Pongezi Dr. Kitila Mkumbo

Pongezi Dr. Kitila Mkumbo

Status
Not open for further replies.
Wana Jf nimefurahishwa sana na tabia ya dr kitila mkumbo,nimemfuatilia sana tangu zilipoibuliwa tuhuma dhidi yake pamoja na zitto na samson mwigamba.dr amekuwa katika hali ya utulivu mkubwa kuliko watuhumiwa wenzie.maana baada ya kamati kuu kuwavua nyadhifa zao na kuwapa siku 14 dr amejitokeza mara mbili tu kwenye media kuzungumzia suala hilo.kutokana na sababu hiyo nimeanza kuamini kwamba maneno aliyosema kwenye kamati kuu kwamba aliingizwa tu kwenye mkenge na zitto pamoja na mwigamba ni ya kweli.nasema hivyo kwa sababu ukiangalia baada ya wote wa 3 kurudisha fomu zilizokuwa na mashtaka 11 dr mkumbo amekuwa kmya akisubiri hatma yake,tofauti na wenzie ambao wameendelea kuhangaika kwa kisngizio cha kupigania haki yao ndani ya chama hata kabla ya chama kutoa hitimisho.zitto kabwe ndio huyo yuko kigoma akiomba huruma ya wananchi,mwigamba ndio huyo katia timu kwa msajili wa vyama.swali linakuja ni kwanini hawa wawili wanatafuta utetezi nje ya chamachao mapema?na kwa nini yy dr mkumbo katulia akisubira maamuzi ya vikao vya chama?je ni kutofautiana kwa viwango vyao vya elimu ndio kulikowatfautisha?hakika dr mkumbo umenikosha sana na ukimya wako hivyo kuthibitisha kwamba hakika ww ni msomi uliye elimika.GUILTY ARE ALWAYS AFRAID.hongera sana dr mkumbo.nawasilisha.
.. No. Kinachomfanya Dr. K kuwa kimya ni kwamba yeye ni mfanya kazi wa serikalini, haruhusiwi kujiunga na vyama vya kisiasa hasa kuwa kiongozi, na ndio maana yeye ametulia, kwa7bu hadi hapobalipofikia keshasimamishwa kuwa kiongozi wa kitivo pale UD, au hulijuwi hilo? Kwahiyo anakuwa mpole ili labda atarudishiwa unga wake. Kawa kiongozi wa chama, alipogundulika akavuliwa uongozi chuoni, alafu hata mmoja anayeenda kumtetea, kwahiyo anaona akijitokeza zaidi asije akamwaga unga na kazi ya kabisa.. Kwahiyo hiyo ndio 7bu ya yy kutulia kuliko wengine. Sio kama hataki ila kazi serikalini na sheria za utumishi wa umma ndio kinamfanya awe hivyo... Sawa we mbulula? ( mi napita tuu sina chama, ni mtazamo tuu)
 
Kaonyesha ustahimilivu na ukomavu wa akili wa hali ya juu. Siyo kama huyu anayepita akibwabwaja kila kukicha na kuandika madudu kule FB kutaka kujionyesha yeye ndio yeye.

Sifa ya kuwa dr ni kufikiri na ndiyo maana kakaa kimya lakin hao wezake fikra zao ni finyu na uchu wa madaraka ndiyo unaowasumbua
 
Ni mchezo wa kuigiza tu, hakuna lolote, mbinu za chadema tumezistukia.
 
Wabongo tujifunzeni kusubiri.naona hili ni tatizo kubwa kwa tulio wengi.
 
Ukimya ni silaha kubwa sana.Kiukweli nilitarajia iwe hivyo kwa Dr Kitila ingawa kuna time alitaka kunistua lakini naona ameamua kutulia na hiyo ndio busara kwa mtu kama yeye.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Achani ushabiki wa watu na vyama vusuvyokua na uelekeo,cdm sio wavumilivu hata kidogo ivi misukosuko ilioukuta ccm km ingeikuta cdm ingekueje? Zito,kitila na mkumbo wote ni wanamapinduzi...
 
Centrehalf
Naamini hujamfuatilia nakushahuri Nenda kwenye facebook wall ya Albert Msando hakika utamkuta huko akiendekeza libeneke la kuwaponda kuwakandia Viongozi wenu.

