth
“ Good.Marcelo show her the
kitchen.She’ll be cooking for us.Wewe
una majukumu makubwa ya kutunza
afya zetu hapa ndani” akasema
Austin
SEHEMU YA 12: SEASON 5
Tayari Job alikuwa na nguvu na
aliweza kuzungumza vizuri japokuwa
mdomo wake ulikuwa
umevimba.Ilikaribia saa kumi na mbili
za jioni na alikuwa tayari kuwaeleza
akina Austin kile kilichotokea usiku
uliopita
“ Usiku wa jana” akasema Job
“ Wakati nikiendelea kukipekua
kitabu kile chenye orodha ya wauza
dawa za kulevya ,simu ya Boaz ikaita
alikuwa ni Mukasha.Nilipandwa na
hasira nikamkumbuka mwanangu
ikanilazimu kuwasiliana
naye.Nikamtumia ujumbe kwa
kutumia simu ya Boaz nikamtaka
tuonane akanielekeza sehemu ya
kukutana nikaenda.Nilipofika mahala
hapo nikamtumia ujumbe mwingine
kwamba nimeahirisha hadi siku
nyingine.Aliamini kwamba alikuwa
anawasiliana na Boaz.Baada ya muda
nikamuona Mukasha akitoka hotelini
na kueleka katika gari lake akaingia na
kuondoka nikaanza
kumfuatilia.Alifuata barabara ya
Bahari drive ambayo kwa usiku huu
haikuwa na magari mengi”
akanyamaza kidogo na kuendelea
“ Ghafla gari la Mukasha
likaanza kuyumba ,likatoka nje ya
barabara na ilibaki kidogo litumbukie
katika mtaro.Nilishuka haraka katika
gari na kulifuata gari la Mukasha
nikachungulia ndani na kuona kuna
mtu anapambana na
Mukasha.Nikafanya haraka nikavunja
kioo na kumdhibiti yule jamaa halafu
nikamuamuru aondoke zake kwani
lengo langu mimi lilikuwa ni kumpata
Mukasha.Niliondoka na Mukasha na
kuja naye hapa nyumbani nikamuhoji
na kumtaka anieleze kuhusiana na
mtandao wake na alipo mwanangu
Millen.Mukasha hakuwa tayari
kunieleza na ndipo nilipomuondoa
sikio moja na akaamua kunieleza kila
kitu” akanyamaza tena kidogo kisha
akaendelea
“ Mukasha alinieleza kwamba
dogo Bill si mkubwa wa mtandao wao
kama nilivyokuwa nadhani bali kuna
mtu anaitwa Don ambaye ndiye
mkubwa.Anayemfahamu huyo Don ni
dogo Bill peke yake.Huyo Don ndiye
ambaye yuko na mke wngu na mtoto
kwa sasa.Dogo Bill alitumika kama
mshenga tu wa Don.Ili kumpata Don
natakiwa kumpata kwanza Bill na
Mukasha akasema yuko tayari
kunipeleka mahali aliko
Bil.Tukaelekea huko na mara
tulipofika katika klabu moja Mukasha
akashuka garini na kupiga ukelele na
ghafla nikajikuta nimezungukwa na
watu zaidi ya ishirini wenye
silaha.Nilijitahidi kadiri ya uweo
wangu kupambana na watu wale
lakini nikazidiwa nguvu nikapoteza
fahamu hadi nilipofumbua machgo na
kujikuta niko hapa ndani.Ahsanteni
sana kwa juhudi zenu mlizofanya
kuniokoa.Hivyo ndivyo ilivyotokea
jana usiku” akasema Job.Austin
akamtazama kwa makini na kusema
“ Job wewe ni mmoja wa watu
ninayekuamini sana na hata kama
nitakufa leo ninaamini wewe
utayaongoza mapambano haya lakini
kwa kitendo ulichokifanya jana usiku
naweza kusema kwamba ninaanza
kufikiria mara mbili uamuzi wangu
wa kukushrikisha katika operesheni
hii.How could you do such a stupid
thing? Ni vipi endapo wangekuua
hawa jamaa? Unafahamu kabisa kuwa
hawa watu ni hatari na wamejizatiti
vilivyo kwa nini ukaamua kwenda
kupambana nao peke yako? Why Job
?? akauliza Austin aliyeonekana
kukasirishwa na kitendo kile cha Job
“I’m sorry Austin.I wasn’t
thinking clearly” akasema Job
“ Sorry isn’t enough.Nawezaje
kukuamini tena endapo haufikiri sawa
sawa? Job you are a proffesional agent
but what you did,makes me think you
are not that Job I know” akasema
Austin
“Austin I’ve said I’m sorry.I did a
mistake .What do you want me to say?
Kichwa changu kinataka kupasuka
nikimuwaza mwanangu Millen.Hata
ugekuwa wewe mahala pangu
ungefanya kama nilivyofanya “
akasema Job
“Nisingefanya ujinga kama
ulioufanya.Nilikuahidi tutapambana
pamoja kuhakikisha tunampata
mwanao .Watu hawa si watu wa
kufanyia mchezo.Ni watu waliojizatiti
sana.Kwa hiki ulichokifanya tayari
umekwisha wastua na itakuwa vita
ngumu sana kati yetu na
wao.Mukasha atawapelekea taarifa
kuwa tunawatafuta na hivyo
watajizatiti zaidi au hata kutoweka
kabisa” akasema Austin
“ Austin I’m sorry.Najua
nimefanya kosa kubwa na
ninakuahidi sintorudia tena kosa la
namna hii.Ninachoomba baada ya
operesheni fagio kumalizika unisaidie
niweze kumpata tena mwanangu
Millen.Naomba sana Austin” akasema
Job
“Ni vyema umegundua kosa lako
na ninaomba usirudie tena na hii si
kwa Job peke yake bali kwenu
wote.Amarachi na Marcelo pia.Sitaki
tena litokee jambo kama alilolifanya
Job.Ni afadhali nikafanya kazi peke
yangu kuliko kuwa na timu ya watu
wasiofikiri sawasawa.You understand
me all? Akauliza Austin
“ Yes we do “ Amarachi na
Marcelo wakajibu
“ Good.Sasa inabidi kujipanga
upya namna ya kuwakabili hawa
jamaa lakini kwanza tuendelee na kazi
iliyoko mezani hivi sasa” akasema
Austin
“ Kabla ya kuendelea kuna jambo
moja ambalo ni vyema
nikawafahamisha” akasema Job
“ Niliwaeleza kwamba kuna mtu
aliyekuwa anapambana na Mukasha
ndani ya gari .Alikuwa amevaa kofia
ya kuficha sura yake.Nilipomdhibiti
nikamwambia Mukasha amvue kofia
na akamtambua kuwa anaitwa
Evans.Baadae akaniambia kwamba
yule ni mlinzi wa rais na anashangaa
kwa nini akamvamia na kutaka
kumdhuru”
“Evans? Austin akashangaa
“Evans ni mlinzi wa rais
anayemuamini sana.Nimeshangaa
kusikia kwamba ndiye aliyemvamia
Mukasha.Kwa nini alifanya hivyo?
Akauliza Austin
“ Hata Mukasha mwenyewe
alishangaa sana na hakuamini”
akasema Job
“Evans hawezi kuwa alitumwa
kumshambulia Mukasha? Amarachi
akauliza
“Hilo linawezekana na je kama
kweli ametumwa ni nani aliyemtuma
na kwa nini? Akauliza Austin ukimya
ukapita Austin akasema
“ Nakumbuka rais aliponitamkia
kwamba anataka kumteua Mukasha
kuwa waziri mkuu,Evans alikuwepo
pia na alionyesha kustuka sana .Nahisi
labda wawili hawa wana mambo yao
binafsi .Nadhani rais anapaswa
kulifahamu hili” akasema Austin na
kuchukua simu akampigia rais
“ Hallo Austin” akasema rais
“ Mzee,samahani kwa
usumbufu,jioni hii ila kuna jambo
nataka nikufahamishe.Kwanza
kuhusu Job anaendelea vyema na
tayari ametueleza kila kitu
kilichotokea jana” akasema Austin
“ Nafurahi k usikia hivyo Austin
lakini ndani ya dakika chache zijazo
nategemea kupokea simu ya muhimu
sana kwa hiyo naomba twende haraka
kidogo.” Akasema rais
“ Sawa mzee.Ni kwamba jana
tukiwa katika chakula Job aliamua
kumtafuta Mukasha akampata lakini
kabla hajampata lililotokea tukio
moja.Mukasha alivamiwa na mtu
aliyejificha ndani ya gari yake na Job
akafanikiwa kumdhibiti mtu
huyo.Baada ya kumvua kofia
aliyokuwa ameitumia kujificha uso
Mukasha akamtambua mtu huyo
kuwa ni Evans mlinzi wako”
“ Evans? Rais akashangaa
“ Ndiyo mzee.Unafahamu
chochote kuhusu hilo? Mukasha
amekueleza chochote?
“ Hapana sifahamu chochote
hadi sasa.Nipe muda nilifuatilie suala
hili kisha nitakupa jibu.Nitawasiliana
nawe baadae Austin” akasema rais na
kukata simu.
“ This is strange.Rais anadai
hafahamu chochote hadi sasa
kuhusiana na Evans kumvamia
Mukasha.Ina maana hadi sasa
hafahamu kilichomtokea Mukasha?
Inawezekanaje Mukasha
asimfahamishe kuhusu kuvamiwa na
Evans?Kingine kinachoshangaza rais
hajataka maelezo mengi kuhusu
jambo hili kwa nini? Akauliza Austin
“ Tuachane na hilo
tutalishughulikia baadae kilichopo
mezani kwa sasa ni kumpata Yasmin
Esfahani.Rais hajatoa jibu lolote kama
amefanikiwa kumpata au bado”
akasema Austin
“ Yasmin Esfahani? Akauliza Job
“ Ndiyo .Leo tumemuhoji Maria
,kwanza akafungua kompyuta yake
ambamo tumekuta mawasiliano ya
barua pepe kati yake na mtu mmoja
anaitwa Bin Omar .Baada ya kumuhoji
amekataa kusema chochote na
ikatulazimu kufanya makubaliano
naye na ametutaka tumtafute mama
yake anaitwa Yasmin Esfahani
aliyefungwa hapa Tanzania mahala pa
siri kwa zaidi ya miaka kumi
sasa.Nimezungumza na rais kama
anataarifa zozote kuhusiana na
Yasmin lakini rais amesema kwamba
hafahamu chochote.Alinitaka nimpe
muda alifanyie kazi suala hili na
atanipa jibu.Mpaka sasa hajasema
chochote.Kuna jambo Maria analo na
hawezi kutueleza hadi tutakapompata
mama yake.Hiyo ndiyo kazi iliyoko
mezani kwa sasa wakati tukisubiri
majibu ya kipimo cha vinasaba.”
Akasema Austin
“ Wakati ninafanya kazi katika
idara ya ujasusi ya taifa niliwahi
kulisikia jina hilo likitajwa.Huyo
mwanamke ni gaidi hatari kabisa
ambaye yuko katika mtandao wa
kigaidi wa IS.Niliwahi kusikia
kwamba ameonekana Tanzania na
tetesi za chini chini zilizozipata ni
kwamba alitakiwa kukamatwa ingawa
jambo hili lilikuwa la siri kubwa
sana.” Akasema Job
“ Kama idara ya ujasusi ilikuwa
na taarifa za Yasmin na kukawa na
mipango ya kumkamata ,basi lazima
yuko hapa hapa nchini amefungwa
mahala kama alivyosema
Maria.Nimestuka sana kusikia
kwamba Yasmin ni gaidi toka IS.Kama
ni hivyo nalazimika kuamini kwamba
hata Maria au Shamin kama
anavyoitwa atakuwa mfuasi wa IS pia
.Ninaamini hivyo kutokana na wepesi
wake wa kutumia silaha na nilijiuliza
maswali mengi amejifunzia wapi
mambo haya ya silaha? Sasa nimepata
jibu.Ni wazi Maria ni mfuasi wa IS.Ili
kulithibitisha hilo tunapaswa
kuyachimba maisha yake toka akiwa
mdogo,sehemu alizotembelea ,mahala
alikosoma na hata safari zake nyingi
huwa anaelekea wapi?” akasema
Austin na kushika kichwa
“ Kwa nini nilikuwa mjinga kiasi
hiki na kushindwa kutambua Maria ni
mtu hatari namna hii? Austin
akasikitika.
“ Austin hata mimi nakubaliana
nawe kwamba huyu Maria anaweza
kuwa mfuasi wa siri wa IS na kama ni
hivyo basi kuna vita kubwa itaibuka
kati yetu na wao.Tunachopaswa
kukifanya ni kuliendea suala hili
taratibu.Tuhakikshe kwanza
tunampata huyo Yasmin na kisha
Maria atueleze hicho anachotaka
kutueleza” akashauri Job
“ Rais ameahidi kunipigia simu
baadae.Nitaongea naye kwa kirefu
zaidi suala hili hata hivyo naomba
niwe wazi kwenu kwamba
tunakoelekea mambo yanazidi kuwa
magumu zaidi kwa hiyo nahitaji nyote
mjiandae kimwili na kiakili kwa
mapambano makali yanayokuja mbele
yetu.Siwaogopeshi bali hiyo ndiyo
hali halisi lazima tujiandae.It’s going
to be tough than we think” akasema
Austin
 
SEHEM YA 10

akaingia garini na kuondoka kuelekea
nyumbani kwake
“ Kumbe hadi mama tayari
amegundua kuhusu tabia chafu za
Daniel.Natakiwa kuanza kukaa naye mbali
ili asije haribu sifa yangu.Ukaribu wetu
unaweza kuzua maswali mengi kwa jamii
na wakadhani labda tuna mahusiano
.Natakiwa haraka sana kupunguza mazoea
naye “ akawaza Monica akiwa garini
kurejea nyumbani kwake.
Alifika nyumbani kwake na
kuwajulia hali watumishi wake wote na
kisha akaingia chumbani kwake akaoga na
kujitupa kitandani.Kichwa chake kilijaa
mawazo
“ Jambo aliloliongea mama ni jambo
la msingi sana.Ni wakati sasa wa mimi
kumtafuta mwanaume wa maisha
yangu.Umri unakwenda kwa kasi na
wakati wa kumpata mwanaume wa ndoto
zangu ni sasa.Nimezungukwa na wanaume
wengi wazuri wenye sifa na tabia nzuri
lakini si kazi nyepesi kujua ni yupi
anayeweza kunifaa.Umakini mkubwa sana
unahitajika katika hili.” Akawaza Monica
halafu sura ya Dr Marcelo ikamjia
akatabasamu
“ Dr Marcelo ni kijana mpole
mtanashati na mpenda watu.Katika
wanaume wote niliokutana nao na
walionizunguka yeye namuona yuko
tofauti sana.Nilimtazama machoni wakati
tukiongea pale ofisini kwangu nikagundua
kitu katika macho yake kwa namna
alivyokuwa ananitazama. Jicho lile
linanipa picha Fulani kwani mimi si mtoto
mdogo kufahamu mtu ambaye anahitaji
kitu Fulani toka kwangu.Siwezi pia
kuudanganya moyo wangu lakini kwa
kweli lazima nikiri kuwa hata mimi
nilihisi moyo wangu umestuka sana pale
nilipomuona .Kwa kweli amenigusa sana
moyoni na kuna kila dalili kwamba kuna
kitu kinazunguka kati yetu.Hata hivyo
sipaswi kuwa na haraka sana
ninachotakiwa kukifanya kwa sasa ni
kumchunguza Marcelo ni mtu wa aina gani
,ana tabia gani na kama anaweza kunifaa
kwani kuna kila dalili kwamba ameugusa
moyo wangu” akawaza Monica akainuka
na kukaa
“ Tena itakuwa vizuri kama
nitamualika
katika
sherehe
niliyoandaliwa nyumbani kesho.Nikiwa
naye karibu nitaweza kumfahamu vizuri
sana ni mtu wa aina gani “ Monica
akatabasamu kidogo
“ That’s a good I dea.Natakiwa
kumualika Dr Marcelo katika sherehe ya
kesho nyumbani kwetu.Lakini tatizo ni je
amekwisha oa? Kama ana mke lazima
ataambatana naye na mimi ninahitaji awe
peke yake ili nipate nafasi nzuri ya
kumfahamu.” Akawaza Monica
“ Inawezekana kweli Dr Marcelo
akawa ana mke? Nakumbuka sikuona pete
ya ndoa katika kidole chake lakini hata
hivyo kuna njia moja tu ya kufahamu
kama ameoa ama vipi.Natakiwa kumtumia
ujumbe wa kumualika katika sherehe ya
kesho aje na mke wake.Kama hatakuwa na
mke atanijulisha.” Akawaza Monica na
kuchukua simu yake akamuandikia
ujumbe wa mualiko Dr Marcelo na
kumtumia .Baada ya kama dakika tatu hivi
toka autume ujumbe ule ukaingia ujumbe
katika simu yake uliotoka kwa Dr Marcelo
akaufungua haraka haraka.
“ Monica ahsante sana kwa
mwaliko.Nitafika bila kukosa” ndivyo
ulivyosomeka ujumbe toka kwa Dr
Marcelo.Baada ya kuusoma Monica
akatabasamu na kuandika tena ujumbe
mwingine
“ Usisahau kuja na wifi yangu”
Baada ya dakika moja ukaingia
ujumbe
“ Wifi yako hayupo niko mwenyewe
bado sijaingia katika daraja la ndoa”
“ Wow !! Kumbe bado hajaoa.”
Akawaza
Monica
huku
akitabasamu.Akaandika tena ujumbe
mwingine
“ I hope utakuwa tayari na mchumba
naomba uje naye.Itapendeza sana kama
ukiongozana naye”
Baada ya sekunde kadhaa ukaingia
ujumbe toka kwa Marcelo
“ Bado sina mchumba,siko katika
mahusiano yoyote ya kimapenzi kwa sasa”
“ Mhh !! hiki anachokisema Dr
Marcelo ni cha kweli? Inawezekanaje
akakosa mke au hata asiwe katika
mahusiano yoyote? Ni nadra sana
kukutana na kijana mzuri kama Yule
halafu akawa hana mchumba wala
mahusiano.Kuna haja ya kumchunguza na
kumfahamu Dr Marcelo kwa undani kama
ni kweli anachokisema basi lazima
atakuwa na tatizo..” akawaza Monica na
kuandika ujumbe mwingine wa kumjibu
“ Ahsante kwa kukubali mwaliko
wangu.Tafadhali ufike bila kukosa.Usiku
mwema” akautuma na baada ya muda
ukaingia ujumbe mwingine toka kwa
Marcelo
“ Ahsante nashukuru .Usiku mwema
nawe”
“ Dah !! kuna kitu ninahisi cha tofauti
sana kila ninapowaza kuhusu Dr
Marcelo.Kesho nitamfahamu vizuri zaidi”
akawaza Monica na kuzima simu zake
akalala
 
SEASON 6: SEHEMU YA 15
Imetimu saa nane za
usiku,bado rais alikuwa katika
kikao na wakuu wa vyombo
mbalimbali vya ulinzi na
usalama wakijadiliana kile
kilichotokea ,hatua za kuchukua
na vile vile waliendelea kupokea
taarifa kutoka kwa vikosi
vilivyoendelea na kazi ya
kufukua vifusi katika majengo
yaliyolipuliwa kutafuta maiti na
watu walionusurika .Mjini
Dodoma mpaka kufikia muda
huyo tayari jumla ya maiti 346
zilikuwa zimepatikana na zoezi
liliendelea kutafuta maiti
wengine kama wapo.Jijini Dar es
salaam maiti zaidi ya mia tatu
zilikuwa zimepatika.Katika
ukumbi uliokuwa wa mikutano
maiti zaidi ya maiti mia mbili
zilipatikana na nyingi zikiwa
zimeharibika vibaya sana kiasi
cha kushindwa kutambulika.
Mjadala mkubwa uliokuwa
ukiendelea katika kikao kile ni
hatua za kuchukua baada ya
Alshabaab kujitangaza kuwa
walihusika na shambulio
lile.Kulikuwa na mabishano
ambapo baadhi ya wajumbe
walitaka uchunguzi wa kina
ufanyike kabla ya kuchukua
hatua zozote.Wengine walitaka
hatua za haraka sana
zichukuliwe dhidi ya wale
waliotekeleza shambulio lile
baya.Mvutano ulikuwa mkali
sana ndani ya kikao kile.Mkuu
wa majeshi akasimamana
kuwatuliza wajumbe waliokuwa
wakivutana kisha akasema
“Mheshimiwa rais,mimi
kama mkuu wa majeshi nina
haya ya
kusema.Tumeshambuliwa.Adui
aliyetushambulia anafahamika
na tayari amejitokeza hadharani
akakiri kuhusika na unyama
huu mkubwa uliotokea na kama
haitoshi bado anaendelea kutoa
vitisho vya mashambulio zaidi
iwapo hatutakuwa tayari
kutekeleza matakwa yake.Mimi
kama mkuu wa majeshi
napendekeza kwamba
tusikubaliane na matakwa yake
kwani huo ni ushindi kwake.Sisi
ni nchi yenye nguvu,sisi
tunajeshi kubwa lenye nguvu na
linaloogopeka afrika kwa nini
tusumbuliwe na kikundi kidogo
kama Alshabaab? Hatuwezi
kukulbali hilo.Kwa kuwa
Alshabaab wametangaza vita
kazi yetu ni kuwaonyesha sisi ni
nani.Dunia inapaswa kutambua
kwamba Tanzania ni nchi ya
amani lakini ikichokozwa kipigo
chake hakina
mfano.Tuwaonyeshe kazi hawa
Alshabaab” akasema Jenerali
Lameck Msuba.Watu wote mle
ndani ya chumba wakabaki
kimya wakisubiri maamuzi ya
rais.
“ Ndugu wajumbe
,nimeyasikia mawazo yenu
kuhusiana na jambo hili na
kama alivyosema Jenerali
Lameck kwamba hiki
kilichofanywa na Alshabaab ni
tangazo la vita.Sisi kama taifa
hatutaweza kukubaliana na
uchokozi huu na ninakubaliana
na mkuu wa majeshi kwamba
hakuna muda wa kupoteza
kufanya uchunguzi wakati tayari
adui tunamfahamu na
anatamba.Mimi kama rais natoa
ruhusa ya kuwaonyesha kazi
hawa mashetani.Nataka mpaka
kutakapopambazuka tayari niwe
nimesikia jeshi letu limeanza
kuwafundisha adabu
maharamia hawa.Hatuwezi
kuishi kwa wasiwasi na kikundi
kidogo kama hiki.Mkuu wa
majeshi kaa na makamanda
wako na mpange namna ya
kuanza kuwafunza adabu hawa
jamaa lakini kabla ya kufanya
shambulio lolote naomba
kwanza nijulishwe.” Akasema
rais kisha akainuka akatoka mle
ndani ya chumba akatoa simu
na kuzitafuta namba za Habib
akampigia
“ Mheshimiwa rais,kuna
taarifa nzuri unataka kunipa?
Akauliza Habib baada ya
kupokea simu
“ Habib kuna jambo nataka
kukutaarifu.Kwanza kuna
taarifa za kutia moyo kuhusiana
na mahala aliko Yasmin.Kuna
kila dalili kwamba anaweza
akapatikana hadi kufikia
asubuhi.Jambo la pili nataka
kukujulisha kwamba kwa saa
kadhaa sasa nimekuwa na kikao
na wakuu wa vyombo vya
usalama na kufuatia lile tamko
lako kuwa Alshabaab ndio
wanaohusika katika
mashambulio yale mawili,kikao
kimeamua kwamba yafanyike
mashambulio katika kambi za
Alshabaab .Nimeona nikujulishe
hilo ili uwataarifu watu wako
wote watoke katika kambi hizo
zitakazoshambuliwa” akasema
rais
“Mnataka kutushambulia?
Mnataka kuharibu kambi zetu
na kuua watu wetu? Akauliza
Habib kwa mshangao
“ Habib lengo la kufanya
hivyo ni kuzuia kutokufanyika
kwa uchunguzi wowote
kuhusiana na mashambulio
yaliyotokea na ndiyo maana
nimeamua kukupigia ili
kushauriana nawe kuhusu
jambo hili.Nakuahidi kwamba
nitagharamia mimi mwenyewe
ujenzi wa kambi hizo baada ya
kuharibiwa.Nitatoa fedha nyingi
katika suala hili.Naomba
tukubaliane katika hilo Habib”
akasema rais na wakajadiliana
na Habib kwa muda wa zaidi ya
dakika kumi kisha wakaagana
kisha akampigia simu Jenerali
Lameck na kumtaka waonane.
“Nimezungumza na Habib
muda mfupi
uliopita.Nimemtaarifu kwamba
tunataka kufanya mashambulio
mawili katika kambi
zake.Haikuwa rahisi lakini
tumekubaliana na amenipa
namba za simu za mmoja wa
makamanda wake ambaye
mtawasiliana na atakupa
maelekezo yote.” Akasema
rais.Wakati akijadiliana na
Lameck simu yake
ikaita,zilikuwa ni namba ngeni
katika simu yake.Akasogea
pembeni na kuipokea
“Hallow”akasema
“Hallow Mr president”
ikasema sauti ya mwanamke
upande wa pili na Ernest
akastuka sana.Akatazama kama
kuna mtu yeyote pale karibu
yake kisha akauliza
“Nazungumza na nani?
Mwanamke Yule akatoa
kicheko kidogo kisha akasema
“Ni kweli umeisahau sauti
hii au umechanganyikiwa baada
ya kuisikia? Akauliza Yule
mwanamke
“ tell me who are you or I’ll
hang up !! akafoka rais
“ Fine .Yuu want to know
who I am? Its me Agatha your
wife”
Ernest akashusha
pumzi.Alikosa neno la kuongea
akabaki ameishikilia simu
sikioni
“ I’m not dead mr
President.I’m still alive.”
Akasema Agatha.Bado rais
aliendelea kukaa
kimya.Hakuamini kile
alichokisikia.
“Mr president samahani
kwa kukusumbua usiku huu
najua una mambo mengi
kuhusiana na shambulio
lililofanywa na
Alshabaab.Nitakupigia tena siku
nyingine kwa sasa nakuacha
umalize kwanza shughuli za
msiba huu mkubwa wa taifa.”
Rais akavuta pumzi ndefu
na kusema
“ Where are you?
“ Just wait for my call mr
president anytime soon”
akasema Agatha na kukata
simu.Ernest akachanganyikiwa.
MPENZI MSOMAJI
USIKOSE SEASON 7
ITAKAYOKUWA SEHEMU YA
MWISHO YA SIMULIZI HII ILI
UFAHAMU MWISHO
UTAKUAJE.

