kwa hiyo kumbe wewe tunakubaliana kwamba tatizo ni watu(wanaochumia matumbo ) na si taasisi! basi tunatakiwa tushirikiane kila mtu kwa nafasi yake kupinga hao watu.......
Ni hakika kabisa,bi.kiroboto alimpeleka puta pale bungeni. kwa mujibu wa CNN Dr.Slaa akilitumia jeshi la makamanda wa CHADEMA amesababisha ccm-(wafuga majangiri, mafisadi, wote wana magamba wakashindwa kuvuana) wabadilishe sekretarieti ya chama chao mara kadhaa.muhongo alichimbiwa biti na yule bibi spika wa bunge akatoa mimacho kwa woga ... teh teh teh
Bishop Hiluka angalau wewe umejenga hoja. Hata kama hajawahi kuutaka Urais haizuii wengine kufikiri kwamba anafaa kuwa Rais!!Kwani Prof. Muhongo ameonesha nia ya kuutaka urais wa TZ?
Kama sivyo sidhani kama ni sahihi kumjadili kwa kulinganisha
na Dk. Slaa. Huu ni mtazamo wangu tu...
Tatizo la nchi sio mtu ni CCM hata slaa akiwa rais kupitia ccm hamna maendeleo ndi maana tunataka kuformat tuweke operating system mpya ambayo ni Chadema
............CCM haina tatizo hata kidogo, kajikundi kawababe fulani ndiyo wametengeneza style ya 10%. Tukipata kiongozi jasiri kama Sokoine (R.I.P), uchumi wetu utapaa kama rocket ! Na si lazima awe wa CHADEMA.
Jadili sera za vyama na siyo watu!Ni sawa na Mawaziri wote wa Kikwete katika lipi. Kufikiri au kutenda?
Umeambiwa tatizo ni mfumo uliowekwa na CCM wa KULINDANA, KUKUMBATIA UFISADI. Hivyo hata Malaika Gabriel atoke mbinguni aje atawale Tanzania ndani ya MFUMO CCM he is doomed to fail. Kama tunataka tuendelea mbele ni kuondokana na MFUMO CCM, that means to VOTE OUT CCM, Tujaribu mfumo mwingine. Don't tell me kuna mtu atakayeweza kubadilisha MFUMO FISADI wa CCM akiwa ndani ya CCM, unless usema anataka kuiua CCM, kitu ambacho hakiwezakani.
Insanity is to repeat the same thing expecting different results. Kama kuna mtu hadi karne hii anajidanganya kwamba there is SINGLE MAN/WOMAN ndani ya CCM ataweza kubadilisha mfumo fisadi wa CCM akiwa ndani ya CCM, then that person is still LIVING IN STONE AGE.
In Summary kila aliyeko CCM NI TATIZO, Lakini si kila aliyeko CDM ni SULUHISHO.
Ni sawa na Mawaziri wote wa Kikwete katika lipi. Kufikiri au kutenda?......
Chama ni dubwasha gani. Chama si watu na hao watu si ndiyo wanatunga hizo "sera" unazotaka "tuzijadili" bila kuwajadili watakaozitekeleza hizo sera? Mwalimu Nyerere, Ally Hassan Mwinyi, Ben Mkapa, na sasa Jakaya Kikwete wote wameshashika nafasi za Urais. Jee Urais umewafanya wafanane? Inakuwaje U-CCM au U-CHADEMA uwafanye watu wafanane?Jadili sera za vyama na siyo watu!
Isitoshe Prof hajatangaza wala kuonyesha nia ya kuutaka urais!
.
- Tofauti yao ni nini kwenye msimamo kuhusu ufisadi? - Kamanda Zitto naona anapigania ufisadi kivitendo mfano kuacha kupokea ruzuku ilhali wengine wote wa CDM wanaendelea kuzitafuna.
- Hadhi yao kwenye kusimamia taasisi ya familia inatofautianaje? Slaa ana kashfa kibao za kifamilia
- Unawatofautishaje linapokuja suala la kuchambua dhana mbalimbali za kiuchumi? Dr Slaa hana elimu ya uchumi ni mtaalamu wa macho lakini Zitto ni mchumi na mwanasiasa
- Nani unamwamini zaidi kati yao na sababu zake ni zipi? Sababu ni vigezo vilivyotolewa
- unafikiri kama hawa wakiwa ni wagombea urais kupitia vyama vyao wanayajua matatizo ya wananchi? Wote wanayajua matatizo yetu
- Unaijua misimamo yao kuhusu utangamano (intergration) wa Afrika Mashariki? Wote wanaisupport EAC
Unaamini kwamba kila aliyeko CCM ni tatizo na kila aliyeko CHADEMA ndiye suluhisho??
Hebu tujaribu kuvitumia hivyo vigezo kuwalinganisha Zitto na Slaa. Nani atafaa zaidi 2015?
Nakuacha na tafakuri ya leo ili akili ichangamke kidogo:
It is better to be hated for what you are than to be loved for what you are not.
-Andre Gide
Usiwe mvivu kufikiri! Ndiyo sababu kuna sera, ilani, mpango kazi nk. Kiongozi bora ni yule anayezingatia malengo ya chama chake! Kwenda nje ya sera za chama kiongozi huyo anastahili kuwajibishwa na hafai! Kwa sababu hata siku moja hakuna atakachokamilisha.Chama ni dubwasha gani. Chama si watu na hao watu si ndiyo wanatunga hizo "sera" unazotaka "tuzijadili" bila kuwajadili watakaozitekeleza hizo sera? Mwalimu Nyerere, Ally Hassan Mwinyi, Ben Mkapa, na sasa Jakaya Kikwete wote wameshashika nafasi za Urais. Jee Urais umewafanya wafanane? Inakuwaje U-CCM au U-CHADEMA uwafanye watu wafanane?
kama tatizo sio watu ni ccm; hebu nambie ccm kama chama tatizo lake ni nini(ukiweka mbali watu ambao unasema si tatizo)?.....
Chama ndio chenye TATIZO kwa sera ya kukumbatia MAFISADI kwa faida ya kuficha aibu,hivyo hata awekwe malaika ni kazi bure......
Usiwe mvivu kufikiri! Ndiyo sababu kuna sera, ilani, mpango kazi nk. Kiongozi bora ni yule anayezingatia malengo ya chama chake! Kwenda nje ya sera za chama kiongozi huyo anastahili kuwajibishwa na hafai! Kwa sababu hata siku moja hakuna atakachokamilisha......