Nadhani ameamua kutupia madongo kule hakiamini yupo chini ya Wakili.
 
Last edited by a moderator:
I said and I say it again, Zitto ni mzigo mzito.

Mzee wa ngano ninakubaliana na wewe kabisa HUYU JAMAA NI MZIGO KABISA. Na kwa kusema ukweli whatever the case ameishavuruga CDM kwa kiwango fulani. Sijui CDM itatoa wapi nguvu za kumuachia UANACHAMA HUYU MTU!
 
Dr. amenasa kwenye mtego wa Mwigulu,sasa amechafuka na hawezi kuwa tishio kwenye jimbo la Mwigulu 2015.
Very sad maana Chuo nako ameharibikiwa;ataacha kuwa kimya?ni full majuto.

Sent from my BlackBerry 9380 using JamiiForums
 
Mwacheni huyo zitto,atapetape tu! kwanza amekwisharahisisha kazi ya kufukuzwa kwake,katangaza msiba wakati hakuna kifo! akifa litakuwa jambo lililotegemewa na sidhani kama atarudi tena kuwapa story za kufukuzwa kwake mara ya pili! waacheni wauzoee msiba mwenye kulia alie,mwenye kuropoka aropoke lakini ukweli utabaki kuwa kwa sasa hasameheki tena kwani amejidhihirisha wazi kufanya kazi ya ccm! Nakipongeza chama changu kwa kutomjali yani kumpuuza na kuendelea na programu za chama CDM NI MSINGI NA M4C kama kawaida.Dawa ya mpumbafu kama yeye ni kumpuuza tu! MAKAMANDA TUENDELEE KUJENGA CHAMA CHETU KATIKA MSINGI NA ATAJIFIA MWENYEWE TENA KIFO CHA MENDE! Tulioko likizo vijijini tuitumie hii nafasi kueneza sera za chama na kuwaeleza ukweli makamanda wa vijijini jinsi huyu MAMLUKI anavyofanya kazi ya ccm.Mimi nipo magu na kazi hiyo naifanya na baadaye mwaka mpya ntakuwa KEKOMBYO BUNDA ntaendelea kuifanya.WEWE JE? KWA PAMOJA TUTASHINDA.PEOPLE'ZZZZZZZ!!!.....
 
CHADEMA bana wanafurahisha, ukikubaliana na upuuzi wa wakina Lema, Mbowe, Slaa na Josephine unaonekana shujaa, una hekima na msomi. Ukiwapinga kwa ubadhirifu wao na uhafidhina unaonekana msaliti! Zitto ndio main character hapa hao wengine walikuwa wancheza supporting roles tu! usiwafananishe! Zitto has a lot at stake!
agreeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeed
 
Huyu kitila anayepongezwa si alitukana humu humu? Ama kweli akili za kufuata upepo mbaya sana. Back kwa zitto,mumtukane,mumzushie na bado mnataka akae kimya? Hakuna dhambi kubwa kama ya uoga
 
.. No. Kinachomfanya Dr. K kuwa kimya ni kwamba yeye ni mfanya kazi wa serikalini, haruhusiwi kujiunga na vyama vya kisiasa hasa kuwa kiongozi, na ndio maana yeye ametulia, kwa7bu hadi hapobalipofikia keshasimamishwa kuwa kiongozi wa kitivo pale UD, au hulijuwi hilo? Kwahiyo anakuwa mpole ili labda atarudishiwa unga wake. Kawa kiongozi wa chama, alipogundulika akavuliwa uongozi chuoni, alafu hata mmoja anayeenda kumtetea, kwahiyo anaona akijitokeza zaidi asije akamwaga unga na kazi ya kabisa.. Kwahiyo hiyo ndio 7bu ya yy kutulia kuliko wengine. Sio kama hataki ila kazi serikalini na sheria za utumishi wa umma ndio kinamfanya awe hivyo... Sawa we mbulula? ( mi napita tuu sina chama, ni mtazamo tuu)

ahsante kwa mawazo yako mazuri.ila nataka kujua maana ya neno mbulula ni nini?au ndio level yako yakufikiri?au ni daraja la uwezo wako wa kufikiri bwana mkubwa?.
 
