GE2025 Prof. Kitila abanwa mbavu na Wajumbe CCM, wakumbusha ahadi ya ujenzi wa ukingo wa Mto Gide

GE2025 Prof. Kitila abanwa mbavu na Wajumbe CCM, wakumbusha ahadi ya ujenzi wa ukingo wa Mto Gide

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Ubungo, wilayani Ubungo mkoani Dar es Salaam wamehoji kwa sauti moja hatua za Mbunge wa jimbo hilo anayemaliza muda wake, Profesa Kitila Mkumbo, kuhusu utekelezaji wa ahadi zake mbalimbali ikiwamo ujenzi wa ukingo wa Mto Gide ambao huleta mafuriko makubwa katika makazi ya wananchi hasa kipindi cha mvua.

Wakiwa katika mkutano wa kampeni za ndani uliofanyika kwenye Kata ya Kimara siku ya Alhamisi, baadhi ya wajumbe walihoji ni kwa nini ukingo wa mto huo haukujengwa licha ya kuwa ni miongoni mwa ahadi kuu za Prof. Kitila katika kipindi chake cha ubunge.

Soma: Makazi ya Wananchi 500 Ubungo - Kisiwani (Dar) yapo hatarini, tunaomba Serikali itujengee mifereji ya kusafirisha maji ya mvua kutoka Barabara Kuu

Akijibu hoja hiyo, Prof. Kitila ameeleza kuwa tayari alichukua hatua kwa kutumia Shilingi milioni tano kutoka kwenye mfuko wake wa Mbunge kwa kila kata inayopakana na mto huo, ikiwemo Kimara. Amesema fedha hizo zilielekezwa katika juhudi za muda mfupi za kupunguza athari za mto huo wakati serikali ikiendelea na taratibu za utekelezaji wa mradi mkubwa wa kudhibiti mafuriko. Amesisitiza kuwa akipewa ridhaa tena, atalifuatilia kwa ukaribu zaidi hadi lifikie mwisho

Mkutano huo ni sehemu ya mwendelezo wa mikutano ya wagombea ubunge na udiwani wa CCM kuomba ridhaa ya kuteuliwa tena kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao wa Oktoba 2025.

 
Prof amekuwa mjanja sana, sio vibaya wajumbe wakimpumzisha kwa miaka mitano ijayo
 
River training (kuimalisha kingo na utlilishqji mto) kwa 5m Prof kweli ?
 
Prof amekuwa mjanja sana, sio vibaya wajumbe wakimpumzisha kwa miaka mitano ijayo
Sikutegemea kwakweli huyu ndugu awe wa namna hii...Ametuangusha sana wengi tuliokuwa tuna mtegemea
 
A

Anasema amefanya river training huyu ndo muandika/ mtoa dira ya 2025-2050 utapeli tu na bado anaomba ridhaa tena eti mitano mingine. Kwanini asirudi akafundishe awaachie na wengine waendelee alipoishia?​
Anarudi kupiga pesa
 
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Ubungo, wilayani Ubungo mkoani Dar es Salaam wamehoji kwa sauti moja hatua za Mbunge wa jimbo hilo anayemaliza muda wake, Profesa Kitila Mkumbo, kuhusu utekelezaji wa ahadi zake mbalimbali ikiwamo ujenzi wa ukingo wa Mto Gide ambao huleta mafuriko makubwa katika makazi ya wananchi hasa kipindi cha mvua.
Soma pia: Prof Kitila: Utafiti unaonesha Watanzania wengi wanaikubali Serikali yao



Wakiwa katika mkutano wa kampeni za ndani uliofanyika kwenye Kata ya Kimara siku ya Alhamisi, baadhi ya wajumbe walihoji ni kwa nini ukingo wa mto huo haukujengwa licha ya kuwa ni miongoni mwa ahadi kuu za Prof. Kitila katika kipindi chake cha ubunge.

Akijibu hoja hiyo, Prof. Kitila ameeleza kuwa tayari alichukua hatua kwa kutumia Shilingi milioni tano kutoka kwenye mfuko wake wa Mbunge kwa kila kata inayopakana na mto huo, ikiwemo Kimara. Amesema fedha hizo zilielekezwa katika juhudi za muda mfupi za kupunguza athari za mto huo wakati serikali ikiendelea na taratibu za utekelezaji wa mradi mkubwa wa kudhibiti mafuriko. Amesisitiza kuwa akipewa ridhaa tena, atalifuatilia kwa ukaribu zaidi hadi lifikie mwisho

Mkutano huo ni sehemu ya mwendelezo wa mikutano ya wagombea ubunge na udiwani wa CCM kuomba ridhaa ya kuteuliwa tena kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao wa Oktoba 2025.

Chanzo: Jambo tv
 
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Ubungo, wilayani Ubungo mkoani Dar es Salaam wamehoji kwa sauti moja hatua za Mbunge wa jimbo hilo anayemaliza muda wake, Profesa Kitila Mkumbo, kuhusu utekelezaji wa ahadi zake mbalimbali ikiwamo ujenzi wa ukingo wa Mto Gide ambao huleta mafuriko makubwa katika makazi ya wananchi hasa kipindi cha mvua.

Wakiwa katika mkutano wa kampeni za ndani uliofanyika kwenye Kata ya Kimara siku ya Alhamisi, baadhi ya wajumbe walihoji ni kwa nini ukingo wa mto huo haukujengwa licha ya kuwa ni miongoni mwa ahadi kuu za Prof. Kitila katika kipindi chake cha ubunge.

Akijibu hoja hiyo, Prof. Kitila ameeleza kuwa tayari alichukua hatua kwa kutumia Shilingi milioni tano kutoka kwenye mfuko wake wa Mbunge kwa kila kata inayopakana na mto huo, ikiwemo Kimara. Amesema fedha hizo zilielekezwa katika juhudi za muda mfupi za kupunguza athari za mto huo wakati serikali ikiendelea na taratibu za utekelezaji wa mradi mkubwa wa kudhibiti mafuriko. Amesisitiza kuwa akipewa ridhaa tena, atalifuatilia kwa ukaribu zaidi hadi lifikie mwisho

Mkutano huo ni sehemu ya mwendelezo wa mikutano ya wagombea ubunge na udiwani wa CCM kuomba ridhaa ya kuteuliwa tena kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao wa Oktoba 2025.


 
Muda ambao profesa anaweza kupata tabu kujibu swali la mtu wa darasa la 7
 
Back
Top Bottom