Mtu wa Pwani
JF-Expert Member
- Dec 26, 2006
- 4,184
- 671
mkjj haya yote unayaandika saa ngapi?
mkuu nashindwa kupata picha
mkuu nashindwa kupata picha
...impressed lakini duh...impressed or dissappointed...?
...impressed lakini duh...
Hizi ni hoja zisizo na msingi:
a. Jamii ya watu ambao wanaishi katika mashaka na hawana usalama katika eneo lolote lile la ardhi ya dunia wanayo haki ya kibinadamu kutafuta mahali pao ambao watakuwa huru kuwa binadamu.
b. Wakati wowote jamii ya watu inanyanyaswa, kuteswa au kutendewa kama nusu binadamu au nusu raia jamii hiyo ina haki ya kutafuta hifadhi mahali popote ambapo wanaweza kupaita ni pao.
c. Jamii ya watu ambao wako ndani ya nchi moja endapo wanajiona kuwa katika nchi hiyo hawatendewi sawa, hawana haki sawa, wananyanyaswa, wananyimwa nafasi ya kunusuru maisha na mali zao na kwa namna moja au nyingi wanatengwa na utawala wa Taifa basi jamii hiyo inayo haki ya kimsingi ya kujitenga na jamhuri au nchi hiyo.
- Wayahudi walipokuwa wanateswa wakati wa vita ya pili ya dunia na kwa muda mrefu wakiteswa na kufanywa duni sehemu mbalimbali duniani, walifikia mahali pa kuamua kujenga Taifa lao, mahali pekee ambapo wanaweza kupaita pao. Ndio mwanzo wa kuundwa kwa Taifa la Israeli baada ya vita ya 1948. Leo hii ni miaka 60 baadaya kuundwa kwa Taifa hilo.
- Watumwa waliokamatwa katika ile meli ya Amistad na kuletwa marekani kwa nguvu walitetea haki yao ya kuwa binadamu na ya kuwa walikuwa na kwao na hivyo kitendo cha kuwakamata kwa nguvu kilikuwa ni kinyume na haki ya watu hao kuishi kwa usalama wa maisha yao. Mahakama Kuu ya Marekani ilikubali na kuwaachilia.
- Wakurdi wa Iraq ambao waliishi katika mateso chini ya utawala wa Saadam kwa muda mrefu wamekuwa wakijitahidi kujitenga ili wawe huru kuishi kama binadamu na raia huru. Licha ya jitihada za Sadam kuwafunga na kuwaua mawazo ya wao kuwa na kwao hayakukoma. Na kwa muda mrefu wamekuwa wakijitahidi kujenga utawala wao. Na sasa hivi eneo la Kurdistan ambako Wakurdi wa Iraq ingawa ni sehemu ya nchi ya Iraq wanajiendeshea mambo yao katika shirikisho la Iraq lakini wakiwa na serikali yao na viongozi wao.
- Taifa la Marekani liliamua kujitangazia uhuru wake toka Dola ya Muingereza baada ya kutoa malalamiko yao (soma declaration of independence) na malalamiko hayo kutofanyiwa kazi na Mfalme. Walifanya hivyo ili wawe na sehemu ambayo wako huru kuamua mambo yao kwani mfalme hakuwa tayari kuwasikiliza. Kujitangaza kwao huko kulisababisha vita iliyozaa uhuru Julai 4, 1776.
- Biafra, wananchi wa Nigeria wa kabila la Igbo na makabila madogomadogo yanayohusiana nayo waliamua kujitoa katika shirikisho la Nigeria na kutangaza uhuru wao na taifa lao. Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi kama tano zilizotambua Taifa hilo jipya kwa misingi niliyoisema hapo juu. Kwa Wanigeria ilikuwa ni kitendo cha uhaini lakini kwa wa Igbo ilikuwa ni kitendo cha kulinda maisha yao na ya watoto na uzao wao. Baada ya muda si mrefu Biafra ikalazimishwa kusalimu amri na kurudishwa kwa nguvu kwenye Shirikisho. Hata hivyo hisia ya kutaka kuwa huru bado ipo na vizazi vya wa Igbo bado wanasimuliana juu ya njozi hiyo ya kuwa watu huru.
