Prof. Kitila Mkumbo: Huwezi kumtikisa Rais bila Kuitikisa nchi

Prof. Kitila Mkumbo: Huwezi kumtikisa Rais bila Kuitikisa nchi

YAY

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2024
Posts
556
Reaction score
537
“Kwa mujibu wa Ibara ya 33(2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana taswira tatu muhimu. Rais wetu ni Mkuu wa Nchi; Rais wetu ni Kiongozi wa Serikali; na Rais wetu ni Amiri Jeshi Mkuu. Kwa utambulisho huu wa kikatiba, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nembo muhimu ya umoja wa kitaifa. Kwa sababu hii, tuzingatie sana wosia wa Baba wa Taifa. Katika kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (uk.59-60), Mwalimu ametuasa: “…huwezi kumtikisa Rais wa Nchi bila kuitikisa nchi yenyewe. Ni vizuri jambo hili likatamkwa waziwazi”. Ndugu wanachama wenzangu na watanzania wote kwa ujumla tunao wajibu kama chama, kama nchi na kama watanzania kulinda taswira ya Rais wetu wakati wote na popopte pale ndani na nje ya nchi”- Prof. Mkumbo.

Prof. Kitila Alexander Mkumbo, Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Kuandaa Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 akizungumza wakati akiwasilisha Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 katika Mkutano Mkuu Maalum wa CCM, Ijumaa tarehe 30 Mei 2025, Dodoma.


 
Mbona Ruto anatikiswa hadi anarushiwa kiatu lakini Kenya haitikisiki? Kama kuna strong institutions nchi itatikisikaje kwa raisi kuambiwa aache kuteka na kuua watu?
Inatikisika
 
===
Akiwasilisha Ilani ya CCM 2025-2030 amesema hakuna mtu anaweza kumtikisa Rais aache Kuitikisa nchi,

Prof Kitila Mkumbo amesema lazima kumtetea Rais wakati wote popote Kwa nguvu zote.

===
Huyu mpumbavu sana, badala tutete maslahi ya nchi, rasilimali zetu, na pesa z aumma zinazofujwa na wahuni wachache,tukae kumtetea mtu abae ameshindwa kusimamia misingi ya haki na rasilimali za watanzania, ameshindwa kuilinda katiba aliyoapa kuilinda
 
Huyu mpumbavu sana, badala tutete maslahi ya nchi, rasilimali zetu, na pesa z aumma zinazofujwa na wahuni wachache,tukae kumtetea mtu abae ameshindwa kusimamia misingi ya haki na rasilimali za watanzania, ameshindwa kuilinda katiba aliyoapa kuilinda
Tena huu ni upumbavu wa kiwango cha lami . Hii nchi bado ina propaganda ya kuwatisha wananchi
 
Kwahio Rais akishindwa kwenye Uchaguzi akaangukia pua, nchi inatikisika?

Kwahio bunge likiazimia Rais afute mkataba wa DPW na awaondoe waarabu Ngorongoro ( maana nako ni kumtikisa) nchi itatikisika?

Na hata Sasa Gen Z wa Kenya wanamtikisa Rais mbona sioni Tanzania inatikisika?

Kauli hizi ndizo zinawachochea TISS kufanya mauaji holela

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom