Kashi
JF-Expert Member
- Jan 6, 2013
- 897
- 747
Jamani, kuna mstaafu hata mmoja wa LAPF ajitokeze hapa. Nijuavyo mimi hiyo LAPF haina hata umri wa miaka 15 hivyo bado haijaanza kulipa mafao ya wastaafu kwa wingi. Kwa sasa wana wanachama wengi ambao bado ni waajiriwa ndo maana wanalipa haya mafao madogo madogo kama ya uzazi kwa uharaka. Nijuavyo mimi hakuna mfuko wa hifadhi ya jamii ambao Serikali yetu haijatia mkono kukopa fedha japo viwango ni tofauti. Ni bora huyo PSPF tunajua analipaje sasa wastaafu kuliko hao ambao hawana uzoefu huo. Muda ukifika nao LAPF wakawa na wastaafu wengi ndio tutajua kama wako vizuri ama laa. Ni mawazo yangu tu.