PSPF yashindwa kuwalipa wastaafu

PSPF yashindwa kuwalipa wastaafu

Serekali ya CCM ni majanga mpaka kwenye sitahili za watumishi,imeshindwa kuwalipa mishahara mizuri imewanyang'anya hata kile walichokuwa nacho.

Pamoja na kwamba JK ameahidi kulipa madeni yote ya PSPF kabla hajaondoka lakini huo ni muendelezo wa kisanii wa kujaribu kuwashawishi watumishi ili waweze kupata kura zao.

Hapo ndipo watumishi wanatakiwa watumie msemo wa Jk mwenyewe wa akili za kuambiwa changanya na zako.
 
Huku wamejenga ghorofa refu kuliko yote Africa Mashariki....only in TZ

Only in TZ!

Tunga sheria ya kukata pesa zao kwa kisingizio cha pension, halafu serikali badala ya kukopa benki inakopa huko. Na ma DG kwa kujipendekeza wanatoa pesa za waajiriwa bila kujali sheria za uundwaji wa mifuko au uwezo wa kulipwa!

Halafu bila haya utasikia serikali sikivu, viongozi makini!

Only in TZ
 
Wacha na wazee wajue kuwa magamba hawafai maana wengi wao ni pro-magamba.
 
Pole sana! Nami nimeiona kitambo lakini haipo tena.
Mimi pia ni mstaafu. Nimestaafu mwaka jana na hali ilikuwa haieleweki kutoka kwa hawa jamaa kwa miezi mitatu.Mimi nipo mikoani na mara nyingi nilikuwa naenda kuwakumbusha ana kwa ana katika ofisi yao ya mkoa hadi nikafanikiwa. Kama jamaa yako aliwasilisha nyaraka zote zinazotakiwa PSPF, basi itakuwa ni uzembe wa huko makao makuu yao kwani kuanzia Machi hadi leo ni muda mrefu mno!
 
yote ni hovyo, hata ppf ni hovyooo kwani wanachowalipa wastaafu wao ni kinyaa kitupu. pesa za wateja wao wamezifanya za kulipana vzr na mafao mazuri kwa wafanyakazi wa mifuko hii! sujui regulator wa mifuko hii kimama Fulani hivi kinafanya kazi gani.
 
Naibu waziri wa fedha leo kawaelekeza pspf walipe mafao ya wastaafu ndani ya siku saba (nadhani wenye hundi walioambiwa hundi ziko tayari lakini fedha hamna kama ndugu yangu mwezi wa nne sasa), kawataka pia waache visingizio vya kutopewa pesa wanayoidai serikali wakati washapewa hela na serikali, na wametakiwa wamalize tatizo la "kupoteza" check maana inatakiwa check itoke pspf iende wizarani (hazina bila shaka) lakini wizarani hazifiki zinapotea katikati haieleweki ni nini hutokea
 
=Wastaafu...

Halafu hizi ni fix na uache kutisha watu wewe kibarua Wa NSSF....

Baada ya kuisemasema NSSF kwa mtindo wao wa kujigeuza mfuko wa hifadhi ya serikali naona na wao wanaleta politics.

Kwa kifupi PSPF wako vizuri hususan huu utaratibu wao wa kuwanunulia viwanja wanachama wao kwa mkopo kitu ambacho NSSF hawana.
 
Uwiiiiiiiii.Huyu mtoto ana mzaha.Mm miezi 12 toka nistaafu na sijaona kitu.Juzi niliongea nao kwa namba ya huduma kwa wateja jibu ni kwamba hazina hawapeleki michango.Nimeamua kukabidhi mikononi mwa Mungu maisha yangu.Watanzania mniombee.Nina uhakika tupo wengi ila pengine wenzangu hawapitiagi jukwaa hili.
 
Naibu waziri wa fedha leo kawaelekeza pspf walipe mafao ya wastaafu ndani ya siku saba (nadhani wenye hundi walioambiwa hundi ziko tayari lakini fedha hamna kama ndugu yangu mwezi wa nne sasa), kawataka pia waache visingizio vya kutopewa pesa wanayoidai serikali wakati washapewa hela na serikali, na wametakiwa wamalize tatizo la "kupoteza" check maana inatakiwa check itoke pspf iende wizarani (hazina bila shaka) lakini wizarani hazifiki zinapotea katikati haieleweki ni nini hutokea

PSPF hamna hela, hali mbaya. mfuko unakaribia kufa!
 
Halafu hizi ni fix na uache kutisha watu wewe kibarua Wa NSSF

no research no right to say...fikiria kabla ya kukoment
 
Halafu hizi ni fix na uache kutisha watu wewe kibarua Wa NSSF

no research no right to say...fikiria kabla ya kukoment

hahahah!!! vibarua mmekutana. haya, teteeni maslahi yenu!
cc Kwamhuzi
 
Last edited by a moderator:
Basi ni siasa zinaendelea na wastaafu waendelee kuishi kwa kuvumilia mateso

ipo siku wote wataenda kulala pale posta ndo wajue mambo yamewafika pabaya....
kujitapa mnakusanya tillion moja point huku wafanyakazi wenu wanawadai na hamtaki kuwalipa ni aibu
 
Wana jf mwenye namba ya sm ya DG Pspf anirushie humu.Nimechoka sasa kuvumilia shirika linaloendelea chezea maisha yangu.Niongee naye anieleze tatizo LA kutotaka kunilipa stahiki yangu na dhamira ya kumpeka mahakamani Kama Si kwa mtumbua majipu.
 
Back
Top Bottom