BRAVO FEMATA. katika maamuzi ya kisiasa yaliyojaa upumbavu mwingi mojawapo nililoliona lilikuwa lile la kumfuta kazi Mtaaluma wa Jiolojia aliyekuwa kwenye nafasi ya sahihi kabisa, eti kukidhi UPEPO wa kisiasa. Unajua Kikwete alifanya mambo sahihi mawili ambayo alitakiwa kukomaa nayo bila kujali UPEPO unavyoenda: Moja ulikuwa uteuzi wa Kagasheki, pili uteuzi wa Muhongo. Sijamsamehe Rais kwa kuyumba katika hizi teuzi mbili.
Muhongo anakera watu kwa kujiamini kwake sana. Wengine wanakerwa pia kutokana na ukweli kuwa Muhongo ana majigambo. Tatizo ni mwamba Tanzania inaundwa na watu wasioheshimu vipaji vya kiakili. Tanzania inaundwa na watu wanaoheshimu watu waongo-waongo hivi, vibakavibaka hivi, matapelitapeli hivi, maboot-leakers na watu wa aina hiyo. Akitokea Mtanzania anayejiamini sana na kutaka kusimama katika ukweli, huyu maisha yake yanaingizwa katika shida mara moja. Hakuna akili nzuri katika watu wenye mamlaka za uteuzi! Muhungo na Kagasheki hawakutakiwa kuwa katika shida. Walitakiwa kupewa kazi kubwa zaidi za kujenga taifa letu. Mimi si mwanachama wa CCM, chama cha hawa watanzania wawili. Lakini namshukuru Mungu naweza kutambua watu wazuri katika chama hicho na kuwatakia kheri, kwa kuwa katika kuwatakiwa watu hao kheri, hatima yake nalitakia taifa letu kheri.
FEMATA mumefanya chaguo zuri. Mumefanya uamuzi wa busara sana. Bravo!