Ndugu wadau, nimekuwa nasafiri katika nchi nyingi za Afrika, nimegundua ile sifa ambayo Tanzania tulikuwanayo hasa hasa kwenye ukombozi wa Afrika na misimamo thabiti kwenye mambo ya kimataifa imepungua. Vilevile ukiongea na vijana wengi hapa Tanzania hawajui mchango wa nchi yetu katika ukombozi wa nchi kama Uganda, Angola, Msumbiji, Afrika ya kusini, seycheles etc. Ni muhimu historia hii ikatunzwa na kuelezewa kwa vizazi vyetu ili kurudisha ile pride ambayo watanzania tulikuwa nayo na vilevile kurudisha status yetu katika Afrika na Dunia. Nadhani hii pride ikirudi tunaweza kuitumia vizuri confidence hii katika nyanja zingine kama uchumi na siasa za kimataifa. Naomba michango yenu nini kifanyike maada hii social capital tuliyojenga ni kubwa sana na naamini bado tunaweza kuitumia vizuri hata sasa