PSPF yashindwa kuwalipa wastaafu

PSPF yashindwa kuwalipa wastaafu

Umenena Mkuu, Mzee wangu kastaafu mwezi wa nne tar 18 mwaka huu, hadi leo hajapata pensioni yake PSPF, mimi mwenyewe niliacha kazi tangia januari nimefuatilia michango yangu nssf, hadi sasa sijapata! Yani haya mashirika ni hopeless kabisa!

Toa kitu kidogo uone utakavyohudumiwa fasta.
 
Ndugu yangu alikuwa anashughulikia mafao yake wiki ya juzi wamemwambia hundi ipo tayari ila pesa hakuna, bi mkubwa wangu kastaafu toka mwaka jana mwanzoni hadi leo hajapata mafao yake mbaya zaidi hata mwajiri wake ambaye ni manispaa anapaswa amlipe nauli hadi leo wanasema hawana pesa na hawajali kabisa hizi halmashauri hizi watendaji wake wanatia hasira
 
Ni kweli kabisa mfuko wa PSPF una hali mbaya kifedha. Nimethibitisha hili hivi karibuni, baada ya kuwasiliana nao ili nijue kwanini wamekua wakimzungusha mzee wangu katika kupata mafao yake, baada ya kuwa amestaafu kwa muda mrefu sasa!

Bila kutafuna maneno, nilijibiwa kwamba fedha hakuna, wanasubiri hazina itakapopeleka makato ndipo waweze kulipa. Na kwamba haijulikani ni lini, ila niendelee tu kuwasiliana nao kila nitakapopata nafasi.

My take: Kwa kweli hali ni mbaya, Serikali inabidi ichukue hatua haraka iwezekanavyo, ili kunusuru wazee wetu hawa!

Labda niongezee au nifafanue pale ulipoishia. Kwa PSPF Kuna Matatizo mawili, ambayo yote chanzo ni Serikali yetu iliyoko madarakani, na nitaelezea kama ifuatavyo;-

1) Pre-'99
Mwaka 1999 serikali iliuomba huu mfuko kuwachukua staff wake wengi tu na kuwasajili kwenye mfuko kana kwamba walikuwepo toka zamani (kabla ya (1999). Hivyo basi mfuko huu uliamua kuwaingiza kwenye database yake hata wale ambao hawakua wamechangia. Yaani mfano mtu kaanza kazi Serikalini tuseme mwaka 1985 na akachangia mafao yake hazina Mpaka mwaka 1998, mtu huyu alihamishiwa PSPF mwaka 1999 na labda kama atastaafu mwaka 2000, PSPF watamlipa mafao ya kuanzia mwaka 1985 ingawa kwao kachangia kuanzia 1999 tu.

Makubaliano haya yalikua kama ni Mkopo ambao hazina/serikali ingedaiwa na huu mfuko sababu mfuko unalipa mafao ambayo makato yake haukuyapokea, na toka ahadi au makubaliano hayo ya deni yafikiwe huo mwaka 1999, serikali haijawahi kuilipa huu mfuko ingawa mfuko umeendelea kuwalipa wastaafu mafao yao yote pamoja na pensheni Mpaka mwaka jana.

2) Monthly Salary Deductions
Hapa napo Kuna delays. Toka January mwaka huu, serikali imeshindwa kupeleka makato inayowakata wafanyakazi wake kwenye mishahara yao. Wewe ukipokea Pay slip yako inaonesha umekatwa PSPF ila in actual sense hiyo hela haijaenda bado kwa watu PSPF.

Deni la kwanza ambalo ni historical linatokana na fact kwamba ni kubwa mno, zaidi ya 1 trillion, hivyo serikali inayolia deficit kwenye bajeti yake kuondoa hela kama hii ni tatizo. Deni hili aliliacha mkapa, na dalili zote ni kua JK nae ataliacha, ingawa likiwa limeongezeka.

Na deni la pili nalo ni hiyohiyo deficit ya serikali, maana hata mishahara yenyewe ni kwa manati ingawa inalipwa.

Data hizi ni kutoka Hazina ambao ndio wadaiwa, hivyo hazina shaka kabisa
 
Labda niongezee au nifafanue pale ulipoishia. Kwa PSPF Kuna Matatizo mawili, ambayo yote chanzo ni Serikali yetu iliyoko madarakani, na nitaelezea kama ifuatavyo;-

1) Pre-'99
Mwaka 1999 serikali iliuomba huu mfuko kuwachukua staff wake wengi tu na kuwasajili kwenye mfuko kana kwamba walikuwepo toka zamani (kabla ya (1999). Hivyo basi mfuko huu uliamua kuwaingiza kwenye database yake hata wale ambao hawakua wamechangia. Yaani mfano mtu kaanza kazi Serikalini tuseme mwaka 1985 na akachangia mafao yake hazina Mpaka mwaka 1998, mtu huyu alihamishiwa PSPF mwaka 1999 na labda kama atastaafu mwaka 2000, PSPF watamlipa mafao ya kuanzia mwaka 1985 ingawa kwao kachangia kuanzia 1999 tu.

