Polisi kuwaachia Wapemba

wamewaachia kwa kuwa hawakuwa na sababu za kuwakamata.
kikwete anaaibisha kuwa hawezi kutumia nguvu zake alizopewa kikatiba mpaka awasikilize wazungu.
hivi tutaendelea kutawaliwa na wazungu hadi lini?
 
Hizi ni hoja zisizo na msingi:

a. Jamii ya watu ambao wanaishi katika mashaka na hawana usalama katika eneo lolote lile la ardhi ya dunia wanayo haki ya kibinadamu kutafuta mahali pao ambao watakuwa huru kuwa binadamu.

b. Wakati wowote jamii ya watu inanyanyaswa, kuteswa au kutendewa kama nusu binadamu au nusu raia jamii hiyo ina haki ya kutafuta hifadhi mahali popote ambapo wanaweza kupaita ni pao.

c. Jamii ya watu ambao wako ndani ya nchi moja endapo wanajiona kuwa katika nchi hiyo hawatendewi sawa, hawana haki sawa, wananyanyaswa, wananyimwa nafasi ya kunusuru maisha na mali zao na kwa namna moja au nyingi wanatengwa na utawala wa Taifa basi jamii hiyo inayo haki ya kimsingi ya kujitenga na jamhuri au nchi hiyo.

- Wayahudi walipokuwa wanateswa wakati wa vita ya pili ya dunia na kwa muda mrefu wakiteswa na kufanywa duni sehemu mbalimbali duniani, walifikia mahali pa kuamua kujenga Taifa lao, mahali pekee ambapo wanaweza kupaita pao. Ndio mwanzo wa kuundwa kwa Taifa la Israeli baada ya vita ya 1948. Leo hii ni miaka 60 baadaya kuundwa kwa Taifa hilo.

- Watumwa waliokamatwa katika ile meli ya Amistad na kuletwa marekani kwa nguvu walitetea haki yao ya kuwa binadamu na ya kuwa walikuwa na kwao na hivyo kitendo cha kuwakamata kwa nguvu kilikuwa ni kinyume na haki ya watu hao kuishi kwa usalama wa maisha yao. Mahakama Kuu ya Marekani ilikubali na kuwaachilia.

- Wakurdi wa Iraq ambao waliishi katika mateso chini ya utawala wa Saadam kwa muda mrefu wamekuwa wakijitahidi kujitenga ili wawe huru kuishi kama binadamu na raia huru. Licha ya jitihada za Sadam kuwafunga na kuwaua mawazo ya wao kuwa na kwao hayakukoma. Na kwa muda mrefu wamekuwa wakijitahidi kujenga utawala wao. Na sasa hivi eneo la Kurdistan ambako Wakurdi wa Iraq ingawa ni sehemu ya nchi ya Iraq wanajiendeshea mambo yao katika shirikisho la Iraq lakini wakiwa na serikali yao na viongozi wao.

- Taifa la Marekani liliamua kujitangazia uhuru wake toka Dola ya Muingereza baada ya kutoa malalamiko yao (soma declaration of independence) na malalamiko hayo kutofanyiwa kazi na Mfalme. Walifanya hivyo ili wawe na sehemu ambayo wako huru kuamua mambo yao kwani mfalme hakuwa tayari kuwasikiliza. Kujitangaza kwao huko kulisababisha vita iliyozaa uhuru Julai 4, 1776.

- Biafra, wananchi wa Nigeria wa kabila la Igbo na makabila madogomadogo yanayohusiana nayo waliamua kujitoa katika shirikisho la Nigeria na kutangaza uhuru wao na taifa lao. Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi kama tano zilizotambua Taifa hilo jipya kwa misingi niliyoisema hapo juu. Kwa Wanigeria ilikuwa ni kitendo cha uhaini lakini kwa wa Igbo ilikuwa ni kitendo cha kulinda maisha yao na ya watoto na uzao wao. Baada ya muda si mrefu Biafra ikalazimishwa kusalimu amri na kurudishwa kwa nguvu kwenye Shirikisho. Hata hivyo hisia ya kutaka kuwa huru bado ipo na vizazi vya wa Igbo bado wanasimuliana juu ya njozi hiyo ya kuwa watu huru.

Nina mifano mingine ambayo nitaicha pembeni kwa wakati huu.

Ninachosema ni kuwa suala la Pemba si suala la uvunjaji wa sheria au Katiba per se. Ni suala la watu na jamii ya watu kuwa na mawazo ya kujitenga. Huwezi kuwalazimisha watu ati watii katiba wakati Katiba iliyopo inatumika kuwakandamiza, kuwatenda au kwa namna yoyote kuwafanya wawe duni.

