Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,634
- 697,845
Kuna ajali mbaya imetokea muda huu kati ya bus la Sai baba na tipper (mende) inasemekana majeruhi ni wengi na vifo pia.. Barabara ya morogoro eneo hilo imefungwa kwa muda... Kwa ambao wanatumia njia hiyo tafadhali tumieni mchepuko wa old Morogoro road
Sai baba ilikuwa linatoka Sumbawanga kama una ndugu ama jamaa jaribu kufuatilia
Jr
=====
Basi ya kampuni ya Saibaba yapata ajali asubuhi hii. Basi hiyo ilikuwa safarini kutokea jijini Dar Es Salaam kuelekea mjini Sumbawanga. Chanzo chake bado hakijafahamika mara moja
Ajali hiyo imetokea maeneo ya Kongowe, basi la kampuni ya Sai baba Express baada ya kugongana uso kwa uso na lori.
PWANI: Basi la abiria Saibaba lapata ajali kwa kugongana uso kwa uso na lori na kujeruhi abiria 18, Kamanda athibitisha
PWANI: Basi la abiria Saibaba lapata ajali kwa kugongana uso kwa uso na lori na kujeruhi abiria 18, Kamanda athibitisha
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani ACP Wankyo Nyigesa, amesema kuwa jumla ya watu 18 wamejeruhiwa katika ajali ya Basi la Saibaba lililogongana uso kwa uso na Lori asubuhi ya leo ya Februari 12, 2020.
Kamanda wa Polisi Pwani, ACP Wankyo Nyigesa
Kamanda Nyigesa amesema kuwa ajali hiyo imetokea katika eneo la kongowe na kusema kuwa majeruhi watano wamekimbizwa katika Hospitali ya Mloganzila kwa ajili ya matibabu na wengine wapo katika Hospitali ya Tumbi.
“Chanzo ni mwendokasi wa Lori uliopelekea kuligonga Basi la Abiria, Basi la Saibaba lilikuwa linatoka Sumbawanga kuelekea Dar es Salaam, hakuna vifo, majeruhi ni 18 na majina yao hayajafahamika kwasababu hawakuweza kuongea” amesema ACP Nyigesa.
Kwa mujibu wa Kamanda Nyigesa amesema kuwa Jeshi la Polisi, linajitahidi kufanya mawasiliano na kampuni ya mabasi hayo ili lilelete gari nyingine kwa ajili ya kuwachukua abiria walionusurika na kuwapeleka Dar es Salaam.
Chanzo EATV
Sai baba ilikuwa linatoka Sumbawanga kama una ndugu ama jamaa jaribu kufuatilia
Jr
=====
Basi ya kampuni ya Saibaba yapata ajali asubuhi hii. Basi hiyo ilikuwa safarini kutokea jijini Dar Es Salaam kuelekea mjini Sumbawanga. Chanzo chake bado hakijafahamika mara moja
Ajali hiyo imetokea maeneo ya Kongowe, basi la kampuni ya Sai baba Express baada ya kugongana uso kwa uso na lori.
PWANI: Basi la abiria Saibaba lapata ajali kwa kugongana uso kwa uso na lori na kujeruhi abiria 18, Kamanda athibitisha
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani ACP Wankyo Nyigesa, amesema kuwa jumla ya watu 18 wamejeruhiwa katika ajali ya Basi la Saibaba lililogongana uso kwa uso na Lori asubuhi ya leo ya Februari 12, 2020.
Kamanda wa Polisi Pwani, ACP Wankyo Nyigesa
Kamanda Nyigesa amesema kuwa ajali hiyo imetokea katika eneo la kongowe na kusema kuwa majeruhi watano wamekimbizwa katika Hospitali ya Mloganzila kwa ajili ya matibabu na wengine wapo katika Hospitali ya Tumbi.
“Chanzo ni mwendokasi wa Lori uliopelekea kuligonga Basi la Abiria, Basi la Saibaba lilikuwa linatoka Sumbawanga kuelekea Dar es Salaam, hakuna vifo, majeruhi ni 18 na majina yao hayajafahamika kwasababu hawakuweza kuongea” amesema ACP Nyigesa.
Kwa mujibu wa Kamanda Nyigesa amesema kuwa Jeshi la Polisi, linajitahidi kufanya mawasiliano na kampuni ya mabasi hayo ili lilelete gari nyingine kwa ajili ya kuwachukua abiria walionusurika na kuwapeleka Dar es Salaam.
Chanzo EATV