Posho za Wabunge na Maisha ya Dodoma

Posho za Wabunge na Maisha ya Dodoma

Maisha magumu kazini ni ya wabunge tu au wafanyakazi karibu wote serikalini?
 
William,

Hii ni hoja ya msingi sana! Lakini nasikitika umeileta in pieces. Ukisema leo wabunge ndo wateule zaidi waongezewe posho, vipi kuhusu ma-dr, manesi, walimu, ma-injinia, na watumishi wote serikalini?!! Na hizo fedha za kuwalipa zinatoka wapi? Mzigo wa matumizi ya kawaida ndani ya serikali ndo kama unvyojua, haikusanyi kodi, hajengi uchumi, kazi yake ni kutumia tuuu! Mimi nadhani ingelikuwa vyema serikali ije na mikakati ya kujenga uchumi na kuhahkikisha inapanua wigo wa kodi, ziba wizi sehemu zote, ijipe uwezo wa kutumia. Nimeona hapo juu umeongelea China, Wa-china ni stori ingine mazee, wanakusanya haswa, na wana reserve ya kutosha!!

Wakati tunachagua ujamaa, tuliondoa fedha kwa wananchi tukaipa uwezo serikali, na ndo maana kulikuwa na sub-sidies, kwa kuwa tumuamua kuwa mabepari bila kutamka hadharani, serikali inabidi itengeneze paying scheme upya, tuwape fedha wananchi kama inavyostahili, hii ihusishe candles zote! At the same time kwa uchumi imara, defenetly inflation itakuwa at the reasonable pace, ndo tuje tuone kama kweli hao "watunge Sheria" ndo wanastahuili ongezeko wenyewe!!

Bila haya yote hii hoja ni null and void mkuu!!! Hizo hosteli hao hao wabunge ndo hawazitaki kwa maslahi yao wenyewe!! FYI, hao unaowatetea, ndo wanajazana kwenye zile za TZS 15,000 to 30,000!! Kuwalipa hela wapiga kura hii si hoja mkuu...hiyo ni hongo yao kwao!!
 
Bunge la waganga njaa ndo kila siku litadai posho ya zaidi. Hao wanaoandaa hizo sheria pale AG chamber wanalipwa sh. ngapi? Graduate unamlipa laki nne Majimarefu mtunga sheria umpa mil 7. Fair distribution ndo muhimu. Halafu hii biashara ya kugawa hela kwa wapiga kura mi siielewi, hili si jukumu la mbunge ni mfumo wa rushwa huu ili uchaguliwe tena so sisi hatupaswi kuchangia miradi ya rushwa. Mi hushangaa sana hili. Mbunge mgawa rushwa? Fanya fundi raising toa general suport kama shule nk ukianza kuhonga individuals basi, ni wabunge wangapi waliokuwa wanawapa watu wao pesa kabla ya ubunge? wabunge wengi nafikiri hawajayajua majukumu yao.
 
- Wabunge ni tofauti sana na hao wengine, WAO NI WATUNGA SHERIA! sasa mwenye kutaka sheria mbovu kwa wananchi akiwapa rushwa na kutupitishia sheria mbovu kwa taifa utasema ni sawa na wengine serikalini?


William.
hili huwa linaniumiza sana akili yangu, labda leo unaweza kuniweka sawa kidogo. kama ulivyosema wabunge kazi yao ni kutunga sheria. na nataka kuamini kuwa wanalipwa mishahara kwa kufanya hiyo kazi ya kutunga sheria. hizo sheria naamini kabisa wanazitunga wanapokuwa bungeni, yaani vikao vya bunge ni sehemu pekee naamini kuwa wanafanya kazi ambayo wamechaguliwa/wameteuliwa kuifanya.
sipati picha mtu kama mwalimu, kaajiriwa kufundisha, analipwa mshahara kwa kufundisha, lakini kila akiingia darasani kufundisha adai kulipwa posho. hii hesabu kwa kweli hainiingii kabisa akilini, yaani wanavyodai kupandishiwa posho ndo wananichanganya kabisaaaaaaaaaaaaaaaa, sijui kama nitafaulu
 
- People, by the way ukiona sikujibu hoja ujue haina mashiko, so naipotezea! ha! ha! ha! ha!

