Hili neno la mfumo kristu limekuwa likitumiwa sana na waislamu kuonyesha kwamba nchi yetu inatawaliwa kikristu kitu ambacho si kweli.Sasa kama nchi hii imejengwa katika mfumo wa kikristu,mbona leo hii kuanzia visiwani mpaka bara watawala wa nchi ni waislamu wote kuanzia rais mpaka makamu wa rais?mnashindwa nini kuifanya nchi iwe ya mfumo islamu iliali kwa sasa inatawaliwa na waislamu?.Nijuavyo mimi nchi yetu tangu uhuru watu wa dini zote wamekuwa wakipewa madaraka,wakati wa Mwl.Nyerere Ndugu Rashid Kawawa alikuwa makamu wa rais na baadae waziri mkuu,najua waislamu wengi huwa wanamlaumu mwl.Nyerere kwa kujenga huo mfumo kristu wa kufikirika,sasa kama kweli Mwl.nyerere alikuwa mdini ni kwa vipi alimuamini Kawawa na kumpa umakamu iliali kulikuwa na wakristo wengi tu wa kushika wadhifa huo?nchi yetu imekuwa na cultural balance tangu uhuru mpaka sasa,hivi wenzetu waislamu hamuoni Kenya na Uganda kuna waislamu lakini sijawahi kuona na wala kusikia muislamu ameshika madaraka ya juu ya nchi ukilinganisha na Tanzania.Je,mpaka hapo mfumo kristu uko wapi Kenya na Uganda au Tanzania?Ndugu waislamu acheni siasa za kibaguzi zitatufikisha kubaya,wakristo wakiamua kutawala nchi hii peke yao wanaweza kwasababu ya wingi wao kama wafanyavyo majirani zetu lakini sisi watanzania taifa letu halikujengwa katika misingi ya ubaguzi bali lilijengwa katika misingi ya usawa na ndio maana siasa ya nchi yetu ipo unique ukilinganisha na chi kama Misri na Nigeria ambapo watu wapo bize kugombea madaraka kwa misingi ya udini.Labda niseme kwa kitu ambacho waislamu wa tanzania hatujakijua ni kwamba ndani ya dini zetu hizi mmbili yaani Uilamu na Ukristo pia kuna udini ndani yake,yaani katika Ukristo kuna matabaka pia,wamo WASABATO,WAPENTECOSTE,WAKATOLIKI,WALUTHERI n.k na katika uislamu pia kuna matabaka pia.Kwaiyo tukitaka tuachie hii dhana ya udini kama ndiyo dira ya kouongoza nchi hatutafika tuendako kamwe ndugu watanzania.Utafanyika uchaguzi leo baada ya kinyang'anyiro kikali,atimaye atashinda mkatoliki,mkumbuke lawama zitakuja tena kwanini sisi WASABATO tutawaliwe na MKATOLIKI na vilevile kwa waislamu akishinda MSHIA,WASUNI watasema aaaah....haiwezekani tutawaliwaje na MSHIA.Kwaiyo ndugu zangu waislamu mliomezeshwa mambo ya mfumo ukristu fikirika tambuaeni kwamba hakuna nadharia iyo kwenye nchi yetu,kuna wajinga wachache ndiyo wanaotaka tuamiani ivyo ili nchi yetu iingie kwenye machafuko.Najua kuna madai mengi ambayo waislamu wanayadai kwa serikali ya CCM lakini kinachotakiwa ni kujenga hoja zitakazoishawishi serikali kukubaliana na hoja zenu na katu si kuingiza mambo ya udini inapoonekana hoja zenu zimeshindwa kuishawishi serikali.Inshort,my fellow Tanzania wether you are muslim or christian let us join our forces to protect our MAMALAND Tanzania by ensuring peace, harmony and tranguility prevail for the betterment of our future generation,yes we have different religious ideologies but we are all tanzanian,so let each one of us ensure that we leave this country peaceful as our forefathers did to us all who live in today.