Prove me wrong Hakuna fundi tajiri.

Nimekuelewa hapo kwenye quotation ya ruge mtahaba kwahiyo tuseme vijana wa sasa hawataki mchakato wa kuanzia chini? Yaani kuanza kwa spana mkononi mpaka kumiliki brand kubwa? Tatizo vijana wenye ujuzi mkubwa sana na wanaoanza game na ni wataalamu kwenye land cruiser na discovery wanalalamika kazi zote anapewa mwinyi (mjuano/nepotism) sasa ipi nafasi ya kukuwa kwa huyu mtaalamu? Je aanze chini/ahame mkoa?
 
Kuna jamaa mmoja yupo Instagram anaitwa fundi wa dunia ni mtanzania yupo south Africa, ana skills mbili fundi umeme wa majumbani, fundi carpenter anasema amefanya kazi Tanzania kulala njaa kwake ilikuwa ni kawaida sana, kapiga mahesabu kaona nafasi ya kufanikiwa na kuchomoka hapa Tanzania ni ngumu sana, mwaka mmoja baada ya kwenda South Africa anasema hawezi kurudi Tanzania kwasababu ya nepotism bora afe kwenye nchi za watu kuliko kurudi kufanya kazi za ufundi hapa Tanzania, opportunity ni chache na zipo limited sana.
 
Nionyeshe fundi tajiri nikupe ten.

Kama unaweza kunipa million 5 za usumbufu cash na njoo nikuonyeshe fundi mwenye

1.work shop yake
2. duka la spea za gari lenye mtaji zaidi wa 100m
3. maduka yenye mchanganyiko wa spea za gari kubwa na ndogo, pikpiki, bajaji na yanafanya kazi masaa 24 mtaji ni 50m mpaka sasa yako sehemu tatu tofauti Tanzania.
4. Scania 3 za mizigo

Hakuna kazi ambayo haiwezi kukupa utajiri wa level zako. kikubwa ni malengo na utekelezaji kuweza kufikia utajiri anao taka muhusika!
 
Kijana wangu niliyemfundisha kazi miaka kadhaa nyuma alinitafuta juzi, amenishukuru na kunionyesha asset anazomiliki, nyumba kubwa tatu na room za wapangaji 60, ana gari mbili za kutembelea na mbili za kazi, na kazi anafanya hiyohiyo, hajawahi kubadilisha, mimi niliamua ku switch, kwa ajili ya umri tu, ufundi unalipa usipokuwa mjinga na mlevi, labda ufundi cherahani ndiyo unauzungumzia wewe.
Nionyeshe fundi tajiri nikupe ten.
 

Tanzania inabadirika mdogo wangu; ufundi wa miaka ya 2020 ni tofauti na ufundi wa miaka ya nyuma. Kwa sasa kuna teknolojia kubwa sana
Ujio wa magari aina mbalimbali kila kukicha kumeongeza wigo.
Utaona gereji nyingi, zinazofanya kazi sasa hivi mjini ni "branded", mtu anashughurika na aina flani tuu ya magari.

Hoja yangu: Bado ufundi unatajirisha hapa hapa bongo. Hata hivyo hatubishani, unaweza kuamini unavyoamini wewe.
 
Nina mshkaji wangu anatengeneza gari zile mini Cooper na BMW tu, ndo ka specialize huko yule jamaa anatengeneza pesaa kwa siku laki 3-4 sio ajabu nimeshuhudia mwenyewe, service tu ya oil hua ana charge mpaka laki pia ana Network kubwa Sanaa!

Kapanga flat kariakoo laki 8 kwa mwezi, mke wake ni high maintenance mtoto wa kiarabu hv ndo anapurura hizo pesa mpaka basi ila jamaa angekua mbali sana
 
Una point lakini umesahau kufika juu lazima uanzie chini
 
Mafundi diagnosis wa scania na Man wanapiga pesa kinyama, mtu anakuangalizia tu shida unatoa 250k-400k, hata wa gari ndogo kiwango Cha chini labda 40k hapo umejiliza sana, pia nimeshuhudia sio simulizi, Kuna mwamba kaajiriwa kwa wahindi airport anapiga hizo show kama side hustle kwao huko iringa ana ma heka ya mashamba ya miti kifupi ni tajiri.
 
Itabidi nibadilishe mtazamo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…