Mwanadamu anayo haki ya kutii dhamira yake zaidi, utu wake, na haki yake kama mwanadamu na raia kuliko kutii sheria ambayo inatishia dhamiri, utu, au haki hiyo. Ndugu zetu wa Zanzibar wana madai tena mazito. Madai hayo ambayo yamekuwa yakitolewa mara nyingi kwa maoni yao yamepuuzwa na kutofuatiliwa. Kitendo cha kuwakamata sasa kinaendeleza mwelekeo huo huo kwamba lazima wapemba waconform kimawazo to the majority. Hili haliwezekani.

Matatizo ya wa Pemba ni matatizo ambayo yanahitaji kutambulika kwa kanuni kadhaa ili kuweza kuyatatua. Kutoa tishio la sheria au nguvu za dola ni udhaifu mkubwa kwani hakuna dola iliyowahi kuzima mawazo ya uhuru, au kutia pingu fikra za mabadiliko. Walishindwa wajerumani, walishindwa Waingereza, walishindwa Afrika Kusini, Alishindwa Mussolini, alishindwa Sadam, alishindwa Stalini, na kwa hakika atashindwa Mwema na Kikwete.

Kama mbegu ya kutaka kuheshimika na kutambulika utu wao imepandwa katika wapembwa hakuna atakayeweza kuizima. Hiyo ndio hali halisi.

Jukumu letu basi ni nini? Je tukubali wapemba wajitenge kwa sababu tumeshindwa kuwasikiliza? Je tuache sehemu ya Jamhuri yetu kujitenga kwa sababu wanasiasa wamekuwa goigoi kufikiri na wa wazito kutatua matatizo yao. La hasha!

Mimi binafsi kama mpenzi wa Muungano wetu na nikiwa mwanafunzi mzuri wa Mwalimu sioni jambo lililoshindikana. Ni wito wa kila mtanzania kuulinda, kuuenzi na kuutetea Muungano na Jamhuri yetu na hatuwezi kuacha jamii ya watu itishie muungano huo. Haiwezekani kikundi cha watu kikatae kusikiliza matatizo ya ndugu zetu wa Pemba hadi kuwalazimisha kutaka kujitenga.

Swali langu?

Je, utawala wa serikali ya CCM wamefanya juhudi gani za kushughulikia matatizo yanayotajwa na Wapemba? Muafaka siyo juhudi za kweli kwani hilo linahusu utawala na mambo ya siasa na hakuna ajenga ya hali ya wananchi wa Pemba au malalamiko yao. Je kwa vile Pemba wengi ni CUF ina maana serikali tawala haitakiwi kuonesha juhudi za kuheshimu maamuzi ya wananchi wa huko?

Ndugu zangu ipo njia ya haki, yenye usawa na yenye umoja. Njia ambayo itaweza kuondoa hisia hizi na kuzizika mara moja.

a. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, iangalie katika uongozi wake ina wananchi wangapi kutoka Pemba. Je ni lazima mtu awe CCM ndio apewe nafasi ya uongozi? Kama Pemba imetoa wabunge wengi tu kwanini wasiingizwe kwenye serikali? Hili halihitaji kura ya maoni linahitaji akili. Huwezi kushinda kwa asilimia 53 halafu ukaishi kama umeshinda kwa asilimia 90! SMZ ilipaswa mara baada ya uchaguzi kukaa chini na CUF na kupanga mkakati wa kushirikiana.

b. Rais Kikwete badala ya kuchagua wakuu wa mikoa na wilaya za Pemba toka CCM angechagua kutoka CUF na hata viongozi wengine angewachanganya wa CUF pia. Hilo halihusu sera au katiba ni suala la akili tu. Kwanini hakufanya hivyo wakati anajua kabisa kuwa Pemba ni kwa kiasi kikubwa mashabiki wa CUF. Angeweza hata kuunda ushirikiano wa aina fulani kati ya viongozi wa CCM na CUF kule Pemba. Lakini hakufanya hivyo.

c. Serikali iwaachilie wananchi hawa mara moja na kukaa meza moja na kuwasikiliza. Tusiingie kwenye mtego wa kufungana kwa mambo haya kwani tutaanza kutengeneza wafungwa wa kisiasa na kuanza kupandikiza zaidi fikra za mapambano. Tusiingie kwenye mtego huo. Serikali ifute madai yake, itengeneze timu ya ushirikiano (nje ya mazingaombwe ya muafaka) na kuamua kwa makusudi kabisa kuwashirikisha wananchi wa Pemba katika maamuzi na utawala. Walikipanda wenyewe, sasa wasishangae wanavuna miiba!

d. Viongozi wa CUF watangaze hadharani kuwa lengo lao si kuvunja muungano au kutangaza Taifa huru bali wanataka nafasi ya kutambuliwa na kuthaminiwa kama raia kamili wa jamhuri yetu. Maneno ambayo yamewahi kusikika ya "Mwarabu hatotawala Zanzibar" wakati mwarabu huyo ni raia ni maneno yanayowafanya waarabu wa eneo letu kuwa nusu raia. Leo hii Botswana inatawaliwa na raia ambaye baba ni mweusi na mama ni mzungu! Sisi tunahangaika na mambo ya ajabu ya nasaba! Leo Marekani inaweza kujikuta ikitawaliwa na kiongozi ambaye baba yake ni mweusi na mama ni mzungu! sisi tunashindana na alilala na Sultani na nani na kijakazi!

