PSSSF kuanza rasmi Agosti mosi 2018

PSSSF kuanza rasmi Agosti mosi 2018

Hakuna kitu kama hicho muongozo ni kwamba kuanzia tarehe 1/8 watakao ajiriwa kwa taasisi za serekali ndo watakua lazima waende kwenye huo mfuko wa PSSSF na wafanyakazi binafsi watatakiwa kwenda NSSF.
Kwa hiyo muongozo ukoje kwa mtu aliye LAPF kwa sasa na huyo mtumishi wa umma aliye NSSF??
 
Ndio hayo maelezo ya serekali yanavyo jieleza. Ila kwakua huku makazini kunawatu wanapenda sifa wanaweza wakahamisha watu kilazima.


Sijapitia maelezo yoyote au kuusoma hiyo sheria mpya, lakini sifikirii mambo yatakua kama unavyoeleza hapa.

Itapunguza mojawapo ya malengo ya kuunganisha hii mifuko na kuondoa maana ya haya mabadiliko.
 
Kama uko private company na mfuko wako hapo awali ulikuwa ni LPF unahamishiwa NSSF??
 
Kuna wale waliokuwa wameshajaza na kupeleka form kabla ya hiyo sheria kuanza kazi hiyo tarehe 1/8/2018 na wakawa wanasubiri tu kupata withdrawal benefits zao, je hao hawataathirika kwa kuzingatia kuwa walishajaza form kabla ya kuanza sheria hiyo mpya?
 
Daaah kuna watu watata kuelewa,Mifuko yote unaijua imefutwa(kuunganishwa na kua kitu kimoja) na kuanza kwa Mfumo wa Hifadhi wa Watumishi wa umma,NSSF kwa sasa itahudumia wafanyakazi sekta binafsi tu.

Watumishi wote,wafaidika/warithi wa mafao wa mifuko iliyoundiwa PSSSF,wataendelea kufanya kazi PSSSF na kupokea stahiki zao kama kawaida kupitia huo mfuko mpya.

Madeni,mali,mikataba iliyokua chini ya iliyofutwa itahamia PSSSF. Hii ni kuanzia kesho 1 mwezi wa 8 2018.Ni NSSF tu imebakia ila sasa ni strictly sekta binafsi.
 
Wanaojitayarisha kustaafu anzeni kujitayarisha kisaikologia, kwani sasa serikali inayohaki kutumia hela zenu za makato, kutoka kwenye mashirika ya jamii kama PSSSF na NSSF kwa sababu zote zimehamishiwa ofisi ya waziri mkuu na haiko SSRA TENA, na wala haihitaji kulipa baada ya kutumia, na wala haikopi, ushauri wangu ni kujiwekea akiba ya kudumu kwenye makampuni ya bima, unaweza kufa bila kupata haki yako.
 
Itatawala milele
Kazi za bongo kama ndoa mpaka kifo kiwatenge
 
20180731_212006.png

PSSSF act 2018, unaweza download sheria website ya utumishi.
sijui kuhusu NSSF kama sheria itabadirika , lakini kwenye PSSSF nimeona mambo mengi mazuri sana kama sheria itafuatwa
 
Last edited:
Mleta mada unachofanya hapa ni upotoshaji na sijui kwanini hadi sasa Mods wamekuacha tu.
 
View attachment 823779
PSSSF act 2018, unaweza download sheria website ya utumishi.
sijui kuhusu NSSF kama sheria itabadirika lakini kwenye PSSSF nimeona mambo mengi mazuri sana kama sheria itafuatwa maana serikali ameanza kuwa na katabia kabaya ka kutofuata sheria siku za hivi karibuni
Sheria vs uhalisia=??
 
Back
Top Bottom