Polisi taarifa za uongo zinawaweka rehani!

Polisi taarifa za uongo zinawaweka rehani!

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,643
Reaction score
14,642
Polisi hawajijui.
Na hawajui kuwa katika miaka ya karibuni jeshi la Polisi limejijengea sifa hasi mbele ya jamii.
Utekaji, ubambikaji kesi na taarifa zisizokuwa na ukweli dhidi ya wananchi kwa ujumla imeshusha sana imani ya watu kwa jeshi letu la polisi.
Polisi kuhusika kiamilifu mauaji ya Okt29 imeongeza chuki kutoka kwa wananchi.

Sasa tunaona reaction ya mtu mmoja mmoja kama huyo Daktari Agonza kwa kutendewa kitu ambacho akaona anyooshane na huyo polisi mhusika.

Akumulikaye mchana, usiku atakuchoma.
Huko ndiko tunaelekea.
Sasa madaktari wamejiapiza nasikia kulipa kisasi kwa mwenzao alivyotendewa, wao wanaona si haki kwa mwenzao Dr Agonza aliyekuwa anawahi hospitali.
Maisha ya askari polisi wadogo na familia zao ni lazima zitapitia wakati mgumu mahospitalini.

Kamanda Muliro anawajibu wa kutoa taarifa zilizo na ukweli badala ya zilizopinda pinda na kuficha uhalifu wa askari wake.
 
kama ni kweli alimpiga askari hapaswi hata kuwa daktari na alipaswa kunyang'anywa kibali cha kutibia watu nchini anaweza kwenda nje ya nchi, again siujui ukweli wote lkn kama ni kweli alimshambulia law enforcement hapaswi kuendelea kutibu nchini na anyanganywe kibali cha utabibu.

anayetoa kibali cha utabibu ni serikali na serikali inaweza kukichukua pia, tuache kuishi kwa mazoea, kumshambulia law enforcement aliyekuwa kazini kutekeleza majukumu yake ni no go, hiyo inavuka mipaka yote, nothing justifies that , kama unaona umeonewa sheria ziko wazi, askari wote wana utambulisho lkn kumshambulia askari aliye kazini ni kosa kubwa, kwa maoni yangu kama ikithibitishwa amemshambulia askari aliyekuwa akitekeleza majukumu yake hapaswi tena kurudi kazini na kuruhusiwa kutibu watu ndani ya jamhuri ya tanzagiza ...
 
kama ni kweli alimpiga askari hapaswi hata kuwa daktari na alipaswa kunyanganywa kibali cha kutibia watu nchini anaweza kwenda nje ya nchi, again siujui ukweli lkn kama ni kweli alimshambulia law enforcement hapaswi kuendele kutibu nchini na anyanganywe kibali cha utabibu ...
Umekisoma ulicho andika ?!
 
kama ni kweli alimpiga askari hapaswi hata kuwa daktari na alipaswa kunyang'anywa kibali cha kutibia watu nchini anaweza kwenda nje ya nchi, again siujui ukweli wote lkn kama ni kweli alimshambulia law enforcement hapaswi kuendele kutibu nchini na anyanganywe kibali cha utabibu.

anayetoa kibali cha utabibu ni serikali na serikali inaweza kukichukua pia, tuache kuishi kwa mazoea, kumshambulia law enforcement aliyekuwa kazini kutekeleza majukumu yake ni no go, hiyo inavuka mipaka yote, nothing justifies that , kama unaona umeonewa sheria ziko wazi, askari wote wana utambulisho lkn kumshambulia askari aliye kazini ni kosa kubwa, kwa maoni yangu kama ikithibitishwa amemshambulia askari aliyekuwa akitekeleza majukumu yake hapaswi tena kurudi kazini na kuruhusiwa kutibu watu ndani ya jamhuri ya tanzagiza ...
Zamani nilifikiri Platnum members hapa JF ni watu wenye akili sana.....
 
kama ni kweli alimpiga askari hapaswi hata kuwa daktari na alipaswa kunyang'anywa kibali cha kutibia watu nchini anaweza kwenda nje ya nchi, again siujui ukweli wote lkn kama ni kweli alimshambulia law enforcement hapaswi kuendele kutibu nchini na anyanganywe kibali cha utabibu.