Ndugu zangu watanzania, matatizo ya Zanzibar yanatatulika na wala hayahitaji mkono mkubwa wa dola ili kuyamaliza. Yanahitaji utashi wa kisiasa, ushirikiano wa kuaminiana na moyo wa udugu. Watawala wa Zanzibar lazima wakubali kwa vitendo kuwa Wapemba ni wananchi sawa na wale wa Unguja na wanahaki sawa katika Taifa hilo bila kuangalia nasaba zao, historia zao n.k Na hili lazima lichukuliwe hadi kwenye serikali kuu. Kujifanya ati tunawakamata na kuwatia pingu na kuwatishia ni kitendo kilichofanywa na serikali ya makaburu na no sir, hatuwezi kuacha serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar kuanza kutenda kama serikali za makaburu au za kibaguzi.

That is my argument and I'm sticking to it.

M. M
.

Good job mwanakijiji,

Masuala ya watanzania yanaweza kuamuliwa na watanzania kwanza na sio lazima wageni watoe matamko ndio watu wakae chini kujadiliana.
 
b. Rais Kikwete badala ya kuchagua wakuu wa mikoa na wilaya za Pemba toka CCM angechagua kutoka CUF na hata viongozi wengine angewachanganya wa CUF pia. Hilo halihusu sera au katiba ni suala la akili tu. Kwanini hakufanya hivyo wakati anajua kabisa kuwa Pemba ni kwa kiasi kikubwa mashabiki wa CUF. Angeweza hata kuunda ushirikiano wa aina fulani kati ya viongozi wa CCM na CUF kule Pemba. Lakini hakufanya hivyo.

c. Serikali iwaachilie wananchi hawa mara moja na kukaa meza moja na kuwasikiliza. Tusiingie kwenye mtego wa kufungana kwa mambo haya kwani tutaanza kutengeneza wafungwa wa kisiasa na kuanza kupandikiza zaidi fikra za mapambano. Tusiingie kwenye mtego huo. Serikali ifute madai yake, itengeneze timu ya ushirikiano (nje ya mazingaombwe ya muafaka) na kuamua kwa makusudi kabisa kuwashirikisha wananchi wa Pemba katika maamuzi na utawala. Walikipanda wenyewe, sasa wasishangae wanavuna miiba!

d. Viongozi wa CUF watangaze hadharani kuwa lengo lao si kuvunja muungano au kutangaza Taifa huru bali wanataka nafasi ya kutambuliwa na kuthaminiwa kama raia kamili wa jamhuri yetu. Maneno ambayo yamewahi kusikika ya "Mwarabu hatotawala Zanzibar" wakati mwarabu huyo ni raia ni maneno yanayowafanya waarabu wa eneo letu kuwa nusu raia. Leo hii Botswana inatawaliwa na raia ambaye baba ni mweusi na mama ni mzungu! Sisi tunahangaika na mambo ya ajabu ya nasaba! Leo Marekani inaweza kujikuta ikitawaliwa na kiongozi ambaye baba yake ni mweusi na mama ni mzungu! sisi tunashindana na alilala na Sultani na nani na kijakazi!
Kaka, hii MIKUKI...

Kama wana nia, basi wamepata pa kuanzia kwa hizo point zenye meno!
 
mnanifanya niwe nervous... what is the problem.... sipendi kuandika makosa.. so you better point 'em out ili nisahihishe au niweke sawa..
...hakuna makosa mkuu, ujumbe mzito ndani ya muda mfupi ndo uliosababisha hiyo "duh..."!! Seems like all keypads are at your fingertips -- hahahh!!
 
JS, unajua mara nyingi wanatulaumu kuwa tunawakosoa tu, hatutoi mapendekezo ya suluhisho la matatizo. I hope mmoja wao atanyaka na kuongezea katika hayo. Binafsi naamini matatizo ya Pemba na Zanzibar kwa ujumla yanatatulika.
 
Hizi ni hoja zisizo na msingi:

a. Jamii ya watu ambao wanaishi katika mashaka na hawana usalama katika eneo lolote lile la ardhi ya dunia wanayo haki ya kibinadamu kutafuta mahali pao ambao watakuwa huru kuwa binadamu.

b. Wakati wowote jamii ya watu inanyanyaswa, kuteswa au kutendewa kama nusu binadamu au nusu raia jamii hiyo ina haki ya kutafuta hifadhi mahali popote ambapo wanaweza kupaita ni pao.

c. Jamii ya watu ambao wako ndani ya nchi moja endapo wanajiona kuwa katika nchi hiyo hawatendewi sawa, hawana haki sawa, wananyanyaswa, wananyimwa nafasi ya kunusuru maisha na mali zao na kwa namna moja au nyingi wanatengwa na utawala wa Taifa basi jamii hiyo inayo haki ya kimsingi ya kujitenga na jamhuri au nchi hiyo.

