Porojo za Wassira kuhusu Dr. Slaa

Ngereja

JF-Expert Member
Feb 27, 2007
798
333
[Mods: Hii mnaweza kuiacha apa ijitegemee kama mtaona inafaa, mimi nadhani inafaa ibaki peke yake]

Katika uchaguzi wa 2010 kuliibuka tuhuma mbalimbali kuhusiana na hasa kwa nini Dr. Slaa ameacha upadri. Ninakumbuka Dr. Slaa alijibu hoja zote hizo kuhusiana na jinsi alivyoacha upadri, na hata kuna kipindi cha TV ambacho alielezea hoja hiyo. Hivyo, kuirudia na kuishikia bango kunakofanywa na Wassira ni kugiribu akili za watanzania waache kufikiria mambo ya maana kwenye uchaguzi wa Arumeru.

Baadhi ya majibu ya Dr. Slaa kuhusu hoha hiyo ni haya yafuatayo:

"BC: Tukiwa hapo hapo kwenye suala la historia yako.Wengi tunatambua kwamba siku za nyuma kabla hujaingia kwenye siasa ulikuwa padre au ulisomea upadre. Unaweza kutueleza kwanini uliacha upadri na kuwa mwanasiasa? Ulifukuzwa au uliacha kwa hiari? Una mke na watoto. Je, kanisa lilikuruhusu kuoa?


WS
: Ni kweli nimekuwa Padre wa Kanisa Katoliki. Nimekuwa kiongozi wa ngazi ya juu sana ndani ya Kanisa kuanzia Jimboni kwangu ambapo nimekuwa Makamu wa Askofu, na Mkurugenzi wa Maendeleo, lakini pia nimekuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu toka 1985 hadi 1991. Ni kweli hayo maswali yanaulizwa mara nyingi, kwa bahati mbaya si wengi wanaofahamu taratibu za kisheria ndani ya Kanisa Katoliki. Niliondoka mimi mwenyewe katika Upadre bila kushinikizwa na yeyote, wala kufukuzwa, wala hata kupewa onyo. Ni kweli kuna mambo ambayo mimi niliyakataa na kwa dhamira yangu nisingeliweza kuendelea, lakini nadhani hayo ni binafsi zaidi, na si mahali pake kuyaeleza. Nimetoka kwa kibali cha Kanisa, kwa utaratibu wa kisheria wa Kanisa Katoliki, ndiyo maana mimi sina tatizo wala ugomvi wa aina yeyote na Kanisa Katoliki na ninashiriki katika shughuli mbalimbali za Kanisa.


Nina Mke na watoto wawili, Emiliana Slaa na Linus Slaa, japo sijafunga ndoa kikanisa kwa utaratibu wa kawaida wa Kanisa Katoliki, pamoja na kuwa sina kipingamizi chochote kufanya hivyo kikanisa, ni uamuzi wangu na wa mke wangu na familia yetu."


Tembelea hapa kwa mahojiano zaidi: Friends of Slaa | FOS |: Huyu Ndio Dr.Willibrod Peter Slaa
 
Mke ambae hamjafunga ndoa?

Sababu za kibinafsi?

Kwi kwi kwi teh teh teh!

Josephine ana watoto wawili wa Slaa? kwi kwi teh teh teh! hiyo talaka alipewa lini, kaolewa tena lini? kazaa tena watoto wawili lini?
 
Mke ambae hamjafunga ndoa?

Sababu za kibinafsi?

Kwi kwi kwi teh teh teh!

Josephine ana watoto wawili wa Slaa? kwi kwi teh teh teh! hiyo talaka alipewa lini, kaolewa tena lini? kazaa tena watoto wawili lini?

Hivi kuna aina ngapi ya NDOA? Nenda darasani mama, tena kidato cha pili civics. Yaani akili yako ni sawa na std7.
 
Mke ambae hamjafunga ndoa?

Sababu za kibinafsi?

Kwi kwi kwi teh teh teh!

Josephine ana watoto wawili wa Slaa? kwi kwi teh teh teh! hiyo talaka alipewa lini, kaolewa tena lini? kazaa tena watoto wawili lini?


Mkuu usikurupuke, jaribu kujisomea na upate habari iliyokamilika.Unajua kuwa Josephine ni mwanamke wa pili kuzaa na Dr!.
 
Hivi kuna aina ngapi ya NDOA? Nenda darasani mama, tena kidato cha pili civics. Yaani akili yako ni sawa na std7.