Nina mifano mingine ambayo nitaicha pembeni kwa wakati huu.
Ninachosema ni kuwa suala la Pemba si suala la uvunjaji wa sheria au Katiba per se. Ni suala la watu na jamii ya watu kuwa na mawazo ya kujitenga. Huwezi kuwalazimisha watu ati watii katiba wakati Katiba iliyopo inatumika kuwakandamiza, kuwatenda au kwa namna yoyote kuwafanya wawe duni.
Mwanadamu anayo haki ya kutii dhamira yake zaidi, utu wake, na haki yake kama mwanadamu na raia kuliko kutii sheria ambayo inatishia dhamiri, utu, au haki hiyo. Ndugu zetu wa Zanzibar wana madai tena mazito. Madai hayo ambayo yamekuwa yakitolewa mara nyingi kwa maoni yao yamepuuzwa na kutofuatiliwa. Kitendo cha kuwakamata sasa kinaendeleza mwelekeo huo huo kwamba lazima wapemba waconform kimawazo to the majority. Hili haliwezekani.
Matatizo ya wa Pemba ni matatizo ambayo yanahitaji kutambulika kwa kanuni kadhaa ili kuweza kuyatatua. Kutoa tishio la sheria au nguvu za dola ni udhaifu mkubwa kwani hakuna dola iliyowahi kuzima mawazo ya uhuru, au kutia pingu fikra za mabadiliko. Walishindwa wajerumani, walishindwa Waingereza, walishindwa Afrika Kusini, Alishindwa Mussolini, alishindwa Sadam, alishindwa Stalini, na kwa hakika atashindwa Mwema na Kikwete.
Kama mbegu ya kutaka kuheshimika na kutambulika utu wao imepandwa katika wapembwa hakuna atakayeweza kuizima. Hiyo ndio hali halisi.
Jukumu letu basi ni nini? Je tukubali wapemba wajitenge kwa sababu tumeshindwa kuwasikiliza? Je tuache sehemu ya Jamhuri yetu kujitenga kwa sababu wanasiasa wamekuwa goigoi kufikiri na wa wazito kutatua matatizo yao. La hasha!
Mimi binafsi kama mpenzi wa Muungano wetu na nikiwa mwanafunzi mzuri wa Mwalimu sioni jambo lililoshindikana. Ni wito wa kila mtanzania kuulinda, kuuenzi na kuutetea Muungano na Jamhuri yetu na hatuwezi kuacha jamii ya watu itishie muungano huo. Haiwezekani kikundi cha watu kikatae kusikiliza matatizo ya ndugu zetu wa Pemba hadi kuwalazimisha kutaka kujitenga.
Swali langu?
Je, utawala wa serikali ya CCM wamefanya juhudi gani za kushughulikia matatizo yanayotajwa na Wapemba? Muafaka siyo juhudi za kweli kwani hilo linahusu utawala na mambo ya siasa na hakuna ajenga ya hali ya wananchi wa Pemba au malalamiko yao. Je kwa vile Pemba wengi ni CUF ina maana serikali tawala haitakiwi kuonesha juhudi za kuheshimu maamuzi ya wananchi wa huko?
Ndugu zangu ipo njia ya haki, yenye usawa na yenye umoja. Njia ambayo itaweza kuondoa hisia hizi na kuzizika mara moja.
a. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, iangalie katika uongozi wake ina wananchi wangapi kutoka Pemba. Je ni lazima mtu awe CCM ndio apewe nafasi ya uongozi? Kama Pemba imetoa wabunge wengi tu kwanini wasiingizwe kwenye serikali? Hili halihitaji kura ya maoni linahitaji akili. Huwezi kushinda kwa asilimia 53 halafu ukaishi kama umeshinda kwa asilimia 90! SMZ ilipaswa mara baada ya uchaguzi kukaa chini na CUF na kupanga mkakati wa kushirikiana.
