Mwafrika wa Kike
JF-Expert Member
- Jul 5, 2007
- 5,186
- 56
Kwa mara nyingine tena inabidi niukubali ukweli na kumeza uchungu wa kupoteza nafasi ya kuleta mabadiliko nchini.
Ni kweli kuwa mimi nimeweka wazi hapa kuwa ni mpinzani wa CCM na sitangojea kwa siku ambayo kutakuwa na serikali nyingine ambayo inajali raia wake tofauti na hii ya ccm ambayo inauza nchi kwa wazungu.
Kwa mara nyingine, nakubali kushindwa na mbinu za ushindi wa ccm na hivyo nameza tena kidonge cha uchungu kama nilichomeza mwaka 1995 waliposhindwa Mrema na Seif Shariff kwenye uchaguzi, mwaka 2000 alivyoshindwa Lipumba, na mwaka 2005 wapinzani wengi walivyoshindwa vibaya sana kwenye uchaguzi.
Katika siasa, mafanikio hujengwa na kisha kuendelezwa kwa kushikilia momentum iliyopo. Mwanasiasa au chama cha siasa akipoteza momentum maisha yake kisiasa yanakuwa matatani.
Upinzani Tanzania ulikuwa umepata momentum nzuri sana ya kuleta mabadiliko kwenye sekta ya madini. Zitto aliomba iundwe kamati huru ya bunge ambayo ingekuwa na nguvu zaidi za kupata ukweli na kuleta mabadiliko ya kweli.
Wananchi wengi walikuwa wameanza kukumbwa na momentum hii na wakafanya ambacho kilikuwa hakijafanyika nchini kwa muda mrefu sana - kuzomea viongozi wa ccm.
Kwa uwezo mkubwa sana wa kisiasa, CCM wamechukua hiyo momentum kwa kuunda kamati ambazo hazitafanya chochote katika kile watu wengi Tanzania walitaka kifanyike. Hebu soma haya maneno toka katika tamko la ccm kuhusu kamati ya Kikwete iliyoundwa:
Haya ni maneno ya Chiligati. Kilichoundwa na Kikwete, sio cha kuchunguza yaliyotokea, bali ni kufanya kile ambacho kimefanywa na kamati ya mboma, masha, na zingine nyingi tu--- kupendekeza maoni ambayo rais anaweza kuamua kuyapuuzia kama alivyofanya kwenye kamati zilizopita bila kujali mamilioni yanatumika katika kamati hizo.
Uteuzi wa Zitto kwenye hii kamati, umetoa momentum toka kwa upinzani na mimi nakiri kuwa hapa ccm wameshinda kwa sasa. Ushindi wao wa kwanza ulifikiwa juzi baada ya tarehe 25/11 ambayo iliwekwa kuwa siku ya mwisho (deadline) kwa ccm kushughulikia ufisadi, wizi na yote la sivyo hatua zitachukuliwa kupita bila chochote kutokea.
Kinachoonekana sasa ni mgongano tu ndani ya upinzani na haionyeshi kama kuna chochote kitatokea kwa sasa. Sijui kama Zitto alitegemea hili alivyokubali na kusisitiza kuwa kwenye kamati ambayo haina nguvu yoyote kisheria.
Kwa sasa, nameza kidonge cha maumivu na kukaa chini kujipanga upya kwa ajili ya next strategy. CCM wameshinda kwa sasa na mimi binafsi nawapongeza kwa strategy nzuri. Kwa vile kulialia sio sehemu ya maisha yangu, nitaendelea kusaka kwa nguvu zote hii mikataba ya serikali na kuitunza mpaka siku nitakapohakikisha fisadi wa mwisho akiwekwa Keko.
Hongera ccm kwa ushindi. Endeleeni kuuza nchi tu mwaya kwa vile mnaweza. Kama vile makocha wa timu wanavyopongezana baada ya mechi, na mimi nawapa pongezi kwa hili. Kwa kweli hapa mmecheza.
Tutakutana tena next time tukiwa tumejiandaa vyema.
Ni kweli kuwa mimi nimeweka wazi hapa kuwa ni mpinzani wa CCM na sitangojea kwa siku ambayo kutakuwa na serikali nyingine ambayo inajali raia wake tofauti na hii ya ccm ambayo inauza nchi kwa wazungu.
