Profesa Nonga: Vifaranga 62,730 kutoka Ubelgiji vilivyokamatwa JNIA vyote vimefia Airport

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
12,830
21,460
Vifaranga.jpg

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo,Herzon Nonga akionesha Vifaranga vya kuku wa mayai vilivyozuiwa kuingia nchini,kutokuwa na vibali na cheti cha afya katika kago ya mizigo ya uwanja wa ndege wa Juliasi Nyerere,jijini Dar es Salaam jana.


Kukamatwa kwa vifaranga vilivyokuwa vikiingizwa nchini kumeibua masuala ya uwajibikaji na kutofuata sheria miongoni mwa viongozi wa Serikali na wadau wa sekta ya ufugaji wa kuku.

Vifaranga vilivyozuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Desemba 22, 2022, ni mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliyopo Mkuranga mkoani Pwani.

Vifaranga hivyo vilivyofungwa kwenye maboksi 697 yenye thamani ya Sh200.262 milioni, vilikamatwa wakati wa ukaguzi walipokuwa wakiingizwa nchini kutoka Ubelgiji.

Mwananchi imebaini kuwa Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliwasilisha barua ya maombi kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuomba kibali cha kuagiza vifaranga kutoka nchi hiyo ya Ulaya.

Pia, imethibitishwa kuwa waagizaji walikuwa wamepewa cheti cha mifugo na mamlaka ya Ubelgiji.

Baadhi ya wadau katika sekta hiyo wameishutumu wizara hiyo kwa kushindwa kutoa leseni za uagizaji bidhaa kutoka nje na kuchukua hatua za ziada kuwalinda wawekezaji wa ndani.

“Mamlaka zimeshughulikia suala hilo kwa njia isiyo ya haki. Walitakiwa kutoa kibali hicho kwa kuzingatia kwamba nchi haina uwezo wa kuzalisha kuku wa kukidhi mahitaji yake,” alisema mdau kwa sharti la kutotajwa jina.

“Vifaranga hivyo vingeweza kupelekwa kwenye shamba la kampuni hiyo na kuwekwa karantini humo. Vingegundulika kuwa na afya njema mwekezaji angeweza kuadhibiwa na vifaranga virudi kwake,” kiliongeza chanzo hicho.

Alipotafutwa, Ofisa Mkuu wa Phoenix Farms Limited, Irfan Mitha alikataa kutoa maoni yake kuhusu uhalali wa hati mbili zilizotajwa hapo juu.

“Niko busy leo; nipigie simu kesho, nitakuwa kwenye nafasi ya kutoa maoni yangu,” aliliambia gazeti hili.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Hezron Nonga alisema ombi la kibali cha kuagiza cha Desemba Mosi, 2022, halijafika ofisini kwake wala wizarani.

“Tuliona barua ya maombi ya vibali kutoka nje ya nchi, muda mfupi baada ya vifaranga kukamatwa JNIA. Kadhalika, cheti cha mifugo kilichoandikwa na Shirikisho la Ubelgiji la Usalama wa Mnyororo wa Chakula (FACFAS),” alisema Profesa Nonga.

Akitoa taarifa ya vifaranga hivyo, Profesa Nonga alisema vyote 62,730 vimekufa baada ya kutelekezwa kwenye uwanja wa ndege.

“Mwagizaji ana kesi nyingine ya kujibu mbele ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwa mipango ya uteketezaji wa kuku inaendelea,” alisema.

Chanzo: Mwananchi
 
vifaranga-pic.jpg

Vifaranga vilivyozuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Desemba 22, 2022, ni mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliyopo Mkuranga mkoani Pwani.
Vifaranga hivyo vilivyofungwa kwenye maboksi 697 yenye thamani ya Sh200.262 milioni, vilikamatwa wakati wa ukaguzi walipokuwa wakiingizwa nchini kutoka Ubelgiji.

