Polisi wanaendelea kurusha risasi juu maeneo ya Mbezi kwa Yusuph

Kalunguine

JF-Expert Member
Jul 27, 2010
2,543
134
now nimejua kwa nini wanafunzi walicharuka, shule ipo umbali wa mita100 kutoka highway, wanafunzi walianza andamana kuelekea barabarani kushinikiza yajengwe matuta baada ya mwenzao kugongwa vibaya na bus la alsaedy jumamosi. wakiwa nanaelekea barabarani kuna mwanafunzi alikuwa mstari wa mbele huku akipiga ngoma ya band ya shule, polisi walivyofika wakaanza kumnyang'anya ngoma, katika purukushani mmoja akatoa bastola na kumpiga begani. hivyo ikaamsha hasira kwa wanafunzi wote hata wakaanza piga mawe magari yasiyowahusu.dereva alimgonga huyo mwanafunzi baada ya kupanua barabara. older post;nimepita maeneo ya mbezi kwa yusuph muda sio mrefu, polisi wapo wakitawanya wanafunzi wa mbezi high school kwa risasi baada ya wanafunzi hao kufunga barabara kwa muda kadhaa. inasemekana kuna mwanafunzi aligongwa hapo, sasa wanahitaji barabara iwekewe matuta kurahisisha wanafunzi kuvuka barabara. wanafunzi nao wapo kwa makundi wakirushia mawe na chupa magari yanayopita eneo hili huku wengine wakikimbia baada ya kuumia.note, nimelazimika update habari baada ya kupata info zaidi.
 
Ipo siku tutakuwa sugu na hizo risasi na mabomu.... hapo ndipo watu watahama nchi....
 
i knew this was going to happen someday,we have lost 2 teachers, 4 students on the same spot.,!!
 
siku hizi kazi kubwa ya polisi ni kupambana na chadema na wanafunzi,,..........................leo majambazi yameua na kuiba mhimbili polisi wetu wako buze kushambulia wanafunzi wa secondary
 
Hivi hawa jamaa hawana akili nyingine yoyote ya kutatua tatizo zaidi ya mabomu ya machozi na maji ya kuwasha?? Hata pale wanapokabiliwa na watoto wadogo wa shule!
 
Hivi hawa jamaa hawana akili nyingine yoyote ya kutatua tatizo zaidi ya mabomu ya machozi na maji ya kuwasha?? Hata pale wanapokabiliwa na watoto wadogo wa shule!

Nafikiri umesahau tatizo lao kubwa..ni weupe kichwani, wengi ni darasa la saba na form four failures...
 
Suala la kuweka matuta sikubaliani nalo. Itakuwa kila sehemu mtu akigongwa watu wanafunga barabara kushinikizwa pawekwe matuta. Tutafika mahali barabara zote zitakuwa matuta tu. Kinachotakiwa ni elimu kwa watumiaji wa barabara. Elimu itolewe kuanzia yule ya msingi na kuendelea.
 
Zamani nikiwa mdogo nilipenda sana upolisi siku moja uncle wangu akaniambia polisi huwa wanakatwa vichwa na kuwekewa vingine toka hapo nikachukia upolisi,hi stori nadhani alitaka kuniambia polisi hawatumi commonsense na reasoning wanafuta tu order,
pili wanafunzi waombe njia mbadala si matuta wapeni wahandisi wa barabara nafasi zao si kila sehemu matuta mwishowe yatakuwa mapambo na aibu kwa barabara we can think beyond matuta au wahandisi hamna?
Hivi itakuwaje siku wananchi wakimpga vizuri 2 polisi mmoja kama mfano?
 
Kama matuta si wawajengee tu kama walivyofanya pale Kibasila Sec Sch kuliko kuwapiga na kuwafyatulia risasi?
 
Suala la kuweka matuta sikubaliani nalo. Itakuwa kila sehemu mtu akigongwa watu wanafunga barabara kushinikizwa pawekwe matuta. Tutafika mahali barabara zote zitakuwa matuta tu. Kinachotakiwa ni elimu kwa watumiaji wa barabara. Elimu itolewe kuanzia shule ya msingi na kuendelea.

Hapa umenena mkuu, kinachotakiwa ni watu kupata elimu juu ya matumizi sahihi ya barabara na sio kung'ang'nia matuta kila mahali..
 
tatizo mtu akishakaa kwenye uskani basi tabu, utapigiwa honi kibao na kutukanwa kwenye zebra. matuta si suruisho, yangejengwa madaraja kama ya manzese ingesaidia kiaina.
 
Ipo siku tutakuwa sugu na hizo risasi na mabomu.... hapo ndipo watu watahama nchi....

Swala siyo usugu wa wananchi, bali kulisaidia jeshi kuacha kutumia nguvu zisizo kuwa na sababu. Polisi wetu watumie akili zaidi badala ya
mabavu. Ni aibu kuona mambo yanayoendelea katika jeshi hili, hayo mambo yalisitahili jeshi la 1960's wakati askari wengi hawakuwa wasomi walizolewa toka TANU YOUTH LEAGUE. Inanipa wasiwasi kwamba kwa sasa wakuu wa jeshi hilo labda ni masalia ya hao wa 1960's.
 
Asee! Wanafunzi wakitaka usalama barabarani wanatwangwa shaba.
Mama wajawazito wanalala chini hospitali na kupoteza maisha kwa uzembe police hawaendi pale magogoni kumwambia kiranja inakuwaje joo!
 
Nadhani imefika muda wa kusema hapana kwa sauti moja kwa ubabe huu wa vyombo vya dola. Haiwezekani kivurugu kidogo cha watoto wa shule badala ya diplomasia na njia za usuruhishi kutumika wao wanakurupuka kutumia risasi za moto hawa jamaa ni mbumbumbu na mabwege ya akili ila mbaya zaidi ni serikali imekuwa ikikaa kimya kila mauaji yanapotokea na hakuna hatua zozote za makusudi zinazochukuliwa kudhibiti hali hiyo.
 
Elimu ya usalama barabarani kwa watumiaji wote wa barabara ndiyo suluhisho. Barabara zenyewe finyu,foleni kibao,tunataka kujaza matuta hiyo busara kweli?!
 
polisi nao wamezidi, wangepambana na aliyegonga na siyo kurusha risasi kwa wanaotaka matuta kwa usalama wao. matuta ni njia mbadala baada ya mistari ya zebra kushindwa kuheshimiwa na madereva wengi, kukiwa hatuoni sababu ya kupuuzwa kwa zebra
 
Back
Top Bottom