William.
Umeambiwa ukweli. Ukweli umekuuma. Unasema hoja haina mashiko. Huna jibu. Utaniambia ni vema Matonya aendelee kuwa maskini.
 
Hapa tunasumbuliwa na watu walioshiba hela na kulelewa na mfumo wa kifisadi.

Ni lazima tupambane kuuondoa huu mfumo. Willy Malechela, Hussein Mwinyi, Nape Nauye, January Makamba, Adam Malima, David Mathayo Msuya, etc.

Kwa ujumla usitegemee kipya ambacho haujakiona kutoka kwa wazazi wao. Ni kubadili sura tu lakini mfumo wa kinyonyaji na udhalilishaji wa wanyonge upo pale pale.
 
- Wabunge ni tofauti sana na hao wengine, WAO NI WATUNGA SHERIA! sasa mwenye kutaka sheria mbovu kwa wananchi akiwapa rushwa na kutupitishia sheria mbovu kwa taifa utasema ni sawa na wengine serikalini?


William.

Mkuu, SALUTE.

Naomba ukumbuke kuwa hii tabia ya differential rates depending on where you work ndio iliyotufikisha hapa. Kila mtu kula urefu wa kamba yake. Bank kuu mhudumu kulipwa zaidi ya nurse (ukija kujifungua utaipata), mwalimu (utaleta mtoto, utaipata), etc.

Tanzania ni yetu wote, na kila mtu ana mahitaji kama mwingine, na anachofanya kina umuhimu wake (Gabbage collectors wakigoma ndipo utakapojua umuhimu wao).

Professor analipwa TShs 80,000 (statutory night allowance) bila sitting au fuel allowance. Kama yeye mnaona inatosha, kwa nini isiwatoshe wabunge wanaolipwa sitting allowance na fuel allowance!

Ungefahamu kuwa wengi wetu hatupingi kuwa maisha hayajapanda, tunapinga wao kujiongezea wenyewe ilhali wote tuna maisha magumu.
 
Vizuri sana mkuu. Kumbe mwanzoni ulikuwa ukitoa maoni bila kujua hali halisi ikoje! Sasa hili ni funzo kuwa watu wawe wanatoa maoni yao kwa kuelewa hali halisi inayowahusu watu wa site. Kwa maana hiyo kuna mengi ulikuwa huelewi hadi uliporudi nyumbani na kabla hujaelewa vizuri ukajitosa kugombea Ubunge wa Afrika Mashariki. Nadhani umejifunza utakaa na kuelewa hali halisi ya watu, uchumi na siasa kabla hujajitosa tena kugombea. Hii itakupa fursa nzuri ya kuwatumikia watu kama utafanikiwa kwa kuwa utakuwa umejua shida na matatizo yao na matatizo ya nchi kwa ujumla.

Huyu kashituka baada ya kuona mbunge wa Afrika mashariki anakamata pesa ndefu na kujiona kumbe alikosea kutoanza kampeni miaka minne iliyopita.

Hii ni moja ya kampeni za ubunge wa Afrika mashariki. Lakini pia amenusa harufu ya uchaguzi kurudiwa kutokana na kesi iliyofunguliwa na KOMU kutaka uchaguzi urudiwe. Nafikiri huu ndiyo msingi mkuu wa post yake and nothing short of that.

Kama ingekuwa mbunge anaishi kwa posho tu ningeona hoja yake ina maana sana, lakini mbunge analipwa mshahara Tzs 7m pm as a full time employee. ukiugawa mshahara huo kwa siku 30 utakuta kuwa ni sawa na Tzs 233,333 kwa siku. Suala la nani kaja kukutembelea na wewe unataka kumpatia nini kutoka kwenye hela, hiyo si kazi ya mbunge. Kazi ya mbunge si kugawa mapesa kwa wananchi wa jimbo lake bali ni kuwawakilisha. Kugawa mapesa ni private issue, tukianza kuendekeza huu utamaduni basi siku zijazo watadai na hela za kuwalipa madada poa na nyumba ndogo zao.

