Profesa Assad ahoji usiri wa uuzaji Nyumba za Serikali

Mzee makoti

JF-Expert Member
Jul 27, 2016
2,587
3,060
Sakata la uuzaji wa nyumba za Serikali limeibuliwa upya na aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Musa Assad akikosoa utaratibu uliotumika kuziuza.

Dodoma. Utaratibu uliotumika kuuza nyumba za Serikali umekosolewa kutokana na kutolihusisha Bunge kama chombo cha wawakilishi wa wananchi.

Hayo yameelezwa na aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG), Profesa Musa Assad ambaye amesema mchakato huo ulihusisha Baraza la Mawaziri na Makatibu wakuu huku Bunge likiwekwa pembeni.

Akizungumza kwenye mdahalo ulioandaliwa na Mtandao wa Asasi za kiraia uliojikita katika kuchagiza uwajibikaji kwenye uziduaji (Hakirasilimali) katika wiki ya Azaki inayofanyika mjini Dodoma.

Amesema Serikali imeuza nyumba hizo na mchakato ulikuwa ni baraza la mawaziri wakishauriwa na makatibu kutengeneza waraka na kupeleka kwa Rais ili akubali kuuza nyumba hizo.

“Nani kakuruhusu? Ni mawaziri na makatibu wakuu. Kwanini halizungumzwi sasa jambo hilo. Lingekuwa wazi tungesema hilo haliwezekani lakini tumekaa kimya na hakuna mtu ambaye amesema hili jambo lazima lirudi bungeni tulizungumze ili tutoe ruhusa maalum jambo hili lifanyike ama lisifanyike,” amesema Profesa Assad

Chanzo: Mwananchi
 
Lirudishwe Bungeni ili jambo hili lifanyike au lisifanyike!! Kwani si jambo lilishafanyika au bado?

Nakumbuka jambo hili lilifanyika wakati wa Hayati Ben, kisha Prof akapata nafasi ya kuwa CAG wakati wa Kikwete na wakati wa Magufuli lakini sikumbuki kama aliwahi kilipeleka jambo hili Bungeni ili lijadiliwe.

Nasikia CAG huwa anapeleka taarifa zake Bungeni, kwa nini hakupeleka jambo hili? Ya Mungu Mengi.
 
Waabudiao maiti iliofukiwa Chato watamtukana huyu mzee mpaka basi.

Professor Assad ni SHUJAA..
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Waabudiao maiti iliofukiwa Chato watamtukana huyu mzee mpaka basi.

Professor Assad ni SHUJAA..
Ni shujaa kweli maana amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwatoa bavicha kwenye reli kuhusu kesi ya Mbowe nk. Kwa sasa watu wanamjadili yeye badala ya kumjadili Mbowe.
 
Mwananchi Habari Za Kitaifa
Profesa Assad ahoji usiri uuzaji nyumba za Serikali
THURSDAY OCTOBER 28 2021


Profesa Musa Assad

Summary
Sakata la uuzaji wa nyumba za Serikali limeibuliwa upya na aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Musa Assad akikosoa utaratibu uliotumika kuziuza.

By Sharon Sauwa
More by this Author

Dodoma. Utaratibu uliotumika kuuza nyumba za Serikali umekosolewa kutokana na kutolihusisha Bunge kama chombo cha wawakilishi wa wananchi.

Hayo yameelezwa na aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG), Profesa Musa Assad ambaye amesema mchakato huo ulihusisha Baraza la Mawaziri na Makatibu wakuu huku Bunge likiwekwa pembeni.

Akizungumza kwenye mdahalo ulioandaliwa na Mtandao wa Asasi za kiraia uliojikita katika kuchagiza uwajibikaji kwenye uziduaji (Hakirasilimali) katika wiki ya Azaki inayofanyika mjini Dodoma.

Amesema Serikali imeuza nyumba hizo na mchakato ulikuwa ni baraza la mawaziri wakishauriwa na makatibu kutengeneza waraka na kupeleka kwa Rais ili akubali kuuza nyumba hizo.

“Nani kakuruhusu? Ni mawaziri na makatibu wakuu. Kwanini halizungumzwi sasa jambo hilo. Lingekuwa wazi tungesema hilo haliwezekani lakini tumekaa kimya na hakuna mtu ambaye amesema hili jambo lazima lirudi bungeni tulizungumze ili tutoe ruhusa maalum jambo hili lifanyike ama lisifanyike,” amesema Profesa Assad
Huyu Prof huwa ananichanganya kweri kweri. Kwahiyo leo unataka Bunge Dhaifu na Mazuzu yashirikishwe? Au ndio ku "bow down" kumeanza baada ya "hali ngumu" mtaani?
 
Back
Top Bottom