- Wayahudi walipokuwa wanateswa wakati wa vita ya pili ya dunia na kwa muda mrefu wakiteswa na kufanywa duni sehemu mbalimbali duniani, walifikia mahali pa kuamua kujenga Taifa lao, mahali pekee ambapo wanaweza kupaita pao. Ndio mwanzo wa kuundwa kwa Taifa la Israeli baada ya vita ya 1948. Leo hii ni miaka 60 baadaya kuundwa kwa Taifa hilo.

- Watumwa waliokamatwa katika ile meli ya Amistad na kuletwa marekani kwa nguvu walitetea haki yao ya kuwa binadamu na ya kuwa walikuwa na kwao na hivyo kitendo cha kuwakamata kwa nguvu kilikuwa ni kinyume na haki ya watu hao kuishi kwa usalama wa maisha yao. Mahakama Kuu ya Marekani ilikubali na kuwaachilia.

- Wakurdi wa Iraq ambao waliishi katika mateso chini ya utawala wa Saadam kwa muda mrefu wamekuwa wakijitahidi kujitenga ili wawe huru kuishi kama binadamu na raia huru. Licha ya jitihada za Sadam kuwafunga na kuwaua mawazo ya wao kuwa na kwao hayakukoma. Na kwa muda mrefu wamekuwa wakijitahidi kujenga utawala wao. Na sasa hivi eneo la Kurdistan ambako Wakurdi wa Iraq ingawa ni sehemu ya nchi ya Iraq wanajiendeshea mambo yao katika shirikisho la Iraq lakini wakiwa na serikali yao na viongozi wao.

- Taifa la Marekani liliamua kujitangazia uhuru wake toka Dola ya Muingereza baada ya kutoa malalamiko yao (soma declaration of independence) na malalamiko hayo kutofanyiwa kazi na Mfalme. Walifanya hivyo ili wawe na sehemu ambayo wako huru kuamua mambo yao kwani mfalme hakuwa tayari kuwasikiliza. Kujitangaza kwao huko kulisababisha vita iliyozaa uhuru Julai 4, 1776.

- Biafra, wananchi wa Nigeria wa kabila la Igbo na makabila madogomadogo yanayohusiana nayo waliamua kujitoa katika shirikisho la Nigeria na kutangaza uhuru wao na taifa lao. Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi kama tano zilizotambua Taifa hilo jipya kwa misingi niliyoisema hapo juu. Kwa Wanigeria ilikuwa ni kitendo cha uhaini lakini kwa wa Igbo ilikuwa ni kitendo cha kulinda maisha yao na ya watoto na uzao wao. Baada ya muda si mrefu Biafra ikalazimishwa kusalimu amri na kurudishwa kwa nguvu kwenye Shirikisho. Hata hivyo hisia ya kutaka kuwa huru bado ipo na vizazi vya wa Igbo bado wanasimuliana juu ya njozi hiyo ya kuwa watu huru.

Nina mifano mingine ambayo nitaicha pembeni kwa wakati huu.

Ninachosema ni kuwa suala la Pemba si suala la uvunjaji wa sheria au Katiba per se. Ni suala la watu na jamii ya watu kuwa na mawazo ya kujitenga. Huwezi kuwalazimisha watu ati watii katiba wakati Katiba iliyopo inatumika kuwakandamiza, kuwatenda au kwa namna yoyote kuwafanya wawe duni.

Mwanadamu anayo haki ya kutii dhamira yake zaidi, utu wake, na haki yake kama mwanadamu na raia kuliko kutii sheria ambayo inatishia dhamiri, utu, au haki hiyo. Ndugu zetu wa Zanzibar wana madai tena mazito. Madai hayo ambayo yamekuwa yakitolewa mara nyingi kwa maoni yao yamepuuzwa na kutofuatiliwa. Kitendo cha kuwakamata sasa kinaendeleza mwelekeo huo huo kwamba lazima wapemba waconform kimawazo to the majority. Hili haliwezekani.

Matatizo ya wa Pemba ni matatizo ambayo yanahitaji kutambulika kwa kanuni kadhaa ili kuweza kuyatatua. Kutoa tishio la sheria au nguvu za dola ni udhaifu mkubwa kwani hakuna dola iliyowahi kuzima mawazo ya uhuru, au kutia pingu fikra za mabadiliko. Walishindwa wajerumani, walishindwa Waingereza, walishindwa Afrika Kusini, Alishindwa Mussolini, alishindwa Sadam, alishindwa Stalini, na kwa hakika atashindwa Mwema na Kikwete.

Kama mbegu ya kutaka kuheshimika na kutambulika utu wao imepandwa katika wapembwa hakuna atakayeweza kuizima. Hiyo ndio hali halisi.

