Premier League: Man City 0-0 Arsenal ni kivumbi, Machi 31, 2024

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
Fo2wHlIX0AIT3GB.jpeg
Mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England ‘Premier League’ 2023/24 zinazidi kushika kasi, Manchester City itakipiga dhidi ya Arsenal kwenye Uwanja wa Etihad, leo Machi 31, 2024.

Msimamo wa Timu Tatu za juu, Arsenal pointi 64, Liverpool (64) na Man City (63), hivyo atakayeshinda leo anaweza kuathiri kiasi fulani mbio za yule atakayepoteza.

Takwimu za jumla, Timu hizo zimekutana mara 210, Arsenal imeshinda mechi 99, City 65 na sare zikiwa ni 46 na mara ya mwisho kukutana (Oktoba 8, 2023) Arsenal ilishinda 1-0.

Rekodi ya ushindi mkubwa, Arsenal 5-0 Manchester City (Oktoba 27, 2000) na Manchester City 5-0 Arsenal (Agosti 28, 2021).

####
MAN CITY 0-0 ARSENAL, LIVERPOOL YASHIKA USUKANI

Mchezo wa Manchester City dhidi ya Arsenal umekamilika kwa suluhu ya 0-0 kwenye Uwanja wa Etihad, matokeo ambayo yanaiwezesha Liverpool kuongoza msimamo wa Premier League

Arsenal imefikisha pointi 65 na hivyo kushuka hadi nafasi ya Pili ilifuatiwa na Man City yenye alama 64.

Liverpool ambayo imeshinda 1-0 dhidi ya Brighton inaongoza msimamo kwa kuwa na pointi 67.
 
Mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England ‘Premier League’ 2023/24 zinazidi kushika kasi, Manchester City itakipiga dhidi ya Arsenal kwenye Uwanja wa Etihad, leo Machi 31, 2024.

Msimamo wa Timu Tatu za juu, Arsenal pointi 64, Liverpool (64) na Man City (63), hivyo atakayeshinda leo anaweza kuathiri kiasi fulani mbio za yule atakayepoteza.

Takwimu za jumla, Timu hizo zimekutana mara 210, Arsenal imeshinda mechi 99, City 65 na sare zikiwa ni 46 na mara ya mwisho kukutana (Oktoba 8, 2023) Arsenal ilishinda 1-0.

Rekodi ya ushindi mkubwa, Arsenal 5-0 Manchester City (Oktoba 27, 2000) na Manchester City 5-0 Arsenal (Agosti 28, 2021).
Watoke sare tu
 
Back
Top Bottom