PostGE2025 Polisi Mwanza: Limewatia mbaroni watu 116 wanaodaiwa kuratibu maandamno ya Desemba 9

PostGE2025 Polisi Mwanza: Limewatia mbaroni watu 116 wanaodaiwa kuratibu maandamno ya Desemba 9

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limewatia mbaroni watu 116 wanaodaiwa kuratibu mipango ya kufanya maandamano yasiyo rasmi tarehe 9 Desemba mwaka huu, tukio linalotajwa kuwa na viashiria vya uvunjifu wa amani.

Akizungumza na Wanahabari, Desemba 6, 2025 katika kituo kikuu cha Polisi kilichopo Wilaya ya Nyamagana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbrod Mutafungwa, amesema upelelezi dhidi ya watuhumiwa hao unaendelea, huku jeshi hilo likiimarisha doria katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha Mkoa wa Mwanza unabaki kuwa salama.

Aidha, Kamanda Mutafungwa ametoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha vijana hawashiriki katika maandamano hayo, akisisitiza kuwa siku ya Desemba 9 itumike kama kumbukizi ya Tanzania kupata uhuru wake, badala ya kusababisha uvunjifu wa amani.

“Imeshatolewa taarifa rasmi kuwa maandamano hayo yamekatazwa. Tunawaomba wazazi kuzuia watoto wao kujiingiza katika maandamano hayo. Badala yake, makundi yote ya kijamii yashirikiane na Serikali kudumisha amani na utulivu katika siku hii muhimu ya kumbukizi ya uhuru wa nchi yetu,” amesema Kamanda Mutafungwa.

Kamanda huyo amesema hatua hizo ni mwendelezo wa jitihada za Jeshi la Polisi mkoani humo katika kulinda mali na usalama wa wananchi, ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea kama ilivyoshuhudiwa kwenye vurugu za maandamano yaliyotokea wakati wa uchaguzi wa Oktoba 29 mwaka huu.

 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limewatia mbaroni watu 116 wanaodaiwa kuratibu mipango ya kufanya maandamano yasiyo rasmi tarehe 9 Desemba mwaka huu, tukio linalotajwa kuwa na viashiria vya uvunjifu wa amani.

Akizungumza na Wanahabari, Desemba 6, 2025 katika kituo kikuu cha Polisi kilichopo Wilaya ya Nyamagana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbrod Mutafungwa, amesema upelelezi dhidi ya watuhumiwa hao unaendelea, huku jeshi hilo likiimarisha doria katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha Mkoa wa Mwanza unabaki kuwa salama.

Aidha, Kamanda Mutafungwa ametoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha vijana hawashiriki katika maandamano hayo, akisisitiza kuwa siku ya Desemba 9 itumike kama kumbukizi ya Tanzania kupata uhuru wake, badala ya kusababisha uvunjifu wa amani.

“Imeshatolewa taarifa rasmi kuwa maandamano hayo yamekatazwa. Tunawaomba wazazi kuzuia watoto wao kujiingiza katika maandamano hayo. Badala yake, makundi yote ya kijamii yashirikiane na Serikali kudumisha amani na utulivu katika siku hii muhimu ya kumbukizi ya uhuru wa nchi yetu,” amesema Kamanda Mutafungwa.

Kamanda huyo amesema hatua hizo ni mwendelezo wa jitihada za Jeshi la Polisi mkoani humo katika kulinda mali na usalama wa wananchi, ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea kama ilivyoshuhudiwa kwenye vurugu za maandamano yaliyotokea wakati wa uchaguzi wa Oktoba 29 mwaka huu.

Cha cha huyo muta anaweza kupiga marufuku mandomando, na kuwachukulia watu Kwa hizo tuhuma za kufanya mipango ya maandamano
 
Wanatafuta sifa kwa Samia Suluhu, dawa yao ni kupiga moto kituo chenyewe cha polisi mamamae
 
Mwanza huwa ipo michezo ya kamata kamata kutafuta sifa kwa wakubwa

Nilipoona wako miliman wanakagua mapango nikajua tu wapo wapunga upepo lazima jumba mbovu litawaangukia

Yaan hapo wamekusanywa wote waliokutana nao huko miliman,

Wakat wa magufuri kama mlikuwa mnafatilia vyombo vya habar kuna wakat polis kila mkoa walikuwa wanatengeneza matukio na kujifanya wamepambana na majambaz na kuwauwa

Sasa mwanza waliwah kusanya vijana saba na wakaenda wapiga risas huko miliman eti ni majambaz
 
“Imeshatolewa taarifa rasmi kuwa maandamano hayo yamekatazwa. Tunawaomba wazazi kuzuia watoto wao kujiingiza katika maandamano hayo. Badala yake, makundi yote ya kijamii yashirikiane na Serikali kudumisha amani na utulivu katika siku hii muhimu ya kumbukizi ya uhuru wa nchi yetu,” amesema Kamanda Mutafungwa.
Ukombozi wa nchi hii hauwezi kuletwa kwa kutegemea hisani ya wakandamizaji.

Kama huyo polisi halijui hilo inampasa alijue.
 
Huu ni mpango wa Mungu kuliponya Taifa.

Kama hawataangalia wapi wamekosea, wapi mzizi wa matatizo, hii nchi kutawalika itakuwa ngumu.

Huwezi kumtawala mtu anayeamini umemuua mwanae na maiti yake umeificha. NEVER.

Mtauzuia tarehe 9 itatangazwa tarehe nyingine. Damu za watu huwa haziendi hivi hivi.

Hiyo kamata kamata inazidi kuchochea jazba mioyoni mwa Watanganyika.
 
Tarehe 9D vituo vyote vya polisi vitasalimiwa na polisi wote wa Mwanza watajua hawajui
 
Kumkamata mtu kwa kitu ambacho hakijatokea ni uhuni.

Huwezi kuhisi tu ukanikamata, huko mahabusu lazima niichome moto.
Huu ndio upumbavu wa watu hawa. Wao wanajitungia sheria na kuitekeleza bila kufuata taratibu zinazotakiwa. Ndio maana tumekuwa nchi ya hovyo sana.
 
Vilaza wakubwa hao, unakamata mtu upelelezi haujakamilika.?
 
Back
Top Bottom