machomanne
JF-Expert Member
- Feb 22, 2017
- 822
- 926
Masturbation ni dhambi, mbele za Mungu.(ni machukizo). Mungu amezuia mwanaume kumwaga mbegu chini. Anayemwaga mbegu chini anaenda kinyume na mlango wa Mungu wa kuzaliana. Kwa mwanamke pia, masturbation ni dhambi. Hebu fikiria, unawezaje kupandisha hamu bila kuweka matamanio kwa mwanaume?. Fahamu kuwa unapojichua lazima kutakuwa na mtu ambaye umemweka mawazoni mwako wakati unapojichua.. Kwa kumweka MTU mawazoni mwako wakati ukijichua, fahamu kuwa unafanya dhambi ya uzinzi au uasherati na huyo mtu rohoni. Hivyo, hata usipofanya naye kimwili, tayari umefanya naye kiroho. Kila anayejichua anafanya ngono na huyo aliyemweka mawazoni unapojichua, awe mwanamke, au mwanaume.. Kuangalia picha za pornogrph, ni vibaya sana, kwa sababu Uume unasimama kwa muda mrefu bila kutimiziwa hamu. Madhara yake ni kuishiwa na nguvu za kiume(impotent). Kwa mwanamke vile vile, kisimi (clitoris)husimama kwa muda mrefu Vila kutimiziwa hamu, matokeo yake ni kupungua kwa tension katika kisimi, na kufanya mwanamke kuwa frigid.