Prof. Sospeter Muhongo VS Dr. Peter Slaa 2015!!

Prof. Sospeter Muhongo VS Dr. Peter Slaa 2015!!

nafikiri tunahitaji Mtu na sio chama,tukiangalia Zambia walipata mtu anaitwa Sata,kila kitu kimebadilika

Zambia kuna kitu gani kilichobadilika? je, Zambia imetoka kwenye list ya nchi masikini duniani? Je, huduma za kijamii vijijini zimebadilika? Tuambie objectively mabadiliko aliyoleta Sata kwa Zambia.
 
Watu wanaokataa kuuliza maswali ndiyo hutawaliwa kijinga na mafashisti huku wakiwaimbia nyimbo za kuwasifia. wewe kama ungekuwa na uwezo ungejibu maswali yaliyoko kwenye hili bandiko!!

Sioni swali lolote kwenye bandiko hilo zaidi ya wewe kuendelea kupigia mistari majibu ya watanzania walio wengi,amka ndugu,
 
Mimi Prof Muhongo namheshimu, ni mtanzania, ni mtu wa mkoani kwangu, shule aliyosoma msingi ndiyo niliyosoma mimi. Ni mwana taaluma mzuri. Lakini linapokuja suala la uongozi wa nchi yangu. Hasa ikiwa imevurugwa kabisa na ccm kiasi cha kutofikia uwezo wa nchi kiuchumi, huku watanzania hata wale wa mtaani kwao Prof Muhongo wakihangaika na umaskini wa kutisha. Hata angeniambia poti wewe utakuwa waziri mkuu nikipata uongozi kuwa rais kupitia ccm sitamuunga mkono hata kwa robo ya kura yangu.
Kwa kifupi hakuna atakayekuja kutoka ccm atupeleke kwenye nchi tunayotaka watanzania. Hiyo ni kama ndoto ya 2005 wakati watanzania hawa wasiofikiria mbali walipodhani Jakaya Mrisho Kikwete, mwanasiasa mwenye haiba angewapeleka kaanani wanayoitaka. Hapo watanzania tutakuwa na akili za samaki wanaoponyoka kwenye mtego wa samaki na kuendelea kuwa hapohapo mpaka wakanaswa na mtego. Hata tukimchagua kijana asiyetulia kama Zito, Lema, Julius Mtatiro au Sugu lakini wasitoke ccm nchi yetu inaweza kufanya vizuri kuliko kuwa na mtu kutoka ccm.
Kitakachofanya mfano wa hao niliowataja kufanya vizuri kuliko mwanataaluma kama Prof Muhongo kutoka ccm ni kwamba wataweka mfumo wa utawala tunaoutaka. Tutawapa utawala ili watupe mfumo wa utawala tunaoutaka ambao utawabana hata wao kwa udhaifu walionao wafanye vizuri kuliko kichwa kizuri cha Prof Muhongo kwa mfumo mbovu wa utawala uliopo sasa hivi unaolindwa kwa nguvu zote na ccm. Prof Muhongo hawezi kubadilisha mfumo mbovu wa ccm. Hawezi hawezi hawezi hawezi hawezi hawezi hawezi mpaka milele na utabaki hivyo mpaka milele.
Kwa maana hiyo ukija kuangalia ccm na Prof Muhongo ulinganishe na Dr. Slaa na na CDM. Dr Slaa anaweza kufanya vyema mara 10 zaidi. Kwanza kwa kutuwekea mfumo mpya wa utawala na yeye mwenyewe akiwa kiongozi shupavu kama tunavyomjua tutakuwa tumeanza kuondoa nchi yetu kwenye gurudumu la umaskini tunaozunguka nao kila siku, kuweka matumaini ya siku zijazo na kuanza enzi mpya ya maendeleo ya nchi yetu. Usihadaike na katiba mpya ya Jaji Waryoba. Hiyo ni funika kombe mwanaharamu apite ya ccm tu. Haiwezi kuleta mabadiliko makubwa tunayoyataka. Italeta tu cream ya mabadiliko na kuacha misingi ya mfumo mbovu ili ccm iendelee kutawala. Huo ndio ukweli wa mambo.
 