Binafsi nampongeza dr. Kitila kwa utulivu wake, tatizo la zitto haeleweki, mara aseme hivi na afanye vile, hakukuwa na haja mapema kwenda kulialia kwa wanakigoma! Kuwaingiza wanakigoma kwenye ugomvi wa zitto na chadema, ili ionekane ni ugomvi wa chadema na wanakigoma sio sawa! Zitto ilitakiwa apambanie uwanachama wake kwenye cc ya chadema na sio kwenda kulialia mwandiga!
wanakigoma ndo waliomfanya afike pale alipo. na hao siku zote ndo wakuwa nao na sio hao akina slaa na mbowe. use common sense. Zitto know what is doing. keep going Zitto.
kitila is doing the same. serikali through chuo ndo wanaomfanya aende choo. na hao ndo wakula nao sahani moja. The same to what mwigamba is doing.
 
We c unajua kibarua chake cha kufundisha kimewekwa kiti moto we ulitaka apige kelele na chadema wakat kazi yake ya msingi ipo shakani
 
wanakigoma ndo waliomfanya afike pale alipo. na hao siku zote ndo wakuwa nao na sio hao akina slaa na mbowe. use common sense. Zitto know what is doing. keep going Zitto.
kitila is doing the same. serikali through chuo ndo wanaomfanya aende choo. na hao ndo wakula nao sahani moja. The same to what mwigamba is doing.
kama ni hivo hakuna haja ya kuwa na taifa, ilitakiwa kila mkoa uende kivyake, let say kila kiongozi akitolewa cheo na serikali au taasisi akienda kulalamika kwao au kushitaki tutakuwa na taifa? Ina maana kina nchimbi waende songea kulialia kwa sababu wamenyang'anywa vyeo vyao? Wanasiasa kama kina zitto ni hatari kwa mshikamano wa taifa letu. Kukubaliana na upuuzi huu ni kuangamiza taifa!
 
Kitila hakuna sehemu amesema ameingizwa mkenge na Zito acha upotoshaji wewe. Tena yeye ndio initiater wa mpango mzima huyo Zito hakuwa anaujua kabisa.
 
Naunga mkono hoja ya ukimya wa Dr. Kitilla ila pia
Kuna ukimya wa aina mbili, ule ukimya wa mtu hana la kusema na ule ukimya wa kuamua tuu kutosema!.

Kuna ukimya wa kusubiria hatima, ila ila kama tayari umeishaijua hatima, huna haja ya kuisubiria kimya!.

Dr. Kitilla anaisubiria hatima!, Zitto anaijua tayari!, wala hausubirii!.

Ila pia kuna kimya kingi chenye mshindo mkuu!.

Pia shishangai kama walivyo kuku, kuna kuku akishikwa kuchinjwa, anatulia tuu anachinjwa kama afanyavyo kondoo!, na kuna kuku akishikwa kuchinjwa, lazima akukuruke!.

Kwenye tuhuma zozote, ukimya ni admission of guilt, Dr. Kitilla alikubali tangu day one, kuwa yeye ndie initiator wa ule waraka na kumshirikisha Mngamba!, hivyo kunyamaza na kusubiria ni halali yake!.

Zitto anasingiziwa!, hatma yake iliishaamuliwa siku nyingi!, alikuwa anatafutiwa sababu tuu!, kwa nini anyamaze?!. Atulie tuu achinjwe kama yule kuku kondoo?!.
Pasco.


umenena vyema mkuu, wenye makengeza ya mapenzi tu ndiyo hawatakubaliana nawe. pia watu wsisahau kuwa kuna kukaa kimya KWA SABABU YA WOGA: kuna watu naturally ni woga regardless of their elimu. la msingi hapa ni kuangalia je, hiko akifanyacho zito ni halali au anakiuka katiba? halafu pia tujiulize mbona yeye zito anatajwa kwenye ziara za slaa na mbowe? hiyo ni halali?
 
Wanaomsapoti Zitto ni vilema wa akili,tena mazuzu wa ukweli,Zitto si zaidi ya cdm kama hawa vilaza wanavyoongea,Maendeleo ya Kilimanjaro Vs. Kigoma.hayapo kichama bali kiwatu zaidi na hatuwezi kudefine maendeleo utopially lazima tuwe na material fact, alichokizungumzia Zitto huko Mwandiga ni kutafuta sympath yenye complexities nyingi za inferios, uzuzu mwingi nalabuk
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom