Mnyamahodzo
JF-Expert Member
- May 23, 2008
- 1,932
- 985
Ukiwapa taarifa Polisi kuwa mahali fulani kuna maiti, kauliwa au kajinyonga, watakuja kichwakichwa bila ya note book ya kuweka michoro wala camera. Watakachokumbuka ni gloves tu. Hivi kwa wao kutokubeba camera ni ujinga, uzembe au umaskini wa Jeshi hilo kutokuwa na camera hata katika ofisi ya Polisi ya wilaya?
Swali hili lilipata nguvu kubwa sana wiki chache zilizopita baada ya kuangalia kipindi cha "Crime investigation" ktk Discovery channel. Nikiwa nyumbani kwa mwenyeji wangu nalipata fursa kuangalia kipindi hicho pamoja na shemeji yake mwenyeji wangu ambaye ni Pathologist huko Uganda. Katika maongezi baada ya habari hiyo Daktari huyo aliniazimisha kwa siku 2 kitabu cha " Concise Text and Manual of FORENSIC MEDICINE, MEDICAL LAW and ETHICS IN EAST AFRICA". Ndani yake nilikutana na mambo mazuri na mengine ya kustaajabisha. Zipo kurasa nilipiga-copy.
Katika Section C (Forensic Pathology) Chapter 1,2 & 3 zimeandikwa na watanzania. Katika Chpt 3, Dr Ahmed Makata (wa Wizara ya Mambo ya Ndani) na Dr Martin Mbonde (wa MUHAS, aliyetoa ushahidi wa postmortem katika kesi ya Zombe) wameandika mambo ambayo hadi sasa sijaona kufanywa na Jeshi la Polisi wanapokwenda kuichukua miili ya maiti mbalimbali huku mitaani, barabarani au ktk fukwe za mito, maziwa au bahari. Nanukuu "It is the role of the scene of crime officer to assess situations in which a visit to the scene by a medic is most relevant. Whenever there is apparent inconsistency between the state of the body and the situation at the scene, it is prudent for the scene crime officer to involve the medic rather than risk losing evidence or creating artifacts. Where the medic cannot visit the scene, a detailed and accurate recording of the status of the scene of crime should be done, including the use of sketches, diagrams, still photographs and even video recording."
Picha zinatakiwa kupigwa kabla ya mwili kunyanyuliwa au kugeuzwa. Na kila unapogeuzwa picha inabidi zipigwe, mazingira nayo yapigwe picha.Na mambo kadhaa wa kadhaa.
Swali hili lilipata nguvu kubwa sana wiki chache zilizopita baada ya kuangalia kipindi cha "Crime investigation" ktk Discovery channel. Nikiwa nyumbani kwa mwenyeji wangu nalipata fursa kuangalia kipindi hicho pamoja na shemeji yake mwenyeji wangu ambaye ni Pathologist huko Uganda. Katika maongezi baada ya habari hiyo Daktari huyo aliniazimisha kwa siku 2 kitabu cha " Concise Text and Manual of FORENSIC MEDICINE, MEDICAL LAW and ETHICS IN EAST AFRICA". Ndani yake nilikutana na mambo mazuri na mengine ya kustaajabisha. Zipo kurasa nilipiga-copy.
Katika Section C (Forensic Pathology) Chapter 1,2 & 3 zimeandikwa na watanzania. Katika Chpt 3, Dr Ahmed Makata (wa Wizara ya Mambo ya Ndani) na Dr Martin Mbonde (wa MUHAS, aliyetoa ushahidi wa postmortem katika kesi ya Zombe) wameandika mambo ambayo hadi sasa sijaona kufanywa na Jeshi la Polisi wanapokwenda kuichukua miili ya maiti mbalimbali huku mitaani, barabarani au ktk fukwe za mito, maziwa au bahari. Nanukuu "It is the role of the scene of crime officer to assess situations in which a visit to the scene by a medic is most relevant. Whenever there is apparent inconsistency between the state of the body and the situation at the scene, it is prudent for the scene crime officer to involve the medic rather than risk losing evidence or creating artifacts. Where the medic cannot visit the scene, a detailed and accurate recording of the status of the scene of crime should be done, including the use of sketches, diagrams, still photographs and even video recording."
Picha zinatakiwa kupigwa kabla ya mwili kunyanyuliwa au kugeuzwa. Na kila unapogeuzwa picha inabidi zipigwe, mazingira nayo yapigwe picha.Na mambo kadhaa wa kadhaa.