Umenisaidia Ngoiva..ilikua nimrushie kombora la mavi usoni..bahati yake!! watu hata elimu ya uraia hawaifahamu af anajichekesha hapa kama shemeji yake mbayuwayu la msoga..Mpssxxyyy
 
Nashukuru majibu yanajitosheleza vipi mke wa kwanza wa dr yuko wapi kwa sasa kama ni marehemu tafadhalini naomba mnijulishe kwa heshima tafadhali
 
Mke ambae hamjafunga ndoa?

Sababu za kibinafsi?

Kwi kwi kwi teh teh teh!

Josephine ana watoto wawili wa Slaa? kwi kwi teh teh teh! hiyo talaka alipewa lini, kaolewa tena lini? kazaa tena watoto wawili lini?

Kesi ya Josephine kudai talaka kwa mme wake mzee Mahimbo iko mahakama ya mwanzo Manzese na bado haijaisha Mahimbo hataki kumpa talaka mkewe Josephine kwa kuwa bado anampenda.
 
Mke ambae hamjafunga ndoa?

Sababu za kibinafsi?

Kwi kwi kwi teh teh teh!

Josephine ana watoto wawili wa Slaa? kwi kwi teh teh teh! hiyo talaka alipewa lini, kaolewa tena lini? kazaa tena watoto wawili lini?


Upungufu wa akili huanza kujionesha pale mtu anapoongea kuhusu jambo lolote; tumekusoma.
 
Hivi kuna aina ngapi ya NDOA? Nenda darasani mama, tena kidato cha pili civics. Yaani akili yako ni sawa na std7.

Ndoa yao ni ya uamuzi wake, mkewe na watoto wao kwa pamoja walilidhia kushia bila ndoa ya kanisani wala ya kimila. Sijawahi kuona kama hii ni moja ya aina za ndoa. Inawezekana unajua zaidi...tujuze aina za ndoa kama ulivyosoma wewe ili tuone hii ya DR wa ukweli ni ya aina gani.
 
Mke ambae hamjafunga ndoa?

Sababu za kibinafsi?

Kwi kwi kwi teh teh teh!

Josephine ana watoto wawili wa Slaa? kwi kwi teh teh teh! hiyo talaka alipewa lini, kaolewa tena lini? kazaa tena watoto wawili lini?

****........
 
Hivi kuna aina ngapi ya NDOA? Nenda darasani mama, tena kidato cha pili civics. Yaani akili yako ni sawa na std7.

Si unaona hata location yake aliko.....unategemea akili na namna gani hapo??
 
Kesi ya Josephine kudai talaka kwa mme wake mzee Mahimbo iko mahakama ya mwanzo Manzese na bado haijaisha Mahimbo hataki kumpa talaka mkewe Josephine kwa kuwa bado anampenda.

Mbaya!!! Kupenda usipopendwa?? Hovyo.....
 
Hivi huyu Wasira ana ndoa na mjane wa marehemu Ndege? Swali jengine, jee walipima ngoma kabla ya kuanza kuishi pamoja?
 
Ni sawa kwa Dr. kwani msomi ni mtu huru na si mfungwa. Anaweza kufanya hayo kwa uelewa wake mpana , ila angalizo tu ni kuangalia taswira anayoitoa kwa jamii, kwani jamii inajifunza kwake. Watanzania wengi kiwango chao cha elimu na uelewa si kikubwa hivyo.
 
wana jf mnapoteza muda bure wasira is not interested in facts hata ukimuwekea usoni, hizi ni siasa tu,
 
Hivi huyu Wasira ana ndoa na mjane wa marehemu Ndege? Swali jengine, jee walipima ngoma kabla ya kuanza kuishi pamoja?

Kweli wafu wanazidiana kunuka HATA Wassira naye anamcheka Slaa huku yeye KAOLEWA Kunduchi beach kwenye nyumba ya Mzee Ndege, huku mkewe akilalamika kukaa bila Mume, Jamani huyu Tyson Muogopesha Watoto vipi? aka Nyan.... Mzee
 
Another discusion isiyo na tija kwa taifa hili!!

Viongozi wa ccm na wafuasi wao, majority ni makenge maji!
Nchii hii ni ombaomba, uchumi kichefuchefu, hali ya maisha inasikitisha!
Lakini ccm wapo mbele wanaongelea mtu na mkewe, wanaongelea Slaa anamvua nani chupi, wanaongelea ndoa ya mtu!!!

Ridiculous!!
Wasira is a biological error!!!
 
Back
Top Bottom