Prof. Shivji katika hili amechanganya madesa

Prof. Shivji katika hili amechanganya madesa

Njia endelevu ni kuwa piga Shindano ya kwa fanya wasiendele kuzaana
Duh, hii inakubalika mahala popote duniani?

Haya, wakishafanywa hivyo, serikali inaleta wageni kwenye eneo hilo kufaidi uhondo, au siyo?
 
1. Loliondo hakuna anayehamishwa, bali imewekwa mipaka kati ya kilomita za mraba 2,500 na 1,500 ambazo jumla ni kilomita za mraba 4,000.

2. Ngorongoro wanaohamishwa ni kutokana na wingi wao wa sasa, usalama wao na kukiuka masharti ya uhifadhi kwa kujenga nyumba za kudumu, kufanya kilimo na mengine mengi.

3. Prof. Shivji anasahau kuwa waliopo Ngorongoro si wazaliwa, bali walihamishiwa hapo mwaka 1958 kutoka Serengeti.

4. Prof. Shivji anapaswa kutambua haki ya urithi kizazi hadi kizazi. Ndani ya Ngorongoro sheria ya NCA iko wazi kabisa hawamiliki ardhi, hivyo hawana cha kurithisha watoto wao.

5. Mimi nami nimebaki na swali litakalonikosesha usingizi, hivi Prof. Shivji hayajui haya au kuna kitu nyuma ya pazia?
Ujuaji mwingi mpaka anakuwa mjinga
 
Kwa hiyo kwa akili yako fupi, huoni kuwa inafaa wahamishiwe Serengeti, kwa mababu zao?

Hawa watu unadhani wao si waTanzania, kwa nini wawe ndio wanafurumushwa kila mara, tena kwa sababu za kipumbavu kabisa na kutotumia akili kwa viongozi waliomo serikalini!

Najua hutanielewa, kwa sababu inaelekea uko huko huko kwenye akili za kipumbavu kutetea ujuha huu wanaotendewa wananchi wenzako kwa maslahi ya wageni na kujaza matumbo ya hao wanaonyanyasa wananchi wenzao.
Ortello Bussiness Corporation ni muhimu kuliko wamasai wote kwa ujumla! Kwanza waarabu wana uasili na raisi wetu!! Wamasai wa nini kwani!? Pochi tu tunasepa zetu! Hii ni laana itawatafuna wote hadi kizazi cha nne.
 
Hawa watu unadhani wao si waTanzania, kwa nini wawe ndio wanafurumushwa kila mara, tena kwa sababu za kipumbavu kabisa na kutotumia akili kwa viongozi waliomo serikalini!
Hao wengine wanaofurumushwa, mfano wale wa Kidunda dam, kwani siyo raia wa nchi hii?
 
Weka hizo tofauti badala ya hizi ngonjera
Ulipewa kichwa uweze kufikiri. Unapoambiwa kuna tofauti jaribu nawe kutumia hicho kichwa, usikibebe tu kama boga unalopeleka sokoni.
 
1. Loliondo hakuna anayehamishwa, bali imewekwa mipaka kati ya kilomita za mraba 2,500 na 1,500 ambazo jumla ni kilomita za mraba 4,000.

2. Ngorongoro wanaohamishwa ni kutokana na wingi wao wa sasa, usalama wao na kukiuka masharti ya uhifadhi kwa kujenga nyumba za kudumu, kufanya kilimo na mengine mengi.

3. Prof. Shivji anasahau kuwa waliopo Ngorongoro si wazaliwa, bali walihamishiwa hapo mwaka 1958 kutoka Serengeti.

4. Prof. Shivji anapaswa kutambua haki ya urithi kizazi hadi kizazi. Ndani ya Ngorongoro sheria ya NCA iko wazi kabisa hawamiliki ardhi, hivyo hawana cha kurithisha watoto wao.

5. Mimi nami nimebaki na swali litakalonikosesha usingizi, hivi Prof. Shivji hayajui haya au kuna kitu nyuma ya pazia?
Hapo mimi nakuelewa mkuu
 
Ortello Bussiness Corporation ni muhimu kuliko wamasai wote kwa ujumla! Kwanza waarabu wana uasili na raisi wetu!! Wamasai wa nini kwani!? Pochi tu tunasepa zetu! Hii ni laana itawatafuna wote hadi kizazi cha nne.
Huenda haya yanayotokea ni muhimu kutupa akili ya kujua kuwa tunapoteza uhuru wetu kwa kisingizio cha uwekezaji.
Tukishajua hilo itatulazimu tuutafute tena uhuru wetu.
 
Hao wengine wanaofurumushwa, mfano wale wa Kidunda dam, kwani siyo raia wa nchi hii?
Ungekuwa na akili ungejua tofauti kubwa sana iliyopo kati ya hao wa Kidunda na hawa wa Loliondo.

Sasa ninakupa 'assignment', nebda katafute tofauti hizo ili nawe uweze kuwa na mchango wa maana kwa waTanzania wenzako.

I am serious, kama hujui tofauti zake ni vyema ukajielemishe juu yake.
 
Ungekuwa na akili ungejua tofauti kubwa sana iliyopo kati ya hao wa Kidunda na hawa wa Loliondo.

Sasa ninakupa 'assignment', nebda katafute tofauti hizo ili nawe uweze kuwa na mchango wa maana kwa waTanzania wenzako.

I am serious, kama hujui tofauti zake ni vyema ukajielemishe juu yake.
Akili ulizonazo wewe zinatosha kujua kwamba wamasai wanajifanya 'untouchables' kwenye taifa hili.

Nikupe assignment wewe unayeshikia bango kwamba OBS ndiyo watapewa hilo eneo kama vile wewe ndiyo umedraft huo mkataba wa kupewa hilo eneo na serikali.
 
Akili ulizonazo wewe zinatosha kujua kwamba wamasai wanajifanya 'untouchables' kwenye taifa hili.

Nikupe assignment wewe unayeshikia bango kwamba OBS ndiyo watapewa hilo eneo kama vile wewe ndiyo umedraft huo mkataba wa kupewa hilo eneo na serikali.
Hapa nilipo nimekwishajiridhisha kwamba serikali ina uongo mwingi sana, hili sihitaji assignment juu yake.

Sasa kuhusu u'untouchable' wa Masai, una maana kwamba wanachwa wanapovunja sheria? Kwa maana hiyo haya wanayofanyiwa ni adhabu kwao kwa kuwa wao wanajifanya kuwa 'untouchable'?
 
Sasa kuhusu u'untouchable' wa Masai, una maana kwamba wanachwa wanapovunja sheria? Kwa maana hiyo haya wanayofanyiwa ni adhabu kwao kwa kuwa wao wanajifanya kuwa 'untouchable'?
Tafadhali usinilishe maneno mdomoni kwangu. Sijasema kwamba wakivunja sheria wanaachwa, ila kuna ile fikra ya 'niguse uone'. Mbona hiyo hatuoni kwa makabila mengine?
 
Back
Top Bottom