William big up kwa strategy ya kujiandaa na marudio ya uchaguzi wa ubunge EA kama mahakama itaridhia. Ila ujifunze kutumia jukwaa ( I mean talking mbele ya umati wa watu) ili kuongeza confidence kwenye presentations zako bungeni wakati wa uchaguzi ujao.
 
Ok bwana WJSM umejifunza kitu hapa kwamba "No research; No right to speak" na hata hivyo wewe swala hili uliliangalia kutokana na angle ya "per diem vs prices index" pekee!! wenzio pamoja na hilo tulikuwa tunapinga wabunge kuongezewa posho kwa sababu serikali "must cut its cloth according to its size"; au vipi?! hii tabia ya serikali kwa maana ya tume ya uchaguzi kubomoa majimbo na kugawagawa vijimbo kama zawadi for political expediency; bila kuzingatia uwiano wa kibajeti na mazingira halisi ya mji kama Idodomya ambao ni mji mdogo sana kuweza kuhudumia watu wazito kama wabunge; kwa hiyo wafanya biashara nao wanakuwa expedient! kwa sababu dodoma bila vikao vya bunge is a jua kali town au machinga capital; kutokana na ufinyu huo wa soko wafanyabiashara wakubwa hawawezi kuwekeza katika mahoteli makubwa zaidi ili kutengeneza mazingira ya ushindani ambayo yangesababisha bei ya malazi kushuka, thus wafanya biashara wana capitalize kweye amri moja ya soko huria ya "supply and demand" na hivyo kusababisha huduma ya malazi mjini Dodoma kuwa juu kiasi hicho; utitiri wa wabunge pale kwa vipindi vifupi vifupi huwa ni "high season" yaani kipindi cha neema kwa watoa huduma, you can not blame them; can you?!
That said hakuna sababu ya kuwaburden zaidi walipa kodi maskini, serikali ione aibu kwamba tangu uamuzi wa kuhamishia makao makuu ya serikali dodoma mwaka 1974 hadi leo bado serikali ya awamu ya nne haiwezi kuaccomodate its own legislators, hata kujenga nyumba nyingi zaidi za kuwapangishia wabunge wake wakati wa vikao vya bunge!! kwa nini udhaifu wa serikali waadhibiwe walipa kodi hawa maskini wanaosulubika na bei ya chumvi, kiberiti, sukari nk nk.
Nifupishe hadithi kwa kusema Serikali iache kuongeza utitiri wa wabunge kwa kutoa vijimbo vya uchaguzi kama zawadi pasipo kuangalia TIJA inayotokana na representation kubwa kiasi hicho at the expense of the poor tax payers! kwa wengi wao DODOMA = KUCHUMIA TUMBO; ziara zisizokwisha nje ya bunge wakati wa vikao, kulala usingizi ndani wa vikao, mnadani kwenye mbuzi kwa saaaana! zomea zomea isiyo na msingi hata kama hoja inayotolewa inastahili kufikiri angalau kidogo! praise singers ndio wengi na wale wanaojaza hesabu ili wapiga kura kule nyumbani wawaone kwamba walihudhuria bungeni!! sawa hiyo?!
 
- Wabunge ni tofauti sana na hao wengine, WAO NI WATUNGA SHERIA! sasa mwenye kutaka sheria mbovu kwa wananchi akiwapa rushwa na kutupitishia sheria mbovu kwa taifa utasema ni sawa na wengine serikalini?


William.

Kiongozi(Mbunge) anayeweza kuhongwa ili atoe maamuzi mabovu au atunge sheria mbovu za kuwaumiza wapiga kura wake ili kumfurahisha mtoa rushwa huyo hatufai. Huyu ndie anayepigania kuongezewa posho bila kujali kwamba kuna kada zingine za wafanyakazi wanaofanya kazi muhimu zaidi lakini kwenye mazingira magumu.Tazama watu kama walimu,madaktari/manesi, polisi wanaofanya kazi hizi nyeti lakini kwa malipo duni kuliko wabunge wengi(sio wote) wanashindana kukoroma wakiwa ndani ya bunge. Maisha ni magumu kwa kila mfanyakazi na wewe ungefanya kitu kizuri kwa kuwatetea wafanyakazi wote,sio WABUNGE tu.
 
