Papaa Mobimba
JF-Expert Member
- Jan 27, 2018
- 754
- 3,097
Mwili wa aliyekuwa Afisa wa Wizara ya Nishati Mery Mkwaya Maramo aliyefariki mwanzoni mwa wiki hii na kuzikwa jana katika Makaburi ya Pugu Mwakanga jijini Dar es Salaam, Usiku wa kuamkia leo watu wasiojulikana wameufukua na kuutoa nje ya jeneza kisha kuuvua nguo .
Kaka wa Marehemu Mary, Deogratius Maramo amesema inasemekana mwili wa marehemu uliingiliwa kimwili lakini bado wanasubiri ripoti ya Polisi ili wajue kilichomtokea ndugu yao.
Kaka huyo wa marehemu amesema kuwa hakuna kitu chochote kilichoibiwa kaburini humo.
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na mtaalam wa Afya wameufanyia Uchaguzi mwili wa Mary Maramo ambaye ni mtumishi wa Wizara ya Nishati na kukubaliana na ndugu wa marehemu kuwa mwili huo uhifadhiwe Tena.
Mwili wa Mary umevalishwa Nguo upya ukiwa ndani ya kaburi na kurudishwa kwenye jeneza na shughuli inayoendelea kwa sasa ni kulijenga kaburi mahala lilipobomolewa.
Kaka wa Marehemu Mary, Deogratius Maramo amesema inasemekana mwili wa marehemu uliingiliwa kimwili lakini bado wanasubiri ripoti ya Polisi ili wajue kilichomtokea ndugu yao.
Kaka huyo wa marehemu amesema kuwa hakuna kitu chochote kilichoibiwa kaburini humo.
Mwili wa Mary umevalishwa Nguo upya ukiwa ndani ya kaburi na kurudishwa kwenye jeneza na shughuli inayoendelea kwa sasa ni kulijenga kaburi mahala lilipobomolewa.