Pwani: Watu wametakiwa kulipia square meter moja kwa sh6,000/= Ili kufidia kile eti kinachoitwa fidia kwa aliyekuwa muwekezaji miaka 30 iliyopita

Rweye

JF-Expert Member
Mar 16, 2011
16,958
7,512
Ni wananchi wanaopatikana ndani ya mkoa wa Pwani, Kibaha mji katika mtaa wa Viziwa ziwa. Hari si shwari hasirani, unyanyasaji huu na tamaa za viongozi huko chini inawahangamiza wananchi wa Tanzania na raia pasipo kuwepo na mhamiaji.

Ni kaeneo kadogo kakiitwa "VIMISA". Hapa ndo panapoongelewa haswa, watu wametakiwa kulipia square meter moja kwa sh6,000/= Ili kufidia kile eti kinachoitwa fidia kwa aliyekuwa muwekezaji miaka 30 iliyopita na hata leo hajulikani ni nani na wala wananchi hawajawahi kumuona kwa macho.

Kuna vitisho, ulaghai na ghiliba za kila aina kutoka kwa viongozi wa mtaa mpaka wilaya na lao wote ni moja kuwabomolea wananchi ama walipe hiyo pesa haraka sana iwezekanavyo ndani ya miezi sita. Wameenda mbali hawaruhusu hata wananchi hao kupata huduma muhimu za kijamii ndani ya hilo eneo.

Swali hapa ni, kwanini 6,000 kwa sqmt1 eneo kama lile bei ambayo ni kama ya kukomoa tena haraka haraka ndani ya miezi 6 tu?

Ni kwanini mbali ya wananchi kukubali kulipia Ili kutii amri ya kibabe hiyo bado watishiwe kubomolewa?

Ni kwanini pamoja na kulipia bado hao wananchi wametengwa Ili wasipate huduma muhimu za kiraia kama raia wa nchi hii na hata umeme wanaambiwa wao hawastahili REA wakati maeneo jirani yao wanawekewa umeme wa REA?

Yako mengi lakini mamlaka tajwa hapo juu ndo wenye kuweza kusaidia wananchi hawa Ili wapatiwe na wao haki zap maana inaonekana kuna genge kubwa nyuma ya hili na wakubwa wengi wamo na wengine wananufaika nalo.
 
Waziri Slaa tenda wema ikupendeza watembelee wananchi hawa katika mtaa wao utafaidika na mengi sana maana jambo linazidi kuwa jambo
 
huko ni kujitafutia laana tu...hata kama ni kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji siyo sawa...
Yaani ndani ya Tanzania kuna watu wanataabika si masihara hata kidogo. Kilichonishangaza zaidi ni pale wenye kudai hizo pesa wamesimama kwa hakimu wanasema eti eneo lile kuna watu 400 tu na eti wamejenga vibanda tu ndo wanaishi na si nyumba wakati kiuhalisi mle kuna watu zaidi ya 700 na familia zao na wamejenga nyumba zao za thamani tofauti tofauti kuanzia chumba kimoja hadi nyumba full na za kisasa kabisa.

Kumbe wanahofia kuusema huko ukweli Ili iwe rahisi kwao kuambiwa wakabomoe maana wanajua ukweli ukijulikana wale wananchi ni zaidi ya 700 na nyumba zaidi ya 400 huenda wakapata ugumu wa kwenda kuwabomolea wananchi, na hili linafichwa na hata wakija viongozi wamekuwa wanazuiwa kuingia ndani ya eneo husika Ili kuupata ukweli ulivyo. Mara nyingi wanaitwa eneo la tofauti na ndo hapo stori za uongo zinapotengenezwa.