-
 
SEASON 7: SEHEMU YA 4

Inakaribia saa kumi na mbili
za asubuhi,Silvanus Kiwembe
mkuu wa idara ya usalama wa taifa
alipowasili ikulu kuonana na
rais.Walielekea katika chumba cha
maongezi ya faragha.
“ Silvanus nililazimika
kusitisha lile zoezi la kumtafuta
Yasmin kule Zanzibar baada ya
kupata taarifa zenye uhakika
kwamba Yasmin tayari yuko jijini
Dar es salaam.”
“ Amekuja Dar es salaam?!!
Akauliza Silva
“ Ndiyo yuko hapa Dar es
salaam”
“ Amewezaje kutoka
Zanzibar? Njia zote za kuingilia na
kutokea Zanzibar zilifungwa na
ulinzi ni mkali sana” akasema
Silva.
“ Silva kuna kitu ambacho
unatakiwa ukifahamu.Ninaye binti
yangu mmoja niliyempata enzi za
ujana wangu .Binti huyo ana
mahusiano ya karibu na kijana
mmoja anaitwa Austin January.”
“ Austin January?! Silva
akastuka
“ Ndiyo.Unamfahamu?
“ Hapana nimewahi kuzisikia
habari zake.Yuko hapa
nchini?akauliza Silva
“ Austin yuko hapa nchini”
akasema rais na kumtazama
Silvanus ambaye alionekana
kustushwa na taarifa zile za Austin
kuwapo Tanzania
“ Jana usiku nilipigiwa simu
na Monica ambaye ndiye
mwanangu akaniambia kwamba
amepata safari ya ghafla kwenda
Zanzibar kwa hiyo akaniomba
nimsaidie apate
usafiri.Nilishindwa kumkatalia
japokuwa kulikuwa na katazo la
kutoruhusu ndege yoyote kutua au
kupaa,ilinilazimu kutoa maelekezo
Monica apelekwe Zanzibar kwa
ndege maalum na kurudishwa
baada ya kumaliza shughuli
zake.Sikuishia hapo nikatoa na
vijana wawili wamlinde hadi
atakaporudi.Nilikupigia
nikakuomba uongeze vijana wawili
pia kule Zanzibar ili ulinzi wa
Monica uwe madhubuti lakini cha
kushangaza walinzi wote hawa
walikutwa katika magari yao
hawana fahamu.Hili ni jambo la
kushangaza sana.Bila ruhusa
yangu,jenerali lameck alitoa amri
Monica na wenzake waliokuwamo
katika ndege wakamatwe mara tu
watakapotua dar es salaam
wakitokea Zanzibar.Monica na
wenzake waligundua mtego
uliowekwa uwanja wa ndege ili
wakamtwe kwa hiyo ikawalazimu
kwenda kutua katika daraja la
Nyerere Kigamboni.Hili ni jambo la
hatari sana.Ilinilazimu kumuita
Monica hapa ikulu usiku huo huo
nikamuhoji na akanieleza ukweli
kwamba Austin ndiye aliyemfuata
nyumbani kwake akamtaka
anipigie simu na kuniomba usafiri
kwa kunidanganya kwamba
amepata dharura.Anasema
kwamba Austin alikuwa na
wenzake wawili na wakawapoteza
fahamu wale walinzi niliotoa
wamsindikize kisha wakawaficha
garini na kuelekea Zanzibar” Rais
akanyamaza na kupiga mwayo
ishara ya uchovu halafu akasema
“ Huwezi kuamini Silva lakini
ukweli ni kwamba Austin
alikwenda Zanzibar kumchukua
Yasmin Esfahani”
“ Austin amefahamu vipi
kuhusu Yasmin? Akauliza Silva
kwa mshangao
“ Hata mimi sijui Austin
amefahamuje kuhusu
Yasmin.Mpaka hivi sasa
tunavyoongea Austin na wenzake
wanaye Yasmin na sifahamu
wamemchukua kwa malengo
yapi.Kitu ambacho ninataka
ukifanye wewe na idara yako ya
usalama wa taifa ni kutumia kila
aina ya uwezo mlio nao kumtafuta
Austin.Tukimpata Austin
tutakuwa tumempata pia Yasmin”
akasema rais.Silva aliyekuwa
akisikilza kwa makini akauliza
“ Mheshimiwa rais kuna
jambo linanitatiza kidogo.Naomba
kufahamu kwa nini tunamtafuta
Yasmin wakati ulikuwa
umemuachia huru?
Ilimchukua rais sekunde
kadhaa za kutafakari kabla ya
kulijibu swali lile la Silva
“ It was a mistake.Kumuachia
huru Yasmin lilikuwa ni kosa
kubwa sana na ndiyo maana kwa
kila namna nataka Yasmin
apatikane na arudishwe kule
gerezani.”
“ Austin anaishi wapi? silva
akauliza
“ Kwa sasa hakuna
anayefahamu ni wapi anaishi
Austin lakini kuna mtu mmoja tu
ambaye anaweza akatusaidia
kumpata Austin.Huyu ni
Monica.Niliongea naye jana usiku
na kumuomba awasiliane na
Austin asubuhi na aombe kuonana
naye baada ya hapo anitaarifu ni
wapi watakutana ili tukamchukue
Austin.” Akasema rais
“ Mheshimwa rais hilo ni wazo
zuri lakini sina hakika kama
linaweza kutusaidia.Ni vipi iwapo
Monica hatampigia simu Austin?
Silva akauliza
“ Ndiyo maana nimekuita hapa
Silva ili na wewe unipe mchango
wa mawazo kwani kwa sasa
kichwa changu kimevurugwa
kabisa na sielewi nianzie wapi
niishie wapi.Please help me”
akasema rais
“ Nionavyo mimi wazo la
kumtumia Monica kumpata Austin
ni sahihi lakini si kwa kumuacha
Monica ampigie simu Austin.kama
ulivyosema kwamba wawili hawa
wana mahusiano ya karibu kuna
uwezekano Monica asiwasiliane na
Austin au amtaarifu kuwa
anatafutwa.Tunachotakiwa
kufanya ni kummulika Monica kila
mahala.Kudukua mawasiliano
yake,kufahamu kila mahala
anakokwenda .tukifanya hivyo
tutagundua kitu.” Akashauri
Silva.Rais akafikiri kwa muda
halafu akasema
“ Silva nakukabidhi jukumu
hilo ufanye unavyoona inafaa ili
mradi Monica asipate madhara
yoyote.”
“ Mzee kazi zetu tunazifanya
kitaalamu sana na sisi lengo letu ni
kumpata Austin pekee na si
Monica.”
“ Good.Ukiacha hilo kuna
suala lingine pia ambalo nataka
ulipe uzito mkubwa.” Akasema rais
akanyamaza kidogo
“ Ni kuhusu mke wangu
Agatha.Tuliamini kwamba
aliwemo katika hoteli ile
iliyolipuliwa lakini kwa bahati
nzuri hakuwemo katika hoteli
ile.Kwa hiyo mke wangu yuko hai”
akanyamaza tena na kuinamisha
kichwa akafikiri kidogo na kusema
“ Amenipigia simu jana usiku
akanitaarifu kwamba yuko hai
lakini hakutaka kunieleza mahala
aliko.Nataka ufanye uchunguzi
mkubwa kufahamu mahala alipo
mke wangu.Nilijaribu kumpigia
simu kwa namba zile alizotumia
kunipigia lakini nikaambiwa
kwamba namba zile si
sahihi.”akasema rais
“ Mzee hili suala
linanishangaza kidogo.Kwa nini
asiweke wazi mahali aliko?Kwa
nini anajificha ? Akauliza Silva
“ Silva hilo ndilo swali ambalo
nataka ulijibu .Nataka utafute
mahala alipo .Nimekupa
majukumu haya mawili mazito
kwa hiyo tumia kila rasilimali
uliyonayo na endapo kuna kitu
chochote kinahitajika usisi…” Rais
akanyamaza baada ya lango
kugongwa.Akainuka na kwenda
kuufungua akakutana na Jenerali
Lameck Msuba akamuomba
amsubiri kwa dakika moja amalize
mazungumzo yake na Silva
“ Silva kuna mtu nahitaji
kuzungumza naye kwa hiyo
naomba uyafanyie kazi hayo
mambo niliyokuambia.Chochote
utakachohitaji nieleze
tafadhali.Tumia nguvu yote
uliyonayo kuhakikisha kabla ya
jua kuzama siku ya leo Austin na
wenzake wawe
wamepatikana.Naomba taarifa za
mara kwa mara” akasema rais na
kumpa Silva namba za simu za
Monica ili wawasiliane kisha Silva
akaondoka na akaingia Jenerali
Lameck
“Lameck nipe ripot.Nini
kimeendelea? Akauliza rais
“ Mzee mambo yanakwenda
vizuri na kabla ya mapambazuko
leo ,ndege zetu za vita
zimeshambulia kambi mbili za
Alshabaab na kuziharibu
kabisa.Tulifanya mashambulio
hayo katika zile kambi
tulizoelekezwa na wao
wenyewe.Kwa hiyo dunia
itaamshwa na habari mpya siku ya
leo na hii itapunguza hasira za
watanzania kwa kuona kwamba
tayari serikali yao imeanza
kuchukua hatua dhidi ya
Alshabaab waliomwaga damu ya
watanzania.Ni hatua nzuri
tumepiga.” Akasema Lameck
“ Good Job lameck” Akasema
rais na kuvuta pumzi ndefu .
“ Lameck naona kama kichwa
changu kinataka
kupasuka.Asubuhi ya leo Habib
anahitaji majibu kama tayari
nimefanikiwa kumpata
Yasmin.Nilimuahidi kumpa jibu
zuri asubuhi na sina cha
kumueleza kwani bado Yasmin
sijampata na hata kama
ningekuwa nimempata sina
mpango wa kumpa Habib ile hati
ya muungano.Nishauri nifanye
nini?
“ Relax Mr President.Huu ni
wakati unaohitaji utulivu mkubwa
na kufanya mambo kwa utulivu na
akili kubwa.Kama Habib
atakupigia simu tell him anything
good just to buy time.Baadae
baada ya mambo kutulia utaongea
naye na kumuomba alipwe kitu
kingine badala ya hati ile ya
muungano anayoitaka.Nafikiri hilo
ndilo jambo pekee zuri la kufanya
kwa sasa kuhusu Habib”akasema
Lameck
“ It’s a good idea.Itanibidi
nifanye hivyo” akajibu rais
“Vipi kuhusu ripoti ya vifo na
majeruhi ,tayari umeipata ili
tufanye tathmini ya kazi
tuliyofanya kama imezaa
matunda? Akauliza Lameck
“Mpaka sasa bado sijapokea
ripoti yoyote ila nategemea kupata
taarifa asubuhi hii ya leo kwani
kazi ya kufukua vifusi na kutafuta
maiti katika majengo
yaliyolipuliwa imeendelea
kufanywa usiku kucha.Katika
kikao cha asubuhi ya leo tutapata
taarifa rasmi na hapo baadae
nategemea kwenda katika hoteli
iliyolipuliwa kisha nitakwenda
Dodoma na kule nitatembelea
jengo la bunge lililolipuliwa halafu
nitahutubia taifa kutokea pale pale
katika eneo la bunge.Nina ratiba
ndefu sana siku ya leo na
ninaomba uambatane nami kila
mahala nitakapokwenda siku ya
leo kwani nahitaji sana mtu wa
karibu wa kunishauri.Kitu kingine
ni kwamba nimemkabidhi Silva
jukumu la kuwatafuta Austin na
wenzake na vile vile kufahamu
mahala aliko Agatha.” Akasema
rais na ukimya mfupi ukatawala
mle chumbani
“ Mheshimiwa rais bado
najiuliza imewezekanaje Agatha
akanusurik…….” Kabla Lameck
hajamaliza sentensi yake simu ya
rais ikalia akaitoa mfukoni
akatazama mpigaji halafu
akamuomba Lameck atoke nje ili
aweze kuzungumza na simu ile.
“ hallow sweetheart” akasema
rais baada ya kuipokea simu ile
“ hallo my love” ikasema sauti
laini ya mwanamke upande wa pili
“ Nashukuru umenipigia
mpenzi wangu Monalisa.Habari za
Arusha? Akauliza rais
“Huku si kwema
mpenzi.Nimeshindwa kupata
usingizi kutokana na tukio
lililotokea jana.Nilitaka kukupigia
usiku nikajua utakuwa katika hali
mbaya nikaona ni vyema nikupigie
asubuhi ya leo ili nijue maendeleo
yako.Pole sana mpenzi wangu kwa
mambo yaliyotokea
jana.Nimeogopa mno” akasema
Monalisa.
“Mona usihofu mimi ni mzima
kabisa japokuwa nilipata mstuko
kidogo lakini ninaendelea vyema
na sina tatizo lolote.Kwa sasa
tunaendelea na uchunguzi
kuhusiana na jambo hili lakini
hawa magaidi hawataweza
kutuchezea ,tutuwafundisha
adabu” akasema rais
“Naomba uwe makini sana
mpenzi wangu katika kazi yako
hiyo imekuwa na hatari
nyingi.Maadui wanaokutafuta ni
wengi.Mimi na Millen
tunakuombea sana uweze kuwa
salama”
“msiwe na hofu yoyote
nitakuwa salama kabisa” Akasema
rais
“Nimepata taarifa nyingine
asubuhi ya leo imenistua sana.Ni
kwamba Bill naye ni miongoni
mwa watu waliokuwamo katika
hoteli hiyo iliyoshambuliwa Dar es
salaam.Naye amefariki dunia”
akasema Monalisa
“ Umepata wapi taarifa hizi?
Mbona mimi bado
sijazipata?akauliza rais
akionekana kustuka
“Nimepigiwa simu na rafiki wa
karibu na Bill akaniambia kwamba
Bill alimpigia simu jana jioni akiwa
hapo hotelini akamwambia
kwamba alikuwa anakusubiri
wewe na baada ya muda mfupi
likatokea hilo shambulio.”
Akasema Mona
“Ni kweli Mona nilikuwa na
miadi ya kukutana na Bill jana pale
hotelini.Nitafuatilia katika taarifa
nitakayopewa ili nijue kama Bill ni
mmoja wa watu
waliofariki”akasema rais
“Hakuna haja ya kufuatilia,
kwani tayari marafiki zake
wamekwisha fuatilia na
kuhakikisha kweli Bill amefariki
dunia” Akasema Mona na kuanza
kulia
“Pole sana Monalisa hata mimi
jambo hili limenigusa mno.Bill
alikua mtu wetu wa karibu sana”
Akasema rais
“Mona ninakuomba kitu
kimoja,hali ya usalama kwa sasa si
nzuri kwa hiyo ile safari ya
kuelekea ulaya inatakiwa iwe
mapema zaidi na mterejea pale
hali ya usalama itakapokuwa
imekaa vizuri.”
“Hapana sweetheart.Ile safari
lazima tuiahirishe kwa
muda.Lazima nihudhurie msiba wa
Bill.Yule ni mtu wangu wa karibu
sana na siwezi kuondoka bila
kuhudhuria mazishi yake.Yeye ni
sababu ya mimi na wewe kuwa
pamoja”akasema Monalisa na rais
akastuka
“Unamaanisha unataka kuja
dar es salaam?
“Ndiyo.kama msiba wa Bill
utakuwa Dar es salaam lazima
nihudhurie”
“Mona hapana usije Dar es
salaam.Hali si shwari kwa
sasa.Nakuomba Mona endelea na
safari ya ulaya na mimi
nitakuwakilisha katika mazishi
hayo ya Bill”
“Hapana siwezi kukosa
kuhuduria msiba kama huu
unaonihusu sana.Hiyo safari
itasubiri kwanza hadi pale msiba
utakapomalizika .Isitoshe hakuna
kitu chochote cha kuhofia”
akasema Monalisa
“Mona nakuomba tafadhali
usije Dar kwa sasa.Hali ya usalama
bado si nzuri” akasema rais
“Darling wewe ni mkuu wa
nchi kwa hiyo fanya kila uwezavyo
kuhakikisha kwamba mimi na
Millen tunakuwa salama
tutakapokuwa Dar.” Akasema
Monalisa
“Mona tafadhali naomba
tusiweke mjadala katika suala
hili.Unafahamu fika hali uliyoiacha
huku kwa hiyo nakushauri Mona
usije Dar”akasema rais
“Darling ni miaka imepita sasa
na isitoshe Job ni kichaa na hawezi
kunitambua tena kwa hiyo hakuna
chochote cha kuogopa.Ninakuja
kuhudhuria msiba na kuondoka ili
tuendelee na ratiba nyingine hizo
za kwenda ulaya.Tafadhali
niruhusu japo mara moja mpenzi
wangu nije Dar niwaslimu hata
ndugu zangu kwani sijawahi
waeleza niko wapi” Akasema
Monalisa.Rais akafikiri kwa muda
halafu akasema
“Nipe muda nilifikirie suala
hilo Mona nitakupa jibu baadae.”
Akasema rais na kuagana na
Monalisa akakata simu.
“Siku imeanza vibaya
.Monalisa anataka kuja Dar !!
akawaza rais.
“Nimeshindwa kumueleza
kama Job si kichaa na
anamtafuta.Hata hivyo nimefurahi
kusikia kwamba Bill tayari
amekufa.Yule pekee ndiye
aliyekuwa anafahamu kuhusu
mimi na Monalisa na Job alikuwa
anamuwinda ili amueleze mahala
alipo mkewe na mwanae
Millen.Pamoja na Bill kuondoka
nina wasi wasi ujio wa Monalisa
hapa Dar unaweza kusababisha
mambo mengine endapo ataonana
na Job au watu wanaweza
wakamuona na kumtaarifu Job”
Akawaza
“Hakuna namna
nitakayofanya kumzuia Mona asije
Dar .Kitu pekee ni kuhakikisha
kwamba anakuwa na ulinzi mkali
muda wote na hakuna mtu yeyote
anayemkaribia.Vile vile anatakiwa
abadili muonekano wake ili
asitambuliwe kirahisi” akaendelea
kuwaza rais

8
 
SEASON 7: SEHEMU YA 11
Taksi waliyokodi akina Daniel
iliwafikisha nyumbani kwa Daniel
wakaingia ndani.Kibarazani
alikuwepo mwanamke mmoja
aliyekuwa akitengeneza kucha
zake.
“Baby mbona umerudi
mapema leo?akauliza mwanamke
Yule lakini Daniel hakumjali
akamkaribisha ndani Irene
ambaye bado alikuwa
analia.Kitendo cha Daniel
kumtomjali yule mwanamke
kilimuudhi akaingia ndani akiwa
amefura kwa hasira
“ Daniel can we talk? Akasema
akiwa amesimama akimtazama
Daniel kwa hasira
“ Not now Angela.” Akasema
Daniel
“ Now ! akasema Angela kwa
ukali.Uso wa Daniel ukabadilika
kwa hasira ,Akainuka na kumshika
mkono Angela wakaenda
chumbani.
“ Ninakwambia kwa mara ya
mwisho don’t disrespect me
again!! Umenisikia Angela?
Akauliza Daniel akiwa amemkaba
Angela shingoni
“ Daniel lini utaacha tabia
yako chafu ya kubadili wanawake
kama nguo? Ninajiheshimu sana
nikitegemea na wewe
utajiheshimu lakini bado
haubadiliki.Kila siku unakuja na
makahaba ndani.Wewe ni
mwanaume wa aina gani? Ulidhani
nimeondoka na ukaamua kumleta
kahaba wako asubuhi yote hii?
Daniel akamnasa Angela
kibao kikali akaanguka kitandani
“ Yule si kahaba.Ni mwanamke
mwenye heshima zake na wewe
huwezi kujifananisha naye hata
kidogo.Inuka chukua mizigo yako
ondoka nisikuone tena hapa
kwangu.!! Akafoka Daniel
“ Daniel nisamehe sintarudia
tena darling!!
“ Dakika tano nakupa ondoka
hapa haraka sana” akasema Daniel
na Angela akaanza kuvaa kisha
akachukua begi lake akaondoka
.Daniel akarejea sebuleni
alikomuacha Irene
“ Irene samahani kwa
kukuacha peke yako.Nyamaza
kulia ili tujadili na tujue nini
kimetokea? Akasema Daniel
“ Daniel wazazi wangu nani
kawachukua? Wamewapeleka
wapi? Akauliza Irene huku
akimwaga machozi
“Irene usilie tafadhali
.Nyamaza ili tulijadili suala hili na
tulipatie ufumbuzi.Kulia
hakutasaidia chochote .” akasema
Daniel na kumfuta Irene machozi
“ Niambie Irene una tatizo
gani? Nini kimetokea? Tukiwa kule
baa walikufuata wale jamaa
wakataka uongozane nao na kwa
bahati nzuri nilikuwepo
nikakusaidia.Tumerejea nyumbani
na kuikuta hali kama ile.Nyumba
imevurugwa hovyo,mtumishi wa
ndani ameuliwa na mbaya zaidi
wazazi wako wamechukuliwa.Nani
amefanya hivi? Kuna nini
wanakitafuta? Akauliza Daniel
“ Sifahamu Daniel.Siwafahamu
hao jamaa wanaonifauta ni akina
nani na wanataka nini
kwangu”Akasema Irene.Daniel
akautoa ujumbe ule aliouchukua
chumbani kwa Flora akampatia
Irene akausoma na kuanza tea
kulia
“ Daniel nisaidie niwapate
wazazi wangu!! Akasema
“ Irene usilie tafadhali.Hili si
suala dogo.Unatakiwa uwe jasiri
sana kwani haya ni
mapambano.watu hawa
wanaokutafuta kuna kitu
wanakitaka aidha toka kwako au
kwa mmoja wa ndugu zako na
ndiyo maana wamevuruga nyumba
yote kutafuta hicho
wanachokihitaji na walipokikosa
wakaondoka na wazazi wako”
Daniel akanyamaza na kumtazama
Irene kwa makini
“Irene kama kuna kitu
unakifahamu au kama kuna tatizo
lolote lile niambie tafadhali.Niko
hapa nitakusaidia.Endapo kuna
kitu unakifahamu halafu
unakificha kinaweza kusababisha
suala hili likawa baya zaidi au hata
wazazi wako wakapata
madhara.Niambie ukweli tafadhali
kuna tatizo lolote katika familia
yako limetokea? Akauliza Daniel
“ Daniel nimekwambia
sifahamu chochote.Mimi na familia
yangu hatuna ugomvi na mtu na
sielewi kwa nini wale jamaa
wanatufuata na kutuletea matatizo
haya yote.Nisaidie tafadhali Daniel
kuwapata wazazi wangu kama
unao uwezo .Baba yangu ni
mgonjwa na anatakiwa apelekwe
nje ya nchi kwa
matibabu.wakiendelea
kumshikilia atakufa” akasema
Irene na kuanza tena kulia
“ Irene ninatamani sana
kukusaidia lakini sielewi nitaanzia
wapi kukusaidia kwani sielewi
chochote .Hawa jamaa wameacha
namba zao hapo chini.Piga namba
hizo halafu tusikie watasema nini”
akasema Daniel.Irene akaonekana
kusita
“ Irene muda unakwenda
wapigie simu hawa jamaa usikie
wanataka kitu gani.” Daniel
akasisitiza
“ Hapana Daniel sitaki
kuzungumza na hawa jamaa.Kama
unataka zungumza nao usikie ni
akina nani na wanataka
nini”akasema Irene.Daniel
akaziandika katika simu yake
namba zile zilizoachwa kwenye
ujumbe akapiga na simu ikaita
“ Simu inaita” Daniel
akamwambia Irene
“ Hallo” ikasema sauti ya
mwanamke upande wa pili
“ Hallow” akasema Daniel
“ Wewe ni nani na unataka
nini? Akauliza Yule mwanamke
kwa ukali
“ Nimepiga simu kwa niaba ya
Irene maboko ambaye nyumbani
kwao kumevamiwa ,yakafanyika
mauaji na wazazi wake wakatekwa
na mkaacha ujumbe kuwa
awapigie.Ninyi ni akina nai?
Mnataka nini kwake? Wazazi wake
mmewapeleka wapi?
“ Tafadhali kijana naomba
usiingie katika mambo
yasiyokuhusu.Simu hii alitakiwa
kupiga Irene mwenyewe na si mtu
mwingine yeyote.Kwa kitendo hiki
ulichokifanya unazidi kuwaweka
hatarini wazazi wake.”
“ Tafadhali naomba
msiwafanye chochote wazazi wa
Irene.Semeni ni kitu gani
mnakitaka ? Kama mnataka pesa
semeni ni kiasi gani mnakitaka?
Niko tayari kulipa kiasi chochote
cha pesa mnachokitaka” akasema
Daniel
“ Shida yetu sisi si
pesa.Tunamtaka Irene.Muonyeshe
video tutakayoituma hivi punde na
hadi kufika leo jioni apige simu na
bila kufanya hivyo ataletewa miili
ya wazazi wake wakiwa
wamekufa.” Akasema Yule
mwanamke na kukata simu.Baada
ya muda ikatumwa video
waliyoisema Daniel
akaifungua.Katika video hiyo
walionekana wazazi wa Irene
wakiwa wamefungwa katika viti
huku baba yake akiwa anavuja
damu mdomoni.Mama yake Irene
huku akilia akasema
“Irene mwanangu nakuomba
sana wape hawa jamaa kitu
wanachokitaka ama sivyo
watatuua.Hali ya baba yako inazidi
kuwa mbaya .Tafadhali tuokoe
mwanangu.Wape kitu chao” Video
ile ikaishia hapo.Irene aliangua
kilio kikubwa
“ Irene hebu nyamaza.Kulia
hakutakusaidia kitu chochote”
akasema Daniel kwa ukali na Irene
akanyamaza akafuta machozi
“ Irene kuna kitu
unanificha.Tafadhali naomba
unieleze ukweli.Hawa jamaa
wanatafuta kitu gani toka kwako?
Kitu gani ambacho mama yako
anakutaka uwape hawa jamaa ili
wawaachie? Tell me the truth
Irene” akasema Daniel
“Daniel sifahamu kitu
chochote.Siwafahamu watu hawa
na wala sifahamu wanataka nini
kwangu.Tafadhali kama unaweza
kunisaidia kuwapata wazazi
wangu nisaidie Dany.Nitakupa kitu
chochote kile ukinisaidia
kuwapata wazazi wangu”
“Irene kama nilivyokueleza
kwamba natamani sana
kukusaidia katika suala hili lakini
nashindwa nitaanzia wapi
.Ningekuwa ninaufahamu ukweli
ningejua nini nifanye lakini hutaki
kunieleza ukweli.Narudia tena
kukuomba kwa mara ya mwisho
kama kuna chochote unakifahamu
kuhusu wale jamaa nieleze.Wale si
wajinga wakakufuata wewe na
kufikia hatua ya kuwateka wazazi
wako.Lazima kuna kitu
wanakitaka toka kwako.Niambie
ni kitu gani hicho? Akasema Daniel
Irene hakujibu kitu akabaki
kimya
“ Irene muda unakwenda na
usalama wa wazazi wako uko
shakani.Nieleze tafadhali kama
una kitu chochote unakifahamu
kuhusu hawa jamaa ili tuone
namna ya kuwaokoa wazazi
wako.Umeona mwenyewe hali zao
si nzuri na baba yako ni mgonjwa
na hawa jamaa wanaonekana
wamempiga.Tukichelewa anaweza
akapoteza maisha .Is that what you
want? Akauliza Daniel.Irene
akainamisha kichwa.
“ Nafahamu wale jamaa
wanachokitaka.Hii ni siri yangu na
siko tayari kuwapa.Huu ni mchezo
unachezwa aidha na rais au
madam Agatha.Wanachokitaka
toka kwangu ni kujua nimefahamu
vipi kuhusu shambulio lile la
jana.Lazima nitafute namna ya
kuwaokoa wazazi wangu lakini siri
hii siwezi kuitoa kamwe kwa hawa
jamaa.Lakini kwa nini nisimueleze
Daniel ukweli labda anaweza
akanisaidia” akawaza Irene halafu
akainua kichwa akamtazama
Daniel
“ Daniel” akaita Irene
“ Kuna kitu nataka nikwambie
.Nafahamu hawa jamaa
wanachokitafuta toka kwangu.”
“ Niambie Irene ili nione
namna ya kukusaidia” akasema
Daniel.Irene akafuta machozi na
kusema
“ I have a record”
“ A record? Akauliza Daniel
“ Ndiyo.Ninayo rekodi ya
maongezi ya simu kati ya rais na
mkuu wa majeshi,jenerali lameck
msuba.Katika maongezi hayo
walikuwa wanaongelea kuhusiana
na shambulio lililotokea
Dar.Nilirekodi maongezi yao kabla
ya shambulio kutokea”
“ Hebu subiri kidogo
Irene.Umesema uliwarekodi rais
na jenerali lameck wakiongelea
kuhusu shambulio lililotokea Dar
es salaam jana?Uliwarekodi vipi?
“ Nilidukua simu ya rais”
“ You did what ?!!! Daniel
akashangaa
“ Nilidukua simu ya rais”
“ How? Akauliza Daniel akiwa
katika mshangao mkubwa
“ Niliingiza program Fulani
katika simu ya rais ambayo
iliniwezesha kusikia simu zote
anazopiga au kupigiwa.”
Daniel akamtazama Irene kwa
mshangao mkubwa
“ kwa nini ulifanya hivyo?
“ Ni hadithi ndefu nitakueleza
siku nyingine lakini naomba tu
ufahamu kwamba nilidukua simu
ya rais nikanasa maongezi yake na
Lameck wakiongelea kuhusu
shambulio litakalotokea”
‘ Umesema maongezi
hayoyalikuwa kabla ya shambulio?
Daniel akauliza
“ Ndiyo.Ni saa mbili hivi kabla
ya shambulio kutokea.” Akajibu
Irene
“ Unataka kuniambia kwamba
rais na mkuu wa majeshi
walifahamu kuhusu uwepo wa
shambulio hilo? Akauliza Daniel na
Irene akatikisa kichwa kukubali.
“ No ! that’s not true
Irene.Please don’t lie to me”
akasema Daniel
“ Daniel huu si uongo.Hiki ni
kitu cha kweli na ushahidi ninao”
“ Nitakuamini endapo utanipa
huo ushahidi wa hayo maongezi
nisikilize” akasema Daniel
“ Daniel huwezi kuniamini
hadi nikupe ushahidi?Unadhani
ninaweza kukudanganya kwa
jambo kama hili?
“ Irene hili unalolisema ni
jambo kubwa sana kwamba rais
alifahamu kuhusiana na shambulio
lile hata kabla halijatokea.Hili si
jambo linaloweza kutamkwa
kirahisi namna hii.Kama una
matatizo yako binafsi na rais
tafadhali usijaribu kumsingizia
katika jambo baya kama hili.You’ll
destroy him” akasema Daniel
“ Daniel sina sababu yoyote ya
kutunga uongo kumuhusu rais
kwani kwa muda wote amekuwa ni
mtu mwema kwangu lakini
niamini nikwambiacho kwamba
nina ushahidi huo wa kumuhusu
rais na jenerali lameck”
“ I don’t believe you
Irene.Kama hautanionyesha huo
ushahidi sintaweza kukuamini na
kukusaidia” akasema Daniel.Irene
akachukua simu yake aliyoizima
akaifungua na kutoa kadi ya
kuhifadhia kumbu kumbu
akaiweka katika simu anayotumia
kisha akatafuta rekodi ile akampa
Daniel aisikilize.
“ Oh my God !! akasema Daniel
kwa mshangao.
“ I cant believe this” akasema
na kuicheza tena rekodi ile
akaisikiliza kwa makini halafu
akamtazama Irene
“ Kuna mtu yeyote
uliyemueleza kuhusiana na rekodi
hii? Akauliza
“ Wewe ni mtu wa kwanza
kuisikiliza.Ila kama ulivyosikia
maongezi yao walikuwa
wanamlenga madam Agatha hivyo
ikanilazimu kumpigia simu na
kumtaka atoke haraka ndani ya
hilo jengo kwani kuna kitu kibaya
kinakwenda kutokea.Alifanikiwa
kutoka salama katika hoteli ile
kabla ya mlipuko kutokea na
baadae akanipigia simu
kunishukuru kwa kumuokoa
.Alitaka nimueleze nilikopata
taarifa za mlipuko ule nikamuahidi
kwamba nitampigia simu baade
kumfahamisha kila kitu na toka
hapo nimeizima simu hiyo na
sijaitumia tena.” Akasema
Irene.Daniel akainuka na
kuchungulia nje kama kuna mtu
yeyote pale karibu
“Do you believe me now?
Akauliza Irene
“I do.But are you sure this is
real?
“ Yes it is real”akajibu Irene
Daniel akavuta pumzi ndefu
akamtazama Irene na kusema
“ Irene sasa nimepata picha
kamili kwa nini unatafutwa.Hili si
jambo dogo .Ni jambo la hatari
sana umelifanya lakini lenye
manufaa makubwa kwa nchi.Watu
hawa watakuandama usiku na
mchana hadi wahakikishe
wamekutia mikononi kwani
inaonekana tayari wamekwisha
fahamu kwamba kuna kitu
unakifahamu” Akasema Daniel
“ How are you going to help
me? Akauliza Irene
“ Irene kwa hapa ilipofika
kuna kitu nalazimika
nikufahamishe ambacho wengi
hawakifahamu” Daniel
akanyamaza kidogo halafu
akasema
“Ninafanya kazi katika idara
ya siri sana ya ujasusi.Hii ni idara
ya siri mno na ina watuwachache
sana na watu kama sisi
hatufahamiki kirahisi.Mfumo huu
wa maisha yangu ninaoishi nikiwa
na wanawake mbalimbali si
kwamba ninapenda bali
ninalazimika kuishi hivi ili kujenga
taswira tofauti katika
jamii.Ninakuomba uniachie suala
hili nitakusaidia lakini kabla ya
yote ninapaswa kukutafutia
sehemu salama utakayoishi
mahala ambako hawa jamaa
hawataweza kukupata” akasema
Daniel
“ Daniel wewe ni mpelelezi?!!
Akauliza Irene kwa mshangao
“ Ndiyo” Akajibu
“ How come I didn’t know
about this? akasema Irene.Daniel
hakumjibu kitu.Akachukua simu
na kuzitafuta namba Fulani
akapiga.
“ Hallow Monica” akasema
Daniel
“ Daniel ! how’re you? Umepoa
sana hadi najiuliza kuna tatizo
gani?
“Nimetingwa na shughuli
nyingi Monica ndiyo maana
nimepotea.Uko wapi sasa hivi?
“ Niko hapa nyumbani
ninajiandaa nina safari ya
kuelekea Kinshasa baadae jioni”
“ Kuna nini Kinshasa?
“ Naenda kuhudhuria mazishi
ya mke wa rais wa Congo” akasema
Monica
“Monica nina shida nataka
unisaidie.Ninakuja hapo kwako
sasa hivi” akasema Daniel na
kukata simu akamchukua Irene
wakatoka pale ndani wakatembea
mita kadhaa na kukodi taksi
kuelekea kwa Monica.

