Prof. Sospeter Muhongo VS Dr. Peter Slaa 2015!!

Prof. Sospeter Muhongo VS Dr. Peter Slaa 2015!!

Kigarama

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2007
Posts
2,492
Reaction score
1,238
Kuelekea uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 kuna changamoto nyingi sana zinazolikabili taifa letu na zinazohitaji uongozi imara mara baada ya uchaguzi wa mwaka 2015. Na kwa uhalisia inavyoonekana mchuano utakuwa kati ya CHADEMA na CCM. Kama CCM ikimsimamisha Profesa Sospeter Muhongo kuwa mgombea wake wa nafasi ya Urais na CHADEMA kama inavyotegemewa na wengi ikamsimamisha Dr. Willbroad Slaa kuwa mgombea wake kwa nafasi hiyo ya Urais unadhani mchuano wake utakuwaje?

  1. Tofauti yao ni nini kwenye msimamo kuhusu ufisadi?
  2. Hadhi yao kwenye kusimamia taasisi ya familia inatofautianaje?
  3. Unawatofautishaje linapokuja suala la kuchambua dhana mbalimbali za kiuchumi?
  4. Nani unamwamini zaidi kati yao na sababu zake ni zipi?
  5. unafikiri kama hawa wakiwa ni wagombea urais kupitia vyama vyao wanayajua matatizo ya wananchi?
  6. Unaijua misimamo yao kuhusu utangamano (intergration) wa Afrika Mashariki?

Haya ni baadhi ya mambo ambayo tunaweza Kayatumia kuwapima Muhongo na Slaa kama ni watu wanaofaa au kutofaa kugombea Urais mwaka 2015.
 
Tatizo la nchi sio mtu ni CCM hata slaa akiwa rais kupitia ccm hamna maendeleo ndi maana tunataka kuformat tuweke operating system mpya ambayo ni Chadema
Unaamini kwamba kila aliyeko CCM ni tatizo na kila aliyeko CHADEMA ndiye suluhisho??
 
Tatizo la nchi sio mtu ni CCM hata slaa akiwa rais kupitia ccm hamna maendeleo ndi maana tunataka kuformat tuweke operating system mpya ambayo ni Chadema
kama tatizo sio watu ni ccm; hebu nambie ccm kama chama tatizo lake ni nini(ukiweka mbali watu ambao unasema si tatizo)?
 
Unaamini kwamba kila aliyeko CCM ni tatizo na kila aliyeko CHADEMA ndiye suluhisho??......

Mkuu unakuwa mgumu sana kuelewa, Mkuu DAMA hapo amekwambia tatizo siyo watu bali tatizo ni mfumo mzima wa CCM.

Kinachotakiwa ni kuachana na uhuu mfumo uliojengeka unaoitwa CCM.
 
nafikiri tunahitaji Mtu na sio chama,tukiangalia Zambia walipata mtu anaitwa Sata,kila kitu kimebadilika
 
Mkuu unakuwa mgumu sana kuelewa, Mkuu DAMA hapo amekwambia tatizo siyo watu bali tatizo ni mfumo mzima wa CCM. Kinachotakiwa ni kuachana na uhuu mfumo uliojengeka unaoitwa ccm.....

wani mifumo inatoka mbinguni si inatengenezwa na watu. Kama watu hawana tatizo kwa nini mifumo wanayoisimamia iwe na matatizo?
 
Mafisadi na wachumia tumbo wametufikisha hapa tulipo napata uchungu sn na huruma mno nawadha bila kupata suluhisho. Watoto wengi sana na wakina mama hawana hata mlo mmoja kwa siku wanahangaika mtaani, wamekuwa omba omba. Nchi yetu ina rasilimali za kutosha hatuhitaji kufika huko. Wanyama wanatoroshwa wazima na mchana kweupe. Tunahitaji ukombozi i am tired so tired i can not tolerate any more!!!! I am crying why this to us no no no !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
..........
kama tatizo sio watu ni ccm; hebu nambie ccm kama chama tatizo lake ni nini(ukiweka mbali watu ambao unasema si tatizo)?
 