Thesi
asante kwa mawazo yako ya kikamanda,
mods tunaomba muweke polls ya hii thread ili tumtoe wasi wasi mkuu Kigarama
 
Last edited by a moderator:
Wile Gamba,

Tunapokuwa tunatoa hoja kuhusiana na utendaji kazi wa huyu Professor tukumbuke pia kuwa amekabidhiwa wizara ikiwa ndani ya crisis tayari, tofauti na wengine walioteuliwa kuchukua wizara ambazo zilikuwa shwari. Zaidi ya hapo, wizara anayoshikilia yeye ni nyeti mno, kiasi kwamba mpaka sasa ameshafanya makubwa mno ikiwamo la kusitisha mgawo wa umeme.

Vinginevyo sasa watanzania mimi nadhani inabidi tuhamie misikitini na kwenye makanisa tumwombe Mungu atushushie malaika kutoka mbinguni waje waendeshe cabinet ya Mh Kikwete! Napita tu lakini ndugu yangu!
Mr. Makanyaga
kwanza kabisa huwa sina ushabiki, kwetu umeme unakatika hovyo hovyo tu, wala sija ona tofauti yoyote hivyo nikianza kumsifia itakuwa unafiki. alafu tatizo la huyu bwana...magao wa umeme utakuwa historia...mgao ukaendelea...ohooo tunaweka miundo mbinu mipya mgao ukaendelea....ohooo huyu jamaa wana muhujumu mgao ukaendelea mwisho akaja kuseme ili tanesco ifanikiwe inabidi ifumuliwe upya...jamaa hajafanya chochote cha maana..sijalianakwamishwa na nini
 
Labda Prof ahame chama lasivyo hawezi akampata Dr ata kwa robo kura aiseee
 
Ndiyo kwa asilimia 100 CCM ndiyo tatizo . Kwa sababu ni chama kilichoacha kuongoza kwa maadili yaliyotokana na azimio la Arusha. Na sasa kinaongoza kkwa mfumo wa rushwa na ufisadi tupu. Kimepoteza imani kwa watu wake.
 
Mr. Makanyaga
kwanza kabisa huwa sina ushabiki, kwetu umeme unakatika hovyo hovyo tu, wala sija ona tofauti yoyote hivyo nikianza kumsifia itakuwa unafiki. alafu tatizo la huyu bwana...magao wa umeme utakuwa historia...mgao ukaendelea...ohooo tunaweka miundo mbinu mipya mgao ukaendelea....ohooo huyu jamaa wana muhujumu mgao ukaendelea mwisho akaja kuseme ili tanesco ifanikiwe inabidi ifumuliwe upya...jamaa hajafanya chochote cha maana..sijalianakwamishwa na nini

WG;
Tatizo la kukatika umeme kumbe unalijua ni miundo mbinu, siyo mgawo. Ulimsikiliza kwenye Kitimoto cha dakika 45 Jumatatu wiki hii lakini?
 
Porojo tupu, narudia tena hii thread ni ya kijinga kabisa.

Tatizo sio profesa wala dk wala suluhisho la matatizo ya watanzania sio chadema suluhisho ni watu gan ama viongozi ambao tutawapata ambao tunawaamini kwa dhati na tunawajua kua wanajua matatizo ya watanzania na wako tayari kutusaidia kuondoa matatizo yanayotukabili na sisi tuwe tayari kuwapokea na kushirikiana nao.Tunahitaji viongozi watendaji zaidi wala sio siasa wala malumbano kwenye mambo ya kiutendaji.Tunaangamia kwa kukosa maarifa
 
Mtawaleta wengi ili mpime kama wanaweza kupambana na Dr.Slaa lakini ukweli ni kwamba he is the best to lead the nation.
 
