Ndio ujinga wenu huu. Kusoma watu hawakubahatika, WALIDHAMIRIA. Unachojaribu kusema hapa ni kwamba, nyie muwe mnafundishana ujinga na chuki, huku wengine mnawapa jukumu la kubeba mizigo ya kudhorota kwenu.
Uliochotakiwa kusema hapa ni kuwa: Waislam waliosoma wawaeleweshe Waislam wenzao waliwezaje kusoma na kufika walipofika. Kama unafikiria kuna hotuba inaweza kubadilisha maisha ya mtu anayejazwa imani potofu na viongozi wa dini yake basi unajidanganya.
Fursa za kusoma zipo kwa wote, lkn hayo mawazo yenu kuwa labda mpewe upendeleo wa kuendelea mbele hata mkifeli ni utoto. Leo hii mnaandamana Dr. Ndalichako amewaonea hapa na pale, lkn cha ajabu, asilimia kubwa ya waandamani ni wale ambao watoto wao wameishia darasa la 3,4,5 na kuzamia kwenye kupiga debe. Sasa mtoto aliyekacha shule darasa la 5, NECTA imemuonea wapi?
Msipende hadithi tamu na ngonjera za manung'uniko. Kujitazama ni ada ya muungwana na mwenye hekima huzichunguza njia zake. Unapooa wake wa3 na kuzaa watoto 11 ukataraji wanaenda shule na kurudi bila wewe mzazi kujali kama wanaandika, wanafanya home-work na hata kama shuleni kwenyewe wanaingia darasani au lah halafu utegemee watafaulu eti kwa kuwa tu na wao wameenda shule miaka 7 kama mtoto wa baba John huo ni ujinga.
Kusoma ni kuamua. Nimesoma na Waislam pia na wote waliokuwa wamekusudia kusoma walisoma na wengine wakaniacha nyuma.