Kwani Prof.Mhongo si gamba? Hafai kwanza mchanga ktk siasa.
 
Mafisadi na wachumia tumbo wametufikisha hapa tulipo napata uchungu sn na huruma mno nawadha bila kupata suluhisho. Watoto wengi sana na wakina mama hawana hata mlo mmoja kwa siku wanahangaika mtaani, wamekuwa omba omba. Nchi yetu ina rasilimali za kutosha hatuhitaji kufika huko. Wanyama wanatoroshwa wazima na mchana kweupe. Tunahitaji ukombozi i am tired so tired i can not tolerate any more!!!! I am crying why this to us no no no !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

........

kwa hiyo kumbe wewe tunakubaliana kwamba tatizo ni watu(wanaochumia matumbo ) na si taasisi! basi tunatakiwa tushirikiane kila mtu kwa nafasi yake kupinga hao watu.
 
Thread ya kijinga kabisa hii, Dr Slaa na Muhongo wapi na wapi!! Muhongo mkoa mmoja wa Mtwara unamshinda kwa swala la gesi tu halafu ndio unaongelea Urais!? wewe ni mtu wa hovyo kabisa.
Uhovyo wangu ni kwa kulitaja jina la Muhongo? Muhongo majibu yake kuhusu Gesi uliyasikia?
 
Huyo muhongo ata akigombea peke yake simchagui, sioni chochote cha maana anacho fanya, kazi kutafuta huruma ya wananchi. Siyo siri nchi hii watu wanaichezea sana! Mi naona muhongo ni tatizo kubwa tu, labda kwasababu anatinmiza itikadi hizo CCM
 
Dk slaa hauwez kumlngansha na wazs wa ccm,dk slaa vs lazma uunganshe mawazr wote wa jk
 
muhongo alichimbiwa biti na yule bibi spika wa bunge akatoa mimacho kwa woga ... teh teh teh
 
Unaamini kwamba kila aliyeko CCM ni tatizo na kila aliyeko CHADEMA ndiye suluhisho??.....

WATU ni moja na mfumo WA chama ni kitu kingine,CCM chama ndo janga la karne HIVYO, hata wakiweka mtu mzuri ataleweshwa na sumu ya jani la tumbaku,Tumeona juzi tu hapa mtu na usomi wake wooote (Prof) anaorodhesha mazao yaliyo changia pato la taifa HAKUTAJA KOROSHO kisa? watu wa mtwara wameandamana na wanapingana na CCM.(msomi ila bado mtumwa).
 
kama tatizo sio watu ni ccm; hebu nambie ccm kama chama tatizo lake ni nini(ukiweka mbali watu ambao unasema si tatizo)?.......

Umeambiwa tatizo ni mfumo uliowekwa na CCM wa KULINDANA, KUKUMBATIA UFISADI. Hivyo hata Malaika Gabriel atoke mbinguni aje atawale Tanzania ndani ya MFUMO CCM he is doomed to fail.

Kama tunataka tuendelea mbele ni kuondokana na MFUMO CCM, that means to VOTE OUT CCM, Tujaribu mfumo mwingine. Don't tell me kuna mtu atakayeweza kubadilisha MFUMO FISADI wa CCM akiwa ndani ya CCM, unless usema anataka kuiua CCM, kitu ambacho hakiwezakani.

Insanity is to repeat the same thing expecting different results. Kama kuna mtu hadi karne hii anajidanganya kwamba there is SINGLE MAN/WOMAN ndani ya CCM ataweza kubadilisha mfumo fisadi wa CCM akiwa ndani ya CCM, then that person is still LIVING IN STONE AGE.

In Summary kila aliyeko CCM NI TATIZO, Lakini si kila aliyeko CDM ni SULUHISHO.
 
Back
Top Bottom