Prof. Anna Tibaijuka atolea Ufafanuzi sakata la Escrow, agoma Kujiuzulu

Mama kwa nini hakupeleka angalau kahela ka ugoro kwenye jimbo lake kuchangia zile shule maarufu za kata?

Ningemuheshimu sana na kumuona wa maana sana kwenye elimu.

Lakini kusema yeye amefanya kazi Umoja wa Mataifa so what? Yaani huko UN ni kama mbinguni kuko kusafi kabisa?

Na zile issues za procurement kwenye idara yake aliyokuwa anaongoza vile ziliishia vipi?
 
watu kama wewe ndio mnafanya mpaka kenya watunge sheria za ajabu ajabu za kuthibiti mitandao, huyu mama Tibaijuka wewe anaweza kukuzaa wewe na baba yako! Hivi uliwahi hata kutembelea website ya hiyo shule halafu ukakosa kuona misaada inatolewaje? Na Mungu wangu akulaani kabisa wewe!

Hizo laana zitamludia mwenyewe fisadi mkubwa, eti msaada kumbe watu wanalipa 4.5 mil huyo niwa kuliwa ndogo
 
Prof. Tibaijuka, mimi nakuonea huruma sana unavyohangaika mama, kwani kuhangaika kote huko ni dalili ya kuhukumiwa ndani yako. Ingekuwaa hakuna hukumu ndani yako usingehangaika vile, na mimi nakushauri tii sauti inayotoka ndani yako ili Mungu akusamehe.
Haiyumkiniki kuwa wewe kwa nafasi yako usijue kuwa kwenye sakata hili zima la IPTL kuna udhalimu kwani ni suala limekuwemo kwenye mitandao tangu mwaka jana kuwa kuna ufisadi kwenye akaunti ya Tegeta ESCROW na kuwa watu wamekwapua pesa kutoka huko isivyo halali. Hata kama si hivyo wewe na usomi wako wote na exposure uliyonayo ya kimataifa hukupata shaka kuona mtu anagawa pesa nyingi hivyo kwa watu mbalimbali ghafla tena kati kati ya wimbi la zile kelele za wizi kutoka kila pande - magazeti, mitandao na hata mitaani.
kuwahusu watu akiwemo huyo kaka yako.
Kule kwetu nilikozaliwa enzi zile watu walikuwa wanaweka matego kwenye mashamba yao na mtu akija akaiba kutoka kwenye shamba la jinsi hiyo familia yake na wote waliokula chakula kilichotoka hapo shambani huanza kupukutika kwa vifo na mwizi mwenyewe anakuja kuwa wa mwisho. Kwa sababu hiyo wezi wa wakati ule walikuwa wakiibakutoka kwenye shamba wanalohisi limefanyiwa tego walikuwa wanawagawiawatu wengi ikiwemo hata wa familia ya mwenye shamba ili ikitokea tego likianza kufanya kazi wataathirika hata hao wenye shamba na hivyo kwenda kulitegua tego ili lisiendelee kufanya madhara kwa wenye shamba. Kutokana na hilo tulikuwa tunafundwa kutilia shaka ukarimu wa ghafla wa mtu ye yote kwa majirani zake au wapita njia kwani yawezekana hivyo anavyogawa ni vya wizi.
Hivyo mama Tiba ulipaswa kutilia shaka ufadhili ule ambao ulihusisha watu wengi kugawiwa pesa nyingi kiasi kile na mtu huyo tena ambaye tayari kulikuwa na tuhuma juu yake za ukwapuaji wa pesa nyingi zinazodhaniwa ni za umma. Na kama unaamini zile pesa zilikuwa halali kwa nini sasa unatumia nguvu nyingi kiasi hiki kujisafisha, kwanini usikae kimya ukingojea uchunguzi unaoutaja humu? Huoni kujitetea wakati bado uchunguzi unaendelea ni kuingilia uchunguzi kama ambavyo wanaoendelea kukushambulia wanafanya.
Ninarudia tena kama kuna hukumu ndani yako dawa ni toba tu, kujaribu kujiokoa kwa jinsi hiyo kutazidi kukuumiza kiroho na kimwili na hata heshima yako inazidi kushuka zaidi.
Hata kama kuna adui zako wa kisiasa wamedhamiria kukunasa kwenye hili mimi nadhani ilikuwa ni bora ukajiudhuru ili kuokoa hadhi yako uliyojijengea kwa miaka mingi tangu enzi za Bawata na UN HABITAT. Niseme ukweli mimi binafsi naumia sana kwani ulikuwa ni role model niliyokuwa nai propagate kwa binti na dada zangu.
 
Kwa nini ajiuzulu? Kupewa pesa kuna kosa gani? Hata ukimpeleka mahakamani, unamshitaki kwa kosa gani?

Kiongozi wa umma uwezi kupewa pesa nyingi kama hizo tena kwa kujificha mpaka soo litokee ndio useme ulipewa. Wewe kama kiongozi wa umma unapopewa fedha nyingi kiasi hicho na mfanyabiashara, utaweza kumkamata akikwepa kodi?
 