 
QUEEN MONICA : FINAL SEASON
SEHEMU YA 12

Siku ilikuwa ndefu sana kwa
Ernest Mkasa rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania.Aliwaongoza
watanzania kuaga miili ya watu
waliopoteza maisha kwenye shambulio
lililofanyika katika ukumbi wa bunge
na Dar es salaam.Baada ya shughuli za
kuaga miili kumalizika mjini Dodoma
rais akaelekea kisiwani Zanzibar
kuhudhuria mazishi ya makamu wa
rais aliyepoteza maisha katika mlipuko
jijini Dar es salaam.
Saa kumi na mbili za jioni rais
akarejea Dar es salaam.Katika uwanja
wa ndege akapokewa na viongozi mbali
mbali na kisha akelekea ikulu.Mara tu
alipofika ikulu akapewa taarifa
kuhusiana na hali ya usalama.Kikundi
cha kigaidi cha Alshabaab kilijitangza
kuhusika na mlipuko uliotokea katika
soko la kimataifa la samaki
asubuhi.Alipewa taarifa ya tukio
liliotokea na walinzi watatu kuuawa
baada ya gari lao kutupiwa bomu na
Monalisa akachukuliwa na watu
wasiojulikana.Taarifa hii ilimstua mno
rais.Hakupewa nafasi ya kupumzika
akataarifiwa kwamba mke wake Agatha
tayari amerejea nyumbani akitokea
hospitali na mwisho akataarifiwa
kwamba mgeni wake Bashar bin
Abdulsalaam tayari amekwisha wasili
na alikuwa anamsubiri.Ernest
akachanganyikiwa.Hakujua aanzie
wapi.Akaamua kwanza akaonane na
Bashar ndipo aendelee na mambo
mengine.Moja kwa moja akaelekeza
Bashar apelekwe katika chumba cha
maongezi ya faragha.
“Habari yako Bashar” rais Ernest
akamsalimu Bashar wakiwa katika
chumba cha maongezi ya faragha
“Habari nzuri sana mheshimiwa
rais”
“Karibu sana” Akasema rais
“Ahsante mheshimiwa rais.Poleni
sana kwa mambo yanayoendelea nchini
kwenu.Naamini baada ya muda si
mrefu mambo yatakaa sawa” Akasema
Bashar
‘Tunaomba iwe hivyo kwani
watanzania hawajazoea kuishi katika
hali ya mashaka mashaka kama
sasa.Hali hii itatulia si muda mrefu.”
“Mheshimiwa rais nafahamu una
majukumu mengine kwa hiyo nataka
nisikupotezee muda.Naomba
nijielekeze moja kwa moja katika kile
nilichotumwa kwako” akasema Basher
na kufungua mkoba wake akatoa
bahasha nyeupe akamkabidhi rais
ambaye aliifungua na kusoma barua
iliyokuwamo ndani yake.Kadiri
alivyozidi kuisoma ndivyo sura yake
ilivyozidi kubadilika na kujikunja.
Alipomaliza akaitupa barua ile mezani
na kumtazama Bashar kwa hasira
“Huu ni upuuzi mkubwa.Siwezi
katu kukubali ujinga kama huu”
akafoka rais huku akigonga meza kwa
hasira.Akaichukua tena barua ile na
kuanza kuisoma halafu akasimama
“Huu ni ujinga mkubwa sana.Watu
hawa waliokutuma ni wapuuzi
wakubwa.Siwezi mimi kutelekeza haya
wanayonitaka niyatekeleze.Katu siwezi
kukubali.” Akasema rais na kuketi
kitini akaichukua barua ile na kuisoma
tena kwa mara ya tatu
“kwako mheshimiwa rais wa
Tanzania
Tunamtuma mjumbe wetu maalum
kwako kufikisha ujumne huu wa
muhimu sana.Rejea makubaliano yetu
ya awali ambayo kwa makusudi kabisa
umemua kuyapuuza.Umetufanyia
kitendo cha kihuni na sisi tumefadhaika
sana kwa kitendo
ulichokifanya.Tumekaa kikao kujadili
suala hili na tumeamua yafuatayo.
Utabaki na hati ya muungano
wenu wa Tanganyika na Zanzibar
ambayo umekataa kwa makusudi
kutupatia,lakini sisi tunakitaka kisiwa
cha Pemba.Siku si nyingi kuanzia sasa
litatolewa tamko la kisiwa cha pemba
kutaka kujiondoa katika jamhuri ya
muungano wa Tanzania na kuwa nchi
huru.Wewe kama rais wa Tanzania
utaliunga mkono jambo hilo na
kuhakikisha linafanikiwa.Tunafahamu
ni suala gumu lakini tunakutaka
usimame imara kuhakikisha kwamba
linafanikiwa na kisiwa cha Pemba
kinajitoa kutoka jamhuri ya muungano
wa Tanzania na kuwa nchi
huru.Muungano utabaki wa Tanganyika
na kisiwa cha unguja pekee.
Mheshimiwa rais hii ni nafasi ya
pili tunakupa na kitendo chochote cha
kujaribu kulizuia suala hili litakuwa ni
tangazo la vita kati ya nchi yako na
mtandao wetu na ninakuhakikishia
kwamba Tanzania haitakuwa tena
kisiwa cha amani.Damu itamwagika kila
uchao.mamia ya watanzania
watapoteza maisha kila
siku.Tutasambaza watu wetu katika kila
mkoa na mashambulio yatatokea
sehemu mbali mbali za Tanzania.Hii
itakuwa ni vita ya vizazi na vizazi
haitakuwa na kikomo.Usitake
kulitumbukiza taifa lako katika vita hii
mheshimiwa rais.Tekeleza maagizo
tuliyokupa na Tanzania itakuwa
salama.
Tunakutakia utekelezaji mwema
Habib
Hivi ndivo barua ile
ilivyoandikwa.
Ndani ya kile chumba cha
maongezi ya faragha kulikuwa
kimya.Rais Ernest alizama katika
mawazo mazito.Bashar akatazama saa
yake na kumstua rais
“Mheshimiwa rais naona muda
unasonga kwa kasi natakiwa kuondoka
nchini ndani ya nusu saa ijayo.Ahsante
kwa mapokezi mazuri na kuupokea
ujumbe wangu.Kabla sijaondoka kuna
chochote unanituma nikawaambie
walionituma kwako?akauliza Bashar
“Ahsante sana kwa kufika na
kuufikisha ujumbe.Nimeupokea ila
wanipe muda niutafakari na nitawapa
majibu”akasema rais.Wakaagana na
Bashar akaondoka
“Kwa mara ya kwanza ninajutia
maamuzi yangu ya kutaka kupambana
na Alberto’s.Haya yote yasingetokea
endapo nisingeamua kupambana
nao.Kila likitoka hili linaingia lingine.”
akawaza rais na kuvua koti kwani
alihisi joto
“Nafahamu hizi ni njama za IS
kukipata kisiwa cha Pemba ili
waanzishe kundi lao kule.Yasmin
alinieleza kuhusu mipango ya
IS.Nitafanya nini ? Nikubaliane na
matakwa yao au niingie nao vitani ?
Akajuliza rais
“Endapo nitaamua kuingia katika
vita na hawa jamaa nchi hii amani
itatoweka kabisa, kwani hawa jama
wanafanya mashambulizi ya kustukiza
na kuua raia.Wangekuwa ni Alshabaab
peke yao ningeingia nao vitani kwani
ningetuma majeshi yetu yangewasaka
ndani ya Somalia na kuwamaliza kabisa
lakini katika hili suala naamini
Alashabaab wanashirikiana na IS na
hawa ni kundi kubwa la kigaidi
linaloitikisa dunia.I don’t know what to
do” akawaza na kumuta Jenerali lameck
ambaye alifika mara moja
“Lameck nimepokea ujumbe muda
mfupi kutoka kwa Habib lakini naamini
ni ujumbe wa IS ila wameupitisha kwa
habib.” Akasema rais na kumpa Lameck
ujumbe ule ausome.
“Mheshimiwa rais huu ni upuuzi
mkubwa sana.Umewapa jibu gani?
“Nimewaambia ujumbe
nimeupokea na nitautafakari ”
“Sikiliza mheshimwa rais jambo
hili haliwezekani kabisa.Hawa watu si
wa kuwapa nafasi na hawawezi
kutulazimisha tufanye wanavyotaka
wao”akasema Lameck
“Unashauri nini Lameck?
“Kataa ombi lao na waweke wazi
kwamba hilo haliwezekani” akasema
Lameck
“Hilo litakuwa ni tamko la vita kati
yetu na wao”akasema rais
“Then let’s go to war!! Hatuwezi
kukubali upuuzi wa namna
hii.Mheshimiwa rais tayari
tumetengeneza matatizo makubwa
ambayo tunakabiliana nayo hapa nchini
hatuwezi kukubali tena kuongeza
matatizo mengine.Ukilikubali ombi lao
hili litakuwa ni tatizo lingine kubwa na
ambalo hatutaweza kulitatua.Nchi hii
ambayo tunaipigania kuisafisha
itagawanyika na juhudi zetu zote
zitakuwa kazi bure.Damu yote
iliyomwagika itakuwa imekwenda
bure” Akasema Lameck
“Lameck unachokisema ni sahihi
na hata mimi sipendi kufanya vile
wanavyotaka lakini hawa jamaa ni
wabaya sana na sasa wanaungana na
IS.Unafahamu hawa jamaa namna
wanavyofaya mashambuluo yao kimya
kimya.Bado mfumo wa kutambua
mashambulio ya kigaidi katika nchi
yetu ni mdogo kwa hiyo wataitumia
nafasi hiyo kufanya mashambulio kila
uchao.Damu nyingi ya watanzania
itamwagika.Lameck sitaki tena
kuiingiza nchi hii katika majanga
mengine.Damu tuliyoimwaga damu
inatosah.No more blood” akasema rais
“Mheshimiwa rais,uliponiapisha
niwe mkuu wa majeshi ya ulinzi wa
nchi ya Tanzania niliapa kuwalinda raia
wa Tanzania dhidi ya wale wote
wanaotishia amani na ustawi wa taifa
hili.Hawa Alshabaab na IS wanatishia
amani yetu kwa hiyo siwezi kukaa
kimya lazima nisimame imara
kuhakikisha kwamba ninayaongoza
mapambano dhidi yao.Tukikubali leo
kisiwa cha Pemba kichukuliwe na IS
itakuwani hatari zaidi kwa usalama wa
nchi.Watajiimarisha na watakichukua
kisiwa cha Unguja pia na mwisho
watataka kuingia Tanzania
bara.Hulioni hilo mheshmwia rais?!!
Akauliza Lameck kwa sauti ya juu
kidogo.Ernest akainamisha kichwa
akatafakari baada ya muda akasema
“Asubuhi ya leo nilipigiwa simu na
Habib tukabishana kidogo na akasema
anataka kunionyesha nguvu yao.Baada
tu ya kukata simu ukatokea ule
mlipuko katika soko la samaki.Lameck
hawa jamaa wamejipanga vilivyo.Si
watu wa kufanyia mchezo.Tazama
mambo yanayotokea katika nchi za
jirani ambao wameingia katika
mapambano nao.Damu ya watu
wasiona hati ainamwagika.kama
wameweza kufanya shambulio jirani
kabis ana ikulu basi ni watu
waliojiandaa vizuri na wanachiokisema
wanawza wakakitekeleza.”
“Mheshimiwa rais walichokifanya
Alshabaab ni kukuogopesha na
kwuaogopesha watanzania lakini
usiingie katika mtego wao.Wanaweza
kuendelea kufanya mashambulio
mfululizo katika sehemu mbalimbali za
nchi kwa lengo la kuleta hofu lakini
nakuomba mzee usikate tamaa na
kuwapa wanachokitaka.Let’s fight.Tuna
jeshi imara na tukiamua kupamba nao
hawataweza kutushinda.Hiki ni kikundi
kidogo tu” akasema Lameck
“Alshabaab ni kikundi kidogo
lakini hatari na hasa wakiungana na
IS.Ni rahisi kupigana vita na adui
mkubwa kama nchi ambaye unajua
nguvu yake na unafahamu utampiga
wapi lakini hawa jamaa ni vigumu
kupigana nao kwa sababu hawajulikani
wako wapi,wako wangapi,uwapige
wapi na mashambulio yao ni ya
kuvizia”akasema rais
‘kwa hiyo umeamua nini
mheshimiwa rais?
“Niachie suala hilo nilitafakari
halafu nitakupa jibu nimeamua kitu
gani” akasema rais.Baada ya muda
kidogo akasema
“Lamec hatimaye zoezi letu
tumelimaliza rasmi leo.Japo
tumekutana na changamoto nyingi na
nyingine bado tunaendelea kukutana
nazo lakini tunastahili kujipongeza
kwani tumefanikiwa kukipata
tulichokihitaji.Alberto’s karibu wote
ninaowafahamu isipokuwa Agatha
pekee wameteketea.Huu ni ushindi
mkubwa japo tunaofahamu ni sisi
wawili pekee.Kinachofuata sasa ni
awamu ya pili ya zoezi letu ambayo ni
kukabiliana na athari zile zilizojitokeza
na zinazoendelea kujitokeza kutokana
na shambulio lile.Tunaendelea
kupambana ili nchi ibaki salama.Kwa
usiku huu nataka tujadili kuhusiana na
David Zumo” Akanyamaza kidogo kisha
akasema
“ Asubuhi kabla ya kwenda
Dodoma nilikueleza azma yangu ya
kutaka kuhitimisha utawala wa David
Zumo.”
“Ndiyo ulinieleza mheshimiwa rais
lakini nina swali dogo kwa nini
umefikiria jambo kama hilo? Kuna
sababu yoyote kubwa ya kukupelekea
ukafikiria kufanya hivyo?
‘Sababu kubwa ni kitendo chake
cha dharau alichokifanya.Nilimuomba
awakamate akina Yasmin lakini kwa
jeuri ameamua kuwaachia huru.Siwezi
katu kuvumilia kitu kama hiki.Endapo
taifa letu litabomoka basi na yeye
atakuwa na mchango mkubwa kwani
mtu ambaye anatembea na hati ya
muungano wetu alimtia mikononi na
akaamua kumuachia.Kingine ni
kwamba hawa jamaa akina Austin
naamini watakuwa wamemueleza kila
kitu kilichotokea kwa hiyo huyu ni mtu
hatari sana kwangu.Sababu ya tatu ni
ya kibinafsi zaidi lakini kwa kuwa
wewe ni mtu wangu wa karibu
nitakueleza.Ni kwamba David Zumo
tayari amempa mimba Monica.Sitaki
mbegu ya msaliti Yule ichanganyike na
damu yangu.Kwa sababu hizo kubwa
nataka nimuondoe
madarakani”akasema rais.Jenerali
Lameck akavuta pumzi ndefu.Alihisi
kuchoka mwili na akili
“Mheshimiwa rais sitaki
kupingana na maamuzi yako lakini
sababu ulizozitoa naona kama hazina
mashiko makubwa kukufanya ufikirie
kuuondoa utawala wa David
Zumo.Tunaweza kutengeneza tatizo
kubwa sana baina ya nchi zetu
hizi.Mimi ushauri wangu ni kutafuta
njia mbadala kupambana na David na si
kumuondoa madarakani”
“Lameck hakuna njia
mbadala.Nimekwisha amua
kumuondoa David Zumo madarakani
na lazima nifanye hivyo.Siwezi kubadili
msimamo wangu kwa hiyo nataka
unipe plani tutalifankishaje sualah
hilo?Nilikupa nafasi ya kutafakari njia
mbalimbali tunazoweza kutumia
kumuondoa David nadhani mpaka sasa
una jibu zuri la kunipa” akasema rais
“Mzee nimetafakari sana suala hili
kama ulivyonitaka na nimefikiria
jambo moja”
“tell me” akasema rais
“Davd Zumo aliwakusanya waasi
wote waliokuwa wakipigana kwa miaka
mingi na serikali ya Congo
akawajumuisha katika jeshi la Congo
ambalo kwa sasa linajulikana kama
jeshi la pamoja.Wale makanda wakuu
wa vikosi vya waasi amewapa nyadhifa
kubwa katika jeshi na uasi umekoma
kabisa Congo.Tunachoweza kukifanya
ili kumondoa David Zumo madarakani
ni kuzungumza na mmoja wa aliyekuwa
kiongozi wa waasi ili awakusanye
wanajeshi wake na kumpindua rais
David” akasema Lameck
“Hili linaonekana ni wazo
zuri.Hebu nifafanulie namna
tunavyoweza kufanya” akasema rais
“Tutazungumza na kiongozi huyo
wa zamani wa waasi ambaye ninamini
lazima atakubali kwani hivi majuzi
alipohojiwa hakuonekana kupendezwa
na kitendo cha nchi ya Congo kutaka
kugeuzwa kuwa nchi ya kifalme kwani
hakutakuwa na uchaguzi wa rais na
badala yake familia moja ndiyo
itakayoongoza Congo kwa vizazi na
vizazi.Siku zote lengo la kuanzisha uasi
huwa ni kukamata madaraka makubwa
na huyu jamaa endapo tutamuahidi
kumsaidia kukamata madara ya
kuiongoza Congo lazima
atakakubali.Sisi tutamsaidia mbinu za
kijeshi na silaha au hata vikosi vya jeshi
endapo vitahitajika.Mchezo mzima
utakakuwa hivi.Tanzania kwa sasa ni
mwenyekiti wa jumuiya ya afrika
mashariki ambayo nchi ya Congo DRC
ni mwanachama aliyejiunga hivi
karibuni.Kama mwenyekiti utaitisha
kikao cha dharura chenye lengo la
kujadili hali ya usalama katika ukanda
wa afrika mashariki.Wakati kikao
kikiendelea vikosi vya wanajeshi
walioasi wataivamia ikulu ya Congo na
kutangaza kuipindua serikali ya David
Zumo.Unaonaje kuhusu mpango huo?
Akauliza lameck
“Ni mpango mzuri sana
lameck.Ninayakubali mawazo yako
asilimia mia moja na kwa kuongezea tu
ni kwamba baada ya mapinduzi
kufanyika David nitampa hifadhi hapa
Tanzania na haraka sana nitafanya
mpango wa kumuondoa.Nataka
auawe”akasema Ernest
Baada ya majadiliano marefu
Lameck akapewa jukumu la kufanya
mazungumzo na meja Jenerali Paul
Ntamanywa mmoja wa viongozi wa
kundi la waasi waliopigana na serikali
ya Congo kwa miaka zaidi ya ishirini na
sasa yeye na kundi lake
wamejumuishwa katika jeshi la Congo.
Baada ya kikao kirefu rais
akaachana na Jenerali Lameck halafu
akazungumza na mkuu wa jeshi la
polisi akamtaka mpaka kufikia kesho
saa sita mchana Monalisa awe
amepatikan kisha akaelekea chumbani
kwake.Agatha mke wake alikwisha
ruhusiwa kutoka hospitali na alikuwa
amejipumzisha chumbani .
“Welcome home darling” akasema
Agatha
“Vipi maendeleo yako? Akauliza
Ernest
“Ninaendelea vyema.Hali yangu
imeboreka sana.Ahsante kwa kunijali”
akasema Agatha
“Pole sana kwa siku ngumu ya
leo.Unahitaji mapumziko” akasema
Agatha
‘Ni kweli nimechoka sana lakini
mimi na wewe bado tuna maongezi
mengi.Nataka kufahamu ulikuwa wapi
na nani aliyekupiga risasi
mguuni?akasema Ernest
“Relax Ernest.Nitakujulisha kila
kitu lakini kwa sasa unapaswa
upumzike.Tutazungumza pale
utakapokuwa umetulia.Kuna mambo
mengi ya muhimu sana ambayo nataka
tuzungumze”akasema Agatha
“Agatha kichwa changu kina
mambo mengi sana kwa sasa na
sifahamu kama nitaweza kupata nafasi
ya kutulia.Nina majukumu mazito ya
kuhakikisha nchi inatulia baada ya
mashambulio yale mawili kutokea.Nchi
haina serikali ,natakiwa kufikira nama
nitakavyoweza kuiongoza nchi kwa
hiyo usitegemee kuwa nitapata naafsi
nzuri ya kutulia.Lets talk now.Siku ile
ulikuwa katika lile jengo tulimopanga
nikutane nanyi Alberto’s wote lakini
baada ya shambulio kutoea
haukuwepo.Nini kilitokea? Ulinusurika
vipi? Akauliza rais.Baada ya muda
kidogo Agatha akasema
“Nilipokea simu toka kwa Irene
Maboko Yule mfanyakazi wa ikulu
anayeshughulikia masualaya mtandao”
“Irene!! Ernest akashanga
‘Ndiyo.Nilipokea simu toka kwake
akanitaka nitoke haraka ndani ya jengo
lile kwani kuna jambo baya linataka
kutokea.Kwa namna alivyonisisitiza
nikaamua kutoka haraka bila kumuaga
mtu yeyote ili kuona kama kweli kuna
jambo litatokea na kweli baada ya
muda jengo likalipuliwa.Irene alikuwa
na taarifa za kuhusiana na shambulio
lile na ndiye aliyenikoa” akasema
Agatha.Ernest akazidi
kuchanganyikiwa
“I cant believe this!!Irene
alifahamuje kama kuna shambulio
linakwenda kutokea? Akauliza rais
“Hata mimi sifahamu
alifahamuje.Baada ya kunusurika
katika shambulio lile nilienda kujificha
mahala salama na mtu pekee
niliyemueleza mahala nilipokuwa ni
Silvanus Kiwembe.”
“Ulimtaarifu Silva?!!Mbona
hakunijulisha wakati nilimpa jukumu la
kukutafuta na kufahamu mahala ulipo?
Akauliza
“Nilimwambia asikujulishe kwani
nilifahamu kuwa miongoni mwa watu
wanaokuzunguka wapo wasaliti kwa
hiyo sikutaka kujulikana nilikuwa
wapi.Nilitaka kwanza nifanye
uchunguzi kujua Irene alipataje taarifa
zile za kuwapo kwa lile
shambulio.Nilimshirikisha Silva suala
hili naye akapanga vijana wake
kumtafuta Irene lakini tukagundua
alikuwa anashirikiana na watu
tusiowafahamu ambao ni hatari.Mara
kadhaa vijana aliowapanga Silva
kumtafuta Irene walijaribu kumkamata
lakini walikutana na upinzani mkali
kutoka kwa watu anaoshirikiana nao
Irene.Hali hiyo ikatulazimu
kuwachukua mateka wazazi wa Irene ili
kulazimisha Irene ajisalimishe na
akafanya hivyo.Wakati tukiendelea
kumuhoji ili kufahamu alipata wapi
taarifa za shambulio lile,watu wake
anaoshirikiana nao wakatokea na
kutushambulia,wakawaua vijana wetu
pamoja na Silva na mimi nikajeruhiwa
mguuni ila niliokolewa na kijana
mmoja baada ya kujitambulisha kama
mke wa rais.Baada ya kufanikiwa
kutoka salama ndipo nikakupigia simu
kukuomba msaada”akasema Agatha
‘This is unbelievable.Irene?!!
Ernest akauliza tena kwa
mshangao.Hakuamini kama Irene
maboko ndiye aliyevujisha taarifa za
kuwepo kwa shambulio lile kwa mke
wake.
“Ernest suala hili si dogo na kuna
ulazima wa kulifuatilia kufahamu Irene
alitoa wapi taarifa za shambulio
lile.Inawezekana labda anashirikiana
na magaidi? Lazima atafutwe kokote
aliko na apatikane aeleze alifahamuje
kuwepo kwa shambulio katika ile
hoteli” Akasema Agatha
“Agatha umezidi kuichanganya
akili yangu.Irene maboko ni msichana
ambaye ni vigumu kuamini kama
anaweza kuwa na taarifa kama
hizo.Mimi na yeye ni sawa na baba na
mwana kwa nini hakuja kwangu moja
kwa moja na kunieleza kuhusiana na
taarifa hizo? Halafu kitu cha ajabu toka
ulipotokea mlipuko ule hajulikani yuko
wapi” akasema Ernest
“Hata mimi nina mashaka na yule
binti yawezekana anashirikiana na
watu waliofanya mashambulio yale.
Anatakiwa atafutwe kwa kila namna na
akipatikana basi tunaweza kupata
taarifa za muhimu sana.Yule binti
anafahamu kila kitu” akasema Agatha
“Swali lingine,kama alifahamu
kuhusu kuwepo kwa shambulio lile
kwa nini basi hakuweza kuripoti katika
vyombo husika ili kulizuia au hata
kuwaokoa watu waliokuwamo ndani na
badala yake akachagua kukuokoa
wewe peke yako? Akauliza Ernest.
“Muda mfupi baada ya kutoka
kwenye ile bustani ya wanyama jana
usiku nilipigiwa simu na baba Alberto
mkuu akanieleza kwamba yale
mashambulio yote mawili yaliyotokea
hapa Tanzania ni mipango yao kwani
walikuwa wanahitaji kutoa sadaka ya
damu inayopaswa kutolewa kila
mwaka.Mimi kubaki hai pia ulikuwa ni
mpango wao” akasema Agatha na
Ernest akajikuta akipandwa na hasira
kama mtu aliyerukwa na akili
akamshika shingo Agatha na kusema
kwa hasira huku akitetemeka
“That’s not true.Mimi si alberto’s I
hate them na nimefanya haya yote ili
kuwafuta kabisa katika ardhi ya
Tanzania !!
“You did that?!! Akauliza Agatha
kwa mshangao mkuwa na kuutoa
mkono wa Ernest shingoni kwake
akamsukumia pembeni.
“Answer me.Ni wewe uliyeratibu
mashambulio yale kwa ajiliya kuwaua
Alberto’s?? akauliza Agatha.Ernest
hakujibu kitu akabaki kimya ameshika
kichwa.
“What have I done? Kwa nini
nimetamka siri hii kubwa mbele ya
huyu shetani.Huyu mwanamke ni
mchawi mkubwa na ametumia nguvu
zake za kichawi mpaka nimejikuta
nikiropoka mimi mwenyewe siri hii
kubwa.Mambo yanazidi kuniharibikia”
akawaza Ernest
“Ernest umetamka kwa mdomo
wako kwamba ulifanya vile ili
kuwaondoa Alberto’s wote hapa
nchini.Ulitaka kuniua na mimi pia?!!
Akauliza Agatha kwa ukali.Ernest
hakujibu kitu.Agatha akamsogelea
“kwa nini umekuwa na roho ya
ukatili kiasi hicho? You wanted to kill
your own wife?Umesahau mambo yote
tuliyopitia na ukataka kuniua? Akauliza
na kumnasa Ernest kibao.
“Wewe una faida gani hapa
duniani hata ukifa?Umewaua watoto
wako wote kwa ujinga wako kuna faida
gani ya kukuacha hai? Ni bora ufe
upunguze idadi ya watu shetani wewe !!
akasema Ernest
“You are so wrong Ernest
.Unadhani utaweza kupambana na
Alberto’s? Ulikula kiapo kwa kunywa
damu na kiapo kile kitadumu hadi siku
yako ya mwisho hapa duniani .Wewe
bado ni Alberto’s na yote haya
uliyoyafanya bado ni kazi za
Alberto’s.Wanaendelea kukutumia na
utaendelea kuwatumikia daima”
akasema Agatha na kuzidi
kumpandisha hasira Ernest.
“Say that again and I’m going to
kill you right here !!! Ernest akasema
kwa ukali, alikuwa na hasira kali mno
hadi mwili ukimtetemeka.
“You wont kill me Ernest.Endapo
bado una mipango hiyo iondoe kabisa
katika akili yako kwani mimi nimebaki
hai peke yanu miongoni mwa Alberto’s
kwa ajili ya kazimoja ya muhimu nayo
ni kuijenga upya Alberto’s.Isitoshe
ukifikiria kunia fikiria pia kumpoteza
mwanao Monica”
Ernest mkasa akahisi kama
nyundo kubwa imetua kichwani
aliposikia Agatha akimtaja
Monica.Akamvaa na kumuangusha
kitandani. Akamkaba shingo na
purukushani ikaanza
“Nikisikia unalitaja tena jina hilo
nitakuchinja !! Umenisikia ? akauliza
kwa ukali Ernest akiwa amemkaba
Agatha kwa nguvu shingoni kiasi cha
kumfanya apumue kwa shida
“Umenisikia wewe shetani?!!
Akauliza Ernest
“Huyu mjinga ataniua kweli kama
nisipojitahidi kujiokoa” akawaza
Agatha na kunyoosha mkono akaishika
taa iliyokuwa pembeni ya kitanda na
kumpiga nayo Ernest kichwani
akaanguka chini.
“You want to fight with me?!
Akauliza Ernest kwa ukali huku
akitetemeka kwa hasira halafu
akajiinua pale chini na kuelekea katika
kabati lake.Agatha alifahamu
alichokuwa anakitafuta Ernest kabatini
na kwa haraka akauchukua mkasi
uliokuwa katika meza ndogo
akamkimbilia Ernest.
Ernest akasikia vishindo vya
Agatha akimkimbilia akageuka mara
moja akiwa na bastora mkononi
akamlenga Agatha lakini kabla
hajafanya lolote Agatha ambaye naye
alikuwa amepandwa na hasira kali
akamvaa Ernest na kumuangusha
chini.Bastora ya Ernest ikaanguka
pembeni na Agatha akamkalia
juu.Ernest akamchapa ngumi nzito
Agatha iliyomuangusha chini akataka
