PSPF yashindwa kuwalipa wastaafu

PSPF yashindwa kuwalipa wastaafu

Kuna walimu wangu wawili wa mkoa wa Singida wamestaafu toka Oktoba 2014, mpaka leo hawajalipwa mafao yao. Hili shirika halina huruma hata kidogo, kumbuka wastaafu hawa hawana mshahara. PSPF ni janga kabisa
 
Inasikitisha sana, ni kweli wastaafu wa PSPF hawajalipwa pension ya January, February na March
Ni kweli kabisa. Mimi ni mmoja wa wastaafu ambao sijapata hiyo pensheni kupitia PSPF! Nimeangalia salio CRDB nimekuta hamna kitu!
 
Nakumbuka CAG alishasema linaweza shindwa kulipa mafao.Pia trillioni 6 wanazolidai serikali sijui Kama zimerudi.
 
Pensheni za April, Mei na Juni? Kumbe wanapewaga advance kabisa? Na huu mwezi si ndio ulikuwa na sikukuu wiki nzima? Mbona kama naona watu wanaonewa hapa......au ndio majungu ya kina NNSF na LAPF....anayejua mfumo wa pensheni wa PSPF hawezi ongea haya....nina mama nesi amestaafu....wenzie walikuwa NSSF na LAPF...najua tofauti zao....
 
Xmass mama alikuwa anaringa pensheni za Januari alilipwa Desemba 22 mie hata mshahara ilikuwa bado alinikopesha nauli ya kwenda home.Mie nachangia PPF ila PSPF nawatamani kinoma......
 
Pensheni za April, Mei na Juni? Kumbe wanapewaga advance kabisa? Na huu mwezi si ndio ulikuwa na sikukuu wiki nzima? Mbona kama naona watu wanaonewa hapa......au ndio majungu ya kina NNSF na LAPF....anayejua mfumo wa pensheni wa PSPF hawezi ongea haya....nina mama nesi amestaafu....wenzie walikuwa NSSF na LAPF...najua tofauti zao....

Je na hao walimu waliostaafu Oktoba 2014 na hawajalipwa mafao na PSPF mpaka leo??, nayo ni majungu eeh??
 
Haya Mashirika YANA pumulia Mashine ...Serikali inayakopa Sana ....na Zaidi wakuu wa haya mashirika ni Wezi Wezi Wezi .....wanabuni miradi ambayo ni white elephant ......na wana exaggerate gharama Za ujenzi ...sijui SSRA wanangoja nini au hawana Nguvu ....

Chakulia mfano ....shirika linaenda kujenga Jengo ILALA KWA Bilioni 76 ...Wakati Jengo Kama Hilo Hilo watu wanajenga kwa Bilioni 35
Ghorofa pale Moshi ambalo partition watafanya wapangaji ...unaambiwa limejengwa kwa Bilioni 70

Jengo ambalo limejengwa pale Makumbusho ..na lile la Ilala ...kwa kuangalia lipi imara na zuri na lenye facilities nyingi ....lakini Jengo la Ilala ( mzizima towers )eti ni la gharama kuliko la makumbusho

Unakuta Jengo Lina Majengo yako tupu ...lakini wakurugenzi au watu wao wa karibu ....wanajenga maghorofa Binafsi na Kupandisha makampuni wanayoyaongoza ....

Mtandao wa kulinda huu uovu ni Mpana Sanaa ..na Hilo mtaliona muda sio mrefu .
 
Naomba unielewe, mimi si husiki kabisa na NSSF.Kwanza NSSF ndio wa hovyo kuliko wote.Ni ukweli kwamba wastahafu wa PSPF hawajalipwa pension zao kwa kipindi cha April,May na Juni kama ilivyo kawaida.Kama hii sio kweli ndio uongee,vinginevyo kaa kimya usidakie maneno usiyo yajua.