Makubaliano haya yalikua kama ni Mkopo ambao hazina/serikali ingedaiwa na huu mfuko sababu mfuko unalipa mafao ambayo makato yake haukuyapokea, na toka ahadi au makubaliano hayo ya deni yafikiwe huo mwaka 1999, serikali haijawahi kuilipa huu mfuko ingawa mfuko umeendelea kuwalipa wastaafu mafao yao yote pamoja na pensheni Mpaka mwaka jana.

2) Monthly Salary Deductions
Hapa napo Kuna delays. Toka January mwaka huu, serikali imeshindwa kupeleka makato inayowakata wafanyakazi wake kwenye mishahara yao. Wewe ukipokea Pay slip yako inaonesha umekatwa PSPF ila in actual sense hiyo hela haijaenda bado kwa watu PSPF.

Deni la kwanza ambalo ni historical linatokana na fact kwamba ni kubwa mno, zaidi ya 1 trillion, hivyo serikali inayolia deficit kwenye bajeti yake kuondoa hela kama hii ni tatizo. Deni hili aliliacha mkapa, na dalili zote ni kua JK nae ataliacha, ingawa likiwa limeongezeka.

Na deni la pili nalo ni hiyohiyo deficit ya serikali, maana hata mishahara yenyewe ni kwa manati ingawa inalipwa.

Data hizi ni kutoka Hazina ambao ndio wadaiwa, hivyo hazina shaka kabisa

Ahsante kwa ufafanuzi wa kina mkuu, kuna watu humu wamezoea kupotosha kila ukweli kwa maslahi yao binafsi na waliowatuma. Bila kupima kwanza hasira wanazoweza kuziibua kutoka kwa wengine, ambao kimsingi ndio wahanga wa haya mambo!

Nafikiri sote kwa pamoja tuendelee kuisihi Serikali yetu ifanye linalohitajika kwasasa, ili kuwaondolea adha hii wazee wetu. Kwa kweli inatia uchungu sana, mzee anapoishi kwa matumaini, asijue ni lini hasa atafanikiwa kupata haki yake. Bado tuna imani na Serikali yetu, na kwakua imekua ikijitambulisha kwamba ni SIKIVU, MAHILI NA MAKINI, huu ndio wakati sasa wakudhihirisha hayo kwa vitendo.
 
Labda niongezee au nifafanue pale ulipoishia. Kwa PSPF Kuna Matatizo mawili, ambayo yote chanzo ni Serikali yetu iliyoko madarakani, na nitaelezea kama ifuatavyo;-

1) Pre-'99
Mwaka 1999 serikali iliuomba huu mfuko kuwachukua staff wake wengi tu na kuwasajili kwenye mfuko kana kwamba walikuwepo toka zamani (kabla ya (1999). Hivyo basi mfuko huu uliamua kuwaingiza kwenye database yake hata wale ambao hawakua wamechangia. Yaani mfano mtu kaanza kazi Serikalini tuseme mwaka 1985 na akachangia mafao yake hazina Mpaka mwaka 1998, mtu huyu alihamishiwa PSPF mwaka 1999 na labda kama atastaafu mwaka 2000, PSPF watamlipa mafao ya kuanzia mwaka 1985 ingawa kwao kachangia kuanzia 1999 tu.

Makubaliano haya yalikua kama ni Mkopo ambao hazina/serikali ingedaiwa na huu mfuko sababu mfuko unalipa mafao ambayo makato yake haukuyapokea, na toka ahadi au makubaliano hayo ya deni yafikiwe huo mwaka 1999, serikali haijawahi kuilipa huu mfuko ingawa mfuko umeendelea kuwalipa wastaafu mafao yao yote pamoja na pensheni Mpaka mwaka jana.

2) Monthly Salary Deductions
Hapa napo Kuna delays. Toka January mwaka huu, serikali imeshindwa kupeleka makato inayowakata wafanyakazi wake kwenye mishahara yao. Wewe ukipokea Pay slip yako inaonesha umekatwa PSPF ila in actual sense hiyo hela haijaenda bado kwa watu PSPF.

Deni la kwanza ambalo ni historical linatokana na fact kwamba ni kubwa mno, zaidi ya 1 trillion, hivyo serikali inayolia deficit kwenye bajeti yake kuondoa hela kama hii ni tatizo. Deni hili aliliacha mkapa, na dalili zote ni kua JK nae ataliacha, ingawa likiwa limeongezeka.

Na deni la pili nalo ni hiyohiyo deficit ya serikali, maana hata mishahara yenyewe ni kwa manati ingawa inalipwa.