anayetoa kibali cha utabibu ni serikali na serikali inaweza kukichukua pia, tuache kuishi kwa mazoea, kumshambulia law enforcement aliyekuwa kazini kutekeleza majukumu yake ni no go, hiyo inavuka mipaka yote, nothing justifies that , kama unaona umeonewa sheria ziko wazi, askari wote wana utambulisho lkn kumshambulia askari aliye kazini ni kosa kubwa, kwa maoni yangu kama ikithibitishwa amemshambulia askari aliyekuwa akitekeleza majukumu yake hapaswi tena kurudi kazini na kuruhusiwa kutibu watu ndani ya jamhuri ya tanzagiza ...
Upupu🗑️
 
Zamani nilifikiri Platnum members hapa JF ni watu wenye akili sana.....

its relative, hairuhusiwi ku-attack law enforcement popote pale dunia hii, nenda hata hapo kenya tu trafiki polisi akikusimamisha kwanza wako 2 au zaidi mmoja kashikilia sub machine gun kakaa nyuma, finger on the trigger ready to fire anaangalia halafu ndiyo uje umpige ngumi na mateke? kuna sababu kwa nini law enforcement karibia wote wako armed na ni dunia nzima, tanzagiza tunaishi kwa mazoea sana, hauwezi ku-attack askari akiwa kazini anaruhusiwa kuku-shoot in self defense, wengine akikwambia mikono juu kweli weka juu ukishusha hata mmoja ana-shoot ofcourse hiyo na mada nyingine lkn kuna sababu kwa nini iko hivyo, halafu tanzagiza unamshambulia mateke wtf.

huyo kichaa mwingine new york city alitaka ku-attack law enforcement, they shot her dead ...


View: https://twitter.com/i/status/2094554615266066726
 
Kwahiyo Mkuu unabariki kitendo cha huyo Daktari kujichukulia sheria mkononi? Heshima kwa vyombo lazima ilindwe kwa wivu mkubwa na yeyote anayejaribu kutweza mamlaka ya vyombo atalipia kwa gharama kubwa utovu wake wa nidhamu.

Sijaona hata mmoja aliyetoka hadharani kukemea ama kulaani kitendo kilichofanywa na huyo daktari as if yeye anastahili sana kuwafanyia wengine vitendo viovu.

To earn respect, yo must show respect in the first place
 
Kwahiyo Mkuu unabariki kitendo cha huyo Daktari kujichukulia sheria mkononi? Heshima kwa vyombo lazima ilindwe kwa wivu mkubwa na yeyote anayejaribu kutweza mamlaka ya vyombo atalipia kwa gharama kubwa utovu wake wa nidhamu.

Sijaona hata mmoja aliyetoka hadharani kukemea ama kulaani kitendo kilichofanywa na huyo daktari as if yeye anastahili sana kuwafanyia wengine vitendo viovu.

To earn respect, yo must show respect in the first place
Sibariki hata kidogo, ila hali isipoelezwa kiukweli matukio yakoje, yaani hiyo kitu ndiyo italeta kutoelewana katika jamii.
Tusifike mahali pa Haiti.
 
Sibariki hata kidogo, ila hali isipoelezwa kiukweli matukio yakoje, yaani hiyo kitu ndiyo italeta kutoelewana katika jamii.
Tusifike mahali pa Haiti.
Hizo failed States unazozitolea mfano kama Haiti hazikutokea ghafla tu bali ni matokeo ya utovu wa nidhamu kufumbiwa macho kwa muda mrefu ndiyo utatufikisha huko.

JMT inajifunza kwa waliokosea ndiyo maana inakabia kwa juu matendo yote ya kihuni na kuwashughulikia wahuni mapema.

JMT haipelekeshwi kwa majority view, inaenenda kwa namna yake kulingana na mahitaji ya mazingira yake.

Ukimruhusu mwanao akupandishie sauti, ni suala la muda tu atakuchapa makofi. Maana mwana umleavyo ndiyo akuavyo.

Kwenye suala la national security, hiyo kitu huwa hakuna compromise. Vyombo havichezewi

A child can play with her mother's breast, but, not father's testicles.
 
Hizo failed States unazozitolea mfano kama Haiti hazikutokea ghafla tu bali ni matokeo ya utovu wa nidhamu kufumbiwa macho kwa muda mrefu ndiyo utatufikisha huko.

