PSSSF kuanza rasmi Agosti mosi 2018

PSSSF kuanza rasmi Agosti mosi 2018

vitu kama hivi vinahitaji maelezo ya kutosha kwa wahusika pasipo kuacha chembe ya shaka, kifupi Mh Waziri anapaswa kutoa tamko au maelezo ya kutosha kwenye mfumo wa kijarida unaoeleza kila kitu kinaga ubaga ili kila mwajiri agawe kwa watu wake na kila mtu asome aelewe "abcd" zote. Kuwaambia watu vitu nusunusu huku mengine muhimu hayasemwi sio jambo jema hata kidogo.

Ushauri; Vijarida au vipeperushi vinavyoelezea mambo yoote muhimu kama faida kwa wadau ambao ni wafanyakazi vitolewe na kugaiwa kwa wafanyakazi na jamii kwa ujumla, bado mpaka sasa kuna mkanganyiko juu ya fao la kujitoa na hakuna anayetoa maelezo yanayojitosheleza zaidi ya blah blah za kisiasa, hakuna pia maelezo ya kutosha namna mchangiaji atakavyonufaika moja kwa moja na mafao yake wakati bado yuko kazini, hakuna maelezo ya kutosha yanayoonyesha hesabu za wazi juu ya pension kwa mstaafu pale atakapostaafu na atachotakiwa kulipwa, zaidi ya mafao kwa mstaafu hakuna faidi nyingine aipatayo kama shukrani kwa yeye kulitumikia taifa na kuchangia mfuko husika miaka yoote huku hela yake ikizungushiwa kwenye biashara, Mabadiriko muhimu kama haya yanapofanyika ni vyema wadau wakashirikishwa moja kwa moja kwa 100% na sio kuwahusisha wabunge ambao hili sio muhimu sana kwao..
 
Anayesupply bangi kwa viongozi wa Tz ajue Mungu anamuona
 
Kabla ya kuunganishwa shirika kama NSSF wanakuzungusha wee. Je wanachama wakiongezeka itakuaje?
 
Ndio hayo maelezo ya serekali yanavyo jieleza. Ila kwakua huku makazini kunawatu wanapenda sifa wanaweza wakahamisha watu kilazima.
Sheria inasema wafanyakazi wa serikali (kuu pamoja na za mitaa na agency zote) mfuko wao utakuwa ni PSSSF na wafanyakazi wa sekta binafsi mfuko wao utakuwa ni NSSF, sheria imeelekeza kuwa wafanyakazi wa serikali waliokuwa mifuko ya LAPF, GEPF, PSPF, NSSF taafifa zao zitahamishwa kwenda PSSSF na watumishi wa sekta binafsi waliokuwa mifuko mingine (ukiutoa NSSF) basi taarif
a zao zinahamishiwa NSSF...kwa hiyo hapa cha kuzingatia ni upandw qa ajira mtumiahi alipo, serikalini mfuko wao ni PSSSF na sekta binafsi ni NSSF
 
Nadhani kuna haja ya kumwita Jenista hapa, mambo hayaeleweki, maskini hela zetu eti fao la kukosa ajira
Siku hizi kama una loan board ukichukua FAO lako mkopo wako unakatwa kwanza
 
Mkuu nadhani hujaelewa. Mimi ni mtumisho wa mfuko mmojawapo wa iliyomerge.
Kwanza tutambue kuwa mifuko yote inapokea 20% ya mshahara kama makato [10%kwa 10% kwa private sector na [5% kwa 10 kwa watumishi wa serikali]
Pia waajiriwa wote wa kabla ya tarehe 1 August 2018 wataendelea kubaki kwenye mifuko yao ya awali. Watumishi wapya tu ndio watalazimika
Nadhani lengo mojawapo ya kuunganisha hii mifuko ilikuwa kuondoa hiyo ishu ya tofauti ya makato. Hivyo makato kwa wote yatakuwa sawa, ndio bado haijulikani itakuwa 10% au 5%. Tusubiri
 
Mkuu nadhani hujaelewa. Mimi ni mtumisho wa mfuko mmojawapo wa iliyomerge.
Kwanza tutambue kuwa mifuko yote inapokea 20% ya mshahara kama makato [10%kwa 10% kwa private sector na [5% kwa 10 kwa watumishi wa serikali]
Pia waajiriwa wote wa kabla ya tarehe 1 August 2018 wataendelea kubaki kwenye mifuko yao ya awali. Watumishi wapya tu ndio watalazimika
Nadhani lengo mojawapo ya kuunganisha hii mifuko ilikuwa kuondoa hiyo ishu ya tofauti ya makato. Hivyo makato kwa wote yatakuwa sawa, ndio bado haijulikani itakuwa 10% au 5%. Tusubiri
 
Hivi hao wafanyakazi wa hiyo mifuko nini hatima zao! Sidhan kama wote wataweza kutawanywa! Vipi kuhusu wale supporting staff... Maisha yanazidi kuwa na changamoto
 
Jambo kubwa hapa siyo issue ya kuanza kutumika kwa Sheria ya PSSSF! Issue ya muhimu kwa Wafanyakazi na jamii nzima ya Watanzania ni "KANUNI YA VIKOKOTOO VYA MAFAO". Iwapo ni kweli kuwa waliokuwa PSPF na LAPF wamepunguziwa mafao yao (Malipo ya Mkupuo) kwa 62.5%, basi wengi watakufa kwa Pressure kutokana na ndoto zao kuota mbawa hasa wale wanaokaribia kustaafu kuanzia Agosti mosi 2018!

Tusubiri yajayo ...!
 
na kama itakuwa 10% ya PSSSF kuongeza 15% ya helsb tutapata tabu sana awamu hii
Rate ya kuchangia haitaathiriwa na uwepo wa huu mfuko mpya, utaendelea nayo ile ile uliyonayo kwa sasa..
 
Hivi hao wafanyakazi wa hiyo mifuko nini hatima zao! Sidhan kama wote wataweza kutawanywa! Vipi kuhusu wale supporting staff... Maisha yanazidi kuwa na changamoto
Isome sheria ipo wazi kabisa hakuna mfanyakazi anayeachishwa kazi, wafanyakazi wote wanarithiwa na mfuko mpya..!!
 
Nna swali Chief,kwa sasa Mimi nakatwa asilimia 10(10%) ya mshahara wangu wakati watumish wenzangu walioko mifuko mingne nadhani ni around 5%...sa tunapoenda kua kwenye mfuko mmoja makato yataendelea kua yaleyale au yatabadlka?
Waachie Serikali wao watajua namna ya kuyaseti mambo.
 
Mfuko huu utoe mikopo ya fedha kwa wanachama wake ili kuwakwamua kiuchumi
 
Back
Top Bottom