kuiokota bastora yake lakini Agatha
akakiona kitendo kile na kuokota
mkasi uliokuwa karibu yake
akauzamisha katika shingo ya Ernest.
“Go to hell you devil !!! akasema
kwa ukali.Ernest akaanguka pembeni
huku akitapa tapa na damu nyingi
ikaanza kumwagika.Agatha akainuka
pale chini huku damu ikimtoka
mdomoni.Ghafla Agatha akawa ni kama
mtu aliyestuka toka usingizini baada ya
kumuona Ernest akitapa tapa huku
akitokwa na damu nyingi.
“Ernest!! Akaita Agatha
“Ernest !! akaita tena kwa nguvu
na kisha akauchomoa ule mkasi
mkubwa shingoni mwa Ernest na damu
nyingi ikaruka.
“Nimeua !! akasema huku
akitetema
“Nimeua !!!
Agatha akaanza kutetemeka kwa
woga.Alishindwa afanye
nini.Akamtazama Ernest aliyekuwa
amelala katika dimbwi la damu.
“Nini kimetokea? Mbona kama
nilikuwa ndotoni? Akajiuliza Agatha
“Hapana hii si ndoto.Nimemuua
Ernest.Nimemuua rais wa nchi.!!
Akawaza na mara simu ya rais ikaita
Agatha akazidi kuogopa.Akaichukua
simu ile akatazama mpigaji alikuwa ni
Jenerali Lameck.Akaikata na kuzima
simu.Baada ya sekunde kadhaa
akasikia mlango wa chumba
ukigongwa.Agatha akazidi
kuchanganyikiwa.Mara akaiona
bastora pembeni na alipokuwa amelala
Ernest mkasa akaichukua.Mlango
ukagongwa kwa mara ya pili.
“Kila kitu
kimeharibika.Nikikamatwa hapa ni
kwenda gerezani na sintoweza kutoka
tena.Maisha yangu yameishia hapa….”
akawaza Agatha huku machozi
yakimtoka na kuuweka mdomo wa
bastora chini ya kidevu.Mlango
ukagongwa kwa mara ya tatu na mara
ukasikika mlio wa risasi.Mlango wa
chumba cha rais ukapigwa na
kufunguka wakaingia walinzi wa rais
na kuwakuita rais na mke wake wakiwa
wamelala chini katika damu.Haraka
haraka gari la wagonjwa likaletwa
wakapakiwa na kukimbizwa hospitali.
KINSHASA – DRC
Msafara wa David Zumo uliwasili
katika nyumba walimofikia Monica na
wenzake akina Austin.Tayari ni saa
tatu za usiku.Ndani ya gari David
alikuwa na Monica ambaye baada ya
shughuli za mazishi ya Pauline
hakurejea katika makazi yake
aliyoandaliwa bali aliungana na
viongozi wa mataifa na wawakilishi
wao katika chakula maalum
kilichoandaliwa na rais David kwa ajili
yao.
“Karibu ndani Monica” akasema
David huku akimfungulia Monica
mlango.Walinzi wote wakabaki
nje.Sebuleni Yasmin na maria walikuwa
wanatazama runinga.Walitaka kuondoa
walipomuona David Zumo lakini
akawataka waendelee kutazama
akamuongoza Monica kuelekea katika
sebule nyingine.Nyumba ile ilikuwa na
sebule tatu.
“Monica sipati neno zuri la
kukushukuru kwa ushirikiano ulionipa
kwa kuacha shughuli zako na kuja
kuungana nami katika mazishi ya
Pauline.Ahsante sana” akasema David
“Usijali David.Ni wajibu wangu
kufanya hivi.Hakuna ambacho
kingenizuia nisifike katika mazishi ya
Pauline.Hata kama Pauline na mmoja
wazazi wangu wangefariki katika siku
moja basi ningehudhuria kwanza
mazishi ya Pauline.Nimebahatika
kukutana na Pauline katika siku za
mwisho za uhai wake lakini nakiri
sijawahi kukutana na mwanamke
mwenye upendo wa ajabu kama yeye
katika maisha yangu. David umepoteza
kitu cha thamani kubwa sana”
“Nakubaliana nawe
Monica.Pauline alikuwa ni mtu mwenye
upendo wa aina yake.Alimpenda kila
mtu na ndiyo maana umeona maelfu ya
watu waliofurika leo kuja kumsindikiza
katika safari yake ya
mwisho.Alipendwa na kila mtu hapa
Congo lakini Mungu ana makusudi yake
,ameondoka Pauline na ameniletea
zawadi nyingine ambayo ni
wewe.Naweza kusema kwamba Mungu
ananipendelea sana mimi kwa
kuniletea wanawake ambao ni adimu
sana kuwapata katika ulimwengu wa
sasa.Monica nina bahati sana kukupata
na sijui nitamshukuruje Mungu kwa
Baraka hizi anazonijalia” akasema
David
“Monica siku imekuwa ndefu sana
na unahitaji upumzike kwa hiyo sitaki
kukuchosha sana nataka kuzungumza
na akina Austin.Nataka tulizungumze
suala lao ili nione namna ya
kuwasaidia”akasema David.Monica
akaenda katika chumba cha akina
Austin akagonga na Austin akaufungua
mlango
“Queen Monica” akasema Austin
na uso wa Monica ukachanua tabasamu
“Mmeshindaje leo? Akauliza
“ Tumeshinda salama.Pole kwa
shughuli nzito ya leo” akasema Austin
“Ahsanteni sana.Shughuli
imekwisha salama.Tutazungumza zaidi
baadae lakini nimekuja na David
anahitaji kuonana nanyi ili tuzungumze
lile suala letu.Kuna taarifa zozote toka
Dar es salam kwa Job? Akauliza Monica
‘Nimezungumza na Job asubuhi na
walifanikiwa kuwakomboa wazazi wa
Irene.They are all safe” akasema Austin
“That’s good news.Tutaongea zaidi
baadae twendeni tukaonane na rais
David” akasema Monica kisha
wakaongozana hadi sebuleni
alikokuwepo David
“Pole sana mheshimiwa rais kwa
shughuli nzito ya leo.Pamojana kuwa
katika kipindi kigumu lakini umetafua
muda na kuja kuonana nasi.Hii ni
heshima kubwa umetupa” akasema
Austin
“Usijali Austin.Suala hili pia ni la
muhimu sana kwani linahusu maslahi
ya nchi ambayo mimi naichukulia Kama
nyumbani.Tanzania ni kama nyumbani
kwetu k wani kwa miaka mingi watu wa
Congo wameishi Tanzania wakati ule
ambao nchi ilikuwa imegubiokwa na
vita vya wenyewe kwa wenyewe.Suala
lolote linalohusu maslahi ya Tanzania
linanihusu kwa sababu Tanzania ndiko
anakotoka malkia mtarajiwa wa Congo”
akasema na wote wakatabasamu
“Jana ulinieleza kwa kifupi juu ya
suala hili lakini kwa kuwa leo ninao
muda wa kutosha ninaomba unieleze
kwa kirefu nilifahamu kwa kina zaidi
suala hili ili na mimi nione nitatoa
mchango gani kutokana na uzito wa
suala lenyewe” akasema David.
Austin akaanza kumuelezea David
toka mwanzo hadi pale
walipofikia.David akabaki kinywa wazi
“Mhh ! haya ni mambo mazito
sana.Sikuwahi kufikiri kama siku moja
Tanzania ingefika hapa
ilipofika.Nimestuka sana.” Akasema
halafu baada ya muda kidogo akauliza
“Kwa hiyo ni msaada upi zaidi
mnaohitaji niwasaidie?
‘Tunahitaji kuwapatia Yasmin na
familia yake sehemu ya kwenda kuishi
mbali mahala ambako haitakuwa rahisi
kwa IS kuwafahamu.Wanahitaji majina
na pasi mpya za kusafiria.wanahitaji
mtaji au biashara yoyote ambayo
itawasaidia kuendesha maisha
yao.Endapo tukivikamilisha hivyo vitu
basi Yasmin atatuonyesha mahala
alipoificha hati ya muungano” akasema
Austin
“Nimewasikia Austin na ombi lenu
nimelipokea ila naomba mfahamu
kwamba kwa kufanya haya tayari
nimeingia katika msuguano na rais
wenu Ernest Mkasa.Asubuhi ya leo
amenipigia simu kuniuliza kama
niliwaweka kizuizini nikamweleza
ukweli kwamba sikuwaweka kizuizini
kwa sababu sikuona kosa lolote
mlilonalo hivyo nikawaachia
huru.Hakufurahishwa na jambo hili
lakini baada ya kunipa picha kamili
sasa nnafahamu kwa nini anatumia
nguvu kubwa namna hii
kuwatafuta.Hata hivyo nawahakikishia
kuwapeni ushirikiano mkubwa sana
hadi mfanikisha suala
lenu.Ninachohitaji kujua ni mipango
yenu baada ya kufanikisha kupata hati
ya mungano.Mmepanga kufanya nini?
“Kitu tulichopanga kukifanya ni
kukusanya ushahidi wa kutosha wa
kumuhusisha rais na mashambulio yale
mawili na kisha tutamfikisha
mahakamani.Hapa ninamaanisha
kwamba lazima tumuondoe
madarakani na kisha tumfikishe mbele
ya sheria”
“Nitawasadia kwa hilo.Nitawapa
ushirikiano wa kutosha na kuhakikisha
Ernest mkasa anafikishwa katika
sheria.Niachieni suala hilo nilifanyie
kazi na kesho nitakuwa na jibu la
kuwapa” akasema David wakaendelea
na maongezi hadi ilipotimu saa sita za
usiku wakaagana na Ernest akaondoka
na Monica wakaelekea chumbani.
“Ahsante sana David kwa kujitolea
kuwasaidia wenzangu hawa
walioyaweka maisha yao hatarini
wakipambana kwa ajili ya nchi
yao.Najua utaingia katika mgogoro na
rais Ernest lakini usikate tamaa
endelea kutusaidia” akasema Monica
wakiwa chumbani
“Monica mambo aliyonieleza
Austin yamenigusa sana na hasa baada
ya kuisikia rekodi ile ya mazungumzo
kati ya rais Ernest na mkuu wa majeshi
wa Tanzania wakiongelea kuhusiana na
yale mashambulizi.Nimeumia sana
kuona mtu kama rais anatumia
madaraka yake kuteketeza roho za
watu wasio na hatia yoyote.Nitatoa
msaada wa kila aina hadi nihakikishe
Yule mzee anafikishwa mbele ya
sheria.Ni wakati wa kuisaidia Tanzania
kwani wakati wa mapigano ya
wenyewe kwa wenyewe hapa Congo
Tanzania walisimama kidete na hata
kutuma vikosi vya jeshi kuja
kupambana na waasi na sasa ni zamu
yetu kusimama kwa ajili ya ndugu zetu
wa Tanzania” Akasema David halafu
wakaingia kuoga na kisha wakarejea
kitandani
“Monica ulinieleza kwamba kuna
jambo unataka kunieleza siku tukipata
nafasi.Wakati ni huu ambao unaweza
ukanieleza” Akasema David.Monica
akastuka na kuingiwa na woga.
“Nieleze malaika wangu
ninakusikia” akasema David na
kumbusu
“David nina jambo zito ambalo
nataka nikueleze na sijui
utalichukuliaje lakini sina budi
kukueleza”
“Nieleze malaika wangu.Hata
kama ni jambo gumu ambalo huwezi
kumueleza mtu mwingie yeyote nieleze
mimi nitakusikiliza.Hata kama
umewahi kuua mtu niambie na itabaki
kuwa siri yangu” akasema David na
wote wakachela
“David wewe ndiye uliyekuwa
mwanaume wangu wa kwanza kuingia
naye katika mahusiano na ni wewe
uliyeniondoa usichana
wangu.”akasema Monica akamtazama
David halafu akaendelea
“Niliporejea Dar es salaam
nilikumbuka kwamba tulifanya
mapenzi katika tarehe zangu za hatari
na hata tarehe zilipofika sikuona siku
zangu.Suala hili limekuwa linanitesa
mno akili yangu.Nikamshirikisha mama
na akaniambia kwamba kuna
uwezekano labda nimeshika ujauzito
japokuwa sina uhakika bado hadi hapo
nitakapop….” Monica hakumaliza
sentesni yake David akamrukia na
kuanza kumporomoshea mabusu
mazito.
“Monica niambie kama taarifa hizi
si utani.”
“Si utani David ni taarifa za kweli
na ndiyo maana sikutaka kukueleza
katika simu nikasubiri nije nikueleze
ana kwa ana.Hilo ndilo jambo ambalo
limekuwa linaniumiza kichwa kwani
sikuwa nimepanga kupata mtoto kabla
ya ndoa” akasema Monica na
kuinamisha kichwa
“Monica malaika wangu
nakuomba tafadhali usiumize kichwa
chako kwa suala hili.Hizi ni Baraka
Mungu ametujalia.Hiki kilikuwa ni kilio
changu cha miaka mingi nikiomba
mtoto hatimaye leo hii ombi langu
limejibiwa na ninakwenda kuitwa
baba.Oh ahsante Mungu”akasema
David na kushindwa kuyazuia machozi
ya furaha kumtoka.Monica naye
akapatwa na hisia kali akamkumbatia
David na wote machozi yakawatoka
“Sijawahi katika maisha yangu
kupata taarifa ambayo imenifurahisha
hadi kunitoa machozi.Hii ni taarifa ya
kwanza kuniliza.Nimefurahi kupita
maelezo na sijui nikwambie nini
Monica malaika wangu.Nimshukuruje
Mungu kwa Baraka hizi ambazo vidole
havitoshi kuzihesabu?Itoshe kusema tu
ahsante Mungu” Akasema David
“David nimeharakisha kukueleza
suala hili lakini bado sina uhakika
kama kweli nina ujauzito ama vipi hadi
hapo tutakapofanya kipimo ndipo
tutajua”
“Monica nina uhakika mkubwa
hiyo lazima itakuwa ni mimba.Kesho
watakuja madaktari hapa watakupima
kama unavyotaka lakini nina uhakika
kabisa lazima humo tumboni mwako
umebeba kiumbe kitakachovishwa taji
la urtawala wa Congo.Umebeba mrithi
wangu.Umebeba mfalme au malkia wa
baadae wa Congo” akasema David kwa
furaha na kumkumbatia tena Monica
kwa nguvu huku akimwagia
mabusu.David alisahau kabisa kama
bado alikuwa katika majozi ya kufiwa
na mke wake kutokana furaha
aliyokuwa nayo
“Endapo kweli utakuwa mja mzito
nitafanya haraka sana ili tuweze
kufunga ndoa na mtoto wetu aanze
kulelewa katika jumba la kifalme toka
akiwa mdogo” akasema David.Ulikuwa
ni usiku wa aina yake ambao David
alihisi kama vile hayuko katika dunia
hii.waliongea na kupanga mambo
mengi kuhusiana na maisha yao ya
usoni.
DAR ES SALAAM - TANZANIA
Baada ya chakula cha usiku Job
akawataka watu wote waende
vyumbani mwao kupumzika.Sebuleni
akabaki na Marcelo na Julieth
akawataka waelekee katika chumba
alimowekwa Monalisa.Aliufungua
mlango wa chumba kile maalum kwa
ajili ya mahojiano na kuingia
ndani.Mstuko alioupata Monalisa
ulkuwa mkubwa sana na hakuamni
macho yake kwa kile alichokiona.
“My God !! akasema Monalisa kwa
mshangao
“This is unbeliavable..!! Job !!
akasema Monalisa bado akishangaa.Job
akavuta kiti na kuketi
“Halo Monalisa.habari za siku
nyingi? Habari za Arusha? Akauliza Job
na Monalisa alishindwa kuongea
midomo ilikuwa inamtetemeka.
“Relax Mona” akasema Job huku
akitabasamu kwa namna Monalisa
alivyokuwa anaweweseka baada ya
kumuona.Baada ya muda akasema
“Karibu tena Dar es salaam Mona”
Akasema na kunyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Samahani sana Monalisa kwa
kukuchukua kwa vurugu namna ile
lakini imenilazimu nifanye hivyo kwani
kukupata kwa njia ya kawaida
isingewezekana.Nimekuleta hapa kwa
ajili ya jambo moja tu ambalo
ukinisaidia nikalipata basi nitakuachia
uende zako lakini endapo utashindwa
kunipa ushirikiano basi nakuhakikishia
utakuwa ndio,mwisho wako wa kuliona
jua” akasema Job na taratibu sura yake
ikaanza kubadilika na kuonyesha
kwamba alianza kupandwa na
hasira.Monalisa akazidi kuogopa.
“Sitaki kufukua kaburi na
kukumbusha mambo yaliyopita baina
yetu kwani imebaki historia lakini
ninachokihitaji kwa sasa ni kufahamu
alipo mwanangu Millen.Nionyeshe alipo
mwanangu na nitakuachia ukaendelee
na maisha yako” akasema Job.Monalisa
akamtazama akashindwa
kuzungumza.Job akainuka
akamsogelea
“Mona huwezi kuongea? Wewe ni
bubu? Nieleze aliko
mwananguMonalisa” akasema Job
lakini bado midomo ya Monalisa
ilikuwa inamtetemeka na akashindwa
kuzungumza.
Ghafla bila kutegemea Job
akamnasa kibao kikali sana na
kumfanya apige kelele.
“Nadhani sasa unaweza
kunijibu.Ukishindwa kunipa jibu
nitakufanyia kitu kibaya sana.Tafadhali
usinilazimishe nikufanyie kitu kibaya
kwani nakuheshimu kama mama wa
mwanangu lakini endapo utaendelea
kukaa kimya utanilazimisha
nikuharibu.Nitachukua kisu na
kuukwangua uso wako na kuuondoa
huo uzuri wote ulio nao.Nakuuliza mara
ya mwisho mwanangu Millen yuko
wapi? Akauliza Job lakini Monalisa
aliendea kulia huku akitetemeka kwa
woga.
“Nadhani bado hujanifahamu
vizuri.I’m a monster!! Mimi ni mtu
mbaya sana
ukinikorofisha.Nitakuonyesha upande
wangu wa pili ambao hujawahi kuuona”
akasema Job na kulifugua sanduku lake
dogo jekundu.Marcelo akamuwahi
“Job subiri kidogo usimfanye
chochote.Let me talk to her” akasema
Marcelo
“Marcelo stay out of this” akasema
Job
“Job nakuomba tafadhali nipe
dakika mbili nizungumze naye ili aweze
kujibu swali ulilomuliza.Usimtese
tafadhali huyu ni mama wa mtoto
wako.Wewe na yeye mmewahi kuwa na
historia.Dakika mbili tu naomba”
akasema Marcelo.Job akamtazama
Marcelo na kusema
“Ok two minutes!! Akasema Job
“Naweza kubaki naye peke yake
tafadhali!! Akasema marelo.Job na
Julieth wakatoka nje
Marcelo akamuendea Monalisa
pale kitini na kumshika mabegani
“Monalisa look at me.My name is
Dr Marcelo.Tafadhali naomba
unisikilize na ufanye kile
nitakachokueleza.Take a deep breath”
akasema Marcelo na Monalisa akavuta
pumzi ndefu mara tatu akimfuatisha
Marcelo
“Good.Sasa nisikilize.Job
unamfahamu vizuri kwani aliwahi
kuwa mumeo lakini Job huyu
umuonaye sasa si yule ambaye
ulimfahamu awali.Katika kipindi
ambacho wewe na yeye mmetengana
amepitia mambo mengi sana magumu
kwa hiyo tafadhali usijaribu kumfanyia
mchezo au kiburi cha aina
yoyote.Msikilize na umjibu kila kile
atakachokuuliza.Nimemshuhudia
wakati akiwa kazini ni mkatili sana na
hana huruma hata kidogo.Amekuambia
kwamba atakuharibu uzuri wako wote
na atafanya hivyo endapo hautamjibu
kile anachokitaka.Narudia tena
kukuomba Mona Job hana shida na
wewe hata kidogo na ndiyo maana
mpaka sasa hajakutesa lakini
usimlazimishe akutese ,mueleze aliko
mwanae kwani hiyo ndiyo shida yake”
akasema Marcelo.Huku akilia Monalisa
akasema
“Ninaogopa kumueeza aliko
mwanangu atamchukua na kuja kuishi
naye katika maisha haya ya taabu.Sitaki
kumpoteza mwanangu” akasema
Monalisa
“Monalisa tafadhali nakuonea
huruma sana.Usipomuonyesha mahala
alipo mwanae sina hakika kama
utatoka salama katika hii
nyumba.Mueleze alipo mwanae na
muyamalize haya mambo.Tafadhali
nakuomba” akasema Marcelo na mara
mlango ukafunguliwa akaingia Job na
Julieth
“Dakika mbili
zimekwisha.Niachieni nafasi niifanye
kazi yangu” akasema Job
“Monalisa fanya kama
nilivyokuelekeza” akasema Marcelo
kisha yeye na Julieth wakatoka nje
akabaki Job peke yake mle ndani
“Sasa tumebaki wawili.Uko tayari
kunionyesha alipo mwanangu au
nianze kuifanya kazi yangu? Akauliza
Job.Monalisa akashindwa kuzungumza
kutokana na woga aliokuwa nao
“Fine.Hutaki kuzungumza kwa
hiari sasa utazungumza kwa lazima”
akasema Job na kuchukua baadhi ya
vifaa vya kutesea akaviweka mezani
“Job usinitese tafadhali !! akasema
Monalisa huku akilia
“Ukitaka nisikutese Mona
nionyeshe alipo mwanangu.Mimi sina
shida na wewe!! Akasema Job
“Job tafadhali usimchukue
mwanangu.Yeye ndiye kila kitu
kwangu!! Akasema Mona huku akilia
“Mona usinipotezee wakati
wangu.Nionyeshe alipo Millen ama
sivyo hatatoka salama humu ndani!!
Akasema Job na kuchukua kifaa kidogo
kinachojlikana kama koleo akakishika
kidole cha Monalisa na kuibana kucha
kwa lengo la kuibandua .
“Basi Job nitakueleza kila
kitu.Tafadhali usinitese!! Akasema
Monalisa.Job akamtazamana kwa
hasira
“Millen anasoma Arusha katika
shule ya kimataifa inaitwa Mama
Theresa international school.” Akasema
Monalisa
“Nitawezaje kumpata?
“Job tafadhali usimchukue mtoto
muache amalize shule!! Akasema Mona
“Mona tafadhali
usinichezee.Nahitaji kumpata
mwanangu.Siwezi kumuacha
mwanangu akasomeshwa kwa fedha
haramu” Akasema Job na kutoa simu ya
Monalisa katika mkoba na kumpatia
“Piga shuleni kwa akina Millen na
uwafahamishe walimu kwamba
umepata msiba na unamuhitaji Millen
Dar es salaam kesho.Waeleze kwamba
wewe hautaweza kufika bali utamtuma
mtu akamchukue” Akasema Job
Monalisa akaishika simu
akazitafuta namba za mkuu wa shule
anakosoma mwanae Millen akampigia
na kumtaarifu kwamba amepata
matatizo ya kifamilia na hivyo
anamuhitaji Millen kesho afike Dar es
salaam.Alimaliza kuzungumza na mkuu
wa shule akaiweka simu mezani na
kuangua kilio.
“Job tafadhali nakuomba
usimchukue mwanangu!! Akasema
Monalisa huku akilia
“Kesho nakwenda kumchukua
mwanangu Arusha na hautamuona tena
katika maisha yako” akasema Job kwa
ukali
“Job nakuomba
tafadhali.Nitafanya kila
utakachoniamuru nifanye lakini
usimchukue mwanangu” akazidi kulia
Monalisa
“Yule ni mwanangu pia na
ninakuhakikishia kwamba hautamuona
tena katika maisha yako.Wewe
mwanamke ni shetani mkubwa!!
Akafoka Job akamtazama Mona kwa
hasira na kusema
“Kwa muda wa miaka kadhaa
nimeteseka sana mateso ambayo
yamesababishwa na wewe.Nililazimika
kuishi kama kichaa nikila na kunywa
majalalani kwa ajili ya kuwakimbia
watu ambao walitaka kuniua kwa
sababu yako.Mambo niliyoyapitia ni
mazito na siwezi kukueleza kwani
ndicho hasa ulichokuwa
unakihitaji,mimi niteseke au niuawe na
wewe ubaki huru ukifurahia maisha na
huyo bwana wako” akasema Job na
kuendelea kumtazama Monalisa kwa
macho makali
“Nilipoamua kuacha wanawake
wote wa dunia hii na kukuchagua wewe
nikiamini kwamba wewe ndiye pekee
uliyeumbwa kwa ajili
yangu,sikutegemea kabisa kama siku
moja ungekuja kufanya jambo kama hili
ulilolifanya.Sikutegemea kama siku
moja ungeweza kufanya kitendo
kikubwa cha usaliti kama
ulichokifanya.Pamoja na kuyatoa
maisha yangu kukupa kila ulichokitaka
lakini bado hukutosheka.Sitaki
kuongeleza zaidi suala hilo
ninachokihitaji kukifahamu huyo Don
ambaye uliamua kuniacha ukakimbia
naye ni nani? Akauliza Job.Monalisa
hakujibu kitu
“Nijibu Monalisa.Nahitaji
kumfahamu huyo mtu
aliyekuchanganya hadi ukaamua
kuniacha ni nani? Akauliza tena lakini
Monalisa alibaki akilia hakujibu kitu.
“Nilikuonya toka awali kwamba
sipendi kupotezewa muda
wangu.Nikikuuliza nataka jibu mara
moja” Akasema Job na kuchukua koleo
akamshika mkono na kukiminya kidole
kimoja.Monalisa akapiga ukelele
mkubwa
“Hata ukipaaza sauti ya namna
gani hakuna atakayekusikia.Ni mimi na
wewe tu humu ndani.Usiponijbu
nitaanza kuziondoa kucha zako nzuri
moja baada ya nyingine.Maumivu yake
siwezi kukuelezea.Nakupa sekunde
tano unijibu Don ni nani? Akauliza Job
na kutazama saa yake.
“Sekunde tano zimekwisha.sasa
nakuonyesha nilivyo mkatili!! Akasema
Job na kuchukua tena koleo.
“Nitakueleza Job usiendelee
kunitesa” akasema Monalisa
“Nijibu haraka sana” akasema Job
“Mtu niliyenaye ambaye sifahamu
kama anaitwa Don ni rais wa Tanzania”
akasema Mona
‘What ?!!
‘hebu rudia tena!!
“Mwanaume niliyenaye ni rais wa
Tanzania”
‘Oh my God !! Ernest Mkasa
again??akasema Job .Alistuka sana
kusikia habari ile.
“Ndiyo maana ulikuwa tayari mimi
nife ili upate nafasi ya kuwa na huyo
mzee wako_Oh Monalisa ulikosea sana
kukubali kuwa hawara ya Yule mzee.Ni
bora kama ungeondoka na mwanaume
mwingine ningekuelewa lakini si Yule!!
akasema Job akiendelea kumtazama
Mona kwa hasira
“Nashindwa nikufanye
nini.Natamani nikukate kate vipande
vipande ili hasira zangu zote ziishe
lakini haitasaidia.Usiku huu nitautumia
kutafakari nini nikufanye shetani wewe
!! Utakaponiona kesho asubuhi ujue
hatima yako imefika !! akasema Job na
kutoka mle chumbani akawakuta
Marcelo na Julieth nje yakile chumba
wakimsubiri.
“Pole sana Job.Make a deep breath
!! akasema Marcelo baada ya kuona
namna Job alivyokuwa amebadilika.
“Siamini nilichokisikia.Kumbe
Ernest mkasa ndiye aliyenipora mke
wangu.Ndiye aliyesabaisha miaka hii
yote mimi nimeteseka na kuishi kama
kichaa nikila na kunywa katika
majalala.Nimechanganyikiwa na sijui
nifanye nini.Sijui nitamfanya nini huyu
mwanamke !! akasema Job
“Usimfanye chochote Job.Kwa
kuwa tayari umekwisha fahamu alipo
mwanao fanya jitihada za kumpata
mwanao na huyu mwanake muache
aende akaendelee na maisha yake.Hata
ukimkata mikono yote haitasaidia
kitu.Let her go.Mungu anayaona mateso
yako na atakusaidia siku moja na wewe
utampata mwanamke mwenye mapenzi
ya kweli” Akasema Marcelo.
Job akaegemea ukuta akawaza
kwa muda halafu akasema
“Julieth nahitaji msaada
wako.Nataka kesho asubuhi upande
ndege uende Arusha ukamchukue
mwanangu Millen.Nitagharamia safari
hiyo” akasema Job
“Hakuna tatizo lolote katika
hilo.Nitakwenda Arusha kesho
kumchukua mwanao na nitahakikisha
anafika hapa salama” akasema Julieth
Job akaachana na akina Marcelo
akaenda kumpigia simu Austin
akamfahamisha kila kitu kilichotokea
naye akataarifiwa kile kinachoendelea
kule Kinshasa na baada ya zaidi ya nusu
saa za maongezi wakaagana.