Uhovyo wangu ni kwa kulitaja jina la Muhongo? Muhongo majibu yake kuhusu Gesi uliyasikia?
Mkuu, majibu ya Muhongo niliyasikia na niliyaona ni mepesi tu.

1. Wananchi wa Mtwara ilibidi washirikishwe kupitia wawakilishi wao (Wabunge na Madiwani) katika hatua ya kwanza kabisa ya kutayarisha mradi. Katika kushirikishwa huko, ilikuwa ni muhimu wajue sababu za kujengwa kwa bomba, na hasara kwao ni nini, na manufaa ya bomba kwao na kwa taifa pia ni nini. Hilo halikufanyika na ni blunder kubwa sana.

2. Wananchi wa Mtwara wana makovu mengi ya kuwekwa pembeni katika fursa mbalimbali za kiuchumi:
a. Reli iling'olewa
b. Barabara bado haijakamilika hadi leo licha ya kusemwa muda mrefu. Miradi iliyokuja nyuma kama ya barabara ya Chato kwenda Mwanza, Nzega Shelui, Shelui Igunga, Nzega Isaka n.k. imekamilika kwa nini wao?
c. Ahadi za wazi za Kikwete juu ya maendeleo ya viwanda ya Mtwara.
d. Dharau ya kudhani kuwa watu wa Mtwara hawawezi kufikiri. Hata katika maswala yanayoathiri afya na shibe yao wakisema eti wanatumiwa na wapinzani.

3. Makubaliano ya Mradi yalitiwa saini Dar, na sherehe ya kukabidhi mradi ilifanyika Dar. Kwa nini?

4. Majibu ya sasa ya serikali ni kuonea aibu mkataba na wawekezaji, ambao tayari umesainiwa.

Muhongo alipoongea hakugusia haya. CCM watakuja kukumbuka mradi huu wa gesi ya Mtwara kama kosa kubwa sana kwao kisiasa. Kigarama siku moja tutarudi hapa na ntakwambia: Didn't I tell you so?
 
Hata CCM Mtwara wanatofautiana na msimamo wa serikali
TAMKO LA CCM: HATUTAKI GESI IENDE DAR
tzccm1.gif

SUALA la wananchi kupinga gesi asilia inayovunwa kijiji cha Msimbati mkoani Mtwara upelekwa Dar es Salaam limechukua sura mpya baada ya Cham Cha Mapinduzi (CCM) Manispaa ya Mtwara Mikindani kuungana na wananchi kupinga mradi huo, huku mbunge wake Hasnain Murji akisema yupo tayari kuvuliwa ubunge kwa kutetea maslahi ya wana-Mtwara.
Mwenyekiti wa CCM wa Manispaa hiyo, Ali Chinkawene amesema kuwa msimamo wa chama chake ni kuungana na wananchi kupinga gesi kusafirishwa kwenda Dar es Salaam na kwamba Serikali inapaswa kujenga mitambo ya kuzalisha umeme mkoani Mtwara badala ya Dar es Salaam.

"Tulipoona hali inakuwa tete, niliitisha kikao cha kamati ya siasa kujadili nini msimamo wa chama katika hili, kamati ya siasa wakasema hawawezi kukisemea chama kwa sababu chama ni wanachama hivyo nikaitisha kikao cha halmsahauri kuu ambapo pia tuliwaalika mabalozi wa mitaa" alisema Chinkawene

Alifafanua kuwa "Katika kikao hicho wajumbe walipinga kwa nguvu zote suala la gesi kupelekwa Dare s Salaam, wakaniambia niseme msimamo wao kuwa hawataki gesi iende Dar es Salaam hadi pale maslai ya Wana Mtwara yatakapowekwa wazi na serikali"

Mwenyekiti huyo alibainisha kuwa msimamo huo sio wake binafsi bali ni maazimio ya vikao halali vya chama hicho vinavyowakilisha wanachama na kwamba historia ya mikoa ya kusini jinsi ilivyonyimwa maendeleo ilitumika na wajumbe kujenga hoja yao hiyo.