b. Rais Kikwete badala ya kuchagua wakuu wa mikoa na wilaya za Pemba toka CCM angechagua kutoka CUF na hata viongozi wengine angewachanganya wa CUF pia. Hilo halihusu sera au katiba ni suala la akili tu. Kwanini hakufanya hivyo wakati anajua kabisa kuwa Pemba ni kwa kiasi kikubwa mashabiki wa CUF. Angeweza hata kuunda ushirikiano wa aina fulani kati ya viongozi wa CCM na CUF kule Pemba. Lakini hakufanya hivyo.
c. Serikali iwaachilie wananchi hawa mara moja na kukaa meza moja na kuwasikiliza. Tusiingie kwenye mtego wa kufungana kwa mambo haya kwani tutaanza kutengeneza wafungwa wa kisiasa na kuanza kupandikiza zaidi fikra za mapambano. Tusiingie kwenye mtego huo. Serikali ifute madai yake, itengeneze timu ya ushirikiano (nje ya mazingaombwe ya muafaka) na kuamua kwa makusudi kabisa kuwashirikisha wananchi wa Pemba katika maamuzi na utawala. Walikipanda wenyewe, sasa wasishangae wanavuna miiba!
d. Viongozi wa CUF watangaze hadharani kuwa lengo lao si kuvunja muungano au kutangaza Taifa huru bali wanataka nafasi ya kutambuliwa na kuthaminiwa kama raia kamili wa jamhuri yetu. Maneno ambayo yamewahi kusikika ya "Mwarabu hatotawala Zanzibar" wakati mwarabu huyo ni raia ni maneno yanayowafanya waarabu wa eneo letu kuwa nusu raia. Leo hii Botswana inatawaliwa na raia ambaye baba ni mweusi na mama ni mzungu! Sisi tunahangaika na mambo ya ajabu ya nasaba! Leo Marekani inaweza kujikuta ikitawaliwa na kiongozi ambaye baba yake ni mweusi na mama ni mzungu! sisi tunashindana na alilala na Sultani na nani na kijakazi!
Ndugu zangu watanzania, matatizo ya Zanzibar yanatatulika na wala hayahitaji mkono mkubwa wa dola ili kuyamaliza. Yanahitaji utashi wa kisiasa, ushirikiano wa kuaminiana na moyo wa udugu. Watawala wa Zanzibar lazima wakubali kwa vitendo kuwa Wapemba ni wananchi sawa na wale wa Unguja na wanahaki sawa katika Taifa hilo bila kuangalia nasaba zao, historia zao n.k Na hili lazima lichukuliwe hadi kwenye serikali kuu. Kujifanya ati tunawakamata na kuwatia pingu na kuwatishia ni kitendo kilichofanywa na serikali ya makaburu na no sir, hatuwezi kuacha serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar kuanza kutenda kama serikali za makaburu au za kibaguzi.
That is my argument and I'm sticking to it.
M. M.
Kaka, hii MIKUKI...b. Rais Kikwete badala ya kuchagua wakuu wa mikoa na wilaya za Pemba toka CCM angechagua kutoka CUF na hata viongozi wengine angewachanganya wa CUF pia. Hilo halihusu sera au katiba ni suala la akili tu. Kwanini hakufanya hivyo wakati anajua kabisa kuwa Pemba ni kwa kiasi kikubwa mashabiki wa CUF. Angeweza hata kuunda ushirikiano wa aina fulani kati ya viongozi wa CCM na CUF kule Pemba. Lakini hakufanya hivyo.
c. Serikali iwaachilie wananchi hawa mara moja na kukaa meza moja na kuwasikiliza. Tusiingie kwenye mtego wa kufungana kwa mambo haya kwani tutaanza kutengeneza wafungwa wa kisiasa na kuanza kupandikiza zaidi fikra za mapambano. Tusiingie kwenye mtego huo. Serikali ifute madai yake, itengeneze timu ya ushirikiano (nje ya mazingaombwe ya muafaka) na kuamua kwa makusudi kabisa kuwashirikisha wananchi wa Pemba katika maamuzi na utawala. Walikipanda wenyewe, sasa wasishangae wanavuna miiba!
