Prof UDSM hoi kwa "kidhungu"

Prof UDSM hoi kwa "kidhungu"

Mungu wangu naangalia kipindi cha this Week in Perspective namsikia Prof.Gaudence mpangala hoi kwa kuchapia nå kuwa nå Löw confidence akificha weaknesses zake Kwa cheko.dah,huyu ni prof au nn.UDSM pro? Ooooh my gosh!!!

english ndo kitu gani we mtumwa.
 
Majita mzee alikunyakaa nini?amenifundisha miaka 13 iliyopita,yuko ngoma droo na marehemu aroub kwa weledi wake
 
Kutawaliwa kubaya,watanzania tumekataa vya kwetu. Lazima tufike mahal tukubal kuwa kiingereza n lugha km kilivyo kihaya au kihehe.
 
wewe jinsia gani? ulikuwa unamtaka prof. wetu nini ukakosa pa kuanzia?
 
hata mi nilimuangalia
nikabaki nimepigwa butwaa,tangu tuondokewe na prof. Othman idara ya DS
mliman imebaki na maprofessor wa kichina.

ubongo wako umeungua wewe....haujaelimika
 
Mungu wangu naangalia kipindi cha this Week in Perspective namsikia Prof.Gaudence mpangala hoi kwa kuchapia nå kuwa nå Löw confidence akificha weaknesses zake Kwa cheko.dah,huyu ni prof au nn.UDSM pro? Ooooh my gosh!!!


Mnachekesha sana tena sana,kusoma ama usomi ama uprof sio kuelewa kingereza,nenda Japan,china,korea,german,spain,mongolia,india baadhi,bangradesh,iran,kuna maprof wamebobea ni high reputed professors,lakini hawawezi hata salamu ya kingereza,kuelewa kuongea kingereza sio ndio usomi,wapo watu UK wanakiongea vyema sana kingereza,lakini hata kukiandika hawawezi kwako wewe unaweza waita wasomi eti kwakuwa wanaweza kukiongea kingereza?
Tuache kasumba,mimi nampongeza kwa hilo na hatuhitaji kukielewa sana hicho kingereza,cha msingi ni kuelewa lile eneo unalotaka kulifanyia kazi.
 
Profesa ni mweledi katika fani yake. Sio maprofesa wote ni maprofesa wa lugha. Nimewahi kuwasikiliza maprofesa kutoka nchi mbalimbali wakiongea Kiingereza. Ukisikiliza Kiingereza cha hawa wataalam kutoka Italy, Germany, Greek, China utakubali kwamba maprofesa wetu wako juu sana kwa lugha.

Mbali na kwamba UDSM sijafundishwa na prof. Mpangala, lakini nimewahi kumsikia japo kupitia kwa wanafunzi wake. Hata kama sijaangalia hicho kipindi lakini siwezi shawishika na kebehi za mtoa mada.

Ebu watanzania tuache kujikandamiza wenyewe tusonge mbele. Kama sikosei Prof. Mpangala ni mtaalam wa sayansi ya siasa, sasa hata akikosea sarufi za kiingereza sio tatizo sana kwani anaweza kukosea hata kwenye Kiswahili pia. Yeye sio mtaalam wa lugha, la muhimu ni yeye kuongea mambo yenye mashiko kwenye fani yake. Mbona hata kwenye Kiswahili tunakosea sana!!
 
Mada nyngne hizi,kazi kweli,kusoma inabidi uwe umeshiba kabisa....kwani kuchapia Dhambi?anachapia Rais ndio. Atakuwa Prof.

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Ni professor mahiri sana na ametunga vitabu vingi tu vinavyotumika kwenye vyuo vikuu ila tatizo moja huwa anaongea kiingereza kigumu kidogo so sio rahisi kumuelewa unaweza fikiri hajui vizuri lakini yupo bomba sana kwenye lugha
 
Mungu wangu naangalia kipindi cha this Week in Perspective namsikia Prof.Gaudence mpangala hoi kwa kuchapia nå kuwa nå Löw confidence akificha weaknesses zake Kwa cheko.dah,huyu ni prof au nn.UDSM pro? Ooooh my gosh!!!

Mawazo ya graduate wa UDOM haya
 
ni profesor wa kiingereza? nchi kama japani na china maprof wao si lazima kujua kizungu japo ni advantage kukijua, lkn sisi ukoloni mamboleo umetutawala hadi tunaona kiingereza ndo uprofesa! hapa ninapoishi kuna binti anaongea kiingereza hadi nikikaa naye inabidi kukatisha mazungumzo lakini amehitimu kidato cha nne mwaka jana na kaibuka na mduara( sifuri) suala kuelewa sio lugha yakigeni hiyo.
 
Mungu wangu naangalia kipindi cha this Week in Perspective namsikia Prof.Gaudence mpangala hoi kwa kuchapia nå kuwa nå Löw confidence akificha weaknesses zake Kwa cheko.dah,huyu ni prof au nn.UDSM pro? Ooooh my gosh!!!