.
 
QUEEN MONICA : FINAL SEASON
SEHEMU YA 12

Siku ilikuwa ndefu sana kwa
Ernest Mkasa rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania.Aliwaongoza
watanzania kuaga miili ya watu
waliopoteza maisha kwenye shambulio
lililofanyika katika ukumbi wa bunge
na Dar es salaam.Baada ya shughuli za
kuaga miili kumalizika mjini Dodoma
rais akaelekea kisiwani Zanzibar
kuhudhuria mazishi ya makamu wa
rais aliyepoteza maisha katika mlipuko
jijini Dar es salaam.
Saa kumi na mbili za jioni rais
akarejea Dar es salaam.Katika uwanja
wa ndege akapokewa na viongozi mbali
mbali na kisha akelekea ikulu.Mara tu
alipofika ikulu akapewa taarifa
kuhusiana na hali ya usalama.Kikundi
cha kigaidi cha Alshabaab kilijitangza
kuhusika na mlipuko uliotokea katika
soko la kimataifa la samaki
asubuhi.Alipewa taarifa ya tukio
liliotokea na walinzi watatu kuuawa
baada ya gari lao kutupiwa bomu na
Monalisa akachukuliwa na watu
wasiojulikana.Taarifa hii ilimstua mno
rais.Hakupewa nafasi ya kupumzika
akataarifiwa kwamba mke wake Agatha
tayari amerejea nyumbani akitokea
hospitali na mwisho akataarifiwa
kwamba mgeni wake Bashar bin
Abdulsalaam tayari amekwisha wasili
na alikuwa anamsubiri.Ernest
akachanganyikiwa.Hakujua aanzie
wapi.Akaamua kwanza akaonane na
Bashar ndipo aendelee na mambo
mengine.Moja kwa moja akaelekeza
Bashar apelekwe katika chumba cha
maongezi ya faragha.
“Habari yako Bashar” rais Ernest
akamsalimu Bashar wakiwa katika
chumba cha maongezi ya faragha
“Habari nzuri sana mheshimiwa
rais”
“Karibu sana” Akasema rais
“Ahsante mheshimiwa rais.Poleni
sana kwa mambo yanayoendelea nchini
kwenu.Naamini baada ya muda si
mrefu mambo yatakaa sawa” Akasema
Bashar
‘Tunaomba iwe hivyo kwani
watanzania hawajazoea kuishi katika
hali ya mashaka mashaka kama
sasa.Hali hii itatulia si muda mrefu.”
“Mheshimiwa rais nafahamu una
majukumu mengine kwa hiyo nataka
nisikupotezee muda.Naomba
nijielekeze moja kwa moja katika kile
nilichotumwa kwako” akasema Basher
na kufungua mkoba wake akatoa
bahasha nyeupe akamkabidhi rais
ambaye aliifungua na kusoma barua
iliyokuwamo ndani yake.Kadiri
alivyozidi kuisoma ndivyo sura yake
ilivyozidi kubadilika na kujikunja.
Alipomaliza akaitupa barua ile mezani
na kumtazama Bashar kwa hasira
“Huu ni upuuzi mkubwa.Siwezi
katu kukubali ujinga kama huu”
akafoka rais huku akigonga meza kwa
hasira.Akaichukua tena barua ile na
kuanza kuisoma halafu akasimama
“Huu ni ujinga mkubwa sana.Watu
hawa waliokutuma ni wapuuzi
wakubwa.Siwezi mimi kutelekeza haya
wanayonitaka niyatekeleze.Katu siwezi
kukubali.” Akasema rais na kuketi
kitini akaichukua barua ile na kuisoma
tena kwa mara ya tatu
“kwako mheshimiwa rais wa
Tanzania
Tunamtuma mjumbe wetu maalum
kwako kufikisha ujumne huu wa
muhimu sana.Rejea makubaliano yetu
ya awali ambayo kwa makusudi kabisa
umemua kuyapuuza.Umetufanyia
kitendo cha kihuni na sisi tumefadhaika
sana kwa kitendo
ulichokifanya.Tumekaa kikao kujadili
suala hili na tumeamua yafuatayo.
Utabaki na hati ya muungano
wenu wa Tanganyika na Zanzibar
ambayo umekataa kwa makusudi
kutupatia,lakini sisi tunakitaka kisiwa
cha Pemba.Siku si nyingi kuanzia sasa
litatolewa tamko la kisiwa cha pemba
kutaka kujiondoa katika jamhuri ya
muungano wa Tanzania na kuwa nchi
huru.Wewe kama rais wa Tanzania
utaliunga mkono jambo hilo na
kuhakikisha linafanikiwa.Tunafahamu
ni suala gumu lakini tunakutaka
usimame imara kuhakikisha kwamba
linafanikiwa na kisiwa cha Pemba
kinajitoa kutoka jamhuri ya muungano
wa Tanzania na kuwa nchi
huru.Muungano utabaki wa Tanganyika
na kisiwa cha unguja pekee.
Mheshimiwa rais hii ni nafasi ya
pili tunakupa na kitendo chochote cha
kujaribu kulizuia suala hili litakuwa ni
tangazo la vita kati ya nchi yako na
mtandao wetu na ninakuhakikishia
kwamba Tanzania haitakuwa tena
kisiwa cha amani.Damu itamwagika kila
uchao.mamia ya watanzania
watapoteza maisha kila
siku.Tutasambaza watu wetu katika kila
mkoa na mashambulio yatatokea
sehemu mbali mbali za Tanzania.Hii
itakuwa ni vita ya vizazi na vizazi
haitakuwa na kikomo.Usitake
kulitumbukiza taifa lako katika vita hii
mheshimiwa rais.Tekeleza maagizo
tuliyokupa na Tanzania itakuwa
salama.
Tunakutakia utekelezaji mwema
Habib
Hivi ndivo barua ile
ilivyoandikwa.
Ndani ya kile chumba cha
maongezi ya faragha kulikuwa
kimya.Rais Ernest alizama katika
mawazo mazito.Bashar akatazama saa
yake na kumstua rais
“Mheshimiwa rais naona muda
unasonga kwa kasi natakiwa kuondoka
nchini ndani ya nusu saa ijayo.Ahsante
kwa mapokezi mazuri na kuupokea
ujumbe wangu.Kabla sijaondoka kuna
chochote unanituma nikawaambie
walionituma kwako?akauliza Bashar
“Ahsante sana kwa kufika na
kuufikisha ujumbe.Nimeupokea ila
wanipe muda niutafakari na nitawapa
majibu”akasema rais.Wakaagana na
Bashar akaondoka
“Kwa mara ya kwanza ninajutia
maamuzi yangu ya kutaka kupambana
na Alberto’s.Haya yote yasingetokea
endapo nisingeamua kupambana
nao.Kila likitoka hili linaingia lingine.”
akawaza rais na kuvua koti kwani
alihisi joto
“Nafahamu hizi ni njama za IS
kukipata kisiwa cha Pemba ili
waanzishe kundi lao kule.Yasmin
alinieleza kuhusu mipango ya
IS.Nitafanya nini ? Nikubaliane na
matakwa yao au niingie nao vitani ?
Akajuliza rais
“Endapo nitaamua kuingia katika
vita na hawa jamaa nchi hii amani
itatoweka kabisa, kwani hawa jama
wanafanya mashambulizi ya kustukiza
na kuua raia.Wangekuwa ni Alshabaab
peke yao ningeingia nao vitani kwani
ningetuma majeshi yetu yangewasaka
ndani ya Somalia na kuwamaliza kabisa
lakini katika hili suala naamini
Alashabaab wanashirikiana na IS na
hawa ni kundi kubwa la kigaidi
linaloitikisa dunia.I don’t know what to
do” akawaza na kumuta Jenerali lameck
ambaye alifika mara moja
“Lameck nimepokea ujumbe muda
mfupi kutoka kwa Habib lakini naamini
ni ujumbe wa IS ila wameupitisha kwa
habib.” Akasema rais na kumpa Lameck
ujumbe ule ausome.
“Mheshimiwa rais huu ni upuuzi
mkubwa sana.Umewapa jibu gani?
“Nimewaambia ujumbe
nimeupokea na nitautafakari ”
“Sikiliza mheshimwa rais jambo
hili haliwezekani kabisa.Hawa watu si
wa kuwapa nafasi na hawawezi
kutulazimisha tufanye wanavyotaka
wao”akasema Lameck
“Unashauri nini Lameck?
“Kataa ombi lao na waweke wazi
kwamba hilo haliwezekani” akasema
Lameck
“Hilo litakuwa ni tamko la vita kati
yetu na wao”akasema rais
“Then let’s go to war!! Hatuwezi
kukubali upuuzi wa namna
hii.Mheshimiwa rais tayari
tumetengeneza matatizo makubwa
ambayo tunakabiliana nayo hapa nchini
hatuwezi kukubali tena kuongeza
matatizo mengine.Ukilikubali ombi lao
hili litakuwa ni tatizo lingine kubwa na
ambalo hatutaweza kulitatua.Nchi hii
ambayo tunaipigania kuisafisha
itagawanyika na juhudi zetu zote
zitakuwa kazi bure.Damu yote
iliyomwagika itakuwa imekwenda
bure” Akasema Lameck
“Lameck unachokisema ni sahihi
na hata mimi sipendi kufanya vile
wanavyotaka lakini hawa jamaa ni
wabaya sana na sasa wanaungana na
IS.Unafahamu hawa jamaa namna
wanavyofaya mashambuluo yao kimya
kimya.Bado mfumo wa kutambua
mashambulio ya kigaidi katika nchi
yetu ni mdogo kwa hiyo wataitumia
nafasi hiyo kufanya mashambulio kila
uchao.Damu nyingi ya watanzania
itamwagika.Lameck sitaki tena
kuiingiza nchi hii katika majanga
mengine.Damu tuliyoimwaga damu
inatosah.No more blood” akasema rais
“Mheshimiwa rais,uliponiapisha
niwe mkuu wa majeshi ya ulinzi wa
nchi ya Tanzania niliapa kuwalinda raia
wa Tanzania dhidi ya wale wote
wanaotishia amani na ustawi wa taifa
hili.Hawa Alshabaab na IS wanatishia
amani yetu kwa hiyo siwezi kukaa
kimya lazima nisimame imara
kuhakikisha kwamba ninayaongoza
mapambano dhidi yao.Tukikubali leo
kisiwa cha Pemba kichukuliwe na IS
itakuwani hatari zaidi kwa usalama wa
nchi.Watajiimarisha na watakichukua
kisiwa cha Unguja pia na mwisho
watataka kuingia Tanzania
bara.Hulioni hilo mheshmwia rais?!!
Akauliza Lameck kwa sauti ya juu
kidogo.Ernest akainamisha kichwa
akatafakari baada ya muda akasema
“Asubuhi ya leo nilipigiwa simu na
Habib tukabishana kidogo na akasema
anataka kunionyesha nguvu yao.Baada
tu ya kukata simu ukatokea ule
mlipuko katika soko la samaki.Lameck
hawa jamaa wamejipanga vilivyo.Si
watu wa kufanyia mchezo.Tazama
mambo yanayotokea katika nchi za
jirani ambao wameingia katika
mapambano nao.Damu ya watu
wasiona hati ainamwagika.kama
wameweza kufanya shambulio jirani
kabis ana ikulu basi ni watu
waliojiandaa vizuri na wanachiokisema
wanawza wakakitekeleza.”
“Mheshimiwa rais walichokifanya
Alshabaab ni kukuogopesha na
kwuaogopesha watanzania lakini
usiingie katika mtego wao.Wanaweza
kuendelea kufanya mashambulio
mfululizo katika sehemu mbalimbali za
nchi kwa lengo la kuleta hofu lakini
nakuomba mzee usikate tamaa na
kuwapa wanachokitaka.Let’s fight.Tuna
jeshi imara na tukiamua kupamba nao
hawataweza kutushinda.Hiki ni kikundi
kidogo tu” akasema Lameck
“Alshabaab ni kikundi kidogo
lakini hatari na hasa wakiungana na
IS.Ni rahisi kupigana vita na adui
mkubwa kama nchi ambaye unajua
nguvu yake na unafahamu utampiga
wapi lakini hawa jamaa ni vigumu
kupigana nao kwa sababu hawajulikani
wako wapi,wako wangapi,uwapige
wapi na mashambulio yao ni ya
kuvizia”akasema rais
‘kwa hiyo umeamua nini
mheshimiwa rais?
“Niachie suala hilo nilitafakari
halafu nitakupa jibu nimeamua kitu
gani” akasema rais.Baada ya muda
kidogo akasema
“Lamec hatimaye zoezi letu
tumelimaliza rasmi leo.Japo
tumekutana na changamoto nyingi na
nyingine bado tunaendelea kukutana
nazo lakini tunastahili kujipongeza
kwani tumefanikiwa kukipata
tulichokihitaji.Alberto’s karibu wote
ninaowafahamu isipokuwa Agatha
pekee wameteketea.Huu ni ushindi
mkubwa japo tunaofahamu ni sisi
wawili pekee.Kinachofuata sasa ni
awamu ya pili ya zoezi letu ambayo ni
kukabiliana na athari zile zilizojitokeza
na zinazoendelea kujitokeza kutokana
na shambulio lile.Tunaendelea
kupambana ili nchi ibaki salama.Kwa
usiku huu nataka tujadili kuhusiana na
David Zumo” Akanyamaza kidogo kisha
akasema
“ Asubuhi kabla ya kwenda
Dodoma nilikueleza azma yangu ya
kutaka kuhitimisha utawala wa David
Zumo.”
“Ndiyo ulinieleza mheshimiwa rais
lakini nina swali dogo kwa nini
umefikiria jambo kama hilo? Kuna
sababu yoyote kubwa ya kukupelekea
ukafikiria kufanya hivyo?
‘Sababu kubwa ni kitendo chake
cha dharau alichokifanya.Nilimuomba
awakamate akina Yasmin lakini kwa
jeuri ameamua kuwaachia huru.Siwezi
katu kuvumilia kitu kama hiki.Endapo
taifa letu litabomoka basi na yeye
atakuwa na mchango mkubwa kwani
mtu ambaye anatembea na hati ya
muungano wetu alimtia mikononi na
akaamua kumuachia.Kingine ni
kwamba hawa jamaa akina Austin
naamini watakuwa wamemueleza kila
kitu kilichotokea kwa hiyo huyu ni mtu
hatari sana kwangu.Sababu ya tatu ni
ya kibinafsi zaidi lakini kwa kuwa
wewe ni mtu wangu wa karibu
nitakueleza.Ni kwamba David Zumo
tayari amempa mimba Monica.Sitaki
mbegu ya msaliti Yule ichanganyike na
damu yangu.Kwa sababu hizo kubwa
nataka nimuondoe
madarakani”akasema rais.Jenerali
Lameck akavuta pumzi ndefu.Alihisi
kuchoka mwili na akili
“Mheshimiwa rais sitaki
kupingana na maamuzi yako lakini
sababu ulizozitoa naona kama hazina
mashiko makubwa kukufanya ufikirie
kuuondoa utawala wa David
Zumo.Tunaweza kutengeneza tatizo
kubwa sana baina ya nchi zetu
hizi.Mimi ushauri wangu ni kutafuta
njia mbadala kupambana na David na si
kumuondoa madarakani”
“Lameck hakuna njia
mbadala.Nimekwisha amua
kumuondoa David Zumo madarakani
na lazima nifanye hivyo.Siwezi kubadili
msimamo wangu kwa hiyo nataka
unipe plani tutalifankishaje sualah
hilo?Nilikupa nafasi ya kutafakari njia
mbalimbali tunazoweza kutumia
kumuondoa David nadhani mpaka sasa
una jibu zuri la kunipa” akasema rais
“Mzee nimetafakari sana suala hili
kama ulivyonitaka na nimefikiria
jambo moja”
“tell me” akasema rais
“Davd Zumo aliwakusanya waasi
wote waliokuwa wakipigana kwa miaka
mingi na serikali ya Congo
akawajumuisha katika jeshi la Congo
ambalo kwa sasa linajulikana kama
jeshi la pamoja.Wale makanda wakuu
wa vikosi vya waasi amewapa nyadhifa
kubwa katika jeshi na uasi umekoma
kabisa Congo.Tunachoweza kukifanya
ili kumondoa David Zumo madarakani
ni kuzungumza na mmoja wa aliyekuwa
kiongozi wa waasi ili awakusanye
wanajeshi wake na kumpindua rais
David” akasema Lameck
“Hili linaonekana ni wazo
zuri.Hebu nifafanulie namna
tunavyoweza kufanya” akasema rais
“Tutazungumza na kiongozi huyo
wa zamani wa waasi ambaye ninamini
lazima atakubali kwani hivi majuzi
alipohojiwa hakuonekana kupendezwa
na kitendo cha nchi ya Congo kutaka
kugeuzwa kuwa nchi ya kifalme kwani
hakutakuwa na uchaguzi wa rais na
badala yake familia moja ndiyo
itakayoongoza Congo kwa vizazi na
vizazi.Siku zote lengo la kuanzisha uasi
huwa ni kukamata madaraka makubwa
na huyu jamaa endapo tutamuahidi
kumsaidia kukamata madara ya
kuiongoza Congo lazima
atakakubali.Sisi tutamsaidia mbinu za
kijeshi na silaha au hata vikosi vya jeshi
endapo vitahitajika.Mchezo mzima
utakakuwa hivi.Tanzania kwa sasa ni
mwenyekiti wa jumuiya ya afrika
mashariki ambayo nchi ya Congo DRC
ni mwanachama aliyejiunga hivi
karibuni.Kama mwenyekiti utaitisha
kikao cha dharura chenye lengo la
kujadili hali ya usalama katika ukanda
wa afrika mashariki.Wakati kikao
kikiendelea vikosi vya wanajeshi
walioasi wataivamia ikulu ya Congo na
kutangaza kuipindua serikali ya David
Zumo.Unaonaje kuhusu mpango huo?
Akauliza lameck
“Ni mpango mzuri sana
lameck.Ninayakubali mawazo yako
asilimia mia moja na kwa kuongezea tu
ni kwamba baada ya mapinduzi
kufanyika David nitampa hifadhi hapa
Tanzania na haraka sana nitafanya
mpango wa kumuondoa.Nataka
auawe”akasema Ernest
Baada ya majadiliano marefu
Lameck akapewa jukumu la kufanya
mazungumzo na meja Jenerali Paul
Ntamanywa mmoja wa viongozi wa
kundi la waasi waliopigana na serikali
ya Congo kwa miaka zaidi ya ishirini na
sasa yeye na kundi lake
wamejumuishwa katika jeshi la Congo.
Baada ya kikao kirefu rais
akaachana na Jenerali Lameck halafu
akazungumza na mkuu wa jeshi la
polisi akamtaka mpaka kufikia kesho
saa sita mchana Monalisa awe
amepatikan kisha akaelekea chumbani
kwake.Agatha mke wake alikwisha
ruhusiwa kutoka hospitali na alikuwa
amejipumzisha chumbani .
“Welcome home darling” akasema
Agatha
“Vipi maendeleo yako? Akauliza
Ernest
“Ninaendelea vyema.Hali yangu
imeboreka sana.Ahsante kwa kunijali”
akasema Agatha
“Pole sana kwa siku ngumu ya
leo.Unahitaji mapumziko” akasema
Agatha
‘Ni kweli nimechoka sana lakini
mimi na wewe bado tuna maongezi
mengi.Nataka kufahamu ulikuwa wapi
na nani aliyekupiga risasi
mguuni?akasema Ernest
“Relax Ernest.Nitakujulisha kila
kitu lakini kwa sasa unapaswa
upumzike.Tutazungumza pale
utakapokuwa umetulia.Kuna mambo
mengi ya muhimu sana ambayo nataka
tuzungumze”akasema Agatha
“Agatha kichwa changu kina
mambo mengi sana kwa sasa na
sifahamu kama nitaweza kupata nafasi
ya kutulia.Nina majukumu mazito ya
kuhakikisha nchi inatulia baada ya
mashambulio yale mawili kutokea.Nchi
haina serikali ,natakiwa kufikira nama
nitakavyoweza kuiongoza nchi kwa
hiyo usitegemee kuwa nitapata naafsi
nzuri ya kutulia.Lets talk now.Siku ile
ulikuwa katika lile jengo tulimopanga
nikutane nanyi Alberto’s wote lakini
baada ya shambulio kutoea
haukuwepo.Nini kilitokea? Ulinusurika
vipi? Akauliza rais.Baada ya muda
kidogo Agatha akasema
“Nilipokea simu toka kwa Irene
Maboko Yule mfanyakazi wa ikulu
anayeshughulikia masualaya mtandao”
“Irene!! Ernest akashanga
‘Ndiyo.Nilipokea simu toka kwake
akanitaka nitoke haraka ndani ya jengo
lile kwani kuna jambo baya linataka
kutokea.Kwa namna alivyonisisitiza
nikaamua kutoka haraka bila kumuaga
mtu yeyote ili kuona kama kweli kuna
jambo litatokea na kweli baada ya
muda jengo likalipuliwa.Irene alikuwa
na taarifa za kuhusiana na shambulio
lile na ndiye aliyenikoa” akasema
Agatha.Ernest akazidi
kuchanganyikiwa
“I cant believe this!!Irene
alifahamuje kama kuna shambulio
linakwenda kutokea? Akauliza rais
“Hata mimi sifahamu
alifahamuje.Baada ya kunusurika
katika shambulio lile nilienda kujificha
mahala salama na mtu pekee
niliyemueleza mahala nilipokuwa ni
Silvanus Kiwembe.”
“Ulimtaarifu Silva?!!Mbona
hakunijulisha wakati nilimpa jukumu la
kukutafuta na kufahamu mahala ulipo?
Akauliza
“Nilimwambia asikujulishe kwani
nilifahamu kuwa miongoni mwa watu
wanaokuzunguka wapo wasaliti kwa
hiyo sikutaka kujulikana nilikuwa
wapi.Nilitaka kwanza nifanye
uchunguzi kujua Irene alipataje taarifa
zile za kuwapo kwa lile
shambulio.Nilimshirikisha Silva suala
hili naye akapanga vijana wake
kumtafuta Irene lakini tukagundua
alikuwa anashirikiana na watu
tusiowafahamu ambao ni hatari.Mara
kadhaa vijana aliowapanga Silva
kumtafuta Irene walijaribu kumkamata
lakini walikutana na upinzani mkali
kutoka kwa watu anaoshirikiana nao
Irene.Hali hiyo ikatulazimu
kuwachukua mateka wazazi wa Irene ili
kulazimisha Irene ajisalimishe na
akafanya hivyo.Wakati tukiendelea
kumuhoji ili kufahamu alipata wapi
taarifa za shambulio lile,watu wake
anaoshirikiana nao wakatokea na
kutushambulia,wakawaua vijana wetu
pamoja na Silva na mimi nikajeruhiwa
mguuni ila niliokolewa na kijana
mmoja baada ya kujitambulisha kama
mke wa rais.Baada ya kufanikiwa
kutoka salama ndipo nikakupigia simu
kukuomba msaada”akasema Agatha
‘This is unbelievable.Irene?!!
Ernest akauliza tena kwa
mshangao.Hakuamini kama Irene
maboko ndiye aliyevujisha taarifa za
kuwepo kwa shambulio lile kwa mke
wake.
“Ernest suala hili si dogo na kuna
ulazima wa kulifuatilia kufahamu Irene
alitoa wapi taarifa za shambulio
lile.Inawezekana labda anashirikiana
na magaidi? Lazima atafutwe kokote
aliko na apatikane aeleze alifahamuje
kuwepo kwa shambulio katika ile
hoteli” Akasema Agatha
“Agatha umezidi kuichanganya
akili yangu.Irene maboko ni msichana
ambaye ni vigumu kuamini kama
anaweza kuwa na taarifa kama
hizo.Mimi na yeye ni sawa na baba na
mwana kwa nini hakuja kwangu moja
kwa moja na kunieleza kuhusiana na
taarifa hizo? Halafu kitu cha ajabu toka
ulipotokea mlipuko ule hajulikani yuko
wapi” akasema Ernest
“Hata mimi nina mashaka na yule
binti yawezekana anashirikiana na
watu waliofanya mashambulio yale.
Anatakiwa atafutwe kwa kila namna na
akipatikana basi tunaweza kupata
taarifa za muhimu sana.Yule binti
anafahamu kila kitu” akasema Agatha
“Swali lingine,kama alifahamu
kuhusu kuwepo kwa shambulio lile
kwa nini basi hakuweza kuripoti katika
vyombo husika ili kulizuia au hata
kuwaokoa watu waliokuwamo ndani na
badala yake akachagua kukuokoa
wewe peke yako? Akauliza Ernest.
“Muda mfupi baada ya kutoka
kwenye ile bustani ya wanyama jana
usiku nilipigiwa simu na baba Alberto
mkuu akanieleza kwamba yale
mashambulio yote mawili yaliyotokea
hapa Tanzania ni mipango yao kwani
walikuwa wanahitaji kutoa sadaka ya
damu inayopaswa kutolewa kila
mwaka.Mimi kubaki hai pia ulikuwa ni
mpango wao” akasema Agatha na
Ernest akajikuta akipandwa na hasira
kama mtu aliyerukwa na akili
akamshika shingo Agatha na kusema
kwa hasira huku akitetemeka
“That’s not true.Mimi si alberto’s I
hate them na nimefanya haya yote ili
kuwafuta kabisa katika ardhi ya
Tanzania !!
“You did that?!! Akauliza Agatha
kwa mshangao mkuwa na kuutoa
mkono wa Ernest shingoni kwake
akamsukumia pembeni.
“Answer me.Ni wewe uliyeratibu
mashambulio yale kwa ajiliya kuwaua
Alberto’s?? akauliza Agatha.Ernest
hakujibu kitu akabaki kimya ameshika
kichwa.
“What have I done? Kwa nini
nimetamka siri hii kubwa mbele ya
huyu shetani.Huyu mwanamke ni
mchawi mkubwa na ametumia nguvu
zake za kichawi mpaka nimejikuta
nikiropoka mimi mwenyewe siri hii
kubwa.Mambo yanazidi kuniharibikia”
akawaza Ernest
“Ernest umetamka kwa mdomo
wako kwamba ulifanya vile ili
kuwaondoa Alberto’s wote hapa
nchini.Ulitaka kuniua na mimi pia?!!
Akauliza Agatha kwa ukali.Ernest
hakujibu kitu.Agatha akamsogelea
“kwa nini umekuwa na roho ya
ukatili kiasi hicho? You wanted to kill
your own wife?Umesahau mambo yote
tuliyopitia na ukataka kuniua? Akauliza
na kumnasa Ernest kibao.
“Wewe una faida gani hapa
duniani hata ukifa?Umewaua watoto
wako wote kwa ujinga wako kuna faida
gani ya kukuacha hai? Ni bora ufe
upunguze idadi ya watu shetani wewe !!
akasema Ernest
“You are so wrong Ernest
.Unadhani utaweza kupambana na
Alberto’s? Ulikula kiapo kwa kunywa
damu na kiapo kile kitadumu hadi siku
yako ya mwisho hapa duniani .Wewe
bado ni Alberto’s na yote haya
uliyoyafanya bado ni kazi za
Alberto’s.Wanaendelea kukutumia na
utaendelea kuwatumikia daima”
akasema Agatha na kuzidi
kumpandisha hasira Ernest.
“Say that again and I’m going to
kill you right here !!! Ernest akasema
kwa ukali, alikuwa na hasira kali mno
hadi mwili ukimtetemeka.
“You wont kill me Ernest.Endapo
bado una mipango hiyo iondoe kabisa
katika akili yako kwani mimi nimebaki
hai peke yanu miongoni mwa Alberto’s
kwa ajili ya kazimoja ya muhimu nayo
ni kuijenga upya Alberto’s.Isitoshe
ukifikiria kunia fikiria pia kumpoteza
mwanao Monica”
Ernest mkasa akahisi kama
nyundo kubwa imetua kichwani
aliposikia Agatha akimtaja
Monica.Akamvaa na kumuangusha
kitandani. Akamkaba shingo na
purukushani ikaanza
“Nikisikia unalitaja tena jina hilo
nitakuchinja !! Umenisikia ? akauliza
kwa ukali Ernest akiwa amemkaba
Agatha kwa nguvu shingoni kiasi cha
kumfanya apumue kwa shida
“Umenisikia wewe shetani?!!
Akauliza Ernest
“Huyu mjinga ataniua kweli kama
nisipojitahidi kujiokoa” akawaza
Agatha na kunyoosha mkono akaishika
taa iliyokuwa pembeni ya kitanda na
kumpiga nayo Ernest kichwani
akaanguka chini.
“You want to fight with me?!
Akauliza Ernest kwa ukali huku
akitetemeka kwa hasira halafu
akajiinua pale chini na kuelekea katika
kabati lake.Agatha alifahamu
alichokuwa anakitafuta Ernest kabatini
na kwa haraka akauchukua mkasi
uliokuwa katika meza ndogo
akamkimbilia Ernest.
Ernest akasikia vishindo vya
Agatha akimkimbilia akageuka mara
moja akiwa na bastora mkononi
akamlenga Agatha lakini kabla
hajafanya lolote Agatha ambaye naye
alikuwa amepandwa na hasira kali
akamvaa Ernest na kumuangusha
chini.Bastora ya Ernest ikaanguka
pembeni na Agatha akamkalia
juu.Ernest akamchapa ngumi nzito