d. Viongozi wa CUF watangaze hadharani kuwa lengo lao si kuvunja muungano au kutangaza Taifa huru bali wanataka nafasi ya kutambuliwa na kuthaminiwa kama raia kamili wa jamhuri yetu. Maneno ambayo yamewahi kusikika ya "Mwarabu hatotawala Zanzibar" wakati mwarabu huyo ni raia ni maneno yanayowafanya waarabu wa eneo letu kuwa nusu raia. Leo hii Botswana inatawaliwa na raia ambaye baba ni mweusi na mama ni mzungu! Sisi tunahangaika na mambo ya ajabu ya nasaba! Leo Marekani inaweza kujikuta ikitawaliwa na kiongozi ambaye baba yake ni mweusi na mama ni mzungu! sisi tunashindana na alilala na Sultani na nani na kijakazi!
...hakuna makosa mkuu, ujumbe mzito ndani ya muda mfupi ndo uliosababisha hiyo "duh..."!! Seems like all keypads are at your fingertips -- hahahh!!mnanifanya niwe nervous... what is the problem.... sipendi kuandika makosa.. so you better point 'em out ili nisahihishe au niweke sawa..
mkjj haya yote unayaandika saa ngapi?
mkuu nashindwa kupata picha
impressed or dissappointed...?
Hizi ni hoja zisizo na msingi:
a. Jamii ya watu ambao wanaishi katika mashaka na hawana usalama katika eneo lolote lile la ardhi ya dunia wanayo haki ya kibinadamu kutafuta mahali pao ambao watakuwa huru kuwa binadamu.
b. Wakati wowote jamii ya watu inanyanyaswa, kuteswa au kutendewa kama nusu binadamu au nusu raia jamii hiyo ina haki ya kutafuta hifadhi mahali popote ambapo wanaweza kupaita ni pao.
c. Jamii ya watu ambao wako ndani ya nchi moja endapo wanajiona kuwa katika nchi hiyo hawatendewi sawa, hawana haki sawa, wananyanyaswa, wananyimwa nafasi ya kunusuru maisha na mali zao na kwa namna moja au nyingi wanatengwa na utawala wa Taifa basi jamii hiyo inayo haki ya kimsingi ya kujitenga na jamhuri au nchi hiyo.
- Wayahudi walipokuwa wanateswa wakati wa vita ya pili ya dunia na kwa muda mrefu wakiteswa na kufanywa duni sehemu mbalimbali duniani, walifikia mahali pa kuamua kujenga Taifa lao, mahali pekee ambapo wanaweza kupaita pao. Ndio mwanzo wa kuundwa kwa Taifa la Israeli baada ya vita ya 1948. Leo hii ni miaka 60 baadaya kuundwa kwa Taifa hilo.
- Watumwa waliokamatwa katika ile meli ya Amistad na kuletwa marekani kwa nguvu walitetea haki yao ya kuwa binadamu na ya kuwa walikuwa na kwao na hivyo kitendo cha kuwakamata kwa nguvu kilikuwa ni kinyume na haki ya watu hao kuishi kwa usalama wa maisha yao. Mahakama Kuu ya Marekani ilikubali na kuwaachilia.
- Wakurdi wa Iraq ambao waliishi katika mateso chini ya utawala wa Saadam kwa muda mrefu wamekuwa wakijitahidi kujitenga ili wawe huru kuishi kama binadamu na raia huru. Licha ya jitihada za Sadam kuwafunga na kuwaua mawazo ya wao kuwa na kwao hayakukoma. Na kwa muda mrefu wamekuwa wakijitahidi kujenga utawala wao. Na sasa hivi eneo la Kurdistan ambako Wakurdi wa Iraq ingawa ni sehemu ya nchi ya Iraq wanajiendeshea mambo yao katika shirikisho la Iraq lakini wakiwa na serikali yao na viongozi wao.
- Taifa la Marekani liliamua kujitangazia uhuru wake toka Dola ya Muingereza baada ya kutoa malalamiko yao (soma declaration of independence) na malalamiko hayo kutofanyiwa kazi na Mfalme. Walifanya hivyo ili wawe na sehemu ambayo wako huru kuamua mambo yao kwani mfalme hakuwa tayari kuwasikiliza. Kujitangaza kwao huko kulisababisha vita iliyozaa uhuru Julai 4, 1776.
