Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,626
- 46,270
Nini kinaendelea Urusi?
Leo Msemaji wa Kremlin bwana Peskov amekiri mbele ya vyombo vya habari kwamba sasa Urusi iko vitani rasmi. Amesema kilichoanza kama oparesheni maalumu ya kijeshi( maarufu kama SMO kwa wafuasi wa Putin) sasa imehamia kuwa vita kamili baada ya West kujiingiza katika mgogoro huo.
Peskov amesema ni muhimu hilo likaeleweka wazi kwa ajili ya kukusanya wanajeshi(mobilization) ndani ya nchi!
Muda mchache baadaye baada ya taarifa hiyo kumetokea shambulio kubwa la kigaidi Moscow!
Pia inaarifiwa kwamba wiki mbili kabla ya tukio la kigaidi leo Moscow ubalozi wa Marekani huko Moscow ulitoa taarifa ya tahadhari kwa raia wake kwa uwezekano wa kutokea tukio kama hili la leo!
Ni wiki hii pia ambapo Putin ameshinda uchaguzi ambao huwa unafanyika tu kama sehemu ya mazoea kukamilisha ratiba na kuendelea kurasimisha utawala.
Wapo watakaosema ni ugaidi wa ukweli, wapo watakaosema ni Ukraine na wapo watakaosema ni false flag operation. Yote kwa yote ni mkanganyiko mkubwa sana unaoendelea huko Moscow.
Leo Msemaji wa Kremlin bwana Peskov amekiri mbele ya vyombo vya habari kwamba sasa Urusi iko vitani rasmi. Amesema kilichoanza kama oparesheni maalumu ya kijeshi( maarufu kama SMO kwa wafuasi wa Putin) sasa imehamia kuwa vita kamili baada ya West kujiingiza katika mgogoro huo.
Peskov amesema ni muhimu hilo likaeleweka wazi kwa ajili ya kukusanya wanajeshi(mobilization) ndani ya nchi!
Muda mchache baadaye baada ya taarifa hiyo kumetokea shambulio kubwa la kigaidi Moscow!
Pia inaarifiwa kwamba wiki mbili kabla ya tukio la kigaidi leo Moscow ubalozi wa Marekani huko Moscow ulitoa taarifa ya tahadhari kwa raia wake kwa uwezekano wa kutokea tukio kama hili la leo!
Ni wiki hii pia ambapo Putin ameshinda uchaguzi ambao huwa unafanyika tu kama sehemu ya mazoea kukamilisha ratiba na kuendelea kurasimisha utawala.
Wapo watakaosema ni ugaidi wa ukweli, wapo watakaosema ni Ukraine na wapo watakaosema ni false flag operation. Yote kwa yote ni mkanganyiko mkubwa sana unaoendelea huko Moscow.