Agatha iliyomuangusha chini akataka
kuiokota bastora yake lakini Agatha
akakiona kitendo kile na kuokota
mkasi uliokuwa karibu yake
akauzamisha katika shingo ya Ernest.
“Go to hell you devil !!! akasema
kwa ukali.Ernest akaanguka pembeni
huku akitapa tapa na damu nyingi
ikaanza kumwagika.Agatha akainuka
pale chini huku damu ikimtoka
mdomoni.Ghafla Agatha akawa ni kama
mtu aliyestuka toka usingizini baada ya
kumuona Ernest akitapa tapa huku
akitokwa na damu nyingi.
“Ernest!! Akaita Agatha
“Ernest !! akaita tena kwa nguvu
na kisha akauchomoa ule mkasi
mkubwa shingoni mwa Ernest na damu
nyingi ikaruka.
“Nimeua !! akasema huku
akitetema
“Nimeua !!!
Agatha akaanza kutetemeka kwa
woga.Alishindwa afanye
nini.Akamtazama Ernest aliyekuwa
amelala katika dimbwi la damu.
“Nini kimetokea? Mbona kama
nilikuwa ndotoni? Akajiuliza Agatha
“Hapana hii si ndoto.Nimemuua
Ernest.Nimemuua rais wa nchi.!!
Akawaza na mara simu ya rais ikaita
Agatha akazidi kuogopa.Akaichukua
simu ile akatazama mpigaji alikuwa ni
Jenerali Lameck.Akaikata na kuzima
simu.Baada ya sekunde kadhaa
akasikia mlango wa chumba
ukigongwa.Agatha akazidi
kuchanganyikiwa.Mara akaiona
bastora pembeni na alipokuwa amelala
Ernest mkasa akaichukua.Mlango
ukagongwa kwa mara ya pili.
“Kila kitu
kimeharibika.Nikikamatwa hapa ni
kwenda gerezani na sintoweza kutoka
tena.Maisha yangu yameishia hapa….”
akawaza Agatha huku machozi
yakimtoka na kuuweka mdomo wa
bastora chini ya kidevu.Mlango
ukagongwa kwa mara ya tatu na mara
ukasikika mlio wa risasi.Mlango wa
chumba cha rais ukapigwa na
kufunguka wakaingia walinzi wa rais
na kuwakuita rais na mke wake wakiwa
wamelala chini katika damu.Haraka
haraka gari la wagonjwa likaletwa
wakapakiwa na kukimbizwa hospitali.
KINSHASA – DRC
Msafara wa David Zumo uliwasili
katika nyumba walimofikia Monica na
wenzake akina Austin.Tayari ni saa
tatu za usiku.Ndani ya gari David
alikuwa na Monica ambaye baada ya
shughuli za mazishi ya Pauline
hakurejea katika makazi yake
aliyoandaliwa bali aliungana na
viongozi wa mataifa na wawakilishi
wao katika chakula maalum
kilichoandaliwa na rais David kwa ajili
yao.
“Karibu ndani Monica” akasema
David huku akimfungulia Monica
mlango.Walinzi wote wakabaki
nje.Sebuleni Yasmin na maria walikuwa
wanatazama runinga.Walitaka kuondoa
walipomuona David Zumo lakini
akawataka waendelee kutazama
akamuongoza Monica kuelekea katika
sebule nyingine.Nyumba ile ilikuwa na
sebule tatu.
“Monica sipati neno zuri la
kukushukuru kwa ushirikiano ulionipa
kwa kuacha shughuli zako na kuja
kuungana nami katika mazishi ya
Pauline.Ahsante sana” akasema David
“Usijali David.Ni wajibu wangu
kufanya hivi.Hakuna ambacho
kingenizuia nisifike katika mazishi ya
Pauline.Hata kama Pauline na mmoja
wazazi wangu wangefariki katika siku
moja basi ningehudhuria kwanza
mazishi ya Pauline.Nimebahatika
kukutana na Pauline katika siku za
mwisho za uhai wake lakini nakiri
sijawahi kukutana na mwanamke
mwenye upendo wa ajabu kama yeye
katika maisha yangu. David umepoteza
kitu cha thamani kubwa sana”
“Nakubaliana nawe
Monica.Pauline alikuwa ni mtu mwenye
upendo wa aina yake.Alimpenda kila
mtu na ndiyo maana umeona maelfu ya
watu waliofurika leo kuja kumsindikiza
katika safari yake ya
mwisho.Alipendwa na kila mtu hapa
Congo lakini Mungu ana makusudi yake
,ameondoka Pauline na ameniletea
zawadi nyingine ambayo ni
wewe.Naweza kusema kwamba Mungu
ananipendelea sana mimi kwa
kuniletea wanawake ambao ni adimu
sana kuwapata katika ulimwengu wa
sasa.Monica nina bahati sana kukupata
na sijui nitamshukuruje Mungu kwa
Baraka hizi anazonijalia” akasema
David
“Monica siku imekuwa ndefu sana
na unahitaji upumzike kwa hiyo sitaki
kukuchosha sana nataka kuzungumza
na akina Austin.Nataka tulizungumze
suala lao ili nione namna ya
kuwasaidia”akasema David.Monica
akaenda katika chumba cha akina
Austin akagonga na Austin akaufungua
mlango
“Queen Monica” akasema Austin
na uso wa Monica ukachanua tabasamu
“Mmeshindaje leo? Akauliza
“ Tumeshinda salama.Pole kwa
shughuli nzito ya leo” akasema Austin
“Ahsanteni sana.Shughuli
imekwisha salama.Tutazungumza zaidi
baadae lakini nimekuja na David
anahitaji kuonana nanyi ili tuzungumze
lile suala letu.Kuna taarifa zozote toka
Dar es salam kwa Job? Akauliza Monica
‘Nimezungumza na Job asubuhi na
walifanikiwa kuwakomboa wazazi wa
Irene.They are all safe” akasema Austin
“That’s good news.Tutaongea zaidi
baadae twendeni tukaonane na rais
David” akasema Monica kisha
wakaongozana hadi sebuleni
alikokuwepo David
“Pole sana mheshimiwa rais kwa
shughuli nzito ya leo.Pamojana kuwa
katika kipindi kigumu lakini umetafua
muda na kuja kuonana nasi.Hii ni
heshima kubwa umetupa” akasema
Austin
“Usijali Austin.Suala hili pia ni la
muhimu sana kwani linahusu maslahi
ya nchi ambayo mimi naichukulia Kama
nyumbani.Tanzania ni kama nyumbani
kwetu k wani kwa miaka mingi watu wa
Congo wameishi Tanzania wakati ule
ambao nchi ilikuwa imegubiokwa na
vita vya wenyewe kwa wenyewe.Suala
lolote linalohusu maslahi ya Tanzania
linanihusu kwa sababu Tanzania ndiko
anakotoka malkia mtarajiwa wa Congo”
akasema na wote wakatabasamu
“Jana ulinieleza kwa kifupi juu ya
suala hili lakini kwa kuwa leo ninao
muda wa kutosha ninaomba unieleze
kwa kirefu nilifahamu kwa kina zaidi
suala hili ili na mimi nione nitatoa
mchango gani kutokana na uzito wa
suala lenyewe” akasema David.
Austin akaanza kumuelezea David
toka mwanzo hadi pale
walipofikia.David akabaki kinywa wazi
“Mhh ! haya ni mambo mazito
sana.Sikuwahi kufikiri kama siku moja
Tanzania ingefika hapa
ilipofika.Nimestuka sana.” Akasema
halafu baada ya muda kidogo akauliza
“Kwa hiyo ni msaada upi zaidi
mnaohitaji niwasaidie?
‘Tunahitaji kuwapatia Yasmin na
familia yake sehemu ya kwenda kuishi
mbali mahala ambako haitakuwa rahisi
kwa IS kuwafahamu.Wanahitaji majina
na pasi mpya za kusafiria.wanahitaji
mtaji au biashara yoyote ambayo
itawasaidia kuendesha maisha
yao.Endapo tukivikamilisha hivyo vitu
basi Yasmin atatuonyesha mahala
alipoificha hati ya muungano” akasema
Austin
“Nimewasikia Austin na ombi lenu
nimelipokea ila naomba mfahamu
kwamba kwa kufanya haya tayari
nimeingia katika msuguano na rais
wenu Ernest Mkasa.Asubuhi ya leo
amenipigia simu kuniuliza kama
niliwaweka kizuizini nikamweleza
ukweli kwamba sikuwaweka kizuizini
kwa sababu sikuona kosa lolote
mlilonalo hivyo nikawaachia
huru.Hakufurahishwa na jambo hili
lakini baada ya kunipa picha kamili
sasa nnafahamu kwa nini anatumia
nguvu kubwa namna hii
kuwatafuta.Hata hivyo nawahakikishia
kuwapeni ushirikiano mkubwa sana
hadi mfanikisha suala
lenu.Ninachohitaji kujua ni mipango
yenu baada ya kufanikisha kupata hati
ya mungano.Mmepanga kufanya nini?
“Kitu tulichopanga kukifanya ni
kukusanya ushahidi wa kutosha wa
kumuhusisha rais na mashambulio yale
mawili na kisha tutamfikisha
mahakamani.Hapa ninamaanisha
kwamba lazima tumuondoe
madarakani na kisha tumfikishe mbele
ya sheria”
“Nitawasadia kwa hilo.Nitawapa
ushirikiano wa kutosha na kuhakikisha
Ernest mkasa anafikishwa katika
sheria.Niachieni suala hilo nilifanyie
kazi na kesho nitakuwa na jibu la
kuwapa” akasema David wakaendelea
na maongezi hadi ilipotimu saa sita za
usiku wakaagana na Ernest akaondoka
na Monica wakaelekea chumbani.
“Ahsante sana David kwa kujitolea
kuwasaidia wenzangu hawa
walioyaweka maisha yao hatarini
wakipambana kwa ajili ya nchi
yao.Najua utaingia katika mgogoro na
rais Ernest lakini usikate tamaa
endelea kutusaidia” akasema Monica
wakiwa chumbani
“Monica mambo aliyonieleza
Austin yamenigusa sana na hasa baada
ya kuisikia rekodi ile ya mazungumzo
kati ya rais Ernest na mkuu wa majeshi
wa Tanzania wakiongelea kuhusiana na
yale mashambulizi.Nimeumia sana
kuona mtu kama rais anatumia
madaraka yake kuteketeza roho za
watu wasio na hatia yoyote.Nitatoa
msaada wa kila aina hadi nihakikishe
Yule mzee anafikishwa mbele ya
sheria.Ni wakati wa kuisaidia Tanzania
kwani wakati wa mapigano ya
wenyewe kwa wenyewe hapa Congo
Tanzania walisimama kidete na hata
kutuma vikosi vya jeshi kuja
kupambana na waasi na sasa ni zamu
yetu kusimama kwa ajili ya ndugu zetu
wa Tanzania” Akasema David halafu
wakaingia kuoga na kisha wakarejea
kitandani
“Monica ulinieleza kwamba kuna
jambo unataka kunieleza siku tukipata
nafasi.Wakati ni huu ambao unaweza
ukanieleza” Akasema David.Monica
akastuka na kuingiwa na woga.
“Nieleze malaika wangu
ninakusikia” akasema David na
kumbusu
“David nina jambo zito ambalo
nataka nikueleze na sijui
utalichukuliaje lakini sina budi
kukueleza”
“Nieleze malaika wangu.Hata
kama ni jambo gumu ambalo huwezi
kumueleza mtu mwingie yeyote nieleze
mimi nitakusikiliza.Hata kama
umewahi kuua mtu niambie na itabaki
kuwa siri yangu” akasema David na
wote wakachela
“David wewe ndiye uliyekuwa
mwanaume wangu wa kwanza kuingia
naye katika mahusiano na ni wewe
uliyeniondoa usichana
wangu.”akasema Monica akamtazama
David halafu akaendelea
“Niliporejea Dar es salaam
nilikumbuka kwamba tulifanya
mapenzi katika tarehe zangu za hatari
na hata tarehe zilipofika sikuona siku
zangu.Suala hili limekuwa linanitesa
mno akili yangu.Nikamshirikisha mama
na akaniambia kwamba kuna
uwezekano labda nimeshika ujauzito
japokuwa sina uhakika bado hadi hapo
nitakapop….” Monica hakumaliza
sentesni yake David akamrukia na
kuanza kumporomoshea mabusu
mazito.
“Monica niambie kama taarifa hizi
si utani.”
“Si utani David ni taarifa za kweli
na ndiyo maana sikutaka kukueleza
katika simu nikasubiri nije nikueleze
ana kwa ana.Hilo ndilo jambo ambalo
limekuwa linaniumiza kichwa kwani
sikuwa nimepanga kupata mtoto kabla
ya ndoa” akasema Monica na
kuinamisha kichwa
“Monica malaika wangu
nakuomba tafadhali usiumize kichwa
chako kwa suala hili.Hizi ni Baraka
Mungu ametujalia.Hiki kilikuwa ni kilio
changu cha miaka mingi nikiomba
mtoto hatimaye leo hii ombi langu
limejibiwa na ninakwenda kuitwa
baba.Oh ahsante Mungu”akasema
David na kushindwa kuyazuia machozi
ya furaha kumtoka.Monica naye
akapatwa na hisia kali akamkumbatia
David na wote machozi yakawatoka
“Sijawahi katika maisha yangu
kupata taarifa ambayo imenifurahisha
hadi kunitoa machozi.Hii ni taarifa ya
kwanza kuniliza.Nimefurahi kupita
maelezo na sijui nikwambie nini
Monica malaika wangu.Nimshukuruje
Mungu kwa Baraka hizi ambazo vidole
havitoshi kuzihesabu?Itoshe kusema tu
ahsante Mungu” Akasema David
“David nimeharakisha kukueleza
suala hili lakini bado sina uhakika
kama kweli nina ujauzito ama vipi hadi
hapo tutakapofanya kipimo ndipo
tutajua”
“Monica nina uhakika mkubwa
hiyo lazima itakuwa ni mimba.Kesho
watakuja madaktari hapa watakupima
kama unavyotaka lakini nina uhakika
kabisa lazima humo tumboni mwako
umebeba kiumbe kitakachovishwa taji
la urtawala wa Congo.Umebeba mrithi
wangu.Umebeba mfalme au malkia wa
baadae wa Congo” akasema David kwa
furaha na kumkumbatia tena Monica
kwa nguvu huku akimwagia
mabusu.David alisahau kabisa kama
bado alikuwa katika majozi ya kufiwa
na mke wake kutokana furaha
aliyokuwa nayo
“Endapo kweli utakuwa mja mzito
nitafanya haraka sana ili tuweze
kufunga ndoa na mtoto wetu aanze
kulelewa katika jumba la kifalme toka
akiwa mdogo” akasema David.Ulikuwa
ni usiku wa aina yake ambao David
alihisi kama vile hayuko katika dunia
hii.waliongea na kupanga mambo
mengi kuhusiana na maisha yao ya
usoni.
DAR ES SALAAM - TANZANIA
Baada ya chakula cha usiku Job
akawataka watu wote waende
vyumbani mwao kupumzika.Sebuleni
akabaki na Marcelo na Julieth
akawataka waelekee katika chumba
alimowekwa Monalisa.Aliufungua
mlango wa chumba kile maalum kwa
ajili ya mahojiano na kuingia
ndani.Mstuko alioupata Monalisa
ulkuwa mkubwa sana na hakuamni
macho yake kwa kile alichokiona.
“My God !! akasema Monalisa kwa
mshangao
“This is unbeliavable..!! Job !!
akasema Monalisa bado akishangaa.Job
akavuta kiti na kuketi
“Halo Monalisa.habari za siku
nyingi? Habari za Arusha? Akauliza Job
na Monalisa alishindwa kuongea
midomo ilikuwa inamtetemeka.
“Relax Mona” akasema Job huku
akitabasamu kwa namna Monalisa
alivyokuwa anaweweseka baada ya
kumuona.Baada ya muda akasema
“Karibu tena Dar es salaam Mona”
Akasema na kunyamaza kidogo halafu
akaendelea
“Samahani sana Monalisa kwa
kukuchukua kwa vurugu namna ile
lakini imenilazimu nifanye hivyo kwani
kukupata kwa njia ya kawaida
isingewezekana.Nimekuleta hapa kwa
ajili ya jambo moja tu ambalo
ukinisaidia nikalipata basi nitakuachia
uende zako lakini endapo utashindwa
kunipa ushirikiano basi nakuhakikishia
utakuwa ndio,mwisho wako wa kuliona
jua” akasema Job na taratibu sura yake
ikaanza kubadilika na kuonyesha
kwamba alianza kupandwa na
hasira.Monalisa akazidi kuogopa.
“Sitaki kufukua kaburi na
kukumbusha mambo yaliyopita baina
yetu kwani imebaki historia lakini
ninachokihitaji kwa sasa ni kufahamu
alipo mwanangu Millen.Nionyeshe alipo
mwanangu na nitakuachia ukaendelee
na maisha yako” akasema Job.Monalisa
akamtazama akashindwa
kuzungumza.Job akainuka
akamsogelea
“Mona huwezi kuongea? Wewe ni
bubu? Nieleze aliko
mwananguMonalisa” akasema Job
lakini bado midomo ya Monalisa
ilikuwa inamtetemeka na akashindwa
kuzungumza.
Ghafla bila kutegemea Job
akamnasa kibao kikali sana na
kumfanya apige kelele.
“Nadhani sasa unaweza
kunijibu.Ukishindwa kunipa jibu
nitakufanyia kitu kibaya sana.Tafadhali
usinilazimishe nikufanyie kitu kibaya
kwani nakuheshimu kama mama wa
mwanangu lakini endapo utaendelea
kukaa kimya utanilazimisha
nikuharibu.Nitachukua kisu na
kuukwangua uso wako na kuuondoa
huo uzuri wote ulio nao.Nakuuliza mara
ya mwisho mwanangu Millen yuko
wapi? Akauliza Job lakini Monalisa
aliendea kulia huku akitetemeka kwa
woga.
“Nadhani bado hujanifahamu
vizuri.I’m a monster!! Mimi ni mtu
mbaya sana
ukinikorofisha.Nitakuonyesha upande
wangu wa pili ambao hujawahi kuuona”
akasema Job na kulifugua sanduku lake
dogo jekundu.Marcelo akamuwahi
“Job subiri kidogo usimfanye
chochote.Let me talk to her” akasema
Marcelo
“Marcelo stay out of this” akasema
Job
“Job nakuomba tafadhali nipe
dakika mbili nizungumze naye ili aweze
kujibu swali ulilomuliza.Usimtese
tafadhali huyu ni mama wa mtoto
wako.Wewe na yeye mmewahi kuwa na
historia.Dakika mbili tu naomba”
akasema Marcelo.Job akamtazama
Marcelo na kusema
“Ok two minutes!! Akasema Job
“Naweza kubaki naye peke yake
tafadhali!! Akasema marelo.Job na
Julieth wakatoka nje
Marcelo akamuendea Monalisa
pale kitini na kumshika mabegani
“Monalisa look at me.My name is
Dr Marcelo.Tafadhali naomba
unisikilize na ufanye kile
nitakachokueleza.Take a deep breath”
akasema Marcelo na Monalisa akavuta
pumzi ndefu mara tatu akimfuatisha
Marcelo
“Good.Sasa nisikilize.Job
unamfahamu vizuri kwani aliwahi
kuwa mumeo lakini Job huyu
umuonaye sasa si yule ambaye
ulimfahamu awali.Katika kipindi
ambacho wewe na yeye mmetengana
amepitia mambo mengi sana magumu
kwa hiyo tafadhali usijaribu kumfanyia
mchezo au kiburi cha aina
yoyote.Msikilize na umjibu kila kile
atakachokuuliza.Nimemshuhudia
wakati akiwa kazini ni mkatili sana na
hana huruma hata kidogo.Amekuambia
kwamba atakuharibu uzuri wako wote
na atafanya hivyo endapo hautamjibu
kile anachokitaka.Narudia tena
kukuomba Mona Job hana shida na
wewe hata kidogo na ndiyo maana
mpaka sasa hajakutesa lakini
usimlazimishe akutese ,mueleze aliko
mwanae kwani hiyo ndiyo shida yake”
akasema Marcelo.Huku akilia Monalisa
akasema
“Ninaogopa kumueeza aliko
mwanangu atamchukua na kuja kuishi
naye katika maisha haya ya taabu.Sitaki
kumpoteza mwanangu” akasema
Monalisa
“Monalisa tafadhali nakuonea
huruma sana.Usipomuonyesha mahala
alipo mwanae sina hakika kama
utatoka salama katika hii
nyumba.Mueleze alipo mwanae na
muyamalize haya mambo.Tafadhali
nakuomba” akasema Marcelo na mara
mlango ukafunguliwa akaingia Job na
Julieth
“Dakika mbili
zimekwisha.Niachieni nafasi niifanye
kazi yangu” akasema Job
“Monalisa fanya kama
nilivyokuelekeza” akasema Marcelo
kisha yeye na Julieth wakatoka nje
akabaki Job peke yake mle ndani
“Sasa tumebaki wawili.Uko tayari
kunionyesha alipo mwanangu au
nianze kuifanya kazi yangu? Akauliza
Job.Monalisa akashindwa kuzungumza
kutokana na woga aliokuwa nao
“Fine.Hutaki kuzungumza kwa
hiari sasa utazungumza kwa lazima”
akasema Job na kuchukua baadhi ya
vifaa vya kutesea akaviweka mezani
“Job usinitese tafadhali !! akasema
Monalisa huku akilia
“Ukitaka nisikutese Mona
nionyeshe alipo mwanangu.Mimi sina
shida na wewe!! Akasema Job
“Job tafadhali usimchukue
mwanangu.Yeye ndiye kila kitu
kwangu!! Akasema Mona huku akilia
“Mona usinipotezee wakati
wangu.Nionyeshe alipo Millen ama
sivyo hatatoka salama humu ndani!!
Akasema Job na kuchukua kifaa kidogo
kinachojlikana kama koleo akakishika
kidole cha Monalisa na kuibana kucha
kwa lengo la kuibandua .
“Basi Job nitakueleza kila
kitu.Tafadhali usinitese!! Akasema
Monalisa.Job akamtazamana kwa
hasira
“Millen anasoma Arusha katika
shule ya kimataifa inaitwa Mama
Theresa international school.” Akasema
Monalisa
“Nitawezaje kumpata?
“Job tafadhali usimchukue mtoto
muache amalize shule!! Akasema Mona
“Mona tafadhali
usinichezee.Nahitaji kumpata
mwanangu.Siwezi kumuacha
mwanangu akasomeshwa kwa fedha
haramu” Akasema Job na kutoa simu ya
Monalisa katika mkoba na kumpatia
“Piga shuleni kwa akina Millen na
uwafahamishe walimu kwamba
umepata msiba na unamuhitaji Millen
Dar es salaam kesho.Waeleze kwamba
wewe hautaweza kufika bali utamtuma
mtu akamchukue” Akasema Job
Monalisa akaishika simu
akazitafuta namba za mkuu wa shule
anakosoma mwanae Millen akampigia
na kumtaarifu kwamba amepata
matatizo ya kifamilia na hivyo
anamuhitaji Millen kesho afike Dar es
salaam.Alimaliza kuzungumza na mkuu
wa shule akaiweka simu mezani na
kuangua kilio.
“Job tafadhali nakuomba
usimchukue mwanangu!! Akasema
Monalisa huku akilia
“Kesho nakwenda kumchukua
mwanangu Arusha na hautamuona tena
katika maisha yako” akasema Job kwa
ukali
“Job nakuomba
tafadhali.Nitafanya kila
utakachoniamuru nifanye lakini
usimchukue mwanangu” akazidi kulia
Monalisa
“Yule ni mwanangu pia na
ninakuhakikishia kwamba hautamuona
tena katika maisha yako.Wewe
mwanamke ni shetani mkubwa!!
Akafoka Job akamtazama Mona kwa
hasira na kusema
“Kwa muda wa miaka kadhaa
nimeteseka sana mateso ambayo
yamesababishwa na wewe.Nililazimika
kuishi kama kichaa nikila na kunywa
majalalani kwa ajili ya kuwakimbia
watu ambao walitaka kuniua kwa
sababu yako.Mambo niliyoyapitia ni
mazito na siwezi kukueleza kwani
ndicho hasa ulichokuwa
unakihitaji,mimi niteseke au niuawe na
wewe ubaki huru ukifurahia maisha na
huyo bwana wako” akasema Job na
kuendelea kumtazama Monalisa kwa
macho makali
“Nilipoamua kuacha wanawake
wote wa dunia hii na kukuchagua wewe
nikiamini kwamba wewe ndiye pekee
uliyeumbwa kwa ajili
yangu,sikutegemea kabisa kama siku
moja ungekuja kufanya jambo kama hili
ulilolifanya.Sikutegemea kama siku
moja ungeweza kufanya kitendo
kikubwa cha usaliti kama
ulichokifanya.Pamoja na kuyatoa
maisha yangu kukupa kila ulichokitaka
lakini bado hukutosheka.Sitaki
kuongeleza zaidi suala hilo
ninachokihitaji kukifahamu huyo Don
ambaye uliamua kuniacha ukakimbia
naye ni nani? Akauliza Job.Monalisa
hakujibu kitu
“Nijibu Monalisa.Nahitaji
kumfahamu huyo mtu
aliyekuchanganya hadi ukaamua
kuniacha ni nani? Akauliza tena lakini
Monalisa alibaki akilia hakujibu kitu.
“Nilikuonya toka awali kwamba
sipendi kupotezewa muda
wangu.Nikikuuliza nataka jibu mara
moja” Akasema Job na kuchukua koleo
akamshika mkono na kukiminya kidole
kimoja.Monalisa akapiga ukelele
mkubwa
“Hata ukipaaza sauti ya namna
gani hakuna atakayekusikia.Ni mimi na
wewe tu humu ndani.Usiponijbu
nitaanza kuziondoa kucha zako nzuri
moja baada ya nyingine.Maumivu yake
siwezi kukuelezea.Nakupa sekunde
tano unijibu Don ni nani? Akauliza Job
na kutazama saa yake.
“Sekunde tano zimekwisha.sasa
nakuonyesha nilivyo mkatili!! Akasema
Job na kuchukua tena koleo.
“Nitakueleza Job usiendelee
kunitesa” akasema Monalisa
“Nijibu haraka sana” akasema Job
“Mtu niliyenaye ambaye sifahamu
kama anaitwa Don ni rais wa Tanzania”
akasema Mona
‘What ?!!
‘hebu rudia tena!!
“Mwanaume niliyenaye ni rais wa
Tanzania”
‘Oh my God !! Ernest Mkasa
again??akasema Job .Alistuka sana
kusikia habari ile.
“Ndiyo maana ulikuwa tayari mimi
nife ili upate nafasi ya kuwa na huyo
mzee wako_Oh Monalisa ulikosea sana
kukubali kuwa hawara ya Yule mzee.Ni
bora kama ungeondoka na mwanaume
mwingine ningekuelewa lakini si Yule!!
akasema Job akiendelea kumtazama
Mona kwa hasira
“Nashindwa nikufanye
nini.Natamani nikukate kate vipande
vipande ili hasira zangu zote ziishe
lakini haitasaidia.Usiku huu nitautumia
kutafakari nini nikufanye shetani wewe
!! Utakaponiona kesho asubuhi ujue
hatima yako imefika !! akasema Job na
kutoka mle chumbani akawakuta
Marcelo na Julieth nje yakile chumba
wakimsubiri.
“Pole sana Job.Make a deep breath
!! akasema Marcelo baada ya kuona
namna Job alivyokuwa amebadilika.
“Siamini nilichokisikia.Kumbe
Ernest mkasa ndiye aliyenipora mke
wangu.Ndiye aliyesabaisha miaka hii
yote mimi nimeteseka na kuishi kama
kichaa nikila na kunywa katika
majalala.Nimechanganyikiwa na sijui
nifanye nini.Sijui nitamfanya nini huyu
mwanamke !! akasema Job
“Usimfanye chochote Job.Kwa
kuwa tayari umekwisha fahamu alipo
mwanao fanya jitihada za kumpata
mwanao na huyu mwanake muache
aende akaendelee na maisha yake.Hata
ukimkata mikono yote haitasaidia
kitu.Let her go.Mungu anayaona mateso
yako na atakusaidia siku moja na wewe
utampata mwanamke mwenye mapenzi
ya kweli” Akasema Marcelo.
Job akaegemea ukuta akawaza
kwa muda halafu akasema
“Julieth nahitaji msaada
wako.Nataka kesho asubuhi upande
ndege uende Arusha ukamchukue
mwanangu Millen.Nitagharamia safari
hiyo” akasema Job
“Hakuna tatizo lolote katika
hilo.Nitakwenda Arusha kesho
kumchukua mwanao na nitahakikisha
anafika hapa salama” akasema Julieth
Job akaachana na akina Marcelo
akaenda kumpigia simu Austin
akamfahamisha kila kitu kilichotokea
naye akataarifiwa kile kinachoendelea
kule Kinshasa na baada ya zaidi ya nusu
saa za maongezi wakaagana.