- Biafra, wananchi wa Nigeria wa kabila la Igbo na makabila madogomadogo yanayohusiana nayo waliamua kujitoa katika shirikisho la Nigeria na kutangaza uhuru wao na taifa lao. Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi kama tano zilizotambua Taifa hilo jipya kwa misingi niliyoisema hapo juu. Kwa Wanigeria ilikuwa ni kitendo cha uhaini lakini kwa wa Igbo ilikuwa ni kitendo cha kulinda maisha yao na ya watoto na uzao wao. Baada ya muda si mrefu Biafra ikalazimishwa kusalimu amri na kurudishwa kwa nguvu kwenye Shirikisho. Hata hivyo hisia ya kutaka kuwa huru bado ipo na vizazi vya wa Igbo bado wanasimuliana juu ya njozi hiyo ya kuwa watu huru.
Nina mifano mingine ambayo nitaicha pembeni kwa wakati huu.
Ninachosema ni kuwa suala la Pemba si suala la uvunjaji wa sheria au Katiba per se. Ni suala la watu na jamii ya watu kuwa na mawazo ya kujitenga. Huwezi kuwalazimisha watu ati watii katiba wakati Katiba iliyopo inatumika kuwakandamiza, kuwatenda au kwa namna yoyote kuwafanya wawe duni.
Mwanadamu anayo haki ya kutii dhamira yake zaidi, utu wake, na haki yake kama mwanadamu na raia kuliko kutii sheria ambayo inatishia dhamiri, utu, au haki hiyo. Ndugu zetu wa Zanzibar wana madai tena mazito. Madai hayo ambayo yamekuwa yakitolewa mara nyingi kwa maoni yao yamepuuzwa na kutofuatiliwa. Kitendo cha kuwakamata sasa kinaendeleza mwelekeo huo huo kwamba lazima wapemba waconform kimawazo to the majority. Hili haliwezekani.
Matatizo ya wa Pemba ni matatizo ambayo yanahitaji kutambulika kwa kanuni kadhaa ili kuweza kuyatatua. Kutoa tishio la sheria au nguvu za dola ni udhaifu mkubwa kwani hakuna dola iliyowahi kuzima mawazo ya uhuru, au kutia pingu fikra za mabadiliko. Walishindwa wajerumani, walishindwa Waingereza, walishindwa Afrika Kusini, Alishindwa Mussolini, alishindwa Sadam, alishindwa Stalini, na kwa hakika atashindwa Mwema na Kikwete.
Kama mbegu ya kutaka kuheshimika na kutambulika utu wao imepandwa katika wapembwa hakuna atakayeweza kuizima. Hiyo ndio hali halisi.
Jukumu letu basi ni nini? Je tukubali wapemba wajitenge kwa sababu tumeshindwa kuwasikiliza? Je tuache sehemu ya Jamhuri yetu kujitenga kwa sababu wanasiasa wamekuwa goigoi kufikiri na wa wazito kutatua matatizo yao. La hasha!
Mimi binafsi kama mpenzi wa Muungano wetu na nikiwa mwanafunzi mzuri wa Mwalimu sioni jambo lililoshindikana. Ni wito wa kila mtanzania kuulinda, kuuenzi na kuutetea Muungano na Jamhuri yetu na hatuwezi kuacha jamii ya watu itishie muungano huo. Haiwezekani kikundi cha watu kikatae kusikiliza matatizo ya ndugu zetu wa Pemba hadi kuwalazimisha kutaka kujitenga.
Swali langu?
Je, utawala wa serikali ya CCM wamefanya juhudi gani za kushughulikia matatizo yanayotajwa na Wapemba? Muafaka siyo juhudi za kweli kwani hilo linahusu utawala na mambo ya siasa na hakuna ajenga ya hali ya wananchi wa Pemba au malalamiko yao. Je kwa vile Pemba wengi ni CUF ina maana serikali tawala haitakiwi kuonesha juhudi za kuheshimu maamuzi ya wananchi wa huko?