Nilikuwepo kwenye press conference. Huyu mama amejieleza vizuri sana nami namuunga mkono hastahili kabisa kujiuzulu. Amesema yeye ni mwanaharakati wa maendeleo na hivyo kupewa pesa kwa ajili ya maendeleo ni furaha kwake. Pia amesema iwapo itathibitika kuwa fedha alizopewa na Rugemalila ni fedha chafu basi atazirejesha kwani taasisi yake haikai na fedha chafu.

Zilikaa masaa 48 pale. Pia Kinondoni kupitia NGO yake ya women habitat, kapewa pesa na wafadhili ili awajengee wanawake lakini kajenga hizo apartment na kuzifanya zake
 
Mwizi hata USO UNATOSHA TU...USO WAKE UNAONYESHA ALIVYO MWIZI NA FISADI MKUBWA HAKA KA BIBI...

BIG THIEF TIBAIJUKA....ardhi ndio kaiba hadi basi...kakiongea ardhi u will think Messiah kumbe mwizi aliyekubuhu...

She started defending her THEFT THRU HER SCHOOL...

eti anasaidia wanawake....FISADI MCHAFU SANA HUYU...babro shule ya matajiri tu...ada 5.2 mil per year...

Huyu jizi kweli huyu...!!!
 
Huyu mama Prof Tiba ni swahiba wa Rais, ndo maana anayojeuri hiyo.We fikiri kama Rais katika ziara zake za Muleba alifikia nyumba kwa mama huyo na kusababisha taaruki kwa wakazi wa Muleba usiku,kwani kila kona kulijaa askari. Kwahivyo basi Prof. anaweza kuelendelea kula nchi kwa nafasi yake ya uwaziri

kweli mkuu nilisahau hili tukio la Rais kulala kwake.basi wameivana sana.
 
kwa matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa jimboni kwake , hata asipojiuzulu amebakiwa na siku chache mno !
 
Nchi hii ilipofika ni balaa,mtu anajua amepokea pesa kimakosa na anatamka mwenyewe lakini anasema sijiuzulu ng'o.
 
Nchi hii ilipofika ni balaa,mtu anajua amepokea pesa kimakosa na anatamka mwenyewe lakini anasema sijiuzulu ng'o.
 
Hizo laana zitamludia mwenyewe fisadi mkubwa, eti msaada kumbe watu wanalipa 4.5 mil huyo niwa kuliwa ndogo

Hakuna binadamu yeyote anayemwelewa mama huyu anaweza kumtetea. Nahisi ni yeye mwenyewe anajitetea humu kwenye mtandao. Mimi niseme Watanzania wakifahamu aliyoyafanya kazi na kuiba UN- Habitat NA baadaye Wizara ya Ardhi, nyumba NA MAENDELEO ya Makazi. Hakika mtamnyonga huyu mama, ni fisadi lililokubuhu.fedha za IPTL alizichukua kwenye sandarusi na hakuna hata senti tano iliyopelekwa kwenye SHULE hizo. Yaani huyu mama ni wa Kunyonga
 
Kaambiwa na boss wake akagome ili yeye aseme mama kajikatalia na kwa udhaifu wake atakubali. Ina maana Muhongo hajapata hiyo akili?
 
Watanzania wote tunajua kuwa leo ijumaa ni siku ambayo rais Kikwete atazungumza na taifa kukata mzizi wa fitina(hata kama ataumwagilia instead ya kuukata),cha kushangaza na kujiuliza ni kwanini Prof Anna Tibaijuka kaitisha press conference saa chache kabla kuzungumzia tuhuma zake zinazomkabili na kuweka msimamo kuwa hawezi kujiuzulu? kuna nini hapa? alikuwa wapi siku zote toka atuhumiwe? sio kujaribu kumchanganya Kikwete ili abadili msimamo wake alio kuwa nao kwa mtu huyu? NAONA PROF ANNA TIBAIJUKA KAFANYA SHAMBULIO LA KIFIKRA KWA RAIS..
 
Naomba nisiseme lolote maana kwa jinsi nilivyo msikiliza huyu mama analopoka bila aibu kidogo nizimie kwa hasira.
 
Hakuna binadamu yeyote anayemwelewa mama huyu anaweza kumtetea. Nahisi ni yeye mwenyewe anajitetea humu kwenye mtandao. Mimi niseme Watanzania wakifahamu aliyoyafanya kazi na kuiba UN- Habitat NA baadaye Wizara ya Ardhi, nyumba NA MAENDELEO ya Makazi. Hakika mtamnyonga huyu mama, ni fisadi lililokubuhu.fedha za IPTL alizichukua kwenye sandarusi na hakuna hata senti tano iliyopelekwa kwenye SHULE hizo. Yaani huyu mama ni wa Kunyonga

Nahis ana washauri ambao ni wa kabila lake zaidi ya yule boy friend mzee wa Vijisenti. Unaweza kuona kiburi cha kijinga kilivyo
 
Back
Top Bottom