Prof. Maghembe asihusishwe na kashfa ya Faru John

Prof. Maghembe asihusishwe na kashfa ya Faru John

kama anaona ngumu aachie ngazi waje wanaoweza. unaongea nini wewe?
Mkuu huyo keshazoea kuishi maisha ya kimalaika hivyo kuachia ngazi ili akaishi maisha ya kishetani huku manzese hawezi
 
Ni kweli kabisa lkn tunashangaa wale wa upande wa pili wanawachukua mafisadi na kuwasafisha kabla ya kuwapa nyadhifa kubwakubwa
Hapa tunaongelea ufisadi wa mali asili za taifa wacha viroba
 
..hivi kwanini hawafuatilii kujua hatima ya wanyama wetu waliotoroshwa na ndege ya jeshi la nchi moja ya Kiarabu?

..au kwanini waziri mkuu hakutembelea Loliondo na kurudisha serikalini ardhi ambayo ina mgogoro tangu miaka ya 90.
huko kote hajaona wala hajapata kusikia,
anamtaka Faru John akiwa mzima, km maiti basi hata fuvu la kichwa
 
Wanadai eti alipeleka pembe la faru khadija badala ya faru john!
 
Baadhi ya watu wanamhusisha Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Maghembe Jumanne na kashifa ya upotevu wa faru john, jamani tuache kutuhumu watu bila kuwa na ushahidi,

Waziri Maghembe aliteuliwa mwanzoni mwa mwaka huu 2016, Kashifa ya kupotea faru john aliikuta imeshatokea mwaka Jana na wakati inatokea kashifa hiyo Prof. Maghembe alikuwa waziri wa Maji na Umwagiliaji, Kwa hali kama hiyo Prof. Maghembe anahusikaje ?

Jamani tuwe na akiba ya maneno. Tusilete Chuki binafsi katika Kazi Za Taifa.

bcf9f4a9143c48da162ec205d56a1ce4.jpg
Ikiwa hajahusika Kwa namna yoyote sawa.

Je,ikiwa pembe zilizopelekwa Kwa Waziri Mkuu usiku wa manane ambapo naye alikuwepo,ikithibitika sio za faru John Bali za Faru Hadija asihushwe Kwa kumdanganya Boss wake?
 
Ccm imeleta umaskini lini tulikuwa matajiri? Kweli ccm ina mafisadi wa kila aina lkn sio lowassa kwa sab hajatoka ccm.
Mahakama ya mafisadi ilishafunguliwa kitambo mnashindwa nini kumpeleka huyo lowasa?wacheni ujinga wenu wa kuchafua majina ya viongozi wa upinzani kisa tu yupo nje ya ccm
 
Hawezi kuwagusa Waarabu wa Loliondo ndiyo wafadhili wakubwa CCM.Kinana anajua hilo yeye ndiye aliyekuwa mwenyeji wao alipokuwa naibu waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga Taifa.
 
Najua rubani hana ubia na abiria anaowarusha kwenye dege lake. Lakini abiria mmoja akipaaza sauti yenye kukuambia juu ya dege unalorusha linawaka moto kutamfanya abiria Hugo kuwa mbia wa dege lako?
Ni busara ya kawaida tu na hulka ya mwanadamu kuwasikiliza binadamu wwnzake ili kurekebisha au kuboresha unayoyafanya.
Hili la faru mbina linatuyumbisha hivi kana kwamba hakuna mwenye uwezo wa kukata huo mzizi? Mbona mengine yaliyokosa ushahidi yalitolewa maamu haraka kwa kutumbuliwa? Siamini kama wahusika Luna jambo linawatisha hadi washindwe kuamua hatma ya faru vinginevyo ni hewa basi!
 
Hawezi kuwagusa Waarabu wa Loliondo ndiyo wafadhili wakubwa CCM.Kinana anajua hilo yeye ndiye aliyekuwa mwenyeji wao alipokuwa naibu waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga Taifa.
Daaaaa kupata aliye salama ndani ya ccm ni sheeeedah
 
Baada ya kukaa na kuondoa tozo ya VAT katika biashara ya utalii ili nchi iongeze mapato,watu wanajadili faru John,faru John!!!
 
