Pwagu na Pwaguzi, Ben Kiko

Pwagu na Pwaguzi, Ben Kiko

Highlander

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2012
Posts
3,093
Reaction score
1,077
Natamani kupata audio clips za Vipindi vya Radio Tanzania ya zamani vikiitwa Pwagu na Pwaguzi jamani. kama kuna mtu alirekodi mikanda ya vipindi vile, pamoja na taarifa za matukio kutoka Dodoma zilizotolewa na Ben Kiko. Tanzania ya zamani vipaji vilikuwa si haba kwa kweli. Tatizo tumeweka rekodi ya muziki na picha tu. Hivi kweli hakuna mahala naweza kupata hizi audio clips? Nitafurahi sana kupata msaada kupitia hapa.

Shida yangu ni mchezo wa Pwagu na Pwaguzi na matangazo ya Ben Kiko. Hivi Ben Kiko yupo wapi?
 
Mkuu naunga mkono hoja, watangazaji wa zamani walikuwa na vipaji na pia nadhani walipata mafunzo yaliyojitosheleza kufanya kazi hiyo. Ni nadra kupata watangazaji kama David Wakati, Jacob Tesha, Ben Kiko nk katika zama hizi.
 
Mkuu naunga mkono hoja, watangazaji wa zamani walikuwa na vipaji na pia nadhani walipata mafunzo yaliyojitosheleza kufanya kazi hiyo.

Jana nilikuwa mwananyamala; kuna mtu alisema ni kama Ben Kiko bado yupo hai. Kilichonishangaza ni kwanini kipaji kile kisitumike. Hivi ujuzi unazeeka jamani? Na ile michezo ya Pwagu na Pwaguzi kama kuna audio clips itakuwa mizuri hadi hii leo ujue,
 
Wakati wa sherehe za sabasaba hizo audio clips zilikuwa zinapatikana ktk banda la radio tanzania
 
Ben Kiko yuko Tabora, na kuna kipindi alikua Coordinator wa Redio Free Africa mkoani humo na akawa anarusha baadhi ya matukio lkn kwasasa naona kimya inawezekana na uzee nao umeisha mnyemelea.
 
Mkuu naunga mkono hoja, watangazaji wa zamani walikuwa na vipaji na pia nadhani walipata mafunzo yaliyojitosheleza kufanya kazi hiyo. Ni nadra kupata watangazaji kama David Wakati, Jacob Tesha, Ben Kiko nk katika zama hizi.
Na Ezekiel Malongo
 
Ben Kiko yuko Tabora, na kuna kipindi alikua Coordinator wa Redio Free Africa mkoani humo na akawa anarusha baadhi ya matukio lkn kwasasa naona kimya inawezekana na uzee nao umeisha mnyemelea.


Ohoo. Ok! Ila hilo la uzee nadhani basi tu Dyalo alikuwa hamlipi hela nzuri. Uzee kitu gani bwana kama unakula vizuri. Walter Cronkite ametangaza CBS news hadi sijui nukta gani za uzeeni. Ilikuwa kama walibidi tu kumnyang'anya Maiki. Na yule mtangazaji kibabu wa BBC jina linanitoka alikuwa anafanya Oponion za Letter from America unamkumbuka. Alitangaza hadi nukta za mwisho kabisa za uhai wake. Ben Kiko akipata chakula kizuri na mahali pazuri pa kuishi atafanya vizuri tu. Kumwacha tu ni kutupa kipaji kwa kweli....
 
Highlander: unachosema huko sawa kabisa, mfanyakazi wa kitanzania asipokua na kipato kizuri kulingana na kazi anayofanya lazima atakongoroka tu....na ndo uzee sasa usiokua na sababu.
 
Fika ofisi tbc na radio zao, utapata.

Wow...this is very good news indeed. Wataniona. Nakumbuka zaidi vipindi viwili: siku pwagu na pwaguzi walipokwenda kuwinda porini kutafuta kitoweo na siku walipofungua ofisi ya ufundi kutengeneza redio mbovu. Kila nikikumbuka nacheka utafikri ni leo kumbe 79. Wale watu walikuwa na vipaji sana jamani. nitazifuata!
 
Highlander: unachosema huko sawa kabisa, mfanyakazi wa kitanzania asipokua na kipato kizuri kulingana na kazi anayofanya lazima atakongoroka tu....na ndo uzee sasa usiokua na sababu.
 
Ben Kiko yuko Tabora, na kuna kipindi alikua Coordinator wa Redio Free Africa mkoani humo na akawa anarusha baadhi ya matukio lkn kwasasa naona kimya inawezekana na uzee nao umeisha mnyemelea.