Jukumu letu basi ni nini? Je tukubali wapemba wajitenge kwa sababu tumeshindwa kuwasikiliza? Je tuache sehemu ya Jamhuri yetu kujitenga kwa sababu wanasiasa wamekuwa goigoi kufikiri na wa wazito kutatua matatizo yao. La hasha!

Mimi binafsi kama mpenzi wa Muungano wetu na nikiwa mwanafunzi mzuri wa Mwalimu sioni jambo lililoshindikana. Ni wito wa kila mtanzania kuulinda, kuuenzi na kuutetea Muungano na Jamhuri yetu na hatuwezi kuacha jamii ya watu itishie muungano huo. Haiwezekani kikundi cha watu kikatae kusikiliza matatizo ya ndugu zetu wa Pemba hadi kuwalazimisha kutaka kujitenga.

Swali langu?

Je, utawala wa serikali ya CCM wamefanya juhudi gani za kushughulikia matatizo yanayotajwa na Wapemba? Muafaka siyo juhudi za kweli kwani hilo linahusu utawala na mambo ya siasa na hakuna ajenga ya hali ya wananchi wa Pemba au malalamiko yao. Je kwa vile Pemba wengi ni CUF ina maana serikali tawala haitakiwi kuonesha juhudi za kuheshimu maamuzi ya wananchi wa huko?

Ndugu zangu ipo njia ya haki, yenye usawa na yenye umoja. Njia ambayo itaweza kuondoa hisia hizi na kuzizika mara moja.

a. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, iangalie katika uongozi wake ina wananchi wangapi kutoka Pemba. Je ni lazima mtu awe CCM ndio apewe nafasi ya uongozi? Kama Pemba imetoa wabunge wengi tu kwanini wasiingizwe kwenye serikali? Hili halihitaji kura ya maoni linahitaji akili. Huwezi kushinda kwa asilimia 53 halafu ukaishi kama umeshinda kwa asilimia 90! SMZ ilipaswa mara baada ya uchaguzi kukaa chini na CUF na kupanga mkakati wa kushirikiana.

b. Rais Kikwete badala ya kuchagua wakuu wa mikoa na wilaya za Pemba toka CCM angechagua kutoka CUF na hata viongozi wengine angewachanganya wa CUF pia. Hilo halihusu sera au katiba ni suala la akili tu. Kwanini hakufanya hivyo wakati anajua kabisa kuwa Pemba ni kwa kiasi kikubwa mashabiki wa CUF. Angeweza hata kuunda ushirikiano wa aina fulani kati ya viongozi wa CCM na CUF kule Pemba. Lakini hakufanya hivyo.

c. Serikali iwaachilie wananchi hawa mara moja na kukaa meza moja na kuwasikiliza. Tusiingie kwenye mtego wa kufungana kwa mambo haya kwani tutaanza kutengeneza wafungwa wa kisiasa na kuanza kupandikiza zaidi fikra za mapambano. Tusiingie kwenye mtego huo. Serikali ifute madai yake, itengeneze timu ya ushirikiano (nje ya mazingaombwe ya muafaka) na kuamua kwa makusudi kabisa kuwashirikisha wananchi wa Pemba katika maamuzi na utawala. Walikipanda wenyewe, sasa wasishangae wanavuna miiba!

d. Viongozi wa CUF watangaze hadharani kuwa lengo lao si kuvunja muungano au kutangaza Taifa huru bali wanataka nafasi ya kutambuliwa na kuthaminiwa kama raia kamili wa jamhuri yetu. Maneno ambayo yamewahi kusikika ya "Mwarabu hatotawala Zanzibar" wakati mwarabu huyo ni raia ni maneno yanayowafanya waarabu wa eneo letu kuwa nusu raia. Leo hii Botswana inatawaliwa na raia ambaye baba ni mweusi na mama ni mzungu! Sisi tunahangaika na mambo ya ajabu ya nasaba! Leo Marekani inaweza kujikuta ikitawaliwa na kiongozi ambaye baba yake ni mweusi na mama ni mzungu! sisi tunashindana na alilala na Sultani na nani na kijakazi!

Ndugu zangu watanzania, matatizo ya Zanzibar yanatatulika na wala hayahitaji mkono mkubwa wa dola ili kuyamaliza. Yanahitaji utashi wa kisiasa, ushirikiano wa kuaminiana na moyo wa udugu. Watawala wa Zanzibar lazima wakubali kwa vitendo kuwa Wapemba ni wananchi sawa na wale wa Unguja na wanahaki sawa katika Taifa hilo bila kuangalia nasaba zao, historia zao n.k Na hili lazima lichukuliwe hadi kwenye serikali kuu. Kujifanya ati tunawakamata na kuwatia pingu na kuwatishia ni kitendo kilichofanywa na serikali ya makaburu na no sir, hatuwezi kuacha serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar kuanza kutenda kama serikali za makaburu au za kibaguzi.

That is my argument and I'm sticking to it.