Ndugu zangu ipo njia ya haki, yenye usawa na yenye umoja. Njia ambayo itaweza kuondoa hisia hizi na kuzizika mara moja.
a. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, iangalie katika uongozi wake ina wananchi wangapi kutoka Pemba. Je ni lazima mtu awe CCM ndio apewe nafasi ya uongozi? Kama Pemba imetoa wabunge wengi tu kwanini wasiingizwe kwenye serikali? Hili halihitaji kura ya maoni linahitaji akili. Huwezi kushinda kwa asilimia 53 halafu ukaishi kama umeshinda kwa asilimia 90! SMZ ilipaswa mara baada ya uchaguzi kukaa chini na CUF na kupanga mkakati wa kushirikiana.
b. Rais Kikwete badala ya kuchagua wakuu wa mikoa na wilaya za Pemba toka CCM angechagua kutoka CUF na hata viongozi wengine angewachanganya wa CUF pia. Hilo halihusu sera au katiba ni suala la akili tu. Kwanini hakufanya hivyo wakati anajua kabisa kuwa Pemba ni kwa kiasi kikubwa mashabiki wa CUF. Angeweza hata kuunda ushirikiano wa aina fulani kati ya viongozi wa CCM na CUF kule Pemba. Lakini hakufanya hivyo.
c. Serikali iwaachilie wananchi hawa mara moja na kukaa meza moja na kuwasikiliza. Tusiingie kwenye mtego wa kufungana kwa mambo haya kwani tutaanza kutengeneza wafungwa wa kisiasa na kuanza kupandikiza zaidi fikra za mapambano. Tusiingie kwenye mtego huo. Serikali ifute madai yake, itengeneze timu ya ushirikiano (nje ya mazingaombwe ya muafaka) na kuamua kwa makusudi kabisa kuwashirikisha wananchi wa Pemba katika maamuzi na utawala. Walikipanda wenyewe, sasa wasishangae wanavuna miiba!
d. Viongozi wa CUF watangaze hadharani kuwa lengo lao si kuvunja muungano au kutangaza Taifa huru bali wanataka nafasi ya kutambuliwa na kuthaminiwa kama raia kamili wa jamhuri yetu. Maneno ambayo yamewahi kusikika ya "Mwarabu hatotawala Zanzibar" wakati mwarabu huyo ni raia ni maneno yanayowafanya waarabu wa eneo letu kuwa nusu raia. Leo hii Botswana inatawaliwa na raia ambaye baba ni mweusi na mama ni mzungu! Sisi tunahangaika na mambo ya ajabu ya nasaba! Leo Marekani inaweza kujikuta ikitawaliwa na kiongozi ambaye baba yake ni mweusi na mama ni mzungu! sisi tunashindana na alilala na Sultani na nani na kijakazi!
Ndugu zangu watanzania, matatizo ya Zanzibar yanatatulika na wala hayahitaji mkono mkubwa wa dola ili kuyamaliza. Yanahitaji utashi wa kisiasa, ushirikiano wa kuaminiana na moyo wa udugu. Watawala wa Zanzibar lazima wakubali kwa vitendo kuwa Wapemba ni wananchi sawa na wale wa Unguja na wanahaki sawa katika Taifa hilo bila kuangalia nasaba zao, historia zao n.k Na hili lazima lichukuliwe hadi kwenye serikali kuu. Kujifanya ati tunawakamata na kuwatia pingu na kuwatishia ni kitendo kilichofanywa na serikali ya makaburu na no sir, hatuwezi kuacha serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar kuanza kutenda kama serikali za makaburu au za kibaguzi.
That is my argument and I'm sticking to it.
M. M.
...ni kweli kaka; tatizo la Pemba ni hicho kisiki kinachoendela kukariri kuwa Babake alifanya mapinduzi ilhali alikuwa mwoga ka' MBWA KOKO!!JS, unajua mara nyingi wanatulaumu kuwa tunawakosoa tu, hatutoi mapendekezo ya suluhisho la matatizo. I hope mmoja wao atanyaka na kuongezea katika hayo. Binafsi naamini matatizo ya Pemba na Zanzibar kwa ujumla yanatatulika.