Wale Twiga waliopandishwa Ndege pale KIA vp au ndo kimya Kimya au watu wanaogopa 7,000,000/=
 
Kwenye Sakata la Escrow Chenge alikuwa Wizara gani?
mimi nadhani tuache uchunguzi uwe huru ili umuweke Magembe akiwa huru
 
CCM bado inatupa na kutuletea umaskini mabaya yote yamejaa CCM, majangili. Mafisadi nk
Na mkuu alisha sema makaburi mengine hawazi kuyafukua kwani akisha yafukua yatamshinda kufukia.
Pia wasiwe na Shaka atawalinda tuuuuu
Tutalalamika sana bila msaada wowote kwani serikali haya inayaona na kuyajua
Hasa ile mradi wa maji maarufu Kama mabomba ya mchina. Zaidi USD 300milioni zilipigwa maumvi
 
Watawala bwana hata Faru John na ukubwa wote Kanywewa hivi hivi pamoja na ukali wa Kiongozi.
Prof kama waziri mwenye dhamana aje hapa jamvini aeleze kidogo what real happened.
 
Baadhi ya watu wanamhusisha Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Maghembe Jumanne na kashifa ya upotevu wa faru john, jamani tuache kutuhumu watu bila kuwa na ushahidi,

Waziri Maghembe aliteuliwa mwanzoni mwa mwaka huu 2016, Kashifa ya kupotea faru john aliikuta imeshatokea mwaka Jana na wakati inatokea kashifa hiyo Prof. Maghembe alikuwa waziri wa Maji na Umwagiliaji, Kwa hali kama hiyo Prof. Maghembe anahusikaje ?

Jamani tuwe na akiba ya maneno. Tusilete Chuki binafsi katika Kazi Za Taifa.

bcf9f4a9143c48da162ec205d56a1ce4.jpg


Hata kama ingelikuwa mwaka huu. Prof Maghembe afukuzwe kwa ujangili wa ndani wakati Mwigulu anadunda bila majibu lolote linaoleweka juu ya watu wanaouawa na kutoswa majini pamoja na wanaopotea?

Kunahitajika analysis makini na fairness.

Majitu yanajimulia kufanya biashara ya faru john, Maghembe kama waziri, sasa tunahakika anafahamu hicho kitu. Na yawezekana siyo faru john tu. Ninamashaka na tembo wetu na faru wengine. Kama waziri anapewa nafasi gani ya kukakati katika hili? Maamuzi yake ni halisi? Yanatekelezeka? Utekelezaji wake unapimika? Lini tutapima mabadiliko na kutumia vigezo gani?
Hatua zake zinatija kwa ustawi wa wizara na maendeleo ya taifa katika upande wake huo?

Tunaweza kuliangalia kwa mapana. Kuna hatua za kutatua tatizo lililopo, kuna hatua za kuzuia uharibifu kwa baadaye, lakini pia kuna hatua za ukuaji na maendeleo ya sekta. Utaalamu wa viongozi wetu unatumiwa namna gani? Tunawapimaje utendaji kazi wao? Kazi yao inamaslahi yapi kwa taifa zaidi ya maslahi yao binafsi?

Ninatamani badala ya kuendesha nchi kwa zomeazomea kama makundi ya ngoma, ni vyema tukafanya kazi kwa utulivu, hekima na maarifa kwa malengo murua kwa taifa badala ya kukomoana na kulipizana visasi pasipo mwelekeo.

TUNAHITAJI MABADILIKO. MABADILILKO YAANZIE TULIPO. USHABIKI WA KUZOMEA ZOMEA NA KUTAKIWA WATU MATATIZO BILA KUFAHAMU NAMNA YA UTENDAJI KAZI NI UMASKINI WA FIKRA AMBAO NI HATARI KWA TAIFA.
 
Back
Top Bottom