M. M.

Asante Mwanakijiji hii nimeiweka kwenye briefcase yangu, ni hazina ya mawazo mazuri ya kizalendo, yaliyo jaa busara. Mifano ya kujitenga mingine ipo hapa hapa karibu tu, hapo Somalia. Somaliland sasa ni nchi inayojitegemea kabisa. Sasa kwanini tufike huko? kwanini mwingine ajione anaonewa ndani ya nchi yetu hii Tanzania? Viongozi na chama dola wanataka kusababisha kuvunjika kwa muungano. Nawaomba watawala watumie busara zaidi kuliko umbwamba wa kisiasa. God bless our United Republic of Tanzania.
 
Mwanakijiji,umenivutia kwa yale uliyoyaandika,ni hoja za uhakika.kam Mheshimiwa anasoma kwenye mtandao huu basi hayo mambo muhimu namshauri ayafuate ili kujijengea heshima hapa duniani.

Kina Mandela walifanya yale mambo ya msingi ya kudadi haki kwa raia na Jk anahitaji kufanya hivyo sasa....otherwise ataonekana kama wengine waliomtangulia ambao hawakutaka ku address masuala ya kimsingi ya demokrasia na haki za binadamu huko Zanzibar.
Kwa cheo chake cha Urais na kama Mwenyekiti wa AU ana mengi ya kuthubutu kufanya ili kuleta hali ya hamnazo kuondoka huko Zanzibar na tanzania kwa jumla.Sitaki Jk akawa fisadi lakini nataka kusikia muziki wa Jk mletaji amani na matumaini ya raia nchini mwetu.

Kama anaweza litakuwa ni moja ya mambo makubwa kufanyika hapa Afrika.Asipoweza....atakuwa kama mafisadi wengine tu hata kama atakuwa hajaiba BOT.
 
JS, unajua mara nyingi wanatulaumu kuwa tunawakosoa tu, hatutoi mapendekezo ya suluhisho la matatizo. I hope mmoja wao atanyaka na kuongezea katika hayo. Binafsi naamini matatizo ya Pemba na Zanzibar kwa ujumla yanatatulika.
...ni kweli kaka; tatizo la Pemba ni hicho kisiki kinachoendela kukariri kuwa Babake alifanya mapinduzi ilhali alikuwa mwoga ka' MBWA KOKO!!
 
ok.. waheshimiwa mwisho hili libichwa litagusa ardhini.. tusonge mbele tuone jinsi gani tunaweza kusaidia kutafuta usuluhishi wa mgogoro huu usio wa lazima. Kuna hatua nyingine nyingi ambazo tunaweza kujifunza kutoka nchi nyingine ambazo kwa hakika zinaweza kumaliza mgogoro huu na kufuta hata hisia za kibaguzi, uonevu, au ukandamizaji.

Kwangu mimi tatizo la mazungumzo ya muafaka ulivyo sasa ni kuwa unashughulikia dalili tu za tatizo na haugusi tatizo lenyewe. Hata mapendekezo ya kuunda serikali ya mseto na kuongeza vyeo vingine vyote vinajaribu kutibu dalili na si chanzo.

Matatizo ya mpasuko wa kisiasa hayakutokea sababu ya uchaguzi wa 95, 00, au 05. Yaliyotokea wakati huo ni ishara ya kiini cha matatizo yenyewe na mazungumzo haya ya sasa hayadeal na issues zenyewe na hivyo kuahidi kuwa mgogoro huu utaendelea kwa kizazi kingine.

Binafsi ningependekeza mgogoro uamuliwe kwa hatua. Nitafafanua kwa kirefu wiki ijayo.
 
''Amani haitafutwi kwa ncha ya Upanga...Tuliwapinga makaburu si kwa sababu ya rangi yao ila kwa dhambi ya ubaguzi wao''

Mara kadhaa imeshadhihiri njia ya kutumia mabavu haijawahi kuleta suluhusho la kudumu na la muda mrefu katika nyanja kadhaa za maisha ya mwanadamu.

Kitendo cha kuwakamata na kuwatishia wale ndg zetu wa Pemba havitaleta suluhisho la kudumu ni lazima akili na busara ya juu ifanye kazi kutatua mpasuko uliopo ktk siasa za visiwa vile vya marashi ya karafuu.

Usanii wa kupeleka maoni kwa wananchi unatia mashaka kama kweli wakulu wa chama tawala wanayo dhamira ya kweli, njema na safi ya kutaka kutafutia suluhisho la kudumu mfukuto uliopo kule visiwani. Kwani mwisho wa yote maoni yatabeba taswira ile ile ya matokea ya uchaguzi mkuu uliopita na zingine zilizopita na hapo sasa ndipo uongozi wa hali juu unatakiwa kuonyweshwa na wale wenye dhamira safi kwa kufanya maamuzi magumu yenye kuleta mwangaza mpya wa matumaini kwa Taifa mfano; Serikali ya pamoja na njia zingine zitakazokuwa muafaka kwa wakati na mazingira tuliyonayo.