Umeambiwa ukweli. Ukweli umekuuma. Unasema hoja haina mashiko. Huna jibu. Utaniambia ni vema Matonya aendelee kuwa maskini.

Hawa wazembe wa kuwaza kam WSJM ndio baadae wanakuja kuwa viongozi wenu
 
- Mimi nimeongelea Wabunge niliowaona tayari na wewe ongelea hao uliowaona, hii hoja ya posho za wabunge inajadilika bro, kama sio leo itakwua kesho tena ikiwa very ugly, badala ya kuwapa 200, 000 tutaishia kuwapa zaidi ha hizo!

- Mengina huwa ninaita kelele za mlango!


William.

Hizo kelele za mlango utazisikia vizuri 2015, Watanzania wanaenda mbele nyie magamba mnaenda walikotoka, Mbunge mwenye akili timamu au Chama makini kilichopo bungeni asilani hakitasikika tena kikiongelea habari ya posho labda baada ya 2015, yeyote atakayedai posho katika kipindi hiki kigumu basi ajue anajitupia kitanzi shingoni, Hii thread yako pekee tayari utaibeba kila mahali utakapoonekana kutaka kura za wanainchi,
 
Kiongozi(Mbunge) anayeweza kuhongwa ili atoe maamuzi mabovu au atunge sheria mbovu za kuwaumiza wapiga kura wake ili kumfurahisha mtoa rushwa huyo hatufai. Huyu ndie anayepigania kuongezewa posho bila kujali kwamba kuna kada zingine za wafanyakazi wanaofanya kazi muhimu zaidi lakini kwenye mazingira magumu.Tazama watu kama walimu,madaktari/manesi, polisi wanaofanya kazi hizi nyeti lakini kwa malipo duni kuliko wabunge wengi(sio wote) wanashindana kukoroma wakiwa ndani ya bunge. Maisha ni magumu kwa kila mfanyakazi na wewe ungefanya kitu kizuri kwa kuwatetea wafanyakazi wote,sio WABUNGE tu.

- Europe ukishitakiwa na kesi ya rape, jaji huwa anataka kujua jinsi victim alivyokuwa amevaa kwanza, kama hakuvaa inavyotakiwa unaanchiwa kwamba aliyataka, sasa mbunge akipewa rushwa inatakiwa tujiulize mazingara yakoje?

William.
 
Hizo kelele za mlango utazisikia vizuri 2015, Watanzania wanaenda mbele nyie magamba mnaenda walikotoka, Mbunge mwenye akili timamu au Chama makini kilichopo bungeni asilani hakitasikika tena kikiongelea habari ya posho labda baada ya 2015, yeyote atakayedai posho katika kipindi hiki kigumu basi ajue anajitupia kitanzi shingoni, Hii thread yako pekee tayari utaibeba kila mahali utakapoonekana kutaka kura za wanainchi,

- Wewe wacha uoga uoga kama fisi, hivi kwa nini mnaogopa ogopa sana ukisema hoja lazima ujue kuisimamia, ninasema hivi hoja ya posho ya wabunge tunaweza kuwa tumei-delay tu, lakini it is coming back haiendi kokote, maana maisha ya wabunge wengi Dodoma sio sawa!

- Kumbuka tulikoanzia na Muungano, katiba, mgombea binafsi, mwaka 1995 Mwalimu alimsahuri Salmin kuungana na CUF kutawala wengi walishangaa kuwa vipi Mwalimu look now, hii hoja ijadilike sasa kama na wengine wanahitaji kuongezewa ijadiliwe, mimi nimeamua kujadili ya wabunge wka leo!

Willaim.
 
Nichofahamu hizo shilingi 70,000/- ni sitting allowance. Pesa ya accommodation, chakula na nauli wanapewa pia kila siku. Ndio maana hoja ni kuwa kwani nini wapewe pesa ya kukalia kiti wakati ni sehemu ya kazi zao za kawaida ili wapate mishahara yao ya kila mwezi?
 
kwani hizo special hostel kwa tanzania zinashindikana kujengeka???,

so far, hiyo posho inayotolewa inatosha kuwa-acommodate hao wabunge; mbona watumishi wengine wa serikali wanaajiriwa na kupangiwa vituo vyao vya kazi ma-wilayani na mikoani ambao hakuna nyumba za kuhishi na wala posho za nyumba hawapewi lakini wanafanya kazi?????