Mwananchi imebaini kuwa Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliwasilisha barua ya maombi kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuomba kibali cha kuagiza vifaranga kutoka nchi hiyo ya Ulaya.
Pia, imethibitishwa kuwa waagizaji walikuwa wamepewa cheti cha mifugo na mamlaka ya Ubelgiji.
Baadhi ya wadau katika sekta hiyo wameishutumu wizara hiyo kwa kushindwa kutoa leseni za uagizaji bidhaa kutoka nje na kuchukua hatua za ziada kuwalinda wawekezaji wa ndani.
“Mamlaka zimeshughulikia suala hilo kwa njia isiyo ya haki. Walitakiwa kutoa kibali hicho kwa kuzingatia kwamba nchi haina uwezo wa kuzalisha kuku wa kukidhi mahitaji yake,” alisema mdau kwa sharti la kutotajwa jina.
“Vifaranga hivyo vingeweza kupelekwa kwenye shamba la kampuni hiyo na kuwekwa karantini humo. Vingegundulika kuwa na afya njema mwekezaji angeweza kuadhibiwa na vifaranga virudi kwake,” kiliongeza chanzo hicho.
Alipotafutwa, Ofisa Mkuu wa Phoenix Farms Limited, Irfan Mitha alikataa kutoa maoni yake kuhusu uhalali wa hati mbili zilizotajwa hapo juu.
“Niko busy leo; nipigie simu kesho, nitakuwa kwenye nafasi ya kutoa maoni yangu,” aliliambia gazeti hili.
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Hezron Nonga alisema ombi la kibali cha kuagiza cha Desemba Mosi, 2022, halijafika ofisini kwake wala wizarani.

“Tuliona barua ya maombi ya vibali kutoka nje ya nchi, muda mfupi baada ya vifaranga kukamatwa JNIA. Kadhalika, cheti cha mifugo kilichoandikwa na Shirikisho la Ubelgiji la Usalama wa Mnyororo wa Chakula (FACFAS),” alisema Profesa Nonga.
Akitoa taarifa ya vifaranga hivyo, Profesa Nonga alisema vyote 62,730 vimekufa baada ya kutelekezwa kwenye uwanja wa ndege.
“Mwagizaji ana kesi nyingine ya kujibu mbele ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwa mipango ya uteketezaji wa kuku inaendelea,” alisema.
 
View attachment 2466447
Vifaranga vilivyozuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Desemba 22, 2022, ni mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliyopo Mkuranga mkoani Pwani.
Vifaranga hivyo vilivyofungwa kwenye maboksi 697 yenye thamani ya Sh200.262 milioni, vilikamatwa wakati wa ukaguzi walipokuwa wakiingizwa nchini kutoka Ubelgiji.

Mwananchi imebaini kuwa Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliwasilisha barua ya maombi kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuomba kibali cha kuagiza vifaranga kutoka nchi hiyo ya Ulaya.
Pia, imethibitishwa kuwa waagizaji walikuwa wamepewa cheti cha mifugo na mamlaka ya Ubelgiji.
Baadhi ya wadau katika sekta hiyo wameishutumu wizara hiyo kwa kushindwa kutoa leseni za uagizaji bidhaa kutoka nje na kuchukua hatua za ziada kuwalinda wawekezaji wa ndani.
“Mamlaka zimeshughulikia suala hilo kwa njia isiyo ya haki. Walitakiwa kutoa kibali hicho kwa kuzingatia kwamba nchi haina uwezo wa kuzalisha kuku wa kukidhi mahitaji yake,” alisema mdau kwa sharti la kutotajwa jina.
“Vifaranga hivyo vingeweza kupelekwa kwenye shamba la kampuni hiyo na kuwekwa karantini humo. Vingegundulika kuwa na afya njema mwekezaji angeweza kuadhibiwa na vifaranga virudi kwake,” kiliongeza chanzo hicho.
Alipotafutwa, Ofisa Mkuu wa Phoenix Farms Limited, Irfan Mitha alikataa kutoa maoni yake kuhusu uhalali wa hati mbili zilizotajwa hapo juu.
“Niko busy leo; nipigie simu kesho, nitakuwa kwenye nafasi ya kutoa maoni yangu,” aliliambia gazeti hili.
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Hezron Nonga alisema ombi la kibali cha kuagiza cha Desemba Mosi, 2022, halijafika ofisini kwake wala wizarani.