Zipo pia dalili za kibaguzi kwa baadhi ya Waunguja kujiona ni bora zaidi ya Wapemba na vivyo hivyo kwa baadhi ya Wapemba kujiona wao ni zaidi. Huu ni ukaburu na ni lazima tukumbushane tuliwapinga makaburi kwa dhambi hii ya ubaguzi na si kwa sababu nyingine. Sisi ni wamoja; usawa, kuheshimiana, kuvumiliana na kutambua vipaji vya wengine miongoni mwetu ndio njia pekee ya kulea jamii ya kistaarabu na itakayokuwa na manufaa kwa wote.

Mungu Ibariki Tanzania
Ee Mungu Utulinde na maadui wa Muungano wetu.
Bara juu, Unguja juu na Pemba juu.
 
kumbe kilichotokea ni kuwa wale 10,000 walituma ujumbe leo kuwa wako tayari kwenda kujisalimisha na wenyewe Polisi ili wote watiwe pingu... ndio kisa cha kina Mwema kuwaachilia.

huko tunakokwenda jela hazitotumika tena kuzima mawazo ya kisiasa!
 
Polisi mkumbuke kwamba nynyi ndio wa kwanza kuvunja sheria na ukiukwaji wa haki za BInadamu katika kisiwa cha Pemba na kama Wapemba wamekiuka sheria na kuhusika na kuivunja Katiba basi Jeshi la Polisi linahusika moja kwa moja na washawasha la Wapemba hao.
Jeshi la Polisi linahusika moja kwa moja katika kuharibu uchaguzi wa Zanzibar sio siri kuwa jeshi la Polisi lilikuwa mstari wa mbele katika kuwalinda Janjaweeds wa Karume katika kupiga mitaa kwa zamu ,njia na mipango yote ikivuja na sehemu nyengine haari zikifika kuwa leo ni sehemu fulani ,magari yanayowachukuwa Janjaweed yakipata escort za jeshi la polisi na kuwafanya mafedhuli hao wapige wananchi kwa kutumia monyororo na nondo zikiwemo silaha zenye ncha kali.
Je ni kesi ngapi ziliripotiwa watu kupigwa na Janjaweeds na Polisi mtuambie mlichukua hatua gani ?
Je ni vituo vingapi vya kupigia kura mapandikizi walikuwa wakishushwa na magari ili kupiga kura na jeshi la polisi likiwawekea ubavu ili wapige kura haraka na kupelekwa kituo kingine ,picha za kideo zipo zinzoonyesha watu hawa ,kuna kituo kimoja janjaweed alikamatwa na kisu na baada ya kukurupushwa polisi walimuekea ubavu na kumtorosha na hakuna alilofanywa kaseti ya kideo ipo.
Je ile kesi ya Polisi kukimbia na masanduku ya kupigia kura kule Pemba ,kama si kuiba uchaguzi ilikuwa ni kitu gani ,sasa mnataka Wapemba na Waunguja wawaamini kwa jambo gani ?
Wapemba na Waunguja waseme mara ngapi hawana imani na jeshi la Polisi ?
Je mmewapa jibu gani kurudisha imani au huko kuwakamata Wapemba usiku ?
Raisi anaposema kuwa Jeshi la polisi linatakiwa kuwa karibu na wananchi ili liweze kukubalika na kubadilika hamaanishi mjiweke karibu na vyama vya siasa na kukingia kifua upande mmoja wa Chama kwa ufupi Jeshi la Polisi linatuka na kukitumikia Kundi la wahafidhina na wapo tayari kuuwa ili kulilinda kundi hilo na ndio kilichofanyka katika mauaji ya January 2001.
Polisi lilikimbia na masanduku ya kura ili kulilinda kundi hilo.
Polisi waliwazingira wafuasi wa CUF pale makao makuu yao ili kulilinda kundi hilo kuhalalisha wizi wake wa kura.
Polisi walisaidia kuruhusu wapiga kura wapandikizwaji ili kulilinda kundi hilo.
Polisi ni watumiliwa wakubwa na walioko mstari wa mbele kwa kuvunja sheria na haki za Binadamu.
Polisi walitumiliwa kuweka road Blocks na kuwasachi wafuasi wa CUF kila wanapoelekea kwenye mikutano yao na wakiwasachi na kuwavua nguo.
Jeshi la polisi lilitumika kuwatesa wakamatajwi waliopinga mapandikizi katika vituo vya Uchaguzi.
Jeshi la Polisi linatumika kwa mara nyengine kuwakamata Wapemba abao kwa kutumia kitengo cha haki za Binadamu wamewakilisha madai yao ya kujitenga kwa kule kuona kuwa hawatendewi haki na Serikali zote mbili kama wao si Raia wa Nchi hii ,hivyo imetaka UN iliangalie hili na ukiwepo uwezekano wa wao kuanzisha serikali yao basi waruhusiwe maana wametengwa kwa kila kigezo.
Kuwaachilia watu hawa sio mwisho wa mapigano dhidi ya Udhalilishaji wa jamii ya watu wa Pemba huko kwao huu ni mwanzo mpaka kieleweke kwa watawala weusi kukaa sawa na kuheshimu wenzao weusi.
 
Habari za kuaminika zinasema bado hajaachiwa mtu.
hajakabidhiwa mtu bado wapo katika vyombo vya ulinzi na usalama na wao wenyewe eti ndio watakaowasafirisha kuwapeleka Pemba ingawa hadi sasa bado hawajapelekwa licha ya kuachiwa huru tokea asubuhi.
Ilikuwa rahisi kuwateka nyara lakini baada ya kuona wamekwenda mchomo na gea waliyoondokea ,eti sasa usafiri wa kuwarudisha hawana Je huu ni Uungwana ??
 
Mwibaaaa
Tunawalaumu hao polisi lakini lazima tujue kwamba hao wanafuata maelekezo ya wakubwa wao ambao wana hasira na harakati zoote za kupelekea kukosa mlo
Kama ksura kikwete alikuwa hayataki hayo basi wala yasingeli fanyika na kutia aibu taifa [ingawa wao hawaiyoni]
Sisi wazee wetu walituachia urithi wa Kumushemu mtu mzima [makamo] kunamsemo hata muumba wa vyoote anamuheshi mtu mzima hivi kweli katika hicho kikundi chenu akina kisura hakuna hata mmoja anaye yafahamu haya? hamuelewi kama hakuna maisha ya milele hapa duniani?wakati kila siku munahudhuria mazishi?yuko wapi Swahiba DITOna wengineo wengiii
hpa dunaia tuna pita kudhalilisha hakuna maana hao wazee wa watu kama mauti yata wafikia huko waliko ninimutajitetea?
jee wale walio peperusha vikaratasi ya kuwa Wapemba warudi kwao walichukuliwa hatua gani na jeshi la polisi au polisi imesema nini kuhusu hilo?
Inamaana ni zuri kwa watawala na wanalipenda khaaswa Lakini la hawavibabu wa watu ni uhaini mimi nina uhakika mkubwa kwamba vile vikaratasi vinge andikwa kuwa 'wa bara warudi kwao' serikali zooote zingeli kemea kwa uchungu saana
eeemungu kila ajae na shari
waijuayake siri
ivunjeyake dhamiri
asiweze kusimama
mungu ibariki tanzania.
 
Jamani Mimi Namshangaa Mwema; Huyu Mwanasheria Tena Wa Kusomea na mwenye shahada Kufanya Makosa ya wazi wazi hivi.
Hawa Wapemba Walifanya Kosa Lipi La Kuvunja Katiba? Wao Hawajavunja Muungano Wala Kutangaza Serikali Yao Mpya; Hapana; Wao Walichofanya Ni Kuomba Umoja Wa Mataifa Uingilie Kati Ili Wao Wawe Ni Serikali Ndani Ya Serikali Kama Inavyotokea Katika Nchi Zingine. Na kwa kweli walikuwa na hoja katika hili.
Shida Ya Serikali Yetu Ni Baadhi Ya Viongozi Wetu Ambao Wao Wanadhani Maamuzi Yao Ndiyo Final Hata Kama Watanzania Wote Watakuwa Hawayapendi.
Wanapozungumzia Katiba Wanajisema Wao. Wanamaana Ya Matumbo Yao. Wana Maana Familia Zao. Wana Maana Rafiki Zao. Hiyo kwao ndiyo Katiba.
Ndiyo Maana Tunahitaji Katiba Mpya.
Hii Katiba Inayotukataza Hata Kuja Na Hoja Hatuitaki.
Mwema Alifanya Makosa Na Bila Shaka Alifanya Makosa Kwa Kutumwa Na Wakubwa Wake Huku Akijua Ni Makosa.
Ni Makosa Haya Haya Aliyafanya Wakati Akiingilia Masuala Ya Jf Na Kuwakamata Wale Vijana Wawili. Aliishia kulalama na kuomba radhi.
Mimi Namshauri Mwema Akamate Wale Mafisadi Wa Epa Kwanza; Na Wale Wa Richmond; Meremeta; Na Huyu Balali; Si Anajua Kuwa Wamevunja Katiba? Kwa Hawa anasemaje? Mbona Kwa Kujifanya Ni Mtaalamu Wa Interpol Kashindwa Kumpata Balali Na Kumrudisha Kujibu Tuhuma Zake za wizi?
Wapemba hawana kosa awaachie huru na awaache walete hoja hata kama ni UN. Yawezekana wamegundua wakiileta mbele ya wanafiki hawa wa CCM hawatasikilizwa.
By the way hivi kwa hili wanadhani watawanyazisha? Subirini tuone!?
 
Back
Top Bottom