Ni kweli mkuu hata mimi nilimsikia redioni kwa mara ya mwisho mwaka jana nilipokuwa safarini Tabora, yuko kwenye Radio ile ya Msomali (Maha-Rage siyo mboga) pale Tabora kama Mkurugenzi. Ila kwa sasa hivi sijui kama bado yupo.
 
Ni kweli mkuu hata mimi nilimsikia redioni kwa mara ya mwisho mwaka jana nilipokuwa safarini Tabora, yuko kwenye Radio ile ya Msomali (Maha-Rage siyo mboga) pale Tabora kama Mkurugenzi. Ila kwa sasa hivi sijui kama bado yupo.

Watu kama huyu Ben Kiko wangekuwa ndiyo asset za TBC kwa sasa kufundisha watoto. Elimu ya practical ni imara kuliko ya vitabuni ujue. Huko Tabora yupo under-employed kwakweli. Kuna stori moja kama naikumbuka vizuri aliisimulia kuhusu Fisi mmoja sijui alivamia nyumba moja pale Dodoma sijui ikawakawaje; alimgeuza yule fisi akawa kama mtu vile kuelezea alichohisi ndizo zilikuwa fikra za fisi. uuuuu it was very funy. Akawa unasimulia na wewe unakuwa kama unamuangalia kabisa yule fisi. Haya...TBC wamemtelekeza huyo Ben Kiko eti yupo Tabora! Rudisha Ben Kiko Dar es Salaam awe ana-mentor hutu tutoto twenu twa dot.com. Sijui Mirad Ayo sijui nani....
 
Nani anawakumbuka watangazaji hawa?: Chama Omari Matata, Godfrey Mngodo, Steven Mlatie , Job Isack Mwamto, Leonard Mambo Mbotela, ..........
 
Watu kama huyu Ben Kiko wangekuwa ndiyo asset za TBC kwa sasa kufundisha watoto. Elimu ya practical ni imara kuliko ya vitabuni ujue. Huko Tabora yupo under-employed kwakweli. Kuna stori moja kama naikumbuka vizuri aliisimulia kuhusu Fisi mmoja sijui alivamia nyumba moja pale Dodoma sijui ikawakawaje; alimgeuza yule fisi akawa kama mtu vile kuelezea alichohisi ndizo zilikuwa fikra za fisi. uuuuu it was very funy. Akawa unasimulia na wewe unakuwa kama unamuangalia kabisa yule fisi. Haya...TBC wamemtelekeza huyo Ben Kiko eti yupo Tabora! Rudisha Ben Kiko Dar es Salaam awe ana-mentor hutu tutoto twenu twa dot.com. Sijui Mirad Ayo sijui nani....

Huyu jamaa nasikia kuna kipindi wabunge walichemsha akiwa bado Dodoma, yeye akalipoti bila chenga ndo kisa cha kutelekezwa, Cheza na system wewe/.
 
Fika TBC NYERERE ROAD utapata hizo sauti
katika mfumo wa kanda wanauza hata
zilipendwa. Nchi hii full usanii
hao wstangazaji wametupwa km galasa


Ona Samadu Hassan(Mzee wa pangu Pakavu)
anapiga mzigo vizuri pale STAR TV
alipita RTD&DW UJERUMANI
 
Fika TBC NYERERE ROAD utapata hizo sauti
katika mfumo wa kanda wanauza hata
zilipendwa. Nchi hii full usanii
hao wstangazaji wametupwa km galasa


Ona Samadu Hassan(Mzee wa pangu Pakavu)
anapiga mzigo vizuri pale STAR TV
alipita RTD&DW UJERUMANI

Umeonaa eh?sio wale ma ripota fulani na lafudhi zao za kijinga "....miiiiimi mtangazaji wakooooooo! puuuuumbavuuu bin bwegeeeeee! wa aaaaaiiiiiiitiiiiiiii viiiiiiii! yaani huwa nachefukwa na roho na watu haokupita maelezo sijui lahaja au lafudhi ya wapi ile!
 
Umeonaa eh?sio wale ma ripota fulani na lafudhi zao za kijinga "....miiiiimi mtangazaji wakooooooo! puuuuumbavuuu bin bwegeeeeee! wa aaaaaiiiiiiitiiiiiiii viiiiiiii! yaani huwa nachefukwa na roho na watu haokupita maelezo sijui lahaja au lafudhi ya wapi ile!

Ni mimi ufooo saroo wa aitiviii(kwa sauti ya chadema)
 
Back
Top Bottom