[Mods: Hii mnaweza kuiacha apa ijitegemee kama mtaona inafaa, mimi nadhani inafaa ibaki peke yake]
Katika uchaguzi wa 2010 kuliibuka tuhuma mbalimbali kuhusiana na hasa kwa nini Dr. Slaa ameacha upadri. Ninakumbuka Dr. Slaa alijibu hoja zote hizo kuhusiana na jinsi alivyoacha upadri, na hata kuna kipindi cha TV ambacho alielezea hoja hiyo. Hivyo, kuirudia na kuishikia bango kunakofanywa na Wassira ni kugiribu akili za watanzania waache kufikiria mambo ya maana kwenye uchaguzi wa Arumeru.
Baadhi ya majibu ya Dr. Slaa kuhusu hoha hiyo ni haya yafuatayo:
"BC: Tukiwa hapo hapo kwenye suala la historia yako.Wengi tunatambua kwamba siku za nyuma kabla hujaingia kwenye siasa ulikuwa padre au ulisomea upadre. Unaweza kutueleza kwanini uliacha upadri na kuwa mwanasiasa? Ulifukuzwa au uliacha kwa hiari? Una mke na watoto. Je, kanisa lilikuruhusu kuoa?
WS: Ni kweli nimekuwa Padre wa Kanisa Katoliki. Nimekuwa kiongozi wa ngazi ya juu sana ndani ya Kanisa kuanzia Jimboni kwangu ambapo nimekuwa Makamu wa Askofu, na Mkurugenzi wa Maendeleo, lakini pia nimekuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu toka 1985 hadi 1991. Ni kweli hayo maswali yanaulizwa mara nyingi, kwa bahati mbaya si wengi wanaofahamu taratibu za kisheria ndani ya Kanisa Katoliki. Niliondoka mimi mwenyewe katika Upadre bila kushinikizwa na yeyote, wala kufukuzwa, wala hata kupewa onyo. Ni kweli kuna mambo ambayo mimi niliyakataa na kwa dhamira yangu nisingeliweza kuendelea, lakini nadhani hayo ni binafsi zaidi, na si mahali pake kuyaeleza. Nimetoka kwa kibali cha Kanisa, kwa utaratibu wa kisheria wa Kanisa Katoliki, ndiyo maana mimi sina tatizo wala ugomvi wa aina yeyote na Kanisa Katoliki na ninashiriki katika shughuli mbalimbali za Kanisa.
Nina Mke na watoto wawili, Emiliana Slaa na Linus Slaa, japo sijafunga ndoa kikanisa kwa utaratibu wa kawaida wa Kanisa Katoliki, pamoja na kuwa sina kipingamizi chochote kufanya hivyo kikanisa, ni uamuzi wangu na wa mke wangu na familia yetu."
Tembelea hapa kwa mahojiano zaidi: Friends of Slaa | FOS |: Huyu Ndio Dr.Willibrod Peter Slaa
Katika uchaguzi wa 2010 kuliibuka tuhuma mbalimbali kuhusiana na hasa kwa nini Dr. Slaa ameacha upadri. Ninakumbuka Dr. Slaa alijibu hoja zote hizo kuhusiana na jinsi alivyoacha upadri, na hata kuna kipindi cha TV ambacho alielezea hoja hiyo. Hivyo, kuirudia na kuishikia bango kunakofanywa na Wassira ni kugiribu akili za watanzania waache kufikiria mambo ya maana kwenye uchaguzi wa Arumeru.
Baadhi ya majibu ya Dr. Slaa kuhusu hoha hiyo ni haya yafuatayo:
"BC: Tukiwa hapo hapo kwenye suala la historia yako.Wengi tunatambua kwamba siku za nyuma kabla hujaingia kwenye siasa ulikuwa padre au ulisomea upadre. Unaweza kutueleza kwanini uliacha upadri na kuwa mwanasiasa? Ulifukuzwa au uliacha kwa hiari? Una mke na watoto. Je, kanisa lilikuruhusu kuoa?
WS: Ni kweli nimekuwa Padre wa Kanisa Katoliki. Nimekuwa kiongozi wa ngazi ya juu sana ndani ya Kanisa kuanzia Jimboni kwangu ambapo nimekuwa Makamu wa Askofu, na Mkurugenzi wa Maendeleo, lakini pia nimekuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu toka 1985 hadi 1991. Ni kweli hayo maswali yanaulizwa mara nyingi, kwa bahati mbaya si wengi wanaofahamu taratibu za kisheria ndani ya Kanisa Katoliki. Niliondoka mimi mwenyewe katika Upadre bila kushinikizwa na yeyote, wala kufukuzwa, wala hata kupewa onyo. Ni kweli kuna mambo ambayo mimi niliyakataa na kwa dhamira yangu nisingeliweza kuendelea, lakini nadhani hayo ni binafsi zaidi, na si mahali pake kuyaeleza. Nimetoka kwa kibali cha Kanisa, kwa utaratibu wa kisheria wa Kanisa Katoliki, ndiyo maana mimi sina tatizo wala ugomvi wa aina yeyote na Kanisa Katoliki na ninashiriki katika shughuli mbalimbali za Kanisa.
Nina Mke na watoto wawili, Emiliana Slaa na Linus Slaa, japo sijafunga ndoa kikanisa kwa utaratibu wa kawaida wa Kanisa Katoliki, pamoja na kuwa sina kipingamizi chochote kufanya hivyo kikanisa, ni uamuzi wangu na wa mke wangu na familia yetu."
Tembelea hapa kwa mahojiano zaidi: Friends of Slaa | FOS |: Huyu Ndio Dr.Willibrod Peter Slaa