Ambaye hataki ubunge aache hakuna aliyemlazimisha.

undoubtedly true!
 
- Watunga sheria ni muhimu sana kuliko wengine wote kwenye taifa, ndio maana China inasonga mbele kwa sababu wanalijua hilo na wanlijali sana kuliko yote, wanahakikisha wabunge wao hawapo kwenye mazingara ya kwua wazi kwa rushwa ndio maan wakiwashika kunakuwa hakuna excuse, maana walishawatengenezea mazingara bora dawa ni Risasi tu!

- Na sisi tujifunze, hii hoja ijadilike sasa, sio lazima posho iwe laki mbili, lakini something must be done now!

William.


Hapo kwenye bold - kwani Wachina wanapiga risasi Wabunge mafisadi au mwananchi yoyote wa China??? Usijaribu kulinganisha China na Tanzania tafadhali ............China inasonga mbele sio issue ya posho nzuri kwa wabunge ila HAKUNA UFUJAJI/WIZI WA FEDHA/MALI YA UMMA

Jamani mbona thread yako inaumiza moyo wangu????? please ukitoka huko Dodoma unapowatetea Wabunge wapewe posho kubwa ..........Tembelea vijiji vya Tanzania........... uone jinsi shule zilivyo ....mwalimu mmoja anafundisha watoto shule nzima.........hao watoto si ndio wengine watakuwa Wabunge wa Kesho???? Watetee hao achana na hawa ambao soon wanakuwa -phased out .......... SHERIA WANAMTUNGIA NANI WAKATI WATANZANIA WENGI TUKO HOI BIN TAABANI...............please dont hurt our feelings ............kwani naona UNAFANYA KUSUDI .... MUNGU AKUSAMEHE KWANI SISI TUMEKUSAMEHE BURE
 
- Unajua itatuchukua muda mrefu sana kwa mataifa masikini kujifunza kutoka kwa wachina, wao kila sheria zao zinajali mazingara yao zaidi kuliko siasa za kimtaifa, nimetoa hoja kutokana na niliyoyaona na ni kawaida yetu sisi waafrika kwa wananchi kuwafuata wabunge Dodoma kwenye kikao kuwaomba misaada!

- Sasa yes, inapotaka kutatua tatizo la posho za wabunge lazima uliangalie hilo cause ni reality, Wabunge wetu pesa tunazo walipa atleast nusu zinaishia kwenye mikono ya wananchi wa majimbo yao, hiyo ni FACT, lakini mimi naongelea niliyoyaona Dodoma as a reality, sio hadithi za mtaani!

William.

Nimekuwa nikijiuliza hivi karibuni nini hasa nia yako katika siasa. Nitakosa majibu lakini unapaswa kutafakari mambo mengi sana. Nisaidie haya:

a) Unaweza kuthibitisha kuwa wabunge, pamoja na kuombwa, wanatoa hizo fedha kwa wananchi? Ni kiasi gani cha pato lao? Je hata wakijengewa hiyo hostel, ndio kusema misaada yao itaongezeka kwa wananchi? Kwa kiasi gani??

b) Si sahihi kudhani mbunge anapaswa kuhudumiwa kwa kuwa ni mtunga sheria. Haki ya kuhudumiwa itokane na mahitaji yake ya kibinadamu na uwezo wa wanaolipia huduma hizo. Wabunge tayari wanalipiwa mafuta, wana mikopo ya magari bila hata uthibitisho wa ununuzi wa magari hayo!! Mawaziri, wakurugenzi na wakuu wa idara wana VX V8, wananunuliwa samani za nyumba zisizosimamiwa, wanapewa nyumba na kulipiwa umeme!! Nchi jirani ya Kenya, wakuu wa Idara bado wana Toyota Hilux kama si magari yao wenyewe. Waziri anatumia VW Passat!!! Huenda nia yako ni kupata maisha ya kifahari kupitia siasa!!
 
Hili gari pia haliko katika hadhi ya Mbunge, inabidi aongezewe hela akanunue lingine. (Kwa kuzingatia akili yako Willy)
IMG_4986.JPG
 
Back
Top Bottom