.
 
Kuna time nahisi Rais Zumo ana akili sana yawezekana huyo mwanamama Paulina akawa sio mkewe ila katengenezwa tu kumpanga Monica manake mke halali awe hivo kweli mhhhhh
Nami ndio nnachokiwaza, mke mwenye kumpend mumewez haiwezi
Nimeomba link ya riwaya zilizokwisha isha mpaka sasa nimepata peniela tu ngoja nianze kuifatilia hii VIPEPEO WEUSI sijui nayo ina utamu au vp
 
SEASON 6: SEHEMU YA 2
Vishindo viwili vikubwa
vililitikisa jiji la Dar na kuzua
taharuki kubwa kwa wakazi
wake ambao kwa muda huu wa
jioni wengi walikuwa katika
harakati za kurejea majumbani
kwao baada ya pilika pilika za
kutwa nzima.Moshi mkubwa
mweusi pamoja na vumbi kubwa
vilitanda eneo ulikotokea
mlipuko ule na hivyo kuwafanya
watu wawe na shauku ya
kutaka kufahamu nini
kimetokea .Zilipita dakika tano
baada ya mlipuko kutokea
ving’ora vya magari ya magari ya
polisi na zimamoto vikasikika na
kwa kasi kubwa wakielekea
sehemu ulikotokea mlipuko ule
mkubwa.Bado moshi mzito
uliendelea kutanda eneo
lile.Wananchi walizuiliwa
kulikaribia eneo lile kwa ajili ya
usalama wao.Vikosi viliwekwa
mbali kidogo na eneo lile huku
jitihada za kuuzima moto
ulioendelea kuwaka na kutafuta
manusura zikiendelea.
Wakati jiji la dar likiwa
katika taharuki ile kubwa taarifa
nyingine zikasikika kwamba
jengo la bunge mjini Dodoma
nalo pia limelipuliwa na
hakukuwa na taarifa za awali
zilidai kwamba hakukuwa na
mtu hata mmoja aliyekuwamo
ndani ya jengo lile aliyetoka
hai.Taharuki kubwa ikatanda
nchini.Vyombo vyote vya ulinzi
na usalama vikawekwa katika
tahadhari kubwa .Ofisi na
majengo yote ya umma na
sehemu zile zenye kubeba
mikusanyiko mikubwa ya watu
yakaongezewa ulinzi mkubwa.
Dunia nzima ikaelekeza macho
yake Tanzania na kulaani vikali
mashambulio mawili makubwa
yaliyopelekea vifo vya watu
wengi hasa viongozi .
Hadi ilipofika saa mbili za
usiku bado hakukuwa na taarifa
yoyote iliyotolewa kwa umma
kuhusiana na tukio lile.Vyombo
vya usalama viliwahimiza
wananchi wajitahidi kuwa
watulivu na watapewa taarifa
baadae kuhusiana na tukio
lile.Wananchi waliendelea
kuaswa kuchukua tahadhari
kuepuka mikusanyiko mikubwa
na yeyote mwenye taarifa zozote
zinazoweza kusaidia alitakiwa
kuziwasilisha katika vyombo vya
usalama ili zifanyiwe kazi..
Viongozi wengi wa dunia
waliendelea kumtumia rais wa
Tanzania salamu za rambi rambi
na pole kwa wananchi wa
Tanzania kufuatia
mashambulio yale makubwa
.Wakati dunia nzima ikilaani
mashambulio yale,video
iliyomuonyesha kiongozi mkuu
wa Alshabaab Habib Alzaraq
ilirushwa na kituo kimoja
kikubwa cha runinga kilichopo
huko nchi za kiarabu.katika
video hiyo habib alikiri
Alshabaab kuhusika katika
mashambulio yale mawili
yaliyotokea nchini Tanzania .
“Naitwa Habib
Alzaraq,kiongozi mkuu wa
Alshabaab” ndivyo alivyoanza
katika video hiyo
“Dunia nzima imeelekeza
macho yake nchini Tanzania
kufuatia mashambulio mawili
yaliyotokea jioni ya leo nchini
humo.Nachukua nafasi hii
kuitaarifu dunia kwamba
Alshabaab ndio tuliotelekeza
mashambulio hayo mawili
.Huu ni mwanzo tu wa vita
yetu na Tanzania na
tutaendelea kuishambulia
kila mara hadi pale serikali
ya Tanzania itakapoondoa
wanajeshi wake walioko
katika ardhi ya Somalia
wakilifundisha jeshi la
Somalia .Tumekwisha ionya
mara nyingi serikali ya
Tanzania kuhusiana na
kuwaondoa wanajeshi wake
walioko nchini Somalia
wanaosaidia kulijenga upya
jeshi la Somalia kwa kuwapa
mafunzo lakini wamepuuza
na sasa tumeamua kutumia
nguvu ili kuwashinikiza
kuwaondoa wanajeshi wake
katika ardhi yetu.
Tunatoa nafasi nyingine
kwa seriali ya Tanzania
kuwaondoa haraka sana
wanajeshi wake walioko
nchini Somalia kama
wanataka damu isiendelee
kumwagika.Bila kufanya
hivyo tutaendelea kumwaga
damu ya watanzania kila
uchao hadi pale serikali ya
Tanzania itakapoondoa
wanajeshi wake katika ardhi
yetu.
Kilichotokea leo Tanzania
ni fundisho kwa mataifa
mengine kwamba mzozo wa
Somalia si wa kuingiliwa .Hii
ni vita yetu na mtuachie
wenyewe.Hatutaki taifa lolote
katika ardhi yetu kwa
kisingizio cha kusuluhisha
mgogoro wa Somalia.Yeyote
atakayekanyaga ardhi ya
Somalia na kuisaidia serikali
iliyopo madarakani
tutamuhesabu ni adui yetu na
tutapambana naye bila kujali
ukubwa wala nguvu
zake.Mwisho narudia tena
kuitaka serikali ya Tanzania
na wale wote wenye majeshi
yao Somalia kuyaondoa mara
moja kabla ya damu nyingi
zaidi kumwagika katika nchi
zao”
Ndivyo alivyomaliza Habib
Alzaraq kiongozi mkuu wa
Alshabaab .

