Prakatatumba abaabaabaa
JF-Expert Member
- Aug 2, 2022
- 2,225
- 7,499
- Thread starter
-
- #41
Basi mafundi wa miaka hii hawataki mchakato kabisa.Kama unaweza kunipa million 5 za usumbufu cash na njoo nikuonyeshe fundi mwenye
1.work shop yake
2. duka la spea za gari lenye mtaji zaidi wa 100m
3. maduka yenye mchanganyiko wa spea za gari kubwa na ndogo, pikpiki, bajaji na yanafanya kazi masaa 24 mtaji ni 50m mpaka sasa yako sehemu tatu tofauti Tanzania.
4. Scania 3 za mizigo
Hakuna kazi ambayo haiwezi kukupa utajiri wa level zako. kikubwa ni malengo na utekelezaji kuweza kufikia utajiri anao taka muhusika!
KweliTafuteni maisha mazuri
Ule vizuri,.
Ulale pazuri,
Usafiri kwenda popote ukitaka.
Upate utulivu wa ndani
Utajiri siyo wa kila mtu
RUGE MUTAHABA (R.I.P) alisema kwamba;
"Tafuta nafasi, ukiipata onyesha uwezo wako, talanta yako, bidii yako. Utajiri na mafanikio yatakuja baada ya hapo".
Sijajua wewe upo mkoa gani, lakini hapa mjini Daslam, kuna watu walianza na gereji za spana mkononi, sasa hivi wana "brand" zao za gereji. Kunq ankoli mmoja wa Mwinyi, alitoka Polisi Ufundi Kurasini, akaanzisha gereji yake hapa mjini, ukiongelea mafundi wazuri wa Land Rover discovery kuanzia matoleo ya chini yale, mpaka hizi mpya. Watakwambia nenda gereji kwa Mwinyi.
Kuhusu utajiri: Kwa macho yangu naona anao. Importers na users wengi wa magari hayo wanamjua huyo bwana. Anashughulika na gari hizo tuu, amejibrand hivyo, kuanzia discovery matoleo yote, Range Rover matoleo yote, zipo chungu nzima gereji kwake.
Unamjua Thomas Lyimbo aliyekuwa anagawa maziwa shule za msingi maeneo ya Kimara na Ubungo mojawapo Ubungo Msewe?Nionyeshe fundi tajiri nikupe ten.
Mwambie akawatafute akina Motech au East cars....vijana kama hao wapo wengi wana maisha mazuri kwa ufundi tu. Tatizo yeye anafikiri fundi ni wale waliochafuka na grease tu.Tanzania inabadirika mdogo wangu; ufundi wa miaka ya 2020 ni tofauti na ufundi wa miaka ya nyuma. Kwa sasa kuna teknolojia kubwa sana
Ujio wa magari aina mbalimbali kila kukicha kumeongeza wigo.
Utaona gereji nyingi, zinazofanya kazi sasa hivi mjini ni "branded", mtu anashughurika na aina flani tuu ya magari.
Hoja yangu: Bado ufundi unatajirisha hapa hapa bongo. Hata hivyo hatubishani, unaweza kuamini unavyoamini wewe.
Hivi yule Dr Toyota sio fundi?Nionyeshe fundi tajiri nikupe ten.
Kijana hana exposure. Yupo ndani ya box.Unamjua Thomas Lyimbo aliyekuwa anagawa maziwa shule za msingi maeneo ya Kimara na Ubungo mojawapo Ubungo Msewe?
Kiwanda chake Cha welding and metal fabrication kipo Kimara Korogwe pale?
Yule ambae alijikuta kwenye anga za FBI sababu ya kuwauzia gesi Al Qaida waliolipua ubalozi wa Marekani Dar Tanzania?
Huyo mmoja tu Ila wapo wengi.
Kaka yangu tumbo moja fundi magari alifanikiwa kujipata akamiliki gari na viwanja kadhaa, gari ya watalii cruiser extended body maarufu War bus.
Ghorofa, dula jumla kubwa la vinjwaji, duka la spare za gari, Car Wash, Bar, n.k.
Mwinge fundi maarufu wa kufunga sound system kwenye magari kule Arusha? Naye kajipata.
Nenda Gerezani Kariakoo kakutane na mafundi tajiri.
Kutoboa na utajiri inategemea juhudi zako na bahati yako.
Kuna matajiri mafundi body za gari na rangi waswahili, wachina, waarabu, na wahindi matajiri sana Dar na Arusha. Bado hujaenda Nairobi.
Kuna fundi electronics , computer n.k. ambao Ni matajiri Tena baadhi Ni authorized dealers wa brand kubwa Kama Dell, HP, Sony, Samsung n.k.
Mtazamo wako dhidi ya mafundi ni wa mafundi wale wa chini ya mwembe ambao wanajitafuta.
Mwambie akawatafute akina Motech au East cars....vijana kama hao wapo wengi wana maisha mazuri kwa ufundi tu. Tatizo yeye anafikiri fundi ni wale waliochafuka na grease tu.
Kweli itabidi nibadilishe mtazamo, mimi naowaona circle yangu ni mafundi wa chini ya muembe ambao ni 95% ya mafundi wote.Unamjua Thomas Lyimbo aliyekuwa anagawa maziwa shule za msingi maeneo ya Kimara na Ubungo mojawapo Ubungo Msewe?
Kiwanda chake Cha welding and metal fabrication kipo Kimara Korogwe pale?
Yule ambae alijikuta kwenye anga za FBI sababu ya kuwauzia gesi Al Qaida waliolipua ubalozi wa Marekani Dar Tanzania?
Huyo mmoja tu Ila wapo wengi.
Kaka yangu tumbo moja fundi magari alifanikiwa kujipata akamiliki gari na viwanja kadhaa, gari ya watalii cruiser extended body maarufu War bus.
Ghorofa, dula jumla kubwa la vinjwaji, duka la spare za gari, Car Wash, Bar, n.k.
Mwinge fundi maarufu wa kufunga sound system kwenye magari kule Arusha? Naye kajipata.
Nenda Gerezani Kariakoo kakutane na mafundi tajiri.
Kutoboa na utajiri inategemea juhudi zako na bahati yako.
Kuna matajiri mafundi body za gari na rangi waswahili, wachina, waarabu, na wahindi matajiri sana Dar na Arusha. Bado hujaenda Nairobi.
Kuna fundi electronics , computer n.k. ambao Ni matajiri Tena baadhi Ni authorized dealers wa brand kubwa Kama Dell, HP, Sony, Samsung n.k.
Mtazamo wako dhidi ya mafundi ni wa mafundi wale wa chini ya mwembe ambao wanajitafuta.
Nimebadilisha mtazamo mkuu mimi nilikuwa naongelea mafundi wa chini ya muembe ambao ni 95% ya mafundi wote, ila ninachokiona kila fundi anaweza kuwa na Maisha mazuri endapo akitumia platform vizuri kujitangaza na kuaminika.Mwambie akawatafute akina Motech au East cars....vijana kama hao wapo wengi wana maisha mazuri kwa ufundi tu. Tatizo yeye anafikiri fundi ni wale waliochafuka na grease tu.
Kwani hapa bongo matajiri kwa jumla ni asilimia ngapi?Kweli itabidi nibadilishe mtazamo, mimi naowaona circle yangu ni mafundi wa chini ya muembe ambao ni 95% ya mafundi wote.
Kwa mujibu wa statistics ni asilimia 0.003% labda sikuweka vizuri au kuonesha utajiri wa namna gani, nachomaanisha ni mtu kuwa na standard ya kawaida ya maisha, nyumba, viwanja, asset mbalimbali, ambapo mimi cycle yangu sioni mafundi wakimiliki asset.Kwani hapa bongo matajiri kwa jumla ni asilimia ngapi?
Arusha Kuna fundi gari wanamilki gari za utalii wanavuta dola kadhaa kwa mwezi. Wapo njema sana.Kweli itabidi nibadilishe mtazamo, mimi naowaona circle yangu ni mafundi wa chini ya muembe ambao ni 95% ya mafundi wote.
Kila kitu hata kama utakua unalipwa milions of money kama huna akili ya kujiongeza ni bure....ninaye jamaa angu tulisoma wote afya ila mshikaji kabla hatujasoma baba ake ni fundi cherehani na yeye mshikaji alikua anajifunza kushona hivi ninavyokuambia mshikaji alipiga chuo chini now ni fundi mkubwa ana miliki duka la jumla la vifaa vya ushonaje na kwasasa ana agiza vitu kutoka china... Yeye anachukua tenda za mauniform nk now ana kaniacha mbali sana ana usagiri kajenga ana biashara zingine bajaji nk na hii nakuambia ni miaka 7 iliyopita tangu aanze jiatfuta.Kweli itabidi nibadilishe mtazamo, mimi naowaona circle yangu ni mafundi wa chini ya muembe ambao ni 95% ya mafundi wote.
Hiki kigezo muhimu.sikuweka vizuri au kuonesha utajiri wa namna gan
Graduate mlioenda VETA mnaendeleaje?
Tarehe 7 Agosti 2025, Waziri Mkuu wa wakati huo, Kassim Majaliwa, aliwataka wazazi na walezi kuhakikisha vijana wanapelekwa kwenye mafunzo ya ufundi stadi yanayoratibiwa na VETA na Ofisi ya Waziri Mkuu. Alisisitiza kuwa lengo ni kuwapa vijana ujuzi wa kuajiriwa au kujiajiri.
Mimi tokea makuzi yangu yoote sijawahi kuona fundi mwenye financial freedom, sjjawahi kuona nilipokuwa mdogo kuna jamaa alikuwa ni fundi wa gari la pale home imepita miaka 20 sasa hakuna chochote anachokimiliki naona maisha yake ni magumu tu.
The same na mjomba wangu alikua fundi mechanics mzuri miaka mingi iliyopita kamaliza ujana wake wote sasaivi yupo na 63 na hakuna chochote anachokimiliki,
Mimi sijawai kuona fundi aliefanikiwa ni wachache sana ambao waliingia kwenye mfumo wa kubadilisha ufundi kuwa biashara nb wachache sana, shida ya hapa Tanzania kwa kijana ambae anachipukia kwenye ufundi ni mjuano (nepotism) mimi nikiwa na kazi nitamtafuta mtu ninayemfahamu anifanyie kazi , unajifunza labda umeme wa magari au mechanics au umeme wa majumbani, nani atakayekupa kazi? Je uwezo wa kufungua workshop yako unao?
Mkombozi kwa vijana ni kuwekeza upande sahii, kuwaelekeza upande sahii ambao ni productive nimeona kwenye biashara watu wengi wakianzia chini kabisa, mpaka kufikia kiwango kikubwa mno, nimeona watu wakilima mpaka kumiliki tractor zao binafsi. Lakini sijaona fundi pikipiki, bajaj, tiles, mechanics, n.k akifanikiwa.