engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,150
- 1,437
Ndugu wana JF,nimefurahishwa sana na kauli ya Mh.E.Lowasa juu ya vyombo vyetu vya habari hapa Tanzania kuhusu kutumia mda mwingi ktk kuzungumzia mambo yasiyo na msingi na kuacha mambo ya msingi yakiambaa na njia,
kwa kweli nampongeza kwa kuwaambia ukweli mtupu kwani ukilinganisha na nchi za wenzetu vyombo vyetu vya habari vimebakia kupiga propaganda ili mradi mkono uende kinywani,
MH.E.Lowasa anasema
"Ndugu wanahabari nazungumza nanyi baada ya kurejea nikitokea katika nchi za Nigeria, Malaysia, Singapore, India, Uingereza, Ufaransa na Ujerumani ambako nilipata fursa ya kujifunza mambo mengi lakini moja muhimu likiwa ni
vyombo vya habari (kwa maana ya waandishi wa habari) na wanasiasa wanavyotumia muda wao mwingi kujadili masuala yanayogusa maisha na maendeleo ya watu wao.
Tofauti na kile wanachofanya wenzetu hapa nyumbani, ninyi wanahabari na sisi wanasiasa tumekuwa tukitumia muda wetu mwingi kujadili watu na propaganda za kisiasa zisizo na tija wakati tukitambua kwamba, taifa linakabiliwa na changamoto nyingi kama zile za kuhamasisha uwezekazji wa ndani na nje ya nchi, kuimarisha mifumo ya utawala bora, kuporomka kwa thamani ya shilingi kila kukicha, mdororo wa uchumi, tatizo kubwa la ajira kwa vijana, kushuka kwa kiwango cha elimu na ugumu wa maisha kwa ujumla. TUNAPASWA KUJISAHIHISHA."
source: Wavuti - Habari"
kwa kweli nampongeza kwa kuwaambia ukweli mtupu kwani ukilinganisha na nchi za wenzetu vyombo vyetu vya habari vimebakia kupiga propaganda ili mradi mkono uende kinywani,
MH.E.Lowasa anasema
"Ndugu wanahabari nazungumza nanyi baada ya kurejea nikitokea katika nchi za Nigeria, Malaysia, Singapore, India, Uingereza, Ufaransa na Ujerumani ambako nilipata fursa ya kujifunza mambo mengi lakini moja muhimu likiwa ni
vyombo vya habari (kwa maana ya waandishi wa habari) na wanasiasa wanavyotumia muda wao mwingi kujadili masuala yanayogusa maisha na maendeleo ya watu wao.
Tofauti na kile wanachofanya wenzetu hapa nyumbani, ninyi wanahabari na sisi wanasiasa tumekuwa tukitumia muda wetu mwingi kujadili watu na propaganda za kisiasa zisizo na tija wakati tukitambua kwamba, taifa linakabiliwa na changamoto nyingi kama zile za kuhamasisha uwezekazji wa ndani na nje ya nchi, kuimarisha mifumo ya utawala bora, kuporomka kwa thamani ya shilingi kila kukicha, mdororo wa uchumi, tatizo kubwa la ajira kwa vijana, kushuka kwa kiwango cha elimu na ugumu wa maisha kwa ujumla. TUNAPASWA KUJISAHIHISHA."
source: Wavuti - Habari"