Prof. Mark James Mwandosya amezindua kitabu chake alichokiandika na kukipa jina la "BRIDGE ACROSS THE RIVER NILE". Uzinduzi wa kitabu hicho umefanyika jana Jumanne tarehe 24 Oktoba, 2017 katika Kituo cha Mikutano, Kigali nchini Rwanda wakati wa Kongamano la Tano la Maendeleo ya Bonde la Mto Nile.
Kongamano hili hufanyika kila baada ya miaka miwili likiwakutanisha Mawaziri, Wabunge, Wanasayansi, Wasomi, Waandaaji wa Sera, Wanahabari, Wanafunzi, Washirika wa Maendeleo, na Wadau wa Bonde la Mto Nile.
Sambamba na uzinduzi huo, Prof.Mwandosya pia alikuwa ni mmoja wa watu mashuhuri waliopewa mada za kuhutubu kwenye kongamano hilo la kimataifa lililoshirikisha nchi mbalimbali.
© Lusako
Kongamano hili hufanyika kila baada ya miaka miwili likiwakutanisha Mawaziri, Wabunge, Wanasayansi, Wasomi, Waandaaji wa Sera, Wanahabari, Wanafunzi, Washirika wa Maendeleo, na Wadau wa Bonde la Mto Nile.
Sambamba na uzinduzi huo, Prof.Mwandosya pia alikuwa ni mmoja wa watu mashuhuri waliopewa mada za kuhutubu kwenye kongamano hilo la kimataifa lililoshirikisha nchi mbalimbali.
© Lusako