Polisi wawajibike ajali ya daladala Temeke

vamda

JF-Expert Member
Aug 1, 2012
865
535
Salamu wana jamvi. Bila ya kupepesa macho, naenda moja kwa moja kwenye mada.

Leo tarehe 5- 10- 2020 watanzania tumeshuhudia ajali mbaya ya daladala na lori la mizigo. Abiria wa daladala takriban wanne wamefariki papo hapo na wengine lukuki kujeruhiwa vibaya (mahututi).

Kwanza naomba kuuliza jeshi la polisi, ni sheria ipi inayoruhusu abiria kusimama kwa kurundikana na kusongamana kwenye mabasi ya abiria maarufu kama daladala?

Naamini endapo abiria wa daladala iliyopata ajali, wangeketi kwenye viti bila ya kusimama huenda vifo visingetokea au madhara yasingekua makubwa kama ilivyotangazwa.

Waliotengeneza magari wameweka kiwango cha mwisho cha idadi ya abiria wanaotakiwa kuwemo ndani ya magari hayo. Askari wa usalama barabarani hamuwezi kukwepa lawama hii kutokana na uzembe wa kushindwa kusimamia sheria za usalama wa abiria. Au mnataka tuamini kwamba mna maslahi bibafsi kwenye biashara hiyo maana hata nauli zilizopangwa na sumatra (LATRA) zinazingatia abiria kuketi bila ya kusimama.

Ajali nyingi hutokana na askari wa barabarani kutochukua hatua stahiki za kisheria. Tunashuhudia, mbali na mabasi kurundika na kusimamisha abiria lukuki pia malori mengine hujaza mizigo zaidi ya uwezo wake. Vilevile magari mengi barabarani ni mabovu hususani daladala. Juzi nilipanda daladala viti vibovu, shokapu (shock absorber) hazifanyi kazi, dashboard haioneshi alama zozote, taa iliyowaka ilikuwa moja tu n. K. Nilishangaa daladala hilo lilikuwa na stika ya nenda kwa usalama (yaani limekaguliwa na polisi na kuruhusiwa kuendelea kubeba abiria).

Watanzania nani aliyetuloga? Nchi jirani zinatucheka kwa kutokuwa makini katika utendaji. Kwa vifo na majeruhi vilivyotokana na ajali hii ya daladala TEMEKE, polisi kitengo cha usalama barabarani watoe maelezo kwa nini wanaruhusu wafanyakazi wa kwenye madaladala kuwarundika abiria kwa kuwasimamisha. Polisi wawajibike kwa ajali hii. Naamini mtanishukuru kwa kuwaambia ukweli.
 
Huyu anaandika huu uzi unakaa mkoa gani?, Kwa Dar hakuna daladala za kutosheleza watu kama zitabeba level siti, pia hii ajali imetokea saa 9.50 alfajiri, kwa muda huu traffic gani atakua barabarani muda huo?
 
Chanzo cha ajali kimeelezwa kuwa ni dereva wa basi kupita kwenye mataa zikiwa nyekundu!

Inasikitisha sana, kwanini amewaua wenzake?

Lakini ni wazi kuwa sababu nyingine ni kwenda mwendo kasi!

Abiria jitambueni jamani

Kwanini ukubali mhuni aangamize maisha yako?

Kwanini mhuni ahatarishe maisha yako?

Hapana aisee!
 
Mimi ndiyo maana huwa napenda kumu observes dereva uendeshaji wake mwanzoni tu mwa Safari iwe fupi au ndefu!

Nikimuona anaonesha dalili za uvunjifu wa sheria naanza kumuonnya sisubiri askari wa usalama barabarani wala Sumatra, yarabi nafsi yangu!
 
Swala la usalama barabarani halipaswi kuachwa kwa traffic police pekee bali wa kwanza anapaswa kuwa abiria mwenyewe!

Sheria za usalama barabarani zinapaswa kujulikana na watu wote!

Yani dereva ameshindwa kuwa na subira kidogo kusubiri taa za kijani?

Mbona muda wa kusubiri uko tolerable?!

Hapana aisee!
 
Halafu Eti kuna watu watasema ni mapenzi ya mungu ,

Yani kwenye uzembe umwingize Mungu?

Mungu gani huyo?

Mungu ameagiza kuyatii mamlaka maana zimewekwa na yeye ,

Mamlaka zimeweka sheria kwamba dereva usiendeshe gari kwenye taa nyekundu dereva hakutii halafu useme kauli ya Mungu?

Mamlaka zimeweka sheria kwamba kwa maeneo ya mijini mwendo isizidi 50 PKH dereva unaenda mwendo kasi zaidi ya 80 ajali ikitokea useme ni Mungu?

Mungu yupi?
 
Huyu anaandika huu uzi unakaa mkoa gani?, Kwa Dar hakuna daladala za kutosheleza watu kama zitabeba level siti, pia hii ajali imetokea saa 9.50 alfajiri, kwa muda huu traffic gani atakua barabarani muda huo?
Tatizo sio level siti bali ni ufukara wa watu wa dar, wengi ni walalahoi wakiweka nauli ya sh 1000 kelele mji mzima. Tembelea nchi jirani uone
 
Hii ni Afrika mkuu...kero kama hizi huwezi zikosa afrika.ukikosa kwenye daldala utakuta hospital.makanisani.shulen.masokon kero kila kona sabab ya chumi zetu hazija tengamaa..cha muhimu ni wew abiria kuchanganya na zako sabab wew ndio mpandaj wa daaldala...ukiona limejaa shuka
 
Kwa daladala ilivyochakatwa ingekuwa imejaza na wengine kusimama ungesikia maafa ni makubwa Sana zaidi ya hivyo ulivyosikia ila
Kwa mda ambao ajali imetokea sio rahisi watu kuwa wamejaa kiasi hicho lakini pia nadhani Ni makosa ya kiufundi ya dereva

Pia

Abiria kusimama kwenye daladala haiepukiki na imekuwa hivyo miaka mingi bila shida ishu Ni kutii Sheria
Hata Kama uko pekeyako kwenye taa na haijakuruhusu kupita inabidi usubiri ndiyo ustaarabu huo
 
Back
Top Bottom