Prove me wrong Hakuna fundi tajiri.

Yeah nimekuelewa vizuri, nilikua nazungumzia mafundi ambao 90% tunashinda nao hapa mtaani, lakini nimekuelewa sana nilichogundua ni kufanya ufundi kuwa biashara hapo mafanikio atayaona.
 
Mifano inawahusu watz waswahili tu? Kama unawahusu na waTz wahindi, muangalie Datan, (Toyota Dodoma) Ni fundi yule babe.

He’s rich.

Uko sahihi kuwa ili uwe tajiri (Financially loaded) lazima ufanye skill yako iwe biashara.
 
Mifano inawahusu watz waswahili tu? Kama unawahusu na waTz wahindi, muangalie Datan, (Toyota Dodoma) Ni fundi yule babe.

He’s rich.

Uko sahihi kuwa ili uwe tajiri (Financially loaded) lazima ufanye skill yako iwe biashara.
Hao wahindi wa Toyota Tanzania wanawapa mashavu sana wahindi wenzao wenye garage ni nchi nzima Authorized service workshops na spare parts dealers wa Toyota Tz wengi ni wadosi na wana hela.
 
Mafundi asilimia chache Sana ndio Wana Hali nzuri kiuchumi, Yaani ukiona fundi Kila siku unaingia front mwenyewe kupiga kazi Jua tu utakufa maskini vibaya Sana...

Mafundi waliofanikiwa kuajiri wengine, kwenda kisasa, kufanya kazi iwe biashara hao ndio wanakuwa na Hali nzuri kiuchumi kuliko hata wakurugenzi wa mashirika makubwa ya serikali...Wahindi wana kampuni kabisa za ufundi mfano Aluminium, mambo ya AC nk wameajiri watu wengi na Wana tenda nyingi viwandani na kwenye makampuni huko nk, sasa ndio naona baadhi ya watz wenzetu wanafuata mkondo wa Aina hii wa kisasa na kuachana na ufundi wa kipumbavu wa chini ya muembe.

Fundi utakuta ni mzuri kabisa lakini hata TIN Hana, Kila siku yupo chini ya mti tu....Kwanza fundi lazima awe katika mazingira sahihi, lazima fundi uwe na Ndoto...

Ufundi ni ishu siriaz Sana, US Plumber Tu ili akabidhiwe kazi kubwa inabidi uwe na uzoefu na hata muda wa miaka hata nane wa kukaa darasani, ufundi Una pesa hivyo unahitaji uvumilivu Sana na ufanye kazi za watu vizuri Kwa uaminifu kabisa then Jiongeze utafikia hatua ya kuajiri hata wasomi wenye Shahada za uhandisi....

Nakubaliana na kichwa Tu cha mada Kwa asilimia 90....
 
Mtu yeyote ambae anafanya kazi ya Nguvu hawezi kuwa Tajiri.

Pia malipo Yao ni kidogo kidogo unapata pesa ya kula tuu.

Mwisho fundi akiwa Tajiri nani atajenga nyumba?
 
Define kwanza Fundi ni nani

Na Utajiri ni upi?
 
Nakazia hapa tz hakuna fundi tajiri maybe mafundi matapeli na mafundi dalali (wanaotarika ni wakandarasi tu ambo nao wanaudalali flani na ufisadi flani na utapeli flan ndani yake)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…