Polisi wakamata dhahabu ya Sh milioni 140 ikitoroshwa, mtuhumiwa atokomea, atelekeza gari

Yaani nanunua dhahabu Nyarugusu ili nikauze Huko Swiss alafu nimwambie yule mchimbaji aniuzie sawa na soko la Dunia ? Hapo takuwa nafanya Biashara au ninafanya kubalidilisha Pesa, na nikishaipata hio dhahabu mimi nakwenda kuwauzia wale duniani kwa bei gani ?

Ipo hivi:

Nunua dhahabu Nyarugusu kwa wachimbaji wadogo walalie aidha kwa njaa zao au ujinga wao.

Au nunua dhahabu Nyarugusu ongeza purity ndo peleka nje ili upate faida.

Au chimba mwenyewe bana matumizi kwenye uchimbaji ili bdae ukiuza upate faida

Au nunua dhahabu, kama una leseni, kisha itunze hadi bei ya dhahabu ikipanda ndo iuze ili upate faida. Bei ya dhahabu inabadilika kila siku kama hisa.

Nje ya hapo bei ya dhahabu yenye purity sawa haipishani sana toka eneo moja hadi lingine duniani kote.

Ingia online search gold price leo TZ na New York ujionee.
 
mtu anakimbiaje dhahabu yake aliyo ihangaikia kwa miezi kadhaa kwenye ma-plant na ma-elusion?
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Maafisa Madini Wilaya ya Chunya limefanikiwa kukamata madini aina ya dhahabu yenye thamani zaidi ya Tsh milioni mia arobaini (140).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei, ameeleza kuwa Februari 9, 2022 majira ya saa 19:30 usiku katika kizuizi cha Polisi Chalangwa kilichopo Kata ya Chalangwa, Tarafa ya Kiwanja, Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya, Askari Polisi kwa kushirikiana na Maafisa Madini Wilaya ya Chunya walikamata Gari T.948 DTM aina ya Toyota Crown iliyokuwa ikiendeshwa na mtu aliyefahamika kwa jina BARAKA SINGU @ NYODA, ambaye baada ya kusimamishwa kwenye kizuizi hicho alikimbia na kutelekeza gari hiyo.

Katika upekuzi uliofanywa kwenye gari hiyo vilikutwa vipande 36 vya madini aina ya dhahabu vyenye uzito wa gramu 1367.07 vyenye thamani ya Tshs. 147,694,961.83/= na fedha taslimu Tshs. 504,600/=, lengo ni kukwepa kodi na tozo za serikali.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na msako wa kumtafuta mtuhumiwa kwa hatua zaidi za kisheria.

Aidha, linatoa rai kwa wafanyabiashara kutambua kuwa mkono wa serikali ni mrefu hivyo ni vyema kufanya biashara halali kwa kufuata sheria na taratibu zilizopo ili kuepuka kukinzana na sheria.

View attachment 2114949
Wapatiwe mil.2 ya Kazi nzuri afu nyingine ipigwe mnada serikali ipate Chao au ipelekwe BOT Mbeya.
 
Uwe unauliza kabla hujaandika huu utopolo.

FYI kuna leseni za utunzaji na usafirishaji dhahabu, ni lazima uwe nayo ili uweke kufanya hivyo. Huyu hakuwa na vibali it's a no brainer ndo maana kakimbia, jidanganye dhahabu ni yako bila vibali upigwe kesi ya uhujumu uchumi.
Mchimbaji mdogo mwenye leseni akipata dhahabu yake akaitunza ni kosa?
 
Back
Top Bottom