Na kilichobainika pia ni kwamba ndani ya eneo hilo miongoni mwa wananchi kuna kakundi ka watu wachache ambao wametengenezwa kama mamluki dhidi ya wengi huku wakihaidiwa pesa nyingi pale azma hii chafu ikifanikiwa, kuusema kweli mambo ni ya ajabu sana kwa mtu aliye nje si rahisi kuugundua ukweli huu pasipo kufanya utafiti wa kina maana hako ka kikundi kamepewa na mamlaka ya kuwakilisha wenzao kwa vitisho kwamba atakayekataa kuwatii hao basi kitamkuta Kibaya
 
Yaani ndani ya Tanzania kuna watu wanataabika si masihara hata kidogo. Kilichonishangaza zaidi ni pale wenye kudai hizo pesa wamesimama kwa hakimu wanasema eti eneo lile kuna watu 400 tu na eti wamejenga vibanda tu ndo wanaishi na si nyumba wakati kiuhalisi mle kuna watu zaidi ya 700 na familia zao na wamejenga nyumba zao za thamani tofauti tofauti kuanzia chumba kimoja hadi nyumba full na za kisasa kabisa.

Kumbe wanahofia kuusema huko ukweli Ili iwe rahisi kwao kuambiwa wakabomoe maana wanajua ukweli ukijulikana wale wananchi ni zaidi ya 700 na nyumba zaidi ya 400 huenda wakapata ugumu wa kwenda kuwabomolea wananchi, na hili linafichwa na hata wakija viongozi wamekuwa wanazuiwa kuingia ndani ya eneo husika Ili kuupata ukweli ulivyo. Mara nyingi wanaitwa eneo la tofauti na ndo hapo stori za uongo zinapotengenezwa.

Na kilichobainika pia ni kwamba ndani ya eneo hilo miongoni mwa wananchi kuna kakundi ka watu wachache ambao wametengenezwa kama mamluki dhidi ya wengi huku wakihaidiwa pesa nyingi pale azma hii chafu ikifanikiwa, kuusema kweli mambo ni ya ajabu sana kwa mtu aliye nje si rahisi kuugundua ukweli huu pasipo kufanya utafiti wa kina maana hako ka kikundi kamepewa na mamlaka ya kuwakilisha wenzao kwa vitisho kwamba atakayekataa kuwatii hao basi kitamkuta Kibaya
Haya mambo wanaoyafanya ni wenzetu wanaoangalia maslahi binafsi lakini tatizo kubwa ni pale viongozi wanapoacha kuyafuatilia kwa wakati au na wao kuwa na maslahi na uonevu
 
Ni wananchi wanaopatikana ndani ya mkoa wa Pwani, Kibaha mji katika mtaa wa Viziwa ziwa. Hari si shwari hasirani, unyanyasaji huu na tamaa za viongozi huko chini inawahangamiza wananchi wa Tanzania na raia pasipo kuwepo na mhamiaji.

Ni kaeneo kadogo kakiitwa "VIMISA". Hapa ndo panapoongelewa haswa, watu wametakiwa kulipia square meter moja kwa sh6,000/= Ili kufidia kile eti kinachoitwa fidia kwa aliyekuwa muwekezaji miaka 30 iliyopita na hata leo hajulikani ni nani na wala wananchi hawajawahi kumuona kwa macho.

Kuna vitisho, ulaghai na ghiliba za kila aina kutoka kwa viongozi wa mtaa mpaka wilaya na lao wote ni moja kuwabomolea wananchi ama walipe hiyo pesa haraka sana iwezekanavyo ndani ya miezi sita. Wameenda mbali hawaruhusu hata wananchi hao kupata huduma muhimu za kijamii ndani ya hilo eneo.

Swali hapa ni, kwanini 6,000 kwa sqmt1 eneo kama lile bei ambayo ni kama ya kukomoa tena haraka haraka ndani ya miezi 6 tu?

Ni kwanini mbali ya wananchi kukubali kulipia Ili kutii amri ya kibabe hiyo bado watishiwe kubomolewa?

Ni kwanini pamoja na kulipia bado hao wananchi wametengwa Ili wasipate huduma muhimu za kiraia kama raia wa nchi hii na hata umeme wanaambiwa wao hawastahili REA wakati maeneo jirani yao wanawekewa umeme wa REA?