JMT inajifunza kwa waliokosea ndiyo maana inakabia kwa juu matendo yote ya kihuni na kuwashughulikia wahuni mapema.

JMT haipelekeshwi kwa majority view, inaenenda kwa namna yake kulingana na mahitaji ya mazingira yake.

Ukimruhusu mwanao akupandishie sauti, ni suala la muda tu atakuchapa makofi. Maana mwana umleavyo ndiyo akuavyo.

Kwenye suala la national security, hiyo kitu huwa hakuna compromise. Vyombo havichezewi

A child can play with her mother's breast, but, not father's testicles.
Uko sahihi kabisa lakini na failure si upande mmoja.
Vyombo vikitoa spin ili kukidhi hali kuteteana na kubebana na kutoeleza ukweli, basi vinakosa uungwaji mkono na wananchi.
 
kama ni kweli alimpiga askari hapaswi hata kuwa daktari na alipaswa kunyang'anywa kibali cha kutibia watu nchini anaweza kwenda nje ya nchi, again siujui ukweli wote lkn kama ni kweli alimshambulia law enforcement hapaswi kuendelea kutibu nchini na anyanganywe kibali cha utabibu.

anayetoa kibali cha utabibu ni serikali na serikali inaweza kukichukua pia, tuache kuishi kwa mazoea, kumshambulia law enforcement aliyekuwa kazini kutekeleza majukumu yake ni no go, hiyo inavuka mipaka yote, nothing justifies that , kama unaona umeonewa sheria ziko wazi, askari wote wana utambulisho lkn kumshambulia askari aliye kazini ni kosa kubwa, kwa maoni yangu kama ikithibitishwa amemshambulia askari aliyekuwa akitekeleza majukumu yake hapaswi tena kurudi kazini na kuruhusiwa kutibu watu ndani ya jamhuri ya tanzagiza ...
Ila askari kuuwa,kuteka na kupiga raia wasio na hatia kwao ni sawa?
 
its relative, hairuhusiwi ku-attack law enforcement popote pale dunia hii, nenda hata hapo kenya tu trafiki polisi akikusimamisha kwanza wako 2 au zaidi mmoja kashikilia sub machine gun kakaa nyuma, finger on the trigger ready to fire anaangalia halafu ndiyo uje umpige ngumi na mateke? kuna sababu kwa nini law enforcement karibia wote wako armed na ni dunia nzima, tanzagiza tunaishi kwa mazoea sana, hauwezi ku-attack askari akiwa kazini anaruhusiwa kuku-shoot in self defense, wengine akikwambia mikono juu kweli weka juu ukishusha hata mmoja ana-shoot ofcourse hiyo na mada nyingine lkn kuna sababu kwa nini iko hivyo, halafu tanzagiza unamshambulia mateke wtf.

huyo kichaa mwingine new york city alitaka ku-attack law enforcement, they shot her dead ...


View: https://twitter.com/i/status/2094554615266066726

Hizo nchi unazosema wao wanazingatia sheria sio huku kwetu, wewe unafikili Tanzania kuna haki?
likikupata ujue umeisha hakuna haki hata huko mahakani
 
Uko sahihi kabisa lakini na failure si upande mmoja.
Vyombo vikitoa spin ili kukidhi hali kuteteana na kubena na kutoeleza ukweli, basi vinakosa uungwaji mkono na wananchi.
Ukifuatilia historia ya vyombo ulimwenguni kote na utendaji wake hautegemei uungwaji mkono wa Wananchi, kwakuwa viko pale kutumikia maslahi ya Taifa na iwe unataka ama hautaki vitakuwepo na vitaendelea kuwepo.

Katika utekelezaji wa majukumu yake hata usiporidhia kushirikiana navyo utashirutishwa kuviheshimu na kuvipa ushirikiano pale inapobidi.

Hata kwenye Civil-Military relations vyombo vinahimizwa kuwa na mahusiano mazuri na raia, lakini mahusiano hayo hayavifanyi vyombo kuwa dhaifu mbele ya raia ama kuondoa yale mamlaka yake hasa unapotokea utovu wa nidhamu ama kuvitweza vyombo.
 
Back
Top Bottom