SEASON 6: SEHEMU YA 3
Taarifa za mashambulio yale
mawili yaliyotokea dar es salaam
na Dodoma ziliwastua na
kuwachanganya sana Austin na
wenzake.Walisimamisha kazi
zote wakakaa sebuleni
wakifuatilia matangazo ya moja
kwa moja katika runinga
kuhusiana na tukio lile la
kustusha sana.
“ Najaribu kutakakari
kuhusiana na matukio haya
mawili.Ukitazama m uda
yaliyotokea unakaribiana sana
na hii inanipa picha kwamba
yawezekana mshambuliaji
anaweza kuwa mmoja.Dah ! hili
ni shambulio kubwa sana
ambalo halijawahi kutokea
katika historia ya Tanzania na
afrika mashariki kwa ujumla.”
Akasema Austin
Wakati wakiendelea kujadili
juu ya tukio lile mara wakapata
taarifa kuwa katika kituo kimoja
cha runinga cha nje ya nchi
kulionyeshwa video ya kamanda
mkuu wa Alshabaab akijtapa
kuhusika katika mashambulio
yale.Kwa kutumia simu yake ya
mkononi Amarach akaitafuta
video ile na kusikia kile
alichokisema Habib.
“Alshabaab !!! akasema
Austin kwa mshangao
“ Alshabaab ndio
waliohusika na mashambulio
haya? Akazidi kushangaa
“Mbona umestuka Austin
kusikia ni Alshabaa ndio
waliofanya shambulio hili?
Akauliza Job
“ Hainiingii akilini job.Kwa
nini iwe sasa ? Kwa nini
washambulie leo? Vikosi vya
wanajeshi wa Tanzania walioko
nchini Somalia kwa ajili ya
kulifundisha jeshi la Somalia
vina wanajeshi wasiozidi
hamsini na wako nchini Somalia
kwa miaka kadhaa sasa kwa
nini kwa muda huo wote
wasishambulie Tanzania hadi
leo hii? Kingine kinachonifanya
niwe na mashaka ni kwamba
nchi zilizojitolea kujenga upya
jeshi la Somalia si Tanzania
pekee bali kuna Afrika
kusini,Angola na Misri lakini
kwa nini wachague kushambulia
Tanzania pekee? Ndugu zangu
hili jambo linanipa ugumu
kidogo.” Akasema Austin na
kuitazama tena video ile ya
Habib
“ Kwa mujibu wa maelezo ya
huyu anayejiita Habib Alzaraq
kiongozi wa Alshabaab
yawezekana wameamua kuanza
na Tanzania ili kuzifanya nchi
nyingine zenye majeshi yake
nchini Somalia kuyaondoa
kabla nazo hazijashambuliwa.”
Akasema Amarachi
“ Mawazo yako yanaweza
kuwa sahihi Amarachi lakini
kwa upande wangu bado akili
yangu inakataa kabisa
kukubaliana na hiki
walichokifanya
Alshabaab.Wanajeshi wa
Tanzania walioko Somalia ni
wachache sana ukilinganisha na
ukubwa wa mashambulio
waliyoyafanya.Kikosi cha
wanajeshi wasiozisdi hamsini
hakiwezi kusababisha ukalipua
hoteli ile yenye watu wengi
wakiwamo wageni toka mataifa
mbali mbali na kama haitoshi
kulipua pia ukumbi wa bunge
na kwa mujibu wa taarifa za
awali hakuna mbunge ambaye
anasemekana kutoka hai.Hata
hivyo tusubiri taarifa kamili
itakapotolewa kuhusiana na
mashambulio haya na hapo
tutapata mwanga zaidi”
akasema Austin na kuendelea
kutazama matukio katika
runinga ambapo juhudi za
kuuzima moto na kuwatafuta
manusura wa mashambulio yale
mawili ya Dar es salaama na
Dodoma zilikuwa zinaendelea.
“Hawa jamaa wameitikisa
nchi na hiki walichokifanya ni
uchokozi na wanastahili
kuadhibiwa vikali sana.”
Akasema Job.
“ Kuna kitu kinanijia akilini
lakini sina hakika kama
kinaweza kuwa na mahusiano
na hiki kilichotokea leo.Yasmin
aliniambia kwamba rais alifanya
makubaliano na Alshabaab na
moja kati ya makubaliano yao ni
yeye kuachiwa huru.Nini hasa
kilichopelekea rais afanye
makubaliano na Alshabaab hadi
akaamua kumuachia huru mtu
hatari kama Yasmin. Rais wa
nchi unawezaje kuwa na
mawasiliano au hata kufanya
makubaliano na magaidi? Au
walibadilishana wafungwa na
ndiyo maana akamuachia
Yasmin?.”akajiuliza
“Austin !! akaita Amarachi
na kumtoa Austin katika
mawazo mengi
“ Tunaendelea na jambo
gani kwa sasa? Baada ya tuko
hili naona kila kitu
kimesimama.Are we going to
watch this all night? Akauliza
Amarachi
“ We have lots to do lakini
hiki kilichotokea kwa kweli
kimestua kila mtu.Kuna
wabunge zaidi ya mia tatu na
themanini ndani ya bunge lile
na hatujui ni wangapi walikuwa
ndani ya ukumbi wa bunge leo
jioni wakati shambulio hilo
likitokea nina amini ni zaidi ya
mia tatu.Hatujui ni wageni
wangapi waliokuwamo ndani ya
hoteli ile wakati inalipuliwa.Huu
ni msiba mkubwa sana kwa
taifa na maisha ya watu wengi
yamekatishwa kikatili.Hata
hivyo tunaweza kuendelea na
majukumu yetu huku
tukifuatilia kwa karibu
kinachojiri.Kilichokuwa mezani
kilikuwa ni majibu ya kipimo
cha vinasaba ambayo tayari
tunayo mkononi.Rais alidai
kwamba asionyeshwe mtu
mwingine majibu hao isipokuwa
yeye pekee lakini kwa hili
lililotokea leo sina hakika kama
atakuwa na nafasi hata ya
kufuatilia suala hili.Mimi
ushauri wangu tufungue
bahasha hii na tuangalie
kilichomo ndani.Marcelo ni
daktari na atatuambia
kilichoandikwa humu kwani
lugha ya kitabibu huwa ngumu
kidogo kuielewa” Akasema
Austin na kuichukua bahasha
ile yenye majibu ya vipimo vya
vinasaba na kuifungua kisha
akampa Marcelo akaanza
kuipitia.Wakati Marcelo akiipitia
barua ile kukatokea habari
mchepuko katika runinga.
“Habari za wakati huu
watazamani wetu.Tunaendelea
kuwaleteeni habari mbali
kuhusiana na mashambulio ya
bomu katika hoteli jijini dar es
salaam na Dodoma katika jengo
la bunge,mashambulio
yaliyosababisha vifo vya watu
wengi ambao mpaka sasa bado
haijajulikana idadi kamili ya
vifo.Wakati vikosi vya u okoaji
vikiendelea na juhudi za
kuwatafuta manusura wa
mashambulio hayo ,kuna taarifa
zinazoendelea kusambaa katika
mtandao ya kijamii kwamba rais
wa Tanzania ni miongoni mwa
watu waliokuwamo katika hoteli
iliyoshambuliwa na magaidi
lakini taarifa tuliyoipata hivi
punde kutoka kwa waandishi
wetu walioko katika eneo la
tukio ni kwamba rais wa
jamhuri ya muungano wa
Tanzania ndugu Ernest Mkasa
alikuwa akienda katika hoteli
hiyo kuhudhuria shughuliya
uchangishaji fedha kwa ajili ya
mradi wa kuwawezesha akina
mama wajasiriamali ,hafla
iliyoandaliwa na mke wa
rais.Kwa mujibu wa taarifa ya
msemaji wa ikulu ni kwamba
shambulio hilo lilitokea wakati
msafara wa rais ukiwa
umebakia mita chache sana
kufika katika hoteli hiyo lakini
walinzi wa rais waliwahi
kumnusuru rais mara tu
shambulio lilipotokea na
kumuondosha eneo la tukio na
msemaji wa ikulu amethibitisha
kwamba rais ni mzima na hana
tatizo lolote .Tunawaomba
wananchi mzipuuzie taarifa
zisizo rasmi zinazoendelea
kusambaa katika mitandao ya
kijamii kuhusiana na matukio
haya.Tutaendelea kuwaleteeni
taarifa za kile kinachoendelea
kadiri tutakavyokuwa
tunazipata.”
Austihn na wenzake
wakatazamana.
“ Inawezekana Alshabaab
walikuwa wanamlenga rais?
Akauliza Amarachi
“Inavyoonekana walikuwa
na lengo hilo na walikusudia
kumuua rais kwani mlipuko
umetokea mita chache kabla ya
rais kuwasili katika jengo
hilo.Inawezekana waliwahi kabla
rais hajaingia katika hoteli hiyo
kwani wangechelewa kidogo na
kusubiri hadi rais aingie hotelini
hivi sasa tungekuwa
tunazungumza mambo
mengine.” Akasema Job
Austin aliyekuwa
ameinamisha kichwa akiwaza
akainua kichwa akamtazama
Marcelo
“ Marcelo tueleze
kilichoandikwa katika karatasi
hizo” akasema
Marcelo ambaye tayari
alikwishayapitia majibu yale
akasema
“Ndani ya report hii kuna
barua iliyoeleza kwa ufupi
kuhusiana na matokeo ya
vipimo na mwisho wa barua hii
wamesema kwamba kutokana
na uchunguzi walioufanya
asilimia 99.9999 inaonyesha
kwamba mlengwa ni baba wa
mtoto.Kwa hiyo Rasmi Monica ni
mtoto wa rais Ernest Mkasa.”
Akasema Marcelo na wote
wakawa kimya kisha Austin
akasema
“ Hizi ni taarifa nzuri kwa
rais lakini zimekuja kwa wakati
mbaya ambao anakabiliwa na
jambo zito .Kitu cha msingi kwa
sasa ni kuiweka taarifa
hiipembeni na kuendelea na
mambo mengine.Tunamsubiri
Yasmin apige simu kama
tulivyokubaliana lakini mpaka
sasa bado hajapiga.Hata hivyo
kuna jambo moja ambalo
linaniumiza mno kichwa na
ambalo nataka kuwashirikisha
na ninyi” akanyamaza kidogo
halafu akaendelea.
“ Tulikuwa wote wakati
nazungumza na Yasmin na
alisema kwamba aliachiwa huru
kutokana na makubaliano kati
ya rais na Alshabaab.Mpaka
sasa bado haijaniingia akilini
iweje rais wa nchi afanye
makubaliano na magaidi? Ni
makubaliano gani hayo hadi
akaamua kumuachia huru
Yasmin ambaye amefungwa
mahala pa siri kwa miaka zaidi
ya kumi? Sitaki kuunganisha
moja kwa moja hiki kilichotokea
leo na haya mahusiano ya rais
na Alshabaab lakini kuna hisia
zinakuja kwamba kuna jambo
limejificha hapa na endapo
kama tukimpata Yasmin
angeweza kutueleza ni kitu gani
kinachoendelea kati ya rais na
Alshabaab.Nimejiuliza labda
kulikuwa na mabadilishano ya
wafungwa lakini kama ingekuwa
hivyo vipo vyombo husika
ambavyo vingeshughulikia suala
hili lakini hapa anaonekana rais
mwenyewe ndiye
amelishughulikia jambo hili na
hadi akadiriki kutaka
kutuzunguka ili amchukue
Maria na kumkabidhi kwa
mama yake.Jamani hebu
jaribuni kupanua akili zenu na
tuliangalie hili suala kwa
mapana yake.” Akasema Austin.
“ Hata mimi ninaona kitu
Fulani katika hoja ya
Austin.Huyu Yasmin Esfahani
alikamatwa na kufungwa
mahala pa siri akiwa katika
jitihada za kukipanua kikundi
cha IS katika ukanda wa afrika
mashariki.Lazima rais
anafahamu kabisa kwamba
Yasmin ni mfuasi wa IS ambalo
ni kundi hatari kabisa la kigaidi
duniani kwa sasa lakini pamoja
na kufahamu huko bado
akaamua kumuachia
huru.Kama haitoshi akakusudia
kumuachia huru pia Maria
mtoto wa Yasmin akiwa
anafahau kabisa kwamba
tunamshikilia kwa mahojiano
baada ya kutaka kumuua
Austin.Yote hayo ameyaweka
pembeni lakini lengo lake ni
moja tu kutaka mpango wake
wa kumuachia Yasmin
ukamilike.Hapa kweli kuna
jambo ” Akasema Amarachi
“ Kwa kawaida mimi
hupenda kulitazama jambo
lolote ninalolitilia shaka kwa
mapana yake.Muda mfupi
uliopita tumetoka kutazama
habari inayosema kwamba
shambulio lilitokea wakati rais
akiwa mita chache toka hoteli
hiyo.Inawezekana labda
mlengwa wa shambulio la Dar
alikuwa ni mheshimiwa rais.Kwa
mtazamo wa kawaida unaweza
kuamini hivyo lakini mimi bado
nina mashaka.Kwanza mke wa
rais alikuwa ni mfuasi wa
Alberto’s ambao tayari rais
amewaasi na kama kungekuwa
na hafla h iyo ya kuchangisha
fedha aliyoiandaa mke wa rais
basi lazima kungekuwa na
Alberto’s wengi sehemu hiyo na
rais asingeweza kwenda kwani si
mwenzao tena na wana
uhasama mkubwa.Swali la
kujiuliza rais alikwenda
kutafuta nini katika hoteli hiyo?
Jambo lingine ni kwamba kwa
mujibu wa Yasmin,rais na hawa
jamaa waliojitangaza kuhusika
katika msahambulio yote mawili
ni watu wanaofahamiana na
wamefikia hadi hatua ya
kufanya makubaliano na
akamuachia huru mtu hatari
kwa usalama wa taifa na Afrika
mashariki ambaye ni Yasmin
Esfahani.Iweje watu hao hao
watake kumuua rafiki yao? Je
kuna makubaliano amekiuka?
Kama shambulio la dar es
salaam lilimlenga rais,lile
shambulio la Dodoma ambako
idadi kubwa ya wabunge
inasemekena wamepoteza
maisha mlengwa ni nani?
Akauliza Austin
“ Austin unanifurahisha
sana kwa namna
unavyochambua mambo na
hata mimi unanifanya nianze
kupata picha Fulani ya kile
unachokisema.Kwa mtazamo
huo ulioutoa ni wazi hapa kuna
jambo limejificha.Tukio hili
halijatokea kwa bahati mbaya
.Lazima limepangwa.Kama
ulivyosema awali kwamba kwa
nini Alshabaab washambulie
sasa wakati wanajeshi wa
Tanzania wako Somalia kwa
miaka kadhaa ? Hapa lazima
kuna sababu nyingine na si hiyo
ya kuitaka Tanzania iondoe
wanajeshi wake
Somalia.Tukifanikiwa kumpata
Yasmin tutafahamu mambo
mengi” akasema Job
“ Ni kweli Job,kama
tungeweza kumpata Yasmin
tungefahamu kuhusu uhusiano
wa rais na Alshabaab.Mwenendo
wa rais umebadilika na ananipa
shaka sana.Ni Jana tu ambapo
tumefahamu kuhusu
makubaliano yake na Alshabaab
na leo haohao Alshabaab
wanafanya mashambulio
makubwa na kumwaga damu
nyingi.” Akasema Austin
“Kwa hiyo unashauri nini
kifanyike Austin? Akauliza
Amarachi
“ Tusubiri kwanza taarifa
rasmi ya tukio hili itoke halafu
tutajua nini cha kufanya,lakini
rais ni mtu ambaye tunapaswa
kumuwekea alama ya
kiulizo.Kuna maswali ambayo
anahitaji kutupatia majawabu
yake.Najua kwa sasa inaweza
kuwa vigumu kuonana naye au
hata kuwasiliana naye kutokana
na hili lililotokea lakini ripoti hii
ya kipimo cha vinasaba
itamfanya atutafute .Kwa sasa
tupumzikeni na tuendeleeni
kufuatilia tukio hili kwa karibu
.” akasema Austin na kuwaacha
wenzake sebuleni akaelekea
chumbani kupumzika.
SEASON 6: SEHEMU YA 4
Yasmin Esfahani na Tariq
walikuwa katika chumba cha
hoteli walimofikia wakifuatilia
habari za kile kilichotokea jijini
Dar es salaam na Dodoma jioni
ya siku hiyo.Walikuwa
wanatazama chaneli moja
inayotangaza kwa lugha ya
kiarabu. Yasmin alikuwa
ameketi katika zuria
laini,pembeni yake kukiwa na
chupa kubwa ya mvinyo .Tariq
yeye alikuwa sofani akiwa na
pakiti la sigara akivuta moja
baada ya nyingine.Mara katika
chaneli ile kukaonyeshwa video
ya Habib akitangaza Alshabaab
kuhusika katika mashambulio
yale mawili yaliyotokea
Tanzania. Video ile ilimstua
sana Tariq
“ Kumbe ni Alshabaab ndio
waliotekeleza mashambulio haya
!! akasema kwa mshangao.
“Kwa miaka kadhaa
sijamuona Habib.Nimestuka
sana nilipomuona .Hajabadilika
na hata sura yake bado ina lile
tabasamu lake la kikatili.”
Akasema Tariq huku akiwasha
sigara nyingine na kuvuta kwa
fujo
“Umeshuhudia Alshabaab
walichokifanya leo.Mamia ya
watu wasio na hatia wamepoteza
uhai .Faida gani inayopatikana
kwa kuua watu wengi hivi wasio
na hatia ? Ndani ya hoteli ile
kulikuwa pia na watoto wadogo
hao wamekosa nini? Kwa hiki
tunachokishuhudia bado kuna
sababu ya kuendelea kuwa
wafuasi wa makundi haya? Bado
unatamani kuendelea kuua
watu wasio na hatia? Huu ni
unyama uliopitiliza.!!! Akasema
Yasmin.Tariq akapuliza moshi
mwingi hewani na kusema
“ Yasmin kuna jambo
ambalo limekuwa linaniumiza
kichwa changu toka jana
ambalo naomba unisaidie
kupata jibu lake kama
unalifahamu.”
“Uliza” akajibu Yasmin
“ Rais alinifuata gerezani
akaniambia kwamba anataka
kuniachia huru lakini atafanya
hivyo iwapo nitamsaidia kupata
mawasiliano ya
Habib.Nilishangaa sana kwa rais
wa nchi kutaka kuwasiliana na
kamanda mkuu wa Alshabaab.
Kwa kuwa nilikwisha choka
kukaa gerezani nilimsaidia rais
na akafanikiwa kuzungumza na
Habib .Sikujua waliongea
nini,hadi jana usiku nilipotolewa
gerezani nikaambiw akwmaba
niko huru na kukabidhiwa kwa
vijana wale walionileta katika ile
nyumba tuliyolala.Wewe
umekuwa unazungumza na rais
kwa muda mwingi na katika
maongezi yenu nimesikia
kwamba kuna makubaliano
yamefanyika kati ya rais na
Alshabaab.Nataka kufahamu
wamekubaliana nini?Nijibu
tafadhali kama unafahamu
chochote” akasema Tariq
“ Tariq ,hata mimi kama
ilivyokuwa kwako rais alinifuata
gerezani akaniambia kwamba
amekuja kuniachia
huru.Nilimuuliza kwa nini
anataka kuniachia huru
akasema kwamba amefanya
makubaliano na Habib na moja
kati ya makubaliano yao ni mimi
kuachiwa huru.Nilishangaa
sana kwani sikuwa
nikimfahamu huyo Habib ni
nani hadi pale aliponitajia
kwamba ni kiongozi wa
Alshabaab.Baada ya kutoka pale
gerezani akanipeleka katika ile
nyumba tuliyolala na
nikafanikiwa kuzungumza na
Habib kwa mara ya kwanza ,
akaniambia kwamba yeye
hanifahamu lakini ameelekezwa
na IS kwamba moja kati ya
makubaliano yake na rais ni
mimi kuachiwa huru.Kitu cha
pili ambacho walikitaka ni hati
ya muungano wa Tanganyika na
Zanzibar hii ambayo tunayo
hapa.” Akamimina pombe katika
glasi akanywa halafu akatikisa
kichwa na kusema
“ Nilifanikiwa kuzungumza
na viongozi wangu wa IS
wakaniambia kwamba rais wa
Tanzania anataka Alshabaab
wamfanyie kazi Fulani nchini
kwake na Alshabaab
wakawasiliana na IS ambao
walitoa masharti hayo
mawili.Endapo Alshabaab
wangefanikisha kupatikana kwa
vitu hivyo viwili basi IS
wangewalipa pesa nyingi na vile
vile wangeunganisha nguvu na
kuanzisha mapambano ili
kuhakikisha wanaiangusha
serikali ya Somalia kitu
ambacho Alshabaab wamekuwa
wakikitafuta kwa miaka
mingi.Kwa sasa IS ni kikundi
cha kigaidi chenye nguvu kubwa
duniani.Alshabaab
walikubaliana na matakwa hayo
ya IS na wakampa masharti rais
wa Tanzania akakubali.Kuhusu
makubaliano ya rais wa
Tanzania na Alshabaab mimi
siyafahamu lakini yawezekana
walikubaliana kuhusu
mashambulio haya ya leo kwani
si mara moja rais wa nchi
kutumia vikundi vya kigaidi
katika kufanikisha mambo yao
Fulani Fulani na inawezekana
kabisa katika mashambulio
haya mawili yaliyotokea leo hii
hata rais wa Tanzania anaweza
kuwa anahusika japokuwa sina
uhakika na hilo ” akasema
Yasmin .Kama madirisha ya
chumba kile yasingekuwa wazi
chumba chote kingejaa moshi
kutokana na sigara mfululizo
alizokuwa anavuta Tariq.
“ Maelezo yako yamenipa
picha kamili ,kweli nilikuwa
gizani na sikujua chochote
kinachoendelea.Bado kuna kitu
kimoja nahitaji kukifahamu.IS
wanaitaka hati ya muungano wa
Tanganyika na Zanzibar kwa
kusudi gani? Akauliza
Tariq.Ilimchukua Yasmin zaidi
ya dakika mbili kujibu.
“Baada ya kupata upinzani
mkubwa katika nchini nyingi za
mashariki ya kati ,ulaya na
Amerika Is wameamua
kuwekeza na kuliimarisha zaidi
kundi lao barani Afrika,hivyo
wakanituma mimi nije afrika
mashariki kuweka sawa
mipango ya kuanzisha kwa tawi
la IS katika ukanda huu.Kwa
muda wa miaka kumi na nne
nimeishi katika sehemu mbali
mbali za afrika mashariki
nikifanya uchunguzi na mipango
ya kueneza kundi la IS na
namna tutakvyoweza kufanya
kazi.Pamoja na kuzunguka
sehemu mbali mbali za afrika
mashariki makao yangu makuu
yalikuwa Dar es salaam
Tanzania ambako nilifanikiwa
kumpata mwanaume mmoja
aliyekuwa anajishughulisha na
biashara ya dawa za kulevya
nikazaa naye mtoto
mmoja.Huyu alinisaidia sana
bila yeye kufahamu mimi ni
nani.Baadae nikakamatwa na
kufungwa gerezani .” akatulia
kidogo akamimina pombe katika
glasi na kunywa .
“ Niliyakosa sana maisha
kama haya .Nilikuwa na kiu ya
mvinyo huu ” akasema Yasmin
na kunywa tena pombe nyingine
halafu akaendelea.
“Katika uchunguzi wangu
niligundua kwamba IS
tungekuwa na mafaniko
makubwa na tungeweza kufanya
kazi zetu kwa uhuru zaidi iwapo
tungefanikiwa kukimiliki kisiwa
cha Pemba.Tungefanikiwa
kukipata kisiwa hiki tungeweza
kulitawala eneo la bahari na
hata eneo zima la afrika
mashariki.Niliwasilisha
mapendekezo hayo kwa wakuu
wangu wakakubaliana nayo
lakini tatizo likawa ni namna ya
kuweza kukipata kisiwa hicho
kwani kiko ndani ya jamhuri ya
muungano wa Tanzania .Kitu
pekee ambacho kingepelekea IS
wakitwae kisiwa cha pemba ni
kwanza kuuvunja muungano
kati ya Tanganyika na Zanzibar
halafu visiwa vya Unguja na
Pemba kila kimoja kiwe
huru.Wakati nakamatwa
tulikuwa katika kutafuta namna
ya kulifanikisha hilo yaani
kuuvunja muungano wa
Tanganyika na Zanzibar na
mpaka sasa bado mawazo yangu
wanaendelea kuyafanyia kazi
kwa kutumia mbinu mbali mbali
za kutaka kuuvunja muungano
huu lakini bado hawajafanikiwa
na ilipojitokeza fursa kama hii
wameamua kuitumia vyema
.Kujibu swali lako IS wanaitaka
hatiya muungano wa
Tanganyikan a Zanzibar kwa
lengo la kuuvunja muungano ili
wakitwae kisiwa cha Pemba..”
Akasema Yasmin na kukawa
kimya.
Yasmin aliendelea kunywa
mvinyo huku Tariq akiendelea
kuvuta sigara kwa fujo huku
akimtazama Yasmin halafu
akatabasamu.
“ Yasmin sikuwa
nikikufahamu na wala sijawahi
kukusikia hadi nilipokutana
nawe jana katika ile nyumba
tuliyolala.Nilipokuona mwanzo
nilikuona kama mwanamke wa
kawaida lakini kwa haya
uliyonieleza na kwa mambo
niliyoshuhudia ukiyafanya leo
hadi tukafanikiwa kutoka
salama katika uwanja ule wa
ndege nimekuogopa.Mimi
nilikuwa mratibu mkuu wa
mashambulio yote ya Alshabaab
lakini nakiri mbele yako kuwa
sina akili za haraka haraka
kama ulizonazo .Ningekuwa
peke yangu nisingeweza kutoka
ndani ya ule uwanja” akatulia
akavuta sigara yake na kusema
“ Kuna jambo ambalo
sikuwa nimekueleza.Nikiwa na
Alshabab niliratibu
mashambulio mengi tu ambayo
yalipelekea vifo vya watu wengi
na kwa taarifa yako ninatafutwa
sana na serikali za Kenya na
Somalia kutokana na kuratibu
mashambulio mengi
yaliyopoteza maisha ya watu
wengi.Toka jana nilipoambiwa
kwamba tumeandaliwa ndege ya
kutupeleka Mogadishu nilikuwa
na mawazo mengi sana ni jinsi
gani nitakavyoweza kushuka
Mogadishu bila kukamatwa?
Japokuwa ni miaka mingi
imepita lakini uhakika wa
kuvuka salama pale uwanjani
ulikuwa mdogo sana. Mawazo
niliyokuwa nayo yalikuwa ni
kuiteka ndege ile kabla ya
kufika Mogadishu na kuibadili
muelekeo ili tupelekwe sehemu
nyingine jambo ambalo
ulilifanya wewe na ninashukuru
na wewe kuwa na wazo kama
langu.Sijui lengo la Habib ni nini
aliposema kwamba tupelekwe
Mogadishu wakati anafahamu
fika kwamba serikali ya Somalia
wananitafuta .Kwa hiyo kitendo
ulichokifanya cha kubadili
uelekeo wa ndege kimenisaidia
sana ni kama vile ulikuwa
katika akiliyangu.Napenda
kukuhakikishia kwamba niko
tayari kufanya kazi nawe
.Maneno uliyonieleza tukiwa
ndegeni kuhusiana na
kuendelea na ushirika na
mitandao yetu ya zamani
nimeyatafakari sana na
nimefanya maamuzi hata mimi
ya kuachana na maisha kama
yale na kuanza maisha
mapya.Kwa hiyo Yasmin kama
una mpango wowote ulionao wa
kuanza maisha mapya naomba
unishirikishe na mimi tafadhali”
akasema Tariq.Yasmin akageuka
akamtazama Tariq usoni kisha
akauliza
“ Una hakika na maamuzi
yako?
“ Ndiyo Yasmin.Nahitaji
kupotea na kwenda kuanza
maisha mapya mbali kabisa na
Alshabaab.Kauli yako
imenifanya nitafakari sana
maisha yangu ndani ya
Alshabaab na faida
nilizozipata.Mpaka sasa sijaona
faida yoyote niliyopata kwa
kulitumikia kundi hili .Nimeua
watu wengi lakini hakuna kitu
cha maana nilichopata sina mke
,sina mtoto sina familia .Nataka
nianze upya. Usiniache tafadhali
kama una mipango yoyote
mizuri ya kuanza maisha mapya
mbali na hapa.” Akasema Tariq
“ Sawa nimekusikia
.Nitakusaidia kama kweli una
nia ya dhati” akasema Yasmin
na kuendelea kunywa mvinyo.
“Ninatakiwa kuwa makini
sana na huyu
jamaa.Ninafahamu namna ya
kuwasoma watu huyu si mtu
mzuri hata kidogo.Nikimtazama
machoni hamaanishi kile
anachokisema.Najua ana lengo
lake lingine lakini hapa kwangu
hawezi kufanya lolote.” Akawaza
Yasmin
“ Yasmin”akaita Tariq na
Yasmin akageuka akamtazama.
“ Habib alikuwa na
mategemeo leo saa kumi na
moja tungefika Mogadishu lakini
mpaka sasa hatujatokea na
hatuna mawasiliano naye
yoyote.Nini kitatokea iwapo
mpaka kesho asubuhi hatakuwa
ametuona ?
“ Ni wazi atafanya
mawasiliano na rais wa
Tanzania kumuuliza nini
kimetokea na hapo ndipo msako
wa kututafuta
utakapoanza.Kesho asubuhi
tunarejea Dar es salaam.”
“ Dar es salaam? !! akauliza
Tariq kwa mshangao
“ Ndiyo tunarejea Dar es
slaam” akajibu Yasmin bila wasi
wasi wowote
“ Tunakwenda kutafuta nini
Dar es salaam? Kule ni hatari
sana kwetu.Kama ulivyosema
mwenyewe kwamba lazima
Habib atawasiliana na rais wa
Tanzania na atamfahamisha
kwamba hatujafika Mogadishu
na tutaanza kutafutwa kila
kona.Kwa sasa tuko mbali na
Dar es salaam kwa nini tusianze
safari yetu na kutokomea mbali
bila kwenda kutafuta hatari
tena? Yasmin maisha ya mateso
niliyokaa gerezani yananitosha
sitaki tena maisha kama yale na
ndiyo maana nimeanua kuanza
maisha mapya.Tafadhali
nakuomba ufikirie upya mpango
wako huo wa kurejea tena Dar
es salaam” akasema
Tariq.Yasmin akanywa mvinyo
kidogo na kusema
“ Kesho tunarejea Dar es
salaam.Kuna kazi ambayo
sijaikamilisha .Natakiwa kwenda
kumchukua mwanangu ambaye
yuko Dar es alaam na safari ya
kuelekea katika maisha mapya
itaanzia hapo.Siwezi kuondoka
bila mwanangu Shamim.kama
uko kitu kimoja na mimi
tutaongozana wote kurejea Dar
es salaam.Tuko pamoja?
Akauliza.Tariq akatumia muda
kidogo kutafakari na kusema
“ Sawa tutaenda huko Dar
es salaam” akasema Tariq huku
akiwasha sigara nyingine.
“ Sipati picha Habib
atakuwa katika hali gani muda
huu .Atakuwa na hasira
zisizomithilika.Ninamfahamu
Yule jamaa ni mkatili sana na
ana roho ya kinyama .Endapo
atagundua kwamba
tumemzunguka na kumfanyia
mchezo huu sijui nini kitatokea
.Atatusaka kwa maisha yake
yote yaliyobaki na akitupata
kitakachofuata ni kutuua.Siwezi
kumsaliti Habib kiasi hiki,lazima
nitafute namna ya kufanya na
kuichukua hii hati
nikamkabidhi Habib.Huyu
mwanamke hawezi kunishinda
kwani tayari nimekwisha
muweka upande wangu na
tayari ananiamini
.Ninachotakiwa kabla ya kesho
asubuhi niwe nimemmaliza
kisha niondoke na hati hii.Kabla
ya yote natakiwa kutafuta nafasi
ya kuzungumza na Habib au
mtu mwingine yeyote katika
Alshabaab nimfahamishe kile
kinachoendelea.pamoja na
kukaa gerezani muda mrefu
lakini siwezi kulisaliti kundi
langu hata kidogo.Nimejiunga
na Alshabaab nikiwa kijana
mdogo sana wa miaka kumi na
nne na nitakufa mtiifu kwa
Alshabaab.”akawaza Tariq na
kukohoa kidogo kisha akaita
“Yasmin”
Yasmin akageuka
akamtazama
“Kwa miaka kadhaa
tumekuwa kifungoni lakini
baada ya kutoka kifungoni bado
tunaendelea kujificha
ndani.Japo kwa mara moja kwa
nini tusitoke tukaenda sehemu
kupoteza mawazo na kutuliza
akili zetu.Tumepitia mambo
mengi sana hadi tumefika hapa
kwa hiyo si vibaya endapo
tukatoka kidogo.Hakuna
anayetufahamu hapa Zanzibar
kwa hiyo tuko huru kwenda
sehemu mbali mbali za
burudani.Ninahisi kuboreka
sana hapa ndani” akasema
Tariq.Yasmin akatabasamu na
kusema
“ Mimi si mwendaji wa
sehemu za burudani na zaidi ya
yote sijaboreka hapa ndani na
ninajisikia furaha
sana.Niliyakosa sana maisha
haya nilipokuwa gerezani.”
Akasema Yasmin na kuinuka
akamfuata Tariq akaketi
pembeni yake.
“ Kitu gani hasa
ulichokikosa ulipokuwa
gerezani? Akauliza Yasmin.Tariq
akatabasamu na kusema
“ Nilikosa vingi lakini
kikubwa nilichokikosa ni
kushuhudia milipuko ya
mabomu niliyoyatega.Mimi ndiye
niliyekuwa mratibu wa
mashambulio yote ya Alshabaab
na nilisikia raha sana kuona
shambulio nililoliratibu
linafanikiwa” akasema Tariq
“ Hicho peke ndicho
kinachokupa furaha katika
maisha yako? Ukiacha milipuko
ya mabomu hakuna kingine
ambacho kinakupa furaha
katika maisha ? Hakuna
wanawake huko katika kambi
zenu wa kuwastarehesha?
“ Wanawake? Akauliza Tariq
“ Ndiyo”
“ Wanawake wapo lakini
mimi starehe yangu si
wanawake bali ni milipuko kama
nilivyokueleza.Wanawake nakaa
nao mbali kabisa na ndiyo
maana mpaka sasa sina mke
wala mtoto” akasema Tariq na
kuwasha sigara nyingine.Yasmin
akamshika bega na kusema
“ Ni vipi endapo
nitakwambia kwamba kitu
nilichokikosa sana nikiwa
gerezani ni mwanaume wa
kufanya naye mapenzi?
Akasema Yasmin huku
akitabasamu.Tariq akastuka.
‘”Mbona umestuka Tariq?
Hicho ndicho kitu nilichokikosa
mno nikiwa gerezani.Ninapenda
sana kufanya mapenzi.Ni
starehe yangu kubwa na kwa
usiku wa leo kwa kuwa niko
nawe humu chumbani utanikata
kiu yangu ya miaka mingi.Kwa
hiyo hatutakwenda kokote
nataka tufanye mapenzi usiku
kucha kufidia miaka yote
ambayo nilikuwa gerezani.”
Akasema Yasmin huku
akimshika shika Tariq maeneo
nyeti.
“ Yasmin subiri
kwanza.Mimi si mpenzi wa
mambo hayo.Japokuwa nimekaa
gerezani kwa miaka mingi lakini
bado sina hamu ya kufanya
mapenzi.” Akasema Tariq lakini
Yasmin hakusikia chochote
kwani tayari mashetani
yalikwisha mpanda.Akavua
gauni alilolivaa na kubakiwa na
nguo za ndani.Pamoja na kukaa
miaka mingi gerezani lakini
bado mwili wa Yasmin ulikuwa
mwororo na wenye
kung’aa.Tariq akahisi mwili
unamchemka baada ya
kuushuhudia mwili ule mwororo
.Yasmin akaendelea na utundu
wake akaifungua suruali ya
Tariq na kwa kutumia mdomo
na ulimi wake akafanya utundu
mkubwa pale ikulu kiasi cha
kumfanya Tariq atoe
miguno.Ghafla kama mbogo
majeruhi Tariq akavua fulana
aliyoivaa akaitupa chini
akamuinua Yasmin na kumbeba
mikononi.Tariq alikuwa ni pande
la mtu mwenye nguvu
nyingi.Hakuwa na subira
akakianzisha kipute.Yasmin
alitoa ukele kufurahia kipute
kile na gwaride alilochezeshwa
na Tariq.Kilikuwa ni kipute hasa
kilichochukua dakika arobain
.Hadi wote wanamaliza vitu
vilikuwa vimetawanyika hovyo
mle chumbani kwani kutokana
na ugumu wa mpangano ule
mechi ilichezwa kila mahali .
Wote wawili walikuwa
wanahema kama wakimbiaji wa
mbio ndefu.
“ Sikutegemea kama una
uwezo mkubwa kiasi
hiki.Ahsante kwa kunikata kiu
japo bado nitahitaji zaidi na
zaidi usiku wa leo” akasema
Yasmin
“ Mapenzi si starehe yangu
lakini nikiamua kufanya nina
uwezo mkubwa sana na
ninaweza kufanya kwa muda
mrefu” akasema Tariq.
Yasmin akainuka
akachukua taulo akaingia
bafuni kujimwagia maji
“ Hii ndiyo nafasi niliyokuwa
naitafuta” akawaza Tariq
akainuka kitandani akajifunga
taulo halafu akanyata hadi
katika begi la Yasmin
akalifungua na kuitafuta simu
.Alipoipata akanyata hadi katika
mlango wa bafu akasikia maji
yakimwagia,Yasmin aliendelea
kuoga.Haraka haraka akaiwasha
halafu akaziandika namba
Fulani katika simu ile akapiga
na kuiweka sikioni ili kusikia
kama inaita taratibu
akaufungua mlango akatoka nje
.Akazungumza na mtu fulani
haraka haraka kwa kiarabu
halafu akakata simu na
kufungua mlango taratibu
kurejea ndani.Alipata mstuko
mkubwa pale alipojikuta
akitazamana na Yasmin
aliyekuwa mtupu akichuruzika
maji mwili huku akiwa
amemnyooshea bastora.
“ Ingia ndani taratibu kama
ulivyotoka” akasema
Yasmin.Tariq akaingia ndani na
kuufunga mlango akaamriwa
apige magoti .Ghafla kikatokea
kitu ambacho Yasmin hakuwa
amekitegemea.Tariq aliruka
mzima mzima na kumvaa
Yasmin wote wakaanguka
chini.Bastora ya Yasmin
ikamponyoka na kuanguka
pembeni.Tariq akampiga Yasmin
ngumi nzito sana na kunyoosha
mkono ili kuichukua bastora ile
lakini Yasmin tarai alikwisha
msoma na hakutawa tayari
kumpa nafasi hiyo.Akamchoma
kidole cha jicho.Tariq
akapandisha hasira na kuanza
kumvurumishia Yasmin
makonde mazito.Yasmin
akaishika stuli iliyokuwa
pembeni na kumpiga nayo Tariq
kichwani akaanguka
chini.Akainuka haraka haraka
na kumpiga teke zito maeneo ya
korodani na kumfanya Tariq
agugumie kwa maumivu makali
aliyoyapata.Kama hiyo haitoshi
akauchukua stuli ile na
kumbamiza nayo mara mbili
kichwani.Tariq akaanza kutokwa
na damu kichwani.Yasmin
akaiokota bastora yake na
kumuelekezea
“ Nani ulikuwa unaongea
naye? Nieleze ukweli ama sivyo
sintakuacha hai” akasema
Yasmin
Tariq hakusema chchote
aliendelea kugugumia maumivu
“ Tariq hii ni mara ya
mwisho nieleze nani uliyempigia
simu? Akauliza lakini Tariq
hakumjbu.Akaiokota simu
akatazama namba aliyopiga
Tariq lakini tayari ilikuwa
imefutwa.
“ Nilifahamu toka awali
lengo lako na nilikuwa
nakusubiri ufanye
ulivyofanya.Ulisema hutaki tena
kushirikiana na Alshabaab ili
nikuamini na mwisho wa siku
uweze kuchukua hati hii na
uondoke nayo.Mimi ni mtu
mwingine Tariq huwezi
kunizunguka hata mara moja na
kwa hili ulilolifanya
sintakusamehe.” Akasema
Yasmin
“ Unadhani utafanikiwa
malengo yako? Usijidanganye
Yasmin hakuna chochote
utakachofanikiwa.Hutafanikiwa
kundoka salama hapa Zanzibar
na hautakwenda
kokote.Jisalimishe kwa Habib
na umrejeshee kilicho mali
yake.Usipofanya hivyo hata
mwanao hautamuona tena .Hivi
tunavyoongea vikosi vyote vya
ulinzi tayari vina taarifa zako
muda wowote toka sasa
utakamatwa” akasema Tariq na
kuzidi kumpandisha hasira
Yasmn na kwa kutumia bastora
ile iliyofungwa kiwambo cha
sauti akammiminia Tariq risasi
kichwani.
“ Yasmin Esfahani huwa
hazungukwi hata mara
moja.Hukujua unacheza na mtu
wa aina gani” akasema Yasmin
kwa hasira.Tariq hakuwa na
uhai.Akamvuta na kumpeleka
bafuni na kuufunga
mlango.Akavaa haraka na
kujitazama katika kioo.
“Lazima niondoke hapa
haraka iwezekanavyo.Natakiwa
kwenda Dar es salaam
kumchukua Shamin ” Akawaza.
SEASON 6: SEHEMU YA 5
Imetimu saa tatu na dakika
ishirini katika makao makuu ya
Alshabaab hali ikiwa ya
ukimya.Ulinzi ulikuwa mkali
kama ilivyo kawaida yake.Mpaka
mida hii hakukuwa na taarifa
zozote kuhusiana na walipo
Tariq na Yasmin ambao
walitegemewa wangewasili
Mogadishu mida ya jioni baada
ya ndege yao kusemekana
kupata hitilafu angani na
kulazimika kutua kwa dharura
kisiwani Unguja.
Habib Alzaraq alirejea
kutoka kuswali,akauliza kama
kuna taarifa zozote kuhusiana
na akina Tariq lakini hadi muda
huo hakukuwa na taarifa zozote
zilizopatikana .Akamuagiza mtu
wake anayehusika na masuala
ya mawasiliano afanye
mawasiliano na uwanja wa
ndege wa Zanzibar kufahamu
kama ndege ile waliyokuwa
wanasafiria akina Tariq iliyotua
kwa dharura pale Zanzibar
kama imekwishaondoka pale
uwanjani au bado inaendelea na
matengenezo.Mawasiliano
yalifanyika na taarifa
iliyopatikana ni kwamba baada
ya kufanyiwa uchunguzi katika
injini yake ndege ile ilifanikiwa
kuruka na kurejea Dare s
salaam.Habib akapewa taarifa
hizo na zikamstua
“ Dar es salaam ? akauliza
Habib kwa mshangao.
“ Ndiyo mkuu.Nimetaarifiwa
kwamba ndege ilifanyiwa
uchunguzi na kisha
ikaruhusiwa kuondoka na
ikarejea Dar es salaam.”
“Yasmin na Tariq
walikuwemo ndani ya hiyo ndege
iliporejea Dar es salaam?
Akauliza Habib
“ Nimepewa jibu la jumla
kwamba ndege hiyo imerejea
Dar es salaam,hawakufafanua
kama akina Tariq nao
walikuwemo ndani yake”
akasema Yule msaidizi wake wa
masuala ya mawasiliano.Habib
akajaribu kupiga zile namba za
simu ambazo Yasmin alimpigia
mara ya mwisho akiwa hospitali
lakini hazikuwa zikipatikana.
“ Naanza kuingiwa na wasi
wasi kwamba yawezekana kuna
mchezo unataka kuchezwa
hapa.Kwa nini ndege irejee Dar
es salaam wakati ilitakiwa
iendelee na safari kuelekea
Mogadishu? Watu wa kutoka IS
watawasili usiku huu kwa ajili
ya kufanya makabidhiano ya ile
hati ya muungano ambayo
tayari Yasmin na tariq
wamekwishakabidhiwa.Nitawael
eza nini? Akajiuliza Habib kisha
akazitafuta namba za simu za
rais akapiga.Sura yake ilikuwa
imejikunja kwa hasira.Simu
iliita bila kupokewa akapiga tena
na safari hii ikapokewa.
“ Hallo Habib niko kwenye
kikao kizito sana kuhusiana na
mambo yaliyotokea hapa nchini
leo.Naomba niwasiliane nawe
baada ya kama saa moja hivi”
akasema rais kwa sauti ndogo.
“Sina muda wa kusubiri rais
nataka tuongee sasa hivi.Kama
ni muhimu wewe kuwepo katika
kikao hicho simamisha kikao
uzungumze nami kwanza.”
Akasema Habib kwa ukali.Rais
akatazama pande zote kama
kuna mtu karibu kisha akauliza
“ Unasemaje Habib?
“ Sikiliza rais,sihitaji ugomvi
na wewe wala vita na nchi
yako.Tulikubaliana vizuri na
nimeifanya kazi yako kama
ulivyotaka.Nataka unipatie
Tariq,Yasmin na ile hati kama
tulivyokubaliana kama si hivyo
utatufahamu sisi ni nani !!
akasema Habib kwa ukali
“ Mbona sikuelewi Habib?
Nilitoa ndege kwa ajili ya
kuwapeleka Tariq na Yasmin
Mogadishu.Hawapo hapa
nchini,tayari wamekwisha
ondoka.”
“Hawajafika
Mogadishu.Niliwasiliana na
Yasmin jioni ya leo walitua kwa
dharura katika uwanja wa ndege
wa Zanzibar kutokana na
hitilafu katika ndege .Mpaka
usiku huu hakuna taarifa zozote
kuwahusu wao.Tumefuatilia
uwanja wa ndege wa Zanzibar
tumetaarifiwa kwamba ndege ile
baada ya kufanyiwa uchunguzi
imepaa na kurejea Dar es
salaa.Mheshimiwa rais naamini
huu ni mchezo
unatuchezea.Nilikuonya hapo
awali kwamba usijaribu kufanya
mchezo wowote wa kihuni na
sisi lakini unaonekana
kulipuuza onyo hilo na unataka
kutuzunguka.Tumeifanya kazi
yako na sisi tunahitaji haki
yetu” akasema habib.
“ Habib naomba unisikilize
vizuri.Mimi sifahamu chochote
kuhusiana na suala hilo.Nilitoa
ndege ambayo ni nzima kabisa
na haina hitilafu yoyote
nashangaa kusikia kwamba
walitua Zanzibar kwa
matengenezo.Kinachonishangaz
a sijataarifiwa chochote
kuhusiana na jambo hilo
nikiamini kwamba mpaka muda
huu tayari Yasmin na Tariq
watakua wamekwisha fika
hapo.Hizi unazonipa ni taarifa
ngeni kabisa.Naomba unipe
muda nilifuatilie suala hili.”
Akasema rais
“ Ninakupa mpaka kesho
saa mbili asubuhi tuwe
tumepata kila kile tulichokuwa
tumekubaliana .Kama
hatutakuwa tumepata haki yetu
nakuhakikishia damu hii
iliyomwagika leo itaendelea
kumwagika kila uchao hapo
Tanzania.” akasema Habib na
kukata simu.Ernest Mkasa
akahisi mwili kuloa jasho.
“ Nini kimetokea? Ni kweli
ndege waliyopanda akina Tariq
ilipata hitilafu na kutua
Zanzibar kwa dharura? Mbona
sijataarifiwa jambo hili?
Akajiuliza.
“ Hili sasa ni suala jipya
ambalo natakiwa
kulishughulikia kwa haraka.
Tariq na Yasmin wako wapi?
Akajiuliza rais.
“ Au huu ni mpango wa
Yasmin ili anirudishie hati ile ya
muungano kwa lengo la
kumpata mwanae? Nahisi hivyo
kwani aliniahidi kufanya kila
atakachoweza ili kumpata
mwanae.Kama huu ni mpango
wake kwa nini basi hajanitaarifu
chochote? Hata hivyo natakiwa
kuanza maandalizi ya
kuhakikisha ninampata Maria
haraka iwezekanavyo ili ikitokea
Yasmin akamuhitaji basi tayari
niwe naye.” Akawaza rais na
kumpigia simu mmoja wa vijana
wake aliyempa jukumu la
kuhakikisha kwamba Yasmin na
Tariq wanaondoka nchini
akamtaka afuatilie suala lile
kama lina ukweli wowote na
amjulishe ndani ya muda
mfupi,halafu akarejea katika
ukumbi wa mikutano
Baada ya kuongea na
rais,Habib akawakusanya
makamanda wake kwa ajili ya
kikao cha dharura kujadili
kilichotokea.Kabla ya kikao
kuanza,Aziz mmoja wa wasaidizi
wake anayemuamini sana
akatokea akiwa anahema na
ilionekana alikuwa anakimbia
“ Samahani nimechelewa
mkuu nilikwenda kuswali lakini
hata hivyo nimekuja na habari
ya muhimu sana”
“ Habari gani Aziz? Akauliza
Habib
“ Nimezungumza na Tariq.”
“ Tariq? Amekupigia simu?
“ Ndiyo mzee.Tariq
amenipigia simu nikiwa njiani
kuja hapa.”
“ Yuko wapi? Nini kimetokea
hadi wakashindwa kufika hapa
kama tulivyokuwa tumepanga?
Akauliza Habib
“Kuna tatizo
limetokea.Amenieleza kwa ufupi
sana kwani alitumia simu ya
Yasmin bila yeye
kufahamu.Tariq anasema
kwamba ndege waliyokuwa
wanaitumia haikupata hitilafu
yoyote bali Yasmin
aliwalazimisha marubani
kubadili muelekeo na kutua
Zanzibar kwa kisingizo cha
hitilafu katika injini.Anasema
kwamba Yasmin amebadilika na
ana mpango wa kutokomea
kusikojulikana na hati ya
muungano.Ameniambia kwamba
tufanye haraka tumuwahi
Yasmin wako Hotel Lepatido”
akasema Aziz na wote
wakamtazama Habib kusikia
atasema nini
“ Niliwakatalia IS kwamba
siwezi kumpa nyaraka kubwa ile
ya hati ya muuungano mtu
nisiyemfahamu vizuri lakini
wakakataa na kudai kwamba
Yasmin hana matatizo ni mtu
wao lakini kumbe hisia zangu
zilikuwa za kweli.Huu ni
mgogoro mwingine kati yetu na
IS.Nilifanya kosa kubwa sana
kumuamini Yasmin badala ya
mtu wangu Tariq.” Akawaza
Habib na kuchukua simu
akampigia rais Ernest ambaye
licha ya kuwa katika kikao kizito
na wakuu wa vyombo vyote vya
usalam wakijadili mashambulio
yale yaliyotokea alilazimika
kutoka nje ya ukumbi wa
mikutano baada ya kuiona
namba ya Habib
“ Habib nilikuomba unipe
muda nilifuatilie suala
lako.Vijana wangu bado
hawajanipa taarifa zozote mpaka
sasa.Nitakujulisha nikipata
taarifa zozote toka kwao”
akasema Ernest
“ Mheshimiwa rais
nimepata taarifa sasa hivi nini
kimetokea.Tariq amemmpigia
simu mmoja wa wasaidizi wangu
na akamweleza kwamba ndege
waliyopanda haikuwa na hitilafu
yoyote bali ni Yasmin ndiye
aliyewatishia marubani kwa
bastora na kuwataka wabadili
uelekeo waelekee
Zanzibar.Yasmn amefanya
usaliti mkubwa na sasa anataka
kutoroka na hati ile
uliyompatia.Kwa mujibu wa
Tariq mpaka sasa bado wako
Hotel Lepatido
walikofikia.Mheshimiwa rais
nakuomba fanya kila unaloweza
uweze kumdhibiti Yasmin na
niweze kuipata hiyo hati usiku
wa leo na umkabidhi
Tariq.Tuma vikosi vya polisi sasa
hivi vilizingire jengo la hoteli
hiyo walimo na Yasmini
akamatwe haraka sana.Tayari
nimekupa taarifa zote na
ukishindwa kufanikisha
kukamatwa Yasmin nitaamini
kwamba wewe na Yasmin mko
kitu kimoja.Nitakupigia tena
baada ya robo saa kujua
maendeleo” akasema Habib na
kukata simu.Rais
akachanganyikiwa.
“ Ninaamini Yasmin
amefanya hivi alivyofanya
kutokana na yale makubaliano
yetu kwamba akinirejeshea hati
na mimi nitampatia mwanae.Ni
juu yangu sasa kuchagua
kwamba ninataka hati au
ugomvi na Alshabaab? Akawaza
na kumuita mkuu wa majeshi
Jenerali lameck Msuba
akamueleza kuhusiana na
jambo lile
“ Mheshimiwa rais hii ni
nafasi imepatikana ambayo
hatupaswi
kuichezea.Tunatakiwa kufanya
kila tunaloweza kumdhibiti
Yasmin na kuichukua hati
yetu.Usiogope vitisho kutoka
kwa Alshabaab kwani hawawezi
kufanya chochote.Tutapambana
nao” akasema lameck
“ Kwa hiyo unanishauri nini
Lameck?
“ Ushauri hapa ni kutuma
kikosi maalum toka usalama wa
taifa kwenda hotelini hapo
kuwadhibiti akina Tariq na
Yasmin.Hawatakiwi kwenda
askari au wanajeshi .Watu wale
wanapaswa kukamatwa kimya
kimya na kurejeshwa mahala
walikokuwa wamefungwa ”
akasema Lameck na rais
akamuita Silvanus Kiwembe
mkurugenzi wa idara ya
usalama wa taifa ambaye naye
alikuwemo katika kikao kile.
“ Silva nimekuita hapa kuna
jambo nataka lifanyike kwa
haraka na ambalo ni muhimu
mno.Yasmin Esfahani pamoja
na mtu mwenzake anaitwa Tariq
wako katika hoteli moja inaitwa
Lepatido kisiwani Zanzibar
.Nataka haraka sana tuma
kikosi cha vijana hodari kumi au
zaidi waende hotelini hapo usiku
huu na wahakikishe
wanawakamata watu hao wawili
na warejeshwe kule
gerezani.Kuna bahasha anayo
Yasmin ambayo nataka
ichukuliwe na isifunguliwe na
mtu yeyote kuona kilichomo
ndani bali iletwe kwangu moja
kwa moja.Kwa umuhimu wa
suala hili nataka wewe
mwenyewe uwepo katika kikosi
hicho ili kila kitu kiende
sawa.No mistake.Nawahitaji
Tariq na Yasmin wakiwa hai.”
Akasema rais na Silvanus
akaondoka kwenda kutekeleza
maagizo yale ya rais..Baada ya
Silva kuondoka ,rais
akamgeukia Jenerali Lameck
“Lameck nataka njia zote za
kuingilia na kutokea Zanzibar
zifungwe kwa muda ili kuzuia
Yasmin asiweze kupata nafasi ya
kutoroka.Viwanja vyote vya
ndege visiruhusu ndege yoyote
kutoka na hata bandari zote
zisiruhusu mtu yeyote kutoka
hadi hapo tutakapofanikiwa
kumpata Yasmin.” Akasema
Rais
Asantee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom