Hao ni hao uliowasikia wewe redioni, umeshafika vijijini na kusikia watu wanasemaje kuhusu vyama vingi, achilia mbali vifo vya juzi?
Shigela naye ni mwananchi. Kuna watu nyuma yake na wengine wanamsikiliza na kumwamini zaidi ya magazeti na redio kwani wanaamini kwa wadhifa wake anafahamu zaidi. Wassira naye ni mwananchi na ana wafuasi nyuma yake. Nape naye ni mwananchi na ana wafuasi.
Usiseme wananchi wanaelewa as if uliongea nao wote. Kama unakaa Sinza unaweza kudhania hivyo lkn ukienda Buguruni ukamsikia mama lishe anachoongea utasikia kichefu chefu. 'Ah hawa CDM wanataka tu kutuletea fujo wengine sisi tutakimbilia wapi. Miaka yote tumejiuzia maandazi yetu hapa bila shida wao kwa uroho wao wa uongozi kazi kufanya fujo tu. Polisi wameshaambia msifanye kikao leo wanabisha, sasa wao na polisi mwenye nguvu nani, aah'
Mtu mwenye maneno ya hivi unaweza ukamuhesabu katika upande wa harakati?