Kwa mara nyingine, nakubali kushindwa na mbinu za ushindi wa ccm na hivyo nameza tena kidonge cha uchungu kama nilichomeza mwaka 1995 waliposhindwa Mrema na Seif Shariff kwenye uchaguzi, mwaka 2000 alivyoshindwa Lipumba, na mwaka 2005 wapinzani wengi walivyoshindwa vibaya sana kwenye uchaguzi.
Katika siasa, mafanikio hujengwa na kisha kuendelezwa kwa kushikilia momentum iliyopo. Mwanasiasa au chama cha siasa akipoteza momentum maisha yake kisiasa yanakuwa matatani.
Upinzani Tanzania ulikuwa umepata momentum nzuri sana ya kuleta mabadiliko kwenye sekta ya madini. Zitto aliomba iundwe kamati huru ya bunge ambayo ingekuwa na nguvu zaidi za kupata ukweli na kuleta mabadiliko ya kweli.
Wananchi wengi walikuwa wameanza kukumbwa na momentum hii na wakafanya ambacho kilikuwa hakijafanyika nchini kwa muda mrefu sana - kuzomea viongozi wa ccm.
Kwa uwezo mkubwa sana wa kisiasa, CCM wamechukua hiyo momentum kwa kuunda kamati ambazo hazitafanya chochote katika kile watu wengi Tanzania walitaka kifanyike. Hebu soma haya maneno toka katika tamko la ccm kuhusu kamati ya Kikwete iliyoundwa:
"Ni vema ikaeleweka kuwa tume huundwa pale ambapo imethibitika kuwa kuna kosa lililotendeka au athari za wazi zimeonekana kwenye utendaji wa chombo cha serikali, lakini kamati huundwa pale ambapo mwelekeo mpya unahitajika katika utendaji wa chombo cha serikali,
"Tunapenda wananchi waelewe kuwa, alichounda rais ni kamati ya kuangalia upya sera, sheria na mikataba ya uchimbaji madini na si tume ya kuchunguza mikataba ya uchimbaji madini,"
Haya ni maneno ya Chiligati. Kilichoundwa na Kikwete, sio cha kuchunguza yaliyotokea, bali ni kufanya kile ambacho kimefanywa na kamati ya mboma, masha, na zingine nyingi tu--- kupendekeza maoni ambayo rais anaweza kuamua kuyapuuzia kama alivyofanya kwenye kamati zilizopita bila kujali mamilioni yanatumika katika kamati hizo.
Uteuzi wa Zitto kwenye hii kamati, umetoa momentum toka kwa upinzani na mimi nakiri kuwa hapa ccm wameshinda kwa sasa. Ushindi wao wa kwanza ulifikiwa juzi baada ya tarehe 25/11 ambayo iliwekwa kuwa siku ya mwisho (deadline) kwa ccm kushughulikia ufisadi, wizi na yote la sivyo hatua zitachukuliwa kupita bila chochote kutokea.
Kinachoonekana sasa ni mgongano tu ndani ya upinzani na haionyeshi kama kuna chochote kitatokea kwa sasa. Sijui kama Zitto alitegemea hili alivyokubali na kusisitiza kuwa kwenye kamati ambayo haina nguvu yoyote kisheria.
Kwa sasa, nameza kidonge cha maumivu na kukaa chini kujipanga upya kwa ajili ya next strategy. CCM wameshinda kwa sasa na mimi binafsi nawapongeza kwa strategy nzuri. Kwa vile kulialia sio sehemu ya maisha yangu, nitaendelea kusaka kwa nguvu zote hii mikataba ya serikali na kuitunza mpaka siku nitakapohakikisha fisadi wa mwisho akiwekwa Keko.
Hongera ccm kwa ushindi. Endeleeni kuuza nchi tu mwaya kwa vile mnaweza. Kama vile makocha wa timu wanavyopongezana baada ya mechi, na mimi nawapa pongezi kwa hili. Kwa kweli hapa mmecheza.
Tutakutana tena next time tukiwa tumejiandaa vyema.