Data hizi ni kutoka Hazina ambao ndio wadaiwa, hivyo hazina shaka kabisa

Ndo mtulipe
 
Ndugu yangu alikuwa anashughulikia mafao yake wiki ya juzi wamemwambia hundi ipo tayari ila pesa hakuna, bi mkubwa wangu kastaafu toka mwaka jana mwanzoni hadi leo hajapata mafao yake mbaya zaidi hata mwajiri wake ambaye ni manispaa anapaswa amlipe nauli hadi leo wanasema hawana pesa na hawajali kabisa hizi halmashauri hizi watendaji wake wanatia hasira

Halafu anatokea mtu na kuanza kutetea madudu hapa! Tungejadiliana namna ambavyo wakubwa wa Serikalini wafanyaje ili stahili za hawa Wazee wetu zilipwe sasa. Inasikitisha na kuchekesha pia, mtu mzima kuambiwa "hundi yako ipo tayari, tunasubiri pesa", maneno hayo hayo kwa zaidi ya mwaka sasa!
 
Ahsante kwa ufafanuzi wa kina mkuu, kuna watu humu wamezoea kupotosha kila ukweli kwa maslahi yao binafsi na waliowatuma. Bila kupima kwanza hasira wanazoweza kuziibua kutoka kwa wengine, ambao kimsingi ndio wahanga wa haya mambo!

Nafikiri sote kwa pamoja tuendelee kuisihi Serikali yetu ifanye linalohitajika kwasasa, ili kuwaondolea adha hii wazee wetu. Kwa kweli inatia uchungu sana, mzee anapoishi kwa matumaini, asijue ni lini hasa atafanikiwa kupata haki yake. Bado tuna imani na Serikali yetu, na kwakua imekua ikijitambulisha kwamba ni SIKIVU, MAHILI NA MAKINI, huu ndio wakati sasa wakudhihirisha hayo kwa vitendo.
Mkuu,
Kua na matumaini si sawa sana, kama matumaini yenyewe ni ya mashaka mashaka. Sababu wadai wa hii serikali sio PSPF tu, hata NSSF nayo inaidai pia serikali. Kuna makubaliano ya kujenga daraja la kigamboni ambalo NSSF wangechangia 60% na Serikali 40% lakini inavyoonekana serikali itashindwa kutoa hii 40% yao sababu ya kilekile kinachotajwa deficit kwenye bajeti hivyo mzigo huu utaiangukia NSSF (pengine).

Wanaodai mafao yao wa NSSF nao pia wanataabika kama wa PSPF. Na wao wanapigwa kalendar kama wa PSPF, na ukikutana na staff mweli ndio anakuambia kua hela benki hakuna.

Pia ikumbukwe mashirika haya pamoja na mengine yalitoa fedha kiasi kadhaa kuikopesha serikali sababu ya kujenga chuo kikuu cha UDOM, deni ambalo nalo halijalipwa.

Ikifikia hapa sasa hata matumaini unayoyaweka uyaweke ukijua kua wadai wa haya mafao hawapo tu PSPF, hivyo mzigo ni mkubwa kwa hiyo unayoiiya serikali sikivu. Binafsi nadhani usiweke matumaini sana kwa siku za karibuni ila pia usikate tamaa pia maana deni liko na linajulikana kisheria.
 
Ha ha ha Mama samia si ana matrillioni ya kugawa vijijini mwambieni awakopeshe PSPF
Sasa hizi ahadi zamagufuli anategemea kuzitimiza na nini ilihali JK ashakopa mpk mifuko ya ndani imeisha

Tunawaambia ipigeni chini ccm tujipange upya hamtaki. Nchi tajiri lakini maskini. Tuwe na utaratibu wa kubadili chama tawala. Tuachane na chama kizoefu kizeefu.
 
We Ulidhani MK nini kwa mfano? Halafu tutafutane basi wewe aisee

Sema tukiwa tuko wenyewe tuonane.
Maana kila siku Twittet uko na mkeo na mimi niko na mme wangu

Kesho njoo bila mkeo nami nitamuaga mume wangu kuwa naenda kwa shangazi kule Mbezi mwisho, afu tukutane.

Au njoo Pm
 
Sema tukiwa tuko wenyewe tuonane.
Maana kila siku Twittet uko na mkeo na mimi niko na mme wangu

Kesho njoo bila mkeo nami nitamuaga mume wangu kuwa naenda kwa shangazi kule Mbezi mwisho, afu tukutane.

Au njoo Pm

Hahahaa! Ninyi mmeugeuza uzi wa watu kuwa wa kimahaba, eti?
 
Kwa ufupi maoni yangu ni haya:-
1. Kuna kasoro kubwa katika sheria za mifuko - PSPF,NSSF,PPF,(na LAPF?) hasa kuhusu kukopesha na kuwekeza.

2. Pata washauri wenye utaalamu mkubwa kama PwC,E&Y, KPMG, Mckinssey kuunganisha baadhi ya mifuko ili kupunguza gharama--maofisi makuu, bodi za mashirika, na katika uwekezaji kuimarisha mitaji.

3. Wanasiasa wasiingilie shughuli za mifuko.
 
Hapa mtoa mada wastaafu wanapata stahiki zao kila Mara kwa wakatii....
Tena kila ikifika wakati wa kupewa bila shida wanachukua nimekaa pale wazee wanasifia ule mfuko
 
Back
Top Bottom