“Tuliona barua ya maombi ya vibali kutoka nje ya nchi, muda mfupi baada ya vifaranga kukamatwa JNIA. Kadhalika, cheti cha mifugo kilichoandikwa na Shirikisho la Ubelgiji la Usalama wa Mnyororo wa Chakula (FACFAS),” alisema Profesa Nonga.
Akitoa taarifa ya vifaranga hivyo, Profesa Nonga alisema vyote 62,730 vimekufa baada ya kutelekezwa kwenye uwanja wa ndege.
“Mwagizaji ana kesi nyingine ya kujibu mbele ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwa mipango ya uteketezaji wa kuku inaendelea,” alisema.
Who the cap fit let them wear it
 
Kuna katabia fulani kapo nchi yetu.

miaka ya nyuma pale daraja la sarender ,walimkamta mpemba kisa kibali alikuwa na samaki wabichi.aliwa bembeleza sana askari walikataa ili apeleke samaki sababu kibali kaacha znz.haka waachia wale samaki kituoni .kilichotokea kila wakioza nawao wanaoza .
sijui ilikuwa ukweli au uongo
 
Nchi hii ina wapuuzi wengi sana,ndio maana Proffesa Asad alisema watumishi wengi na viongozi serikalini wana uwezo mdogo sana

Ndio maana hatuendelei, maana wenye uwezo na akili wengi wakipata nafasi wanakimbilia nje,kuanzia wawekezaji, wanasiasa na wasomi,tunabaki na wapumbavu watupu

Wanaofaa kuwa maraisi wazuri na wabunge wamekimbia nchi,wafanyabiashara wakubwa wanawekeza nje,wasomi nao wakipata shavu nje hawarudi.
 
View attachment 2466447
Vifaranga vilivyozuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Desemba 22, 2022, ni mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliyopo Mkuranga mkoani Pwani.
Vifaranga hivyo vilivyofungwa kwenye maboksi 697 yenye thamani ya Sh200.262 milioni, vilikamatwa wakati wa ukaguzi walipokuwa wakiingizwa nchini kutoka Ubelgiji.

Mwananchi imebaini kuwa Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliwasilisha barua ya maombi kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuomba kibali cha kuagiza vifaranga kutoka nchi hiyo ya Ulaya.
Pia, imethibitishwa kuwa waagizaji walikuwa wamepewa cheti cha mifugo na mamlaka ya Ubelgiji.
Baadhi ya wadau katika sekta hiyo wameishutumu wizara hiyo kwa kushindwa kutoa leseni za uagizaji bidhaa kutoka nje na kuchukua hatua za ziada kuwalinda wawekezaji wa ndani.
“Mamlaka zimeshughulikia suala hilo kwa njia isiyo ya haki. Walitakiwa kutoa kibali hicho kwa kuzingatia kwamba nchi haina uwezo wa kuzalisha kuku wa kukidhi mahitaji yake,” alisema mdau kwa sharti la kutotajwa jina.
“Vifaranga hivyo vingeweza kupelekwa kwenye shamba la kampuni hiyo na kuwekwa karantini humo. Vingegundulika kuwa na afya njema mwekezaji angeweza kuadhibiwa na vifaranga virudi kwake,” kiliongeza chanzo hicho.
Alipotafutwa, Ofisa Mkuu wa Phoenix Farms Limited, Irfan Mitha alikataa kutoa maoni yake kuhusu uhalali wa hati mbili zilizotajwa hapo juu.
“Niko busy leo; nipigie simu kesho, nitakuwa kwenye nafasi ya kutoa maoni yangu,” aliliambia gazeti hili.
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Hezron Nonga alisema ombi la kibali cha kuagiza cha Desemba Mosi, 2022, halijafika ofisini kwake wala wizarani.

“Tuliona barua ya maombi ya vibali kutoka nje ya nchi, muda mfupi baada ya vifaranga kukamatwa JNIA. Kadhalika, cheti cha mifugo kilichoandikwa na Shirikisho la Ubelgiji la Usalama wa Mnyororo wa Chakula (FACFAS),” alisema Profesa Nonga.
Akitoa taarifa ya vifaranga hivyo, Profesa Nonga alisema vyote 62,730 vimekufa baada ya kutelekezwa kwenye uwanja wa ndege.
“Mwagizaji ana kesi nyingine ya kujibu mbele ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwa mipango ya uteketezaji wa kuku inaendelea,” alisema.
Hii serekali inawatu wa hovyo cjapata kuona
 
Tuna watu wapuuzi sana ndani ya Serikali. Badala ya Serikali kuwa chombo cha kuwezesha wanaifanya Setikali kuwa chombo cha kuwaumiza wananchi.

Kulikuwa na uwezekano kabisa wa kuhakikisha huyo muagizaji hapati hasara lakini wakati huo huo hakuna hatari ya kuingiza magonjwa nchini.
 
Back
Top Bottom