Wiki iliyopita alikuja Wilson Mashaka yule mtetezi wa haki za abiria akiwa na other scholars.Kwa kweli aliwapiga chini sana kwa "kidhungu".nilimpenda sana kwa namna alivyokuwa anaongea utafikiri yupo kwenye debate sekondari kwa namna alivyokuwa anatema kizungu vizuri na kinachoeleweka.Wazee wazima walikuwa wanachapia tu.Kwa kweli "kidhungu" ni tatizo hata kwa wahadhiri wetu.Adam Simbeye alimpongeza sana Mashaka kwa "good presentation".
 
elimu si kingereza wandugu

kama umeamua kutumia lugha ya wenzako basi jaribu kuwa kama wao wanavyotaka.Kama elimu si kiingereza kwanini hamatki kutumia lugha yenu kwenye elimu yote toka msingi hadi chuo kikuu?Utaandikaje kama hujui lugha ya mtu kwenye hayo masomo yako?kiukweli huku ni kutaka kujitetea tu lugha ni muhimu.Sisi watanzania tunang'ang'ania lugha za watu wakati hatuzijui
 
Mnachekesha sana tena sana,kusoma ama usomi ama uprof sio kuelewa kingereza,nenda Japan,china,korea,german,spain,mongolia,india baadhi,bangradesh,iran,kuna maprof wamebobea ni high reputed professors,lakini hawawezi hata salamu ya kingereza,kuelewa kuongea kingereza sio ndio usomi,wapo watu UK wanakiongea vyema sana kingereza,lakini hata kukiandika hawawezi kwako wewe unaweza waita wasomi eti kwakuwa wanaweza kukiongea kingereza?
Tuache kasumba,mimi nampongeza kwa hilo na hatuhitaji kukielewa sana hicho kingereza,cha msingi ni kuelewa lile eneo unalotaka kulifanyia kazi.

Mhandisi usitake kuficha ugonjwa. Hao maprofessor unaowataja ambao hawajui hata kusalimia walisoma hadi kuwa maprofessor kwa lugha yao na si ya kigeni kama tunavyotaka sisi.kama angekuwa ni profesor kwa kupitia lugha yetu toka chini halafu akaja kusoma lugha hiyo akikosea sitamkosoa sana.lakini Mpangala kasoma kiingereza toka alivyoanza kidato cha kwanza.Wahindi wanatufundisha computer kwenye chuo chao kiingereza ni kibovu hata form 1 hawezi kuhahatisha vile.lakini bado wao wanakiri kuwa kwao lugha ya kufundishia na mtaani ni Kitamil kwa mfano kwenye majimbo ya kusini.Wale walosoma kwa kiingereza utaona wanavyoongea kiingereza cha kueleweka na kizuri.Sisi hapa tuamue moja kutumia lugha yetu Kiswahili.

Hao waingereza wanaojua kiingereza lakini hawajui kuandika ni sahihi kwani ndio lugha yao ni sawa na hapa kwetu bibi yangu anajua kiswahili lakini hawezi kuandika.Hapa hakuna kosa.Sifikirii kama Mpangala hiyo lugha kajifunza mtaani kama si darasani.
 
Profesa ni mweledi katika fani yake. Sio maprofesa wote ni maprofesa wa lugha. Nimewahi kuwasikiliza maprofesa kutoka nchi mbalimbali wakiongea Kiingereza. Ukisikiliza Kiingereza cha hawa wataalam kutoka Italy, Germany, Greek, China utakubali kwamba maprofesa wetu wako juu sana kwa lugha.

Mbali na kwamba UDSM sijafundishwa na prof. Mpangala, lakini nimewahi kumsikia japo kupitia kwa wanafunzi wake. Hata kama sijaangalia hicho kipindi lakini siwezi shawishika na kebehi za mtoa mada.

Ebu watanzania tuache kujikandamiza wenyewe tusonge mbele. Kama sikosei Prof. Mpangala ni mtaalam wa sayansi ya siasa, sasa hata akikosea sarufi za kiingereza sio tatizo sana kwani anaweza kukosea hata kwenye Kiswahili pia. Yeye sio mtaalam wa lugha, la muhimu ni yeye kuongea mambo yenye mashiko kwenye fani yake. Mbona hata kwenye Kiswahili tunakosea sana!!

SAYANSI ni pana sana kuna sayansi ya lugha, sayansi ya jamii, sayansi ya siasa, sayansi ya sanaa, sayansi ya tiba, sayansi ya sanaa za maonesho, sayansi ya urais wa Tanzania, n.k., kila mtu angependa aitwe scientist.
 
Kwani huyo prof. Ana Phd ya kidhungu.... Kama ni hivo basi kweli phd yake ya "kichina" othrwise uache majungu.. usomi haupimwi kwa kujua kidhungu
 
Back
Top Bottom