Yako mengi lakini mamlaka tajwa hapo juu ndo wenye kuweza kusaidia wananchi hawa Ili wapatiwe na wao haki zap maana inaonekana kuna genge kubwa nyuma ya hili na wakubwa wengi wamo na wengine wananufaika nalo.
Mmevamia eneo la watu mlitaka muachwe tu? Lipa hiyo fidia au ondoka nenda kwingine kwani nchi hii ni kubwa.
 
Mzee kijana inaonesha hujaelewa kinachoongelewa na pengine umekurupuka huko ulikokuwa ukaitwa na jamaa zako mje kutetea uharamia wenu.

Hakuna pahala nimeandika wananchi wanapinga kuingia eneo la muwekezaji maana ukitaka mikoa Tanzania ambayo leo inaonekana ni mikoa iliyokuwa imezungukwa mashamba pori 90% na leo yamekuwa ni mitaa mipya ndani ya Kibaha mfano ni maeneo zaidi ya 20 na yote staili ni ile ile moja, wenye nayo waliyasusa yakageuka mapori na uhalifu ukatendeka huko ndani ndipo wananchi wanaona eneo linageuka kuwa hatari kwao na watoto na mifugo yao wanaamua kulichukua eneo. Na hii ndo ukweli kwa sehemu kubwa ya mkoa wa Pwani mitaa mingi leo imeundwa kwa mfumo huo ama la, leo usingekuwa una mitaa hata ya pale Picha ya ndege, kwa Mfipa, Boko mnemela Msangani n.k

Pili, hakuna mahala nimesema wananchi hawako tayari kulipia. Tatizo lililopo ni kiwango kinachotakiwa (2,400,000 kwa sq my 400) ndani ya miezi sita tena kwa vitisho ndo kinachohojiwa na wananchi.

Tatu, wananchi wanahoji kama wamekubali kulipia na maelezo yangu ya awali pia nilisema wananchi wamekubali kulipia, shida yao ni kwanini sasa hawaruhusiwi kupatiwa huduma za kibinadamu na muhimu kama maji, barabara, umeme n.k wakati wanastahili kama raia?


Na mwisho, ishu za kulipia kama zinavyofanyika maeneo mengine niliyokutajia hata hawa wanaelewa na wanalipia mfano mzuri ni eneo jirani pakiitwa KAPA wanalipia na ndo Kibaha inavyopata mitaa lakini si kwa vitisho, uzuiaji wa huduma muhimu na hata viwango vya pesa haviko fair. Wenzeo wa KAPA jirani kabisa na wa VIMISA wanalipia si zaidi ya 2500 kwa sq mt ila pembeni kidogo wenzao wanaambiwa walipie 6000 hivi ni kweli iko sawa?

Kama utakuwa ni wa kureason bila kuwa na chembe ama upande wako Mzee kijana utaona hoja lakini kama na wewe unakaza shingo uko upande wa hao matapeli basi pengine huenda na wewe ni mmoja wa wafaidika na hizi dhuruma.
 
Walipe tu.Ila watu wa Pwani ni hodari sana.Wanakuuzia eneo kisha ukiwa unajipanga wanadai hawana eneo la kulima wanalitaka kwa kuwa ni shamba pori.Sina hamu na watu wa Pwani.Wanapenda kukaza shingo kwa Maeneo ya wawekezaji.Ugonjwa huu mkubwa sana Bagamoyo,Chalinze,Mkuranga na Kibiti.
Kama mwekezaji ana nyaraka za kumilki eneo basi waondoke maana watakuwa wamevamia kwa staili ile ya kisingizio cha Shamba pori.Walkurupuka hivyo Kibiti hadi ikabidi kuwafurumusha kwenye kijiji 1 mbele ya Jaribu Mpakani.
 
Back
Top Bottom