Mimi nafikiri ifike mahala miradi na gharama zake inayofanywa na pesa Za wafanyakazi iwe inawekwa wazi ...vyama Vya wafanyakazi ..Kama TUCTa ..CWT ..etc ..ambao wanakatwa viwe na uwakilishi kwenye Bodi
 
mbona hiyo kitu haipo haiwezekani yani ingekua inaezekana ningeshahama zamani mnooo
Fanya homework kodogo kabla ya maamuzi....karibu mnibadili mawazo nimepitia ripori ya bosi wao SSRA 2014...hakuna mfuko unaololipa kama PSPF hao LAPF hawana hata wa kuwalipa NSSF labda ni shirika la nyumba na mbwembwe zoote za mijengo na wanachama lukuki wamelipa kidoonyoo.....
 
Fanya homework kodogo kabla ya maamuzi....karibu mnibadili mawazo nimepitia ripori ya bosi wao SSRA 2014...hakuna mfuko unaololipa kama PSPF hao LAPF hawana hata wa kuwalipa NSSF labda ni shirika la nyumba na mbwembwe zoote za mijengo na wanachama lukuki wamelipa kidoonyoo.....
usidhan nimekurupuka au naongea ili kuharibu biashara nnaongea nna uhakika 100%...mtu wangu wa karibu yupo LAPF alishafanya kazi sehemu tatu tofauti na kila akiquit anachukua contribution zake LAPF na last time mie mwnyw ndo nlimjazia fomu za kuomba hela zake nkapeleka j3 alhamisi hela ikaingia kwenye account!!!muda huo nlikua ma kijacho nikapewa fomu nijaze mafao ya uzazi roho iliniuma nkiwaza sipo LAPF nkatoka hapo na moto hadi PSPF kuuliza mafao ya uzazi wananijibu ujinga usioeleweka mara hawajaanzisha nyambafff wakat wanajinadi wana mafao ya uzazi...PSPF HAKUNA KITU
 
Mimi nafikiri ifike mahala miradi na gharama zake inayofanywa na pesa Za wafanyakazi iwe inawekwa wazi ...vyama Vya wafanyakazi ..Kama TUCTa ..CWT ..etc ..ambao wanakatwa viwe na uwakilishi kwenye Bodi

Mkuu,

Naamini hapa umeandika vitu usivyovijua. No offence whatsoever.

Katika bodi ya mashirika ya hifadhi ya jamii, mmoja wa wajumbe uwa anatoka kwenye vyama vya wafanyakazi. Hili lipo wazi na nashangaa iweje hulijui hili!

Pia, hata ikitokea mjumbe wa bodi ana mashaka juu ya gharama za ujenzi kwa miradi ya real estate. Je, ataweza kuifafanua na kuichambua Bill of Quantities (BOQ)? Maana ni ripoti ya kitaalamu ile.
 
wiki iliyopita nilienda kuripoti kazin, nilijaza LAPF sijajua kama nilifanya chaguo sahihi maana haya mashirika hata siyaelewii
 
Alichosema ndugu hapo JUU ni sahihi,kuna watoto wanasumbuliwa na mirathi ya mzazi wao mmoja ni mwaka sasa unakaribia ukatike na waakienda wao njoo j4 au ijumaa,tusikatae lisemwalo wakuu NA WAKATI WAKISUMBUA STAHIKI ZA WATU HIVYO WAO WANAENDELEA KUJENGA YALE MAJENGO MAREFU DAAAAH
 
Fanya homework kodogo kabla ya maamuzi....karibu mnibadili mawazo nimepitia ripori ya bosi wao SSRA 2014...hakuna mfuko unaololipa kama PSPF hao LAPF hawana hata wa kuwalipa NSSF labda ni shirika la nyumba na mbwembwe zoote za mijengo na wanachama lukuki wamelipa kidoonyoo.....
Achana na hizo report za 2014 tunazungumzia hali halisi,wastaafu wa PPF hawajalipwa pensheni yao ya January,February na March 2015
 
Bwana Bello pensheni za Jan, Feb na March zililipwa Desemba 22 kabla ya xmass..mie nlikopa mama nkaendea likizo mishahara ilikuwa bado..huwa wanatoa in advance kwa sasa ni za April, May na Juni...nazo zimetoka...anachukulia postal bank....
 
Back
Top Bottom