"Wakati sisi hatuna umeme hakuna aliyefirikia kutuunganisha kwenye gridi ya Taifa…barabara ya kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam miaka 51 ya uhuru sasa haijakamilika, lakini bomba wanataka kujenga kwa miezi 18, hivi kuna Watanzania muhimu zaidi ya wengine?" alihoji Chinkawene akinukuu kauli za wajumbe wa kikao hicho
Alibainisha kuwa "Walizungumza mambo mengi, suala la kung'olewa kwa reli, kukatazwa kulima Pamba, kuuawa kwa kilimo cha Karanga, Mkonge, haya yote wanadai yamesababisha mkoa uendelee kuwa masikini na kwamba tumaini lao limebaki kwenye gesi, wamesema wapo pamoja na wananchi"
Katika hatua nyingine Murji jana alikutana na umoja wa vyama vya siasa vilivyoratibu maandamano na kuwapongeza rasmi kwa kazi nzuri walioifanya ya kuieleza serikali kuwa wana haki ya kutetea rasilimali yao na kuongeza kuwa yupo pamoja na viongozi hao.
Tofauti na ilivyokuwa awali sasa vyama hivyo vimefikia kumi baada ya kuongezeka kwa Chama cha Wananchi (CUF) na CCM, huku vyama vya awali vikiwa ni Chadema, NCCR-Mageuzi, SAU, TLP, APPT Maendeleo, ADC, VDP na DP, vikiwa na kaulimbiu ya gesi kwanza vyama baadeye, hapa hakitoki kitu.
Mkutano huo uliofanyika ukumbi wa Kanisa la Pentekoste mjini Mtwara uliendeleshwa na mwenyekiti wa umoja wa vyama vya siasa, Hussen Mussa Amri na kuudhuriwa na viongozi mbalimbali wa vyama hivyo akiwemo Chinkawene na mjumbe wa halmashauri kuu CCM Taifa kutoka Mtwara mjini, (Nec), Godbless Kweka.
Murji alisema kwa kuwa yeye si mbunge anayewakilisha mawazo yake bungeni bali mawazo ya wananchi anaona bora aungane na wananchi ili kutetea maslahi yao.

"Nawapongeza viongozi wa vyama vya siasa kwa ujasiri na uthubutu wenu wa kutetea rasilimali hii (gesi)… tusidharau hata kidogo malalamiko ya wananchi…usilazimishe mawazo yako kuwa mawazo ya wananchi, hilo haliwezekani…nakubaliana na ninyi kuwa wachawi wa maendeleo ya kusini ni viongozi, tuache woga tushikamane" alisema Murji huku akishangiliwa na wajumbe

Alibainisha kuwa "Nipo pamoja nanyi na hata ikibidi nivue ubunge nipo tayari kufanya hivyo kwa maslahi ya wananchi….ni heri niondoke madarakani kwa heshima kuliko kuwa kiongozi kwa ufedhuli….tuache unafiki…wapo wabunge wenzangu wanasema wananchi wamekubali hivi ni kweli?"

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Umoja huo, Uledi Abdallah ambaye pia ni mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Mtwara mjini alimpongeza mbunge huyo kwa kuungana na wananchi hao na kuahidi kumpa ushirikiano huku akisisitiza kuweka kando tofauti zao za kisiasa na kutanguliza maslahi ya wengi.

"Tumefarikijika kuona wenzetu wa CCM na wewe mbunge wetu umeungana na sisi….tofauti zetu za kisiasa tuziweke kando, tusimamie rasilimali yetu" alisema Uledi.
mwisho

Narudia tena. Serikali ya CCM makao makuu imefanya kosa la kisiasa ambalo watalijutia sana baadaye.
 
Back
Top Bottom