Pwani kuna viwanda 371... How!??

Pwani kuna viwanda 371... How!??

Viwanda vya nini!??
Ifike mahala watu wansoma taarifa za maendeleo ya Mkoa wawe makini..
Hivi neno 'kiwanda' watu wanajua maana yake!??

Taarifa hii mimi siiamini kabisa. Labda kama wamewajumlisha na washona cherehani.
Tuwe wakweli.
View attachment 528783

===============================================

MUHTASARI WA ORODHA YA VIWANDA MKOA WA PWANI NI KAMA IFUATAVYO:-
(a) Jumla ya Viwanda Vikubwa, vya Kati na Vidogo 260 vimejengwa kama ifuatavyo (Mkuranga viwanda 54, Kibaha Vijijini viwanda 76, Kibaha Mji viwanda 71, Chalinze viwanda 32, Bagamoyo viwanda 18, Kisarawe viwanda 4 na Mafia viwanda 5. Viwanda vingi Chalinze ni vya kokoto (Quarry) na Kibaha ni vya Matofali. Angalia Kiambatisho A.

Vifuatavyo ni baadhi ya viwanda vikubwa vilivyopo Mkoa wa Pwani:-

(i) Kiwanda cha Vigae (Tiles) cha Goodwill (Tanzania) Ceramic Co., Ltd kilichopo Mkuranga. Kiwanda hiki kinamilikiwa na Mwekezaji kutoka nchini China, na kinatarajiwa kuanza uzalishaji wa Mapema 2017

(ii) Kiwanda cha Nondo cha Mohamed Kiluwa Group and Company Ltd cha Mlandizi ambacho kinatarajiwa kuanza uzalishaji mapema 2017.

(iii) Kiwanda cha Kusindika matunda, (Sayona Fruits) kilichopo Kijiji cha Mboga - Chalinze - Bagamoyo. Mwekezaji ni Makampuni ya MMI (Motisun Group) ambayo yatawekeza jumla ya Dola za Kimarekani milioni 55. Kiwanda kinaendelea kujengwa na kitakamilika Oktoba, 2017.

(iv) Kiwanda cha Saruji itakayojulikana kama “Mamba Cement” kilichopo Kijiji cha Talawanda na Magulumatali- Bagamoyo. Mwekezaji ni Makampuni ya MMI (Motisun Group). Nao pia kibali cha ujenzi kimepatikana na ujenzi uko mbioni kuanza.

(v)Kiwanda cha Nondo cha MMI Intergrated Steel Mill kilichopo eneo la Zegereni, Halmashauri ya Mji Kibaha. Mwekezaji amepewa kibali cha ujenzi na ujenzi utaanza wakati wowote.

(vi) Kiwanda cha Kuunganisha Magari ya Zimamoto na Matrekta cha ubia kati ya SUMA JKT na EQUATOR Automech Co. Ltd. na kuunda Kampuni iitwayo “EQUATOR SUMAJKT LIMITED”.

· Wataunganisha magari ya zimamoto kwa kushirikiana na Kampuni ya ST AUTO iliyopo nchini Russia.
· Magari yatatengenezwa kwa kutumia viwango vya Kimataifa.
· EQUATOR SUMAJKT LTD itakuwa ni kiwanda cha pili katika Bara la Afrika, cha kwanza kipo Afrika ya Kusini.

· Ajira zitakazotengenezwa ni 200
· Eneo la kiwanda ni Ekari 63, zipo Ruvu JKJ
· Kiwanda kimekamilika, kitaanza ‘Operation” Januari, 2017.

(vii) Kiwanda cha Elven Agria Company Ltd. kinajengwa Mapinga Bagamoyo kwa ajili ya ukaushaji wa matunda ya aina mbalimbali. Kiwanda kitafunguliwa Januari, 2017.

(viii) Kiwanda cha Kusindika Matunda cha Kampuni ya Bakhresa Food Products Ltd. kimezinduliwa Septemba, 2016.

(ix) Kiwanda cha Vigae (Tiles) cha Kampuni ya TWYFORD (Tanzania Ceramic Tiles Factory) kutoka China kinachojengwa eneo la Pingo katika Halmashauri ya Chalinze, Bagamoyo. Kitatengeneza ajira za moja kwa moja (direct) 2,000 na ajira nyingine 4,000 ambazo siyo za moja kwa moja (indirect). Ujenzi wa Kiwanda unaendelea na kinatarajia kuanza uzalishaji tarehe 1 Julai, 2017 .

(x) Kiwanda cha Sabuni ya Unga cha Kampuni ya KEDS (T) CO LTD kutoka China kinachojengwa eneo la Viwanda la Mkoani katika Halmashauri ya Mji Kibaha. Ujenzi wa Kiwanda unaendelea na kinatarajia kuanza uzalishaji Mwezi Juni, 2019

(xi) Kiwanda cha kuunganisha matrekta TAMCO katika Halmashauri ya Mji Kibaha. Kimeanza ujenzi Mwaka 2017 Kinatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2017.mradi huu utagharimu kiasi za dola za kimarekeni milioni 55 pindi utakapokamilika,ukijumuisha ujenzi wa kiwanda cha matrekta na mitambo yake, vituo nane kwaajili ya huduma kwa wateja( service centers) mafunzo kwa wafanyakazi na manunuzi kwa vifaa vya kuunganishia matrkta jumla ya 2,400

(xii) GLOBAL PACKAGING (T) LTD: Kiwanda hiki kilianza kujengwa mwaka 2015 na kuanza uzalishaji mwaka 2016. Kiasi cha Billion 7.6 zimewekezwa, Kiwanda kipo Halmashauri ya Mji Kibaha. Mmiliki wa kiwanda hiki ni Wande Printing and Packaging Co. LTD na NDC.

(xiii) Kiwanda cha kuunganisha Bodi za Magari cha BENBROS kipo katika hatua ya kutwaa ardhi katika Halmshauri ya Wilaya ya Kibaha.



Chanzo; pwani.go.tz/project-details/viwanda
Na wewe unapopinga hoja uwe mkweli. Fanya utafiti japo kidogo kwanza kabla ya kupinga hoja. Wacha kuishi kwa mazoea
 
SASA HUELWEKI UNAPINGA NINI, Idadi ya viwanda au faida ya viwanda.
siku wakizungumzia economic impact ya viwanda kwa wananchi utapinga nini. jifunze kufocus kwenye kile ulichoanza kuzungumzia
Jifunze ku broaden unachoelezea sio kuwa single minded.
 
Jifunze ku broaden unachoelezea sio kuwa single minded.
I will be single minded on single minded things. nimejifunza kumaintain scope ya kinachojadiliwa.
thread ingezungumzia economic value ya hivyo viwanda pia tungeomba kujua hayo au tungejadili pia hayo kwa kina.
 
Mafia viwanda 5. Viwanda vingi Chalinze ni vya kokoto (Quarry) na Kibaha ni vya Matofali. Angalia Kiambatisho A.
Mtu anidanganye mengine lakini sio Mafia... ngoja nipige simu sasa hivi!!!
 
I will be single minded on single minded things. nimejifunza kumaintain scope ya kinachojadiliwa.
thread ingezungumzia economic value ya hivyo viwanda pia tungeomba kujua hayo au tungejadili pia hayo kwa kina.
Kwahiyo ukishatuambia idadi ya viwanda then what next au topic ifungwe.
 
Rufiji na kibiti vp ??? Huu kweli ubaguzi ndiomaana vijana wanaingia mstuni
 
Kumbe hata machimbo ya kokoto ni kiwanda!, mi nilikuwa sijui
 
Mmmmh ila vinafika hiyo namba mkuu?? Au vikubwa ni kma mia tu afu hivyo vingine vinakuwa vya kawaida ila exaggerated??? Nakubali viwanda vipo vingi ila sio heavy/medium kma unavyoongelea wwe!!! Unless mpaka vya wakata mbao vinahesabika
Sasa mnatakaje wabongo,mi siwaelew,..ni kweli idada sio kubwa sana,lakin ndo mwanzo,..halaf cha ajab wabongo hivyo viwanda vichache vilivyopo hawavitumii,mchina analalamika hapat material ya kutosha had machine zinakula tuu umeme,wabongo tunabak kubeza tuu
 
Sasa mnatakaje wabongo,mi siwaelew,..ni kweli idada sio kubwa sana,lakin ndo mwanzo,..halaf cha ajab wabongo hivyo viwanda vichache vilivyopo hawavitumii,mchina analalamika hapat material ya kutosha had machine zinakula tuu umeme,wabongo tunabak kubeza tuu
Embu acha upotoshaji wwe hivyo 371 vyote vilikuwepo toka enzi za awamu ya mr dhaifu ssa kivp credit kwa magufuli kuwa ni ''mwanzo tu''????

Wabongo sio tunalalamika tulichotaka ni serikali kujenga mazingira ya watu kujenga viwanda ssa kwa mwaka huu bajeti ni bilion 10 pekee, hya umeme magumashi, maji magumashi, kilimo kimekufa sasa hivo viwanda vya aina gani tutajenga wakati 70% ya viwanda duniani ni vya mazao ya kilimo???

Hakuna anayelalamika ssa kwa mfumo huo kweli viwanda vitamaliza tatizo la ajira laki 6 kila mwaka kma walivyoahidi kwenye kampeni??? Acheni upotoshaji mkuu hausaidii lolote hivyo viwanda 300 vimetoa ajira sio zaidi ya elfu 2 ssa si its better than nothing but far from objectives????

Mkuu huu ni mwaka 2017 mind you
 
Embu acha upotoshaji wwe hivyo 371 vyote vilikuwepo toka enzi za awamu ya mr dhaifu ssa kivp credit kwa magufuli kuwa ni ''mwanzo tu''????

Wabongo sio tunalalamika tulichotaka ni serikali kujenga mazingira ya watu kujenga viwanda ssa kwa mwaka huu bajeti ni bilion 10 pekee, hya umeme magumashi, maji magumashi, kilimo kimekufa sasa hivo viwanda vya aina gani tutajenga wakati 70% ya viwanda duniani ni vya mazao ya kilimo???

Hakuna anayelalamika ssa kwa mfumo huo kweli viwanda vitamaliza tatizo la ajira laki 6 kila mwaka kma walivyoahidi kwenye kampeni??? Acheni upotoshaji mkuu hausaidii lolote hivyo viwanda 300 vimetoa ajira sio zaidi ya elfu 2 ssa si its better than nothing but far from objectives????

Mkuu huu ni mwaka 2017 mind you
Unaweza ukawa sahih,ila faham kuiweka sawa nchi hii iliyo corrupt si rahis,halaf pia viwanda ving navyovisemea mim vimeanza kaz recently,kipind cha jk vilikua kwenye matengenezo,anyways,..kuendesha nchi si lelemama,na sjui wa tz hua wanataka nin mpka leo.kwakwel,manake hvyo viwanda vilivyopo ni wa tz wachache sana wanao supply raw materials,ni maneno maneno tuu,misiwaamin tena wa tz hua wanataka nin
 
Unaweza ukawa sahih,ila faham kuiweka sawa nchi hii iliyo corrupt si rahis,halaf pia viwanda ving navyovisemea mim vimeanza kaz recently,kipind cha jk vilikua kwenye matengenezo,anyways,..kuendesha nchi si lelemama,na sjui wa tz hua wanataka nin mpka leo.kwakwel,manake hvyo viwanda vilivyopo ni wa tz wachache sana wanao supply raw materials,ni maneno maneno tuu,misiwaamin tena wa tz hua wanataka nin
Tunataka viwanda ila viwanda haviji bila kukuza sekta ya nishati,maji,kilimo n.k sasa bioa hivo huoni ni changa la macho

Viwanda tunataka ila haviji hivi hivi kizembe tu lazma efforts ziwekwe
 
Tunataka viwanda ila viwanda haviji bila kukuza sekta ya nishati,maji,kilimo n.k sasa bioa hivo huoni ni changa la macho

Viwanda tunataka ila haviji hivi hivi kizembe tu lazma efforts ziwekwe
Sasa mzee si ndo effort znafanywa nw,kodi inakusanywa nying,matumiz yasio lazma hamna,miundombinu ya maji inawekwa,kama uzinduz wa jana alikotumbuliwa mtu huko,..haya umeme wa gas ndo huo,plants znafunguliwa,..one thing at a time,ila hawawez kaa kimya yaan kutosisitiza sera ya viwanda.lazma sera iongelew,iwe familiar kwenye maskio ya watu na mazingira ya uwekezaj yawekwe,.sasa tutakaa had lin bila kujarib,..au labda we unataka iwe vip,.kila kitu kiwezekane in one night?
 
Sasa mzee si ndo effort znafanywa nw,kodi inakusanywa nying,matumiz yasio lazma hamna,miundombinu ya maji inawekwa,kama uzinduz wa jana alikotumbuliwa mtu huko,..haya umeme wa gas ndo huo,plants znafunguliwa,..one thing at a time,ila hawawez kaa kimya yaan kutosisitiza sera ya viwanda.lazma sera iongelew,iwe familiar kwenye maskio ya watu na mazingira ya uwekezaj yawekwe,.sasa tutakaa had lin bila kujarib,..au labda we unataka iwe vip,.kila kitu kiwezekane in one night?
Sasa mkuu kipi kigumu si unaacha kununua bombardier afu unatoa material za kukuza kilimo!!!!

Unaacha kujenga airport chato mnaongeza capacity ya uzalishaji umeme

Unaacha uhakiki wa vyeti unafanya uhakiki wa fursa za kilimo

Unaacha flyovers unaongeza bajeti ya wizara ya maji

Kipi kigumu mkuu??? Bajeti ya kukuza viwanda ni billion 10 tu ssa hapo ndio MAANDALIZI??

shida ni vipaumbele mkuu lasihivyo sahivi tungeona viwanda vizito vya kuajiri vijana 5000 per kiwanda

Viongozi waache siasa
 
Sasa mkuu kipi kigumu si unaacha kununua bombardier afu unatoa material za kukuza kilimo!!!!

Unaacha kujenga airport chato mnaongeza capacity ya uzalishaji umeme

Unaacha uhakiki wa vyeti unafanya uhakiki wa fursa za kilimo

Unaacha flyovers unaongeza bajeti ya wizara ya maji

Kipi kigumu mkuu??? Bajeti ya kukuza viwanda ni billion 10 tu ssa hapo ndio MAANDALIZI??

shida ni vipaumbele mkuu lasihivyo sahivi tungeona viwanda vizito vya kuajiri vijana 5000 per kiwanda

Viongozi waache siasa
Thats true..kilichomshinda huyu jamaa ni hiko tuu ila mengine yuko vizur na anadhamira ya dhati..ishu ni vipaumbele tuu ndo tatzo lake,aanze na kipi aache kipi..akishaurika hapa kwenye vipaumbele,